Samia ana hadhi na haki kufuta sherehe za uhuru wa Tanzania 2024

Samia ana hadhi na haki kufuta sherehe za uhuru wa Tanzania 2024

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
20241205_082553.jpg


Bendera yetu halisi.

Screenshot_20241205_082819_X.jpg


Ndugu zangu.

Maamuzi ya Rais Samia kufuta sherehe za uhuru wa Tanzania ni sahihi kwa wakati huu tunapoelekea kupata katiba mpya na bora.

Tanzania haikupata uhuru wake Desemba 9, 1961. Bali nchi ya Tanganyika ndiyo inayosherehekea Uhuru wake siku hiyo. Nyerere na wenzake hawakupigania uhuru wa 9 Desemba kwa Tanzania bali kwa Tanganyika na Watanganyika.

Tumpongeze bi Samia kwa kuamua kuuishi ukweli. Ameona ni upuuzi kusheherekea uhuru wa Tanganyika chini ya kivuli cha Tanzania. Tanzania ni zao la muungano ambapo Zanzibar baada ya Mapinduzi ya 12 January 1964 ikaungana na Tanganyika ili kuzaa Tanzania mnamo tarehe 26 April 1964 kiasi cha miezi mitatu mbele baada ya Mapinduzi.

RAI
Sisi Watanganyika, tusheherekee siku ya Uhuru wetu bila kificho. Tuvae Tshirts zenye bendera yetu na tarehe ya uhuru, tubebe skafu zenye kuipamba Tanganyika na siku yake ya uhuru. Tusheherekee kutoka mioyoni mwetu huku tukiendesha mijadala ya wazi na mitandaoni kuhusu uhuru na manufaa ya muungano.

Siku ya Tanzania ni 26 April na siyo 9 Desemba.

Happy Independency Day for Tanganyika 1961
 
Mimi sioni kama amefanya kosa. Maana huo uhuru wa Tanganyika, unatuhusu sisi Watanganyika. Na hauihusu Zanzibar, Kenya, Uganda, au Burundi! Au wananchi wa hizo nchi majirani.

Na hata kama amezifuta hizo sherehe, Watangayika bado tutazisherehekea kwenye mioyo yetu, huku tukitambua fika kwa sasa tunatawaliwa na Mkoloni mweusi (CCM). Na huyu naye lazima tumuondoe! Ikiwezekana hata kwa kutumia nguvu.
 
Mimi sioni kama amefanya kosa. Maana huo uhuru wa Tanganyika, unatuhusu sisi Watanganyika. Na hauihusu Zanzibar, Kenya, Uganda, au Burundi! Au wananchi wa hizo nchi majirani.

Na hata kama amezifuta hizo sherehe, Watangayika bado tutazisherehekea kwenye mioyo yetu, huku tukitambua fika kwa sasa tunatawaliwa na Mkoloni mweusi (CCM). Na huyu naye lazima tumuondoe! Ikiwezekana hata kwa kutumia nguvu.
Hakuna namna. Mkoloni lazima aondoke kwa hiyari au lazima
 
Tatizo ni aina ya muungano tulionao ambao haukueleweka muundo wake toka siku ya kwanza, Nyerere kafanya mengi mazuri lakini kwenye hili la Muungano alichemsha sana na kwa bahati mbaya kila kiongozi anayeshika madaraka ni kama anaogopa kuliweka sawa kwa kuogopa eti Muungano unaweza kuvunjika lakini kwa hali ilivyo bora hata huo Muungano uvunjike kuliko kuendelea na hali hii tuliyonayo sasa.

Leo tumefikia hatua Watanganyika kutawaliwa na Mzanzibari kwa kisingizio cha serikali ya muungano wakati kiuhalisia iliyopo ni serikali ya Tanganyika kwa sababu haina mamlaka yoyote huko Zanzibar bali mamlaka yake yanaishia Tanganyika tu,aibu tupu kwetu Watanganyika.
 
Sijawahi ona Nchi yenye Upimbi kama hii.

Sherehe ya UHURU ni sikukuu ya tukio kihistoria, tukio ambalo watanganyika wanatakiwa kulifurahia na kulienzi miaka na miaka.

Historia hii inatakiwa uendelee kuenziwa Enzi na Enzi.

Unanunua Pikipiki na kusambaza Tanzania nzima, Siku Moja ya uhuru italitia Taifa umasikin?

Ikiwa mwanadamu atafanya sherehe ya kuzaliwa kwake Kila mwaka, Vipi kuhusu TAIFA?

KWANINI WAZANZIBAR WALIENDELEA NA SHUGHULI ZAO ZA MAISHA, SIKU AMBAYO TANGANYIKA ILIKUA NA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA?

IKIWA KWAO HILO HALIKUWAHUSU, KWANINI MZANZIBAR AFUTE SHEREHE ZA UHURU WA TANGANYIKA?.

MAPINDUZI HUWA WANAFUTA?

MITAMGANYIKAAA IPO TU NA NDO INAMZUNGUKA NA KUMSHAURI UPUUUZI MKUBWA WA NAMNA HII.

SHAME !!.
 
Mantiki ya sherehe kama hizi ni kuuza nationalism propaganda (nothing else).

Na hakuna jukumu kubwa la usalama wa taifa kama nationalism propaganda,

Tukikota hapo tunaanza kutafuta wachawi miongoni mwetu.

Sidhani kama kuna kazi kubwa ya usalama kama nationalism propaganda.

Kwa kazi waliofanya waingereza japo mimi ni mtanzania ninae ipenda nchi yangu ya asili.

Ila siku hiki kijiji chetu kikivamiwa nina uhakika mimi Sniper , Teknocrat na wachangiaji wengine wa huku kijijini siku hiki kisiwa kikivamiwa tupo tayari kukilinda; hao niliowataja siwajui personal lakini nina uhakika wa 100% hawawezi pinga hiyo dhana at heart.

Swala la nationalism propaganda sio la mzaha hata kidogo kama watanzania mnavyolichukulia.

Shida tunarudi pale, pale asilimia kubwa ya maafisa usalama hawana uwezo; you can tell.
 
View attachment 3169305

Bendera yetu halisi.


View attachment 3169306

Ndugu zangu.
Maamuzi ya Rais Samia kufuta sherehe za uhuru wa Tanzania ni sahihi kwa wakati huu tunapoelekea kupata katiba mpya na bora.

Tanzania haikupata uhuru wake Desemba 9, 1961. Bali nchi ya Tanganyika ndiyo inayosherehekea Uhuru wake siku hiyo. Nyerere na wenzake hawakupigania uhuru wa 9 Desemba kwa Tanzania bali kwa Tanganyika na Watanganyika.

Tumpongeze bi Samia kwa kuamua kuuishi ukweli. Ameona ni upuuzi kusheherekea uhuru wa Tanganyika chini ya kivuli cha Tanzania. Tanzania ni zao la muungano ambapo Zanzibar baada ya Mapinduzi ya 12 January 1964 ikaungana na Tanganyika ili kuzaa Tanzania mnamo tarehe 26 April 1964 kiasi cha miezi mitatu mbele baada ya Mapinduzi.

RAI
Sisi Watanganyika, tusheherekee siku ya Uhuru wetu bila kificho. Tuvae Tshirts zenye bendera yetu na tarehe ya uhuru, tubebe skafu zenye kuipamba Tanganyika na siku yake ya uhuru. Tusheherekee kutoka mioyoni mwetu huku tukiendesha mijadala ya wazi na mitandaoni kuhusu uhuru na manufaa ya muungano.

Siku ya Tanzania ni 26 April na siyo 9 Desemba.

Happy Independency Day for Tanganyika 1961
Dunia ni gunia limesheheni taka taka mbali mbali yupo kitandani saa hii amepiga msamba muda huu aje ayaseme hayo!
 
Wakati Magufuli alifuta sherehe za nchi ilikuwa hakuna Masuwali lkn Leo Rais Samiha ametupa Uhuru wa kujieleza Apewe mauwa yake
 
Back
Top Bottom