Sare ya Yanga na Coast Kombe la Azam na ugomvi wa Haji na Karia ulitokana na wachezaji wa Yanga kuhongwa

kambale mnene

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2022
Posts
271
Reaction score
197
Wajuzi hebu mje kama mnajua lolote kuhusu hilo.

Inasemekana kuna wachezaji watatu akiwemo Mwamnyeto walihongwa na Karia ili Yanga ifungwe katika ile mechi. Habari zilivuja na kumfikia Haji, ikawa ndiyo chanzo cha ugomvi na patashika pale jukwaani iliyopekea Haji kufungiwa.

Wakongwe hili likoje?
 
Kwamba haji anauchungu sana na utopolo? Izo ni story za vijiwen tu
 
Hizi tetesi umezisikia lini?
 
Wale KICHEFUCHEFU ni Wahuni waliojificha kwenye uongozi wa Soka!
 
Habari zivuje Kwa watu wote zikafike kwanza kwa Haji?

Ukiachana na mechi ile, mechi nyingi zilizofatia tumeona namna gani Mwamnyeto amekuwa uchochoro, kuanzia kwenye siku ya mwananchi, ligi na hata timu ya Taifa, vipi huko alihongwa na nani?

Tatizo bongo tumezoea kushikana uchawi kwenye kila jambo, wakati mengine yapo wazi kabisa.

Nondo kwasasa ni uchochoro, ametumika sana tokea akiwa Coastal, timu ya Taifa na Yanga. Wachezaji sio mashine, form ikishuka, wapumzishwe, hata mashine zinafanyiwa service.
 
Yaani Yanga itoke kwenye kushutumiwa kuhonga timu pinzani na mashabiki wa mbumbumbu fc, mpaka kuhongwa na timu ndogo na inayoikamia Yanga mara zote kama Coastal Union!! Hauko kabisa serious.
Umesoma vizuri au umetoka kukatwa sunga?
 
Umesoma vizuri au umetoka kukatwa sunga?
Haijalishi! Bado huyo Karia hana hela za kumhonga mchezaji wa Yanga! Kiufupi timu ilifanya makosa ya kiufundi kwenye eneo lake la ulinzi. Mwamnyeto alihusika, Kibwana Shomari alifanya makosa! Na mlinda mlango naye alifanya makosa kwa nafasi yake! Hivyo kumhukumu Mwanyeto peke yake, ni kumuonea! Ingawa amekuwa na changamoto ya kujisahau awapo uwanjani.

Na nikuhakikishie; hakuna shabiki wa Yanga mwenye akili timamu, anaweza kuamini story za kijiweni kama hizi.
Mimi ninachofahamu Manara na huyo Karia, wote ni waropokaji na watu wenye maneno machafu na ya kejeli vinywani mwao!

Na ndiyo maana mpaka kesho nimebakiwa na mshangao!
Ni kwa nini hiyo kamati ya maadili ilimhukumu Haji Manara peke yake, na wakati hata huyo Wallace Karia kwa mtazamo wangu alihusika kwenye kujibizana maneno ya kijiweni na huyo mwenzake Haji Manara.
 
Hii chapter isha kua closed tuendelee na mambo mengine
 
Mleta mada anajaribu kuanzisha mada hasi kwa Yanga ili kuzima fukuto liliopo Simba!
 
Tumia akili kidogo tu
 
Manara aitumie hii kwenye rufaa yake huenda akachomoka
 

Haji Manara huyu huyu Simba lia lia awe na uchungu na Yanga kiasi hicho?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…