Sarah Baartman: Mwanamke mweusi kutoka Afrika Kusini aliyesafirishwa Ulaya kwa maonesho ya makalio makubwa

Saartjie aliteseka sana huyu dada na ndo alishikiria history ya kunyanyasika na kudhalilika kwa mwanamke wa Africa.
 
Dada huyu aliishi kwa mateso makubwa!
Hii ni sababu nyingine ya kuwachukia wazungu!!
 


Naona unyanyasaji siku hizi umegeuka kuwa kitu cha kawaida tu ?? Japo huko Instagram wanawake hawawekwi kwenye Cages ila sehemu kubwa ya miili yao ni utupu tu
Mkuu UncleBen hao wa Insta wanafanya kwa hiyari yao,Sarah Baartman ilikuwa ni shuruti

Zaidi ya Sarah,kulikuwa na kijana anaitwa Otta Benga,huyu nilimsoma wakati nafanya masomo yangu ya "Cultural Anthropology" kuna kitu wanaita "Cultural Ethnocentrism"....huyu kijana walimchukuwa na kumuweka kwenye zoo na nyani na wazungu wakawa wanakuja kumtazama,dogo alikuwa na meno yamechongoka kitu kilichokuwa kinawashangaza wazungu,wengi wakawa wanakuja kumcheki Benga wakiamini kabisa kuwa muafrika hana tofauti na nyani.

Lakini sehemu nyingine wazungu walikuwa wanawachukuwa wanawake walio uchi na kuwaweka ktk maonesho kwa kiingilio sbb kuna wazungu walikuwa hawajawahi kuona mwanamke wa kiafrika anafananje akiwa uchi.Huwa nashangaa sana tunavyowaamini wazungu,mzungu hajawahi kumpenda wala kumthamini muafrika,ukiona mzungu anajifanya kukupenda ujuwe ana maslahi na ukaribu wenu.Ama hakika waafrika tunadharaulika sana
 
Asante Mkuu japo huo udhalilishaji ninao usema wa Instagram kiasi fulani wazungu wamekuja tu na advanced tool ya unyanyasaji badala ya kulazimishwa mtu anaweka tu mwenyewe ,Waafrika tunadharaulika sana ,wakati mwingine huwa namuuliza Mungu hivi siku ya hukumu kama kutakua na session ya maswali na majibu ,Mtu kama Sarah ama Otta wakimuuliza Mungu ni kwanini uliamua nipitie haya sijui atakuja na majibu gani ila naamini ni muweza wa yote na sipaswi kuwa na wasiwasi nae, Waafrika kwa sehemu kubwa nadhani tumeumbiwa mateso ,
 
Kuna wakati nilipata kukaa na jamaa yangu aliyelelewa na wazungu wamisionari,jamaa mmoja msheshi,bright na mcha Mungu.Kuna wakati ulifika ilikuwa kipindi cha Kwaresma,akawa ananisimulia kuwa ye aliwahi kaa na wazungu,siku wakagundua jamaa anafunga Kwaresma...Jamaa walimshangaa sana,mpka wakamuuliza we unafunga ili iwe nini?Maana kwa ugumu wako tu wa maisha we kwako kila siku ni kwaresma..Yaani waliona maisha ya kila siku ya jamaa wakaona kuwa life tu la jamaa ni kwaresma tosha
 
Wee jamaa barafu si ndio mwenye ule mkasa wa kuiba almasi?naona na huku unashusha sana nondo za historia,kule jukwaa la siasa naona tena upo...We jamaa wapi ni wapi??au mkuu UncleBen mwenzangu unapata picha gani hapa?Though asante kwa nondo zako kwenye uzi huu
 
Hahaha jamii forum ni kisiwa cha elimu ukiwa mpole unafuatilia utajua mambo mengi , jamaa anajua mambo mengi
 
Kijana we soma,elimika then chapa lapa....Mambo ya humu kujuana kwingi hakupo!!burudika penye kuburudika na elimika kwenye kuelimika....ashukuriwe aliyebuni JamiiForums
 
nmekmbka post moja MMU,kwamb wanawake wengi wenye makalio makubwa wazur kuangalia tu
 
so sad
 
Asee huyo dada angekua hai saa hii angepata soko sana.....

Churaaaaa....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…