Bongo movie bila ya maudhui ya ushirikina hamna kitu cha Ubunifu.
Ndo maana Mussa banzi akishika soko kitambo kwa movies zake na watu walipenda sana.
Kujitoa ni kawaida kwanza kakosea kundi kuliita jina lake halisi eti "mkojani gang" ni makosa huyo jamaa ni mkubwa kwa kuigiza kama huyo mkojani so wasingeweza kabisa kukaa sehemu moja .
Kama unabisha fuatilia like kundi la "Tales of the crazy kennar" yule jamaa anajiitaa usefulyidioty alijitoa kwa sababu kwanza jina linaakisi mkubwa ni crazy kennar ,kingine ni ishu ya maslahi hamna cha uchawi wala nn wengi ni waoga.
Nilipokuwa advance niliibiwa paketi ya boxer zilikuwa tatu nilikuwa ndo nimetoka kununua basi ..wananijua mi fika ni mtu wa Pwani basi siku pale shule palikuwa na uwizi wa hatar ,mi nikajua hapa nishapigwa kabisa na sitopata maana ...Jioni tunakuwa na mda wa matangazo tukichukua chakula ile saa 12 nikaomba niongee kitu kwamba nimeibiwa ila natangaza siku 3 kitakachotokea tusipeane lawama.
Na ilikuwa likizo inakaribia kama wiki tusepe ..Dah siku ya tatu nimezikuta juu ya sanduku langu😂😂na zilikuwa zishafunguliwa yaani watu wa bara mnatuogopa sana ....Na huo uchawi ni nadharia wala haupo kabisa.
Nimesoma pale sijawahi kuibiwa mpaka namaliza form six ila nilikuwa nawapanga sana kwa story za uongo za uchawi 😂😂ikawa wananiogopa sana maana sio nipo serious nikitoka dormitory nipo msikitini au darasani yaani sina time kabisa