Samweli Sitta aanza kazi kwa kukiuka kanuni za bunge la katiba

Samweli Sitta aanza kazi kwa kukiuka kanuni za bunge la katiba

Candid Scope

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2010
Posts
11,897
Reaction score
6,925
tundu lissu.jpg Sitta ajue bunge la sasa lina wanasheria mahiri DSC05487.JPG

Mwenyekiti wa Bunge la Katiba Samweli Sitta ameanza vibaya kazi yake siku ya kwanza kwa kukiuka kanuni za Bunge la katiba.

Sitta alitangaza kwamba Jaji Warioba atawasilisha Rasimu ya Katiba mpya kabla ya Rais Kikwete kuhutubia, jambo ambalo ni uvunjaji wa kanuni za Bunge hilo, maana kanuni inasema wazi Rais Kikwete atahutubia Bunge hilo kabla ya Warioba kuwasilisha rasimu hiyo.

Tundu Lisu mjumbe wa Bunge hilo akitaka mwongozo alimtahadharisha Sitta juu ya ukiukwaji huo, na kwamba sababu ya kuwekwa sheria hiyo ni kuondoa kile ambacho kingeonekana Kikwete kumjibu Mwenyekiti anayewasilisha mswada, hivyo ilikubaliwa Rais ahutubie kwanza Bunge ndipo mwenyekiti Warioba awasilishe rasimu.

Hali halisi inaonekana CCM wanaendelea kucheza faulo kwenye Bunge hili.
 
All the same,mimi nadhani tatizo liko pale pale watajaribu kumjibu warioba kupitia wale wasanii wao ambao wako hapo kwa muda mfupi tu wa miaka kumi tangu kuacha kuchunga ng'ombe alafu wanajidai wanajua kanuni huku kuna watu wenye zaidi ya miaka 24 wako kimya
 
TL inabidi apewe ulinzi. Ni mtu muhimu sana kwa taifa hili!
 
Mi ccm huwa haisomi chochote wanachopewa wanawaza posho tuu,ndiyo maana hata mikataba inakuya ya kishenzi kuumiza wananchi
 
Mambo mengine ni suala la logic, huwezi kuzindua bunge wakati watakachojadili hapo hawanacho.
 
This is sheer prejudice and mind-numbing stereotype. Do you assess mastery of the rules by the number of years spent in parliament alone? Wouldn't that assumption fit awkwardly with the excellent job that Tundu Lissu is doing, less than five years in the house. As a person belonging to the digital age, unlearn destructive mind reflexes common to old politicians-cultivate an open mind. Acha kukariri porojo za wanasiasa.

All the same,mimi nadhani tatizo liko pale pale watajaribu kumjibu warioba kupitia wale wasanii wao ambao wako hapo kwa muda mfupi tu wa miaka kumi tangu kuacha kuchunga ng'ombe alafu wanajidai wanajua kanuni huku kuna watu wenye zaidi ya miaka 24 wako kimya
 
Mzimu wa kalenga unakuchanganya hujakaa sawa unajua kanuni wewe tangu lini.
 
Mambo mengine ni suala la logic, huwezi kuzindua bunge wakati watakachojadili hapo hawanacho.
Kabisa kabisa ingekuwa ni wehu wa hali ya juu rais anazindua bunge hata rasimu haipo mezani sijui ingekuwa kitu gani.
 
matokeo ya kalenga ndo habari ya mujini na mpango mzima kwa sasa hivi.
 
Mzimu wa kalenga unakuchanganya hujakaa sawa unajua kanuni wewe tangu lini.

Povu lote la nini. Jadili mada iliyo letwa, kwa kawaida asiye na upeo mkubwa katika kujadili mada huja kwa speed ya mipasho.

Kwa taarifa yako mie si mponea dezo za kisiasa, naponea jasho langu, na katu siwezi kushinda majukwaani nikishupaza mishipa kama sina akili timamu, bora nikalime tuta la mbatata na hakuna mwenye kunisuta au kuja kunikagua ilivyo mfanyiwavyo vinavyotokana na dezo.
 
Sitta mlimsifia sana ila mimi nasema wazi kuwa ni janga la Taifa
 
Sitta mlimsifia sana ila mimi nasema wazi kuwa ni janga la Taifa

Ndoto za taifa letu kupata katiba itokanayo na wananchi zimezimika rasmi leo baada ya kushuhudia ubabe wa kipummabaavu wa 6 bungeni
 
Kama kanuni ndivyo ilivyo huyu 6 anataka kuonyesha
nini? Viongozi wote waliochaguliwa kwa akura nyingi duniani huwa ni majanga.
 
Halafu hiki kizee kisipokuwa makini kitakuja kufa kama kuku bila heshima yoyote!
 
Ndoto za taifa letu kupata katiba itokanayo na wananchi zimezimika rasmi leo baada ya kushuhudia ubabe wa kipummabaavu wa 6 bungeni

Ni mara Mia moja Pandu Kificho angakaa kwenye kiti hichi hakika angefanya makubwa kwa hekima na Busara zake ila Sitta anaendesha Bunge kibabe akifikiri ni kile kipindi chake ambacho wabunge lile lisilojitambua.......Leo hii ajue kuna watu wanasoma kanuni na kulala nazonhivyo kuwaburuza hakutakuwa na mwisho mzuri.
 
Back
Top Bottom