Sasa hivi watumishi wa dini zote wanatumia mafuta/maji, mashambulizi ni kwa aliyefanikiwa tu

Mkuu covex acha kutetea vitu vilivyo dhahili. Unaposema watu kama akina sheik Yahaya wanatengwa na hawaruhusiwi hata kuongoza swala unamdanganya nani?. Sheikh Yahaya kaongoza swala Ijumaa nyingi tu nenda you tube jionee. Unatetea nini sasa wakati masheik kibao ni wanajimu, waganga, wapiga ramli, wafuga majini na swala msikitini wanaongoza?.
 
Kwa
Kwa Wachungaji wa kisabato hakunaga hiyo mambo ya mafuta wala maji ya upako. na kama yupo atakuwa ni muasi au anajiita yeye binafsi mchungaji wa kisabato. Vilevile unaweza thibitisha kwa ushahidi uliyemwona na kichupa cha maji ya upako ni mchungaji wa kisabato
 
Muongozo wake unamuhitaji awe na mafuta kwa ajili ya wagonjwa. Waulize vizuri watakusaidia. Sio uasi ni kwa msingi wa Yakobo5:14. Huwezi kujua kwa sababu yanatumika kwenye kesi chache na wengi hawapendi kutumia
 
Muongozo wake unamuhitaji awe na mafuta kwa ajili ya wagonjwa. Waulize vizuri watakusaidia. Sio uasi ni kwa msingi wa Yakobo5:14. Huwezi kujua kwa sababu yanatumika kwenye kesi chache na wengi hawapendi kutumia
Yawezekana. Ila ingekuwa bora zaidi ungeweka humu sehemu ya huo mwongozo, inayotoa maelekezo kwa mchungaji wa kisabato kutumia mafuta ya upako. Kwa faida ya wote ambao hatujawahi fahamu hiyo kanuni
 
mimi sina aja ya vichupa vya maji ,,,napiga zangu mbizi baharini{nikiwa dar},ziwani[nikiwa kanda ya ziwa] au mtoni nikiwa kwe2 kibosho-moshi.......napiga mbizi huko huku nikisali kwa muda wa masaa mawili,,nikitoka humo mambo yangu yote yanakuwa safi,na vimaradhi vidogovidogo vyote kwishne!!!!........
 
Yawezekana. Ila ingekuwa bora zaidi ungeweka humu sehemu ya huo mwongozo, inayotoa maelekezo kwa mchungaji wa kisabato kutumia mafuta ya upako. Kwa faida ya wote ambao hatujawahi fahamu hiyo kanuni
Sio tu Muongozo wa hao wachungaji, hadi roho ya unabii kitabu cha Pastoral ministries kimeeleza ila kwa tahadhari.
Mgonjwa awe mahututi, pia yasitumike kwa wale ambao wanavunja amri kumi makusudi, sio kitu cha kutumika mara kwa mara ndio maana unashangaa. Na wapo wachungaji ninawafahamu kama wawili hivi EA huwa wanavyovichupa ila hadi vitumike ni kesi zile kubwa kubwa.

Sio tu wachungaji E.G. White mwenyewe alikuwa anatumia.

Ukiwa na imani lazima uijue vizuri. Mimi nii ni imani yangu, naipenda, imenilea, imenifundisha kumpenda Mungu na Imenipa mke muadilifu, hovyo najitahidi nijue kila kitu kabla ya kupotoshwa au kuishi kwa kukalili.

Shetani anatumia vitu halali kufanyia uchafu. Hayuwezi kuacha kutumia vitu halali kwa kuogopa kuwa shetani anavitumia. Ndio maana husikii mtu kauziwa, au kapakwa mafuta SDA maana Kwanza Neno ndio linanguvu kubwa kuliko hivyo vitu, na kikitumika basi ni mara chache sana tena bila kuweka public. Hata wanafunzi wa Yesu walitumia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…