Samia: Msiruhusu Wageni Kufanya Biashara za Wenyeji

Samia: Msiruhusu Wageni Kufanya Biashara za Wenyeji

Rais Samia amewashangaa watendaji wa Serikali kutoa leseni za biashara ndogo ndogo Kwa wageni akitokea mfano Mchina muuza Mitumba Kariakoo.

Naungana na Rais Samia,hili ni jambo amenifurahisha sana maana nimewahi andika humu jf kwamba inkuaje Wachina wanafanya biashara ndogo ndogo badala ya uwekezaji,nani aliwapa vibali vya kuingia Nchini Kwa Ajili ya biashara ndogo.

Wamefika mbali saizi wamejigeuza Wachimbaji Wadogo wa Madini.Hii tabia ikomeshwe mara Moja kwa Wizara zinazohusika.
View attachment 3034740
Rais Samia Suluhu amemwagiza Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo kuangalia suala la raia wa kigeni kupewa leseni za kufanya biashara zinazofaa kufanywa na wenyeji.

Pia soma Dar: Raia wa China wageuka machinga, Wananchi washitushwa

My Take
Hongera sana Samia Kwa kuliona hili.

Viongozi wa Serikali sijui hawaelewi,hivi Kila kitu tutasybiria Rais aseme ndio sheria zitekelezwe? Kwa nini tunakuwa Nchi ya watu wasioelewa wajibu wao?

Pia soma Video: Mwekezaji wa Kigeni( Mchina) Amshushia Kichapo Mzawa Wakigombea Eneo la Kuchimba Madini.
Safi sana kumbe Rais Huwa anapitia humu jf 👇 👇

View: https://youtu.be/U0d1P-CJ3zQ?feature=shared
 
Sasa analalamika nini wakati alipoingia ni yeye ndiye Aliruhusu haya mambo kwa kuruhusu kila mgeni kuja kufanya atakavyo?

Watendaji wake wanakwenda na biti tu.
Unaweza thibitisha?
 
Back
Top Bottom