Sasa ni mwendo wa kutumia maandiko ya Biblia kupiga hela!

Sasa ni mwendo wa kutumia maandiko ya Biblia kupiga hela!

Morning_star

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2018
Posts
6,042
Reaction score
17,320
Leo nimepita kituo cha mwendokasi cha mbezi mwisho! Hiki kituo kilikuwa na utitiri wa watu wanaojinasibu wanahubiri injili ilihali ni kutafuta hela kwa njia ya sadaka! Sasa leo nimekuta spika kubwa ya kiwete akitumia maandiko ya Biblia kuhalalisha kuchangiwa!

(Matayo 25:40) Kitendo hicho bila shaka kimewakimbiza hao wahubiri (watafutaji) na bila shaka watakuwa wamekasirika sana! Muda si mlefu nikamuona mdada mtanashati malidadi kaja kamwaga hela kwenye beseni (zilizokuwa kwenya kimfuko) na kuanza kuhesabu na zilikuwa nyingi kwelikweli (za silver na noti hadi msimbazi) na kuondoka nazo na kumuacha huyo kiwete akiendelea kutengeneza maokoto! Sasa hivi ni mwendo wa kutumia viwete kupiga hela! Wahubiri soko lenu limevamiwa!

Tafuta kazi nyingine!
 
Kiwete alikuwa anatumia mstari huu kuhalalisha kuomba na kupewa hela:

Matayo 25:40
40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.
 
Back
Top Bottom