Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
Yabidi nikiri bila ya kificho
ya kuwa haya ni kweli kabisa..
na hili situngi na ya kwamba yamenikuta kiukweli ukweli.
ni kweli mlandizi husahau bali mtupa maganda hasahau..
Hivi yawaje baada ya miaka kibao kupita
bado samahani yangu yakataliwa?
sababu sipewi bali kukunjiwa "X" tu
ni kweli mla ndizi husahau bali mtupa maganda hasahau...
Kuna siku nilikutana naye ghafla
mwandani wangu wa madongo kuinama
naye kuniona akaniangalia kwa dharau kisigino hadi utosini
ni kweli mla ndizi husahau bali mtupa maganda hasahau..
salamu nilimtupia lakini ni walakini niliambulia
nilitupiwa korosi na alinifyonya kwa ufedhuli
nikamwomba yaishe yeye ngumu akatia..
ni kweli mla ndizi husahau bali mtupa maganda hasahau..
makosa niliuliza na nikaambiwa yabidi nijaze mwenyewe!
sasa nimehukumiwa kwa makosa ambayo hata siyajui
nilichoambulia ni kujuzwa hakuna msamaha hata akiingia kaburini..
ni kweli mla ndizi husahahu bali mtupa maganda hasahau..
kosa langu ni lipi ambalo halina cha ubani?
kama ni bikira yake mbona na yangu aliitafuna bila ya huruma?
mie sina kinyongo naye, sasa yeye mbona purukshani hivyo?
ni kweli mla ndizi husahau lakini mtupa maganda hasahau..
ndizi yangu ni kweli aliimung'unya mung'unya bila cha msalie..
miye nilimvumilia lakini sasa mlalamishi ni yeye yawaje hivyo?
Sukari tulilambishana na sote kufurahiana sasa kejeli na dharau zatoka wapi?
ni kweli mla ndizi husahau lakini mtupa maganda hasahau...
alikula ndizi yangu nami sijasahau lakini yeye hakumbuki hilo
anachokumbuka ni kunisigina kila mahali, hivi yawaje hivyo?
mwafaka nautafuta lakini sioni wa kutusuluhisha..
AMA kwa hakika ni kweli mla ndizi husahau lakini mtupa maganda hasahau...
ya kuwa haya ni kweli kabisa..
na hili situngi na ya kwamba yamenikuta kiukweli ukweli.
ni kweli mlandizi husahau bali mtupa maganda hasahau..
Hivi yawaje baada ya miaka kibao kupita
bado samahani yangu yakataliwa?
sababu sipewi bali kukunjiwa "X" tu
ni kweli mla ndizi husahau bali mtupa maganda hasahau...
Kuna siku nilikutana naye ghafla
mwandani wangu wa madongo kuinama
naye kuniona akaniangalia kwa dharau kisigino hadi utosini
ni kweli mla ndizi husahau bali mtupa maganda hasahau..
salamu nilimtupia lakini ni walakini niliambulia
nilitupiwa korosi na alinifyonya kwa ufedhuli
nikamwomba yaishe yeye ngumu akatia..
ni kweli mla ndizi husahau bali mtupa maganda hasahau..
makosa niliuliza na nikaambiwa yabidi nijaze mwenyewe!
sasa nimehukumiwa kwa makosa ambayo hata siyajui
nilichoambulia ni kujuzwa hakuna msamaha hata akiingia kaburini..
ni kweli mla ndizi husahahu bali mtupa maganda hasahau..
kosa langu ni lipi ambalo halina cha ubani?
kama ni bikira yake mbona na yangu aliitafuna bila ya huruma?
mie sina kinyongo naye, sasa yeye mbona purukshani hivyo?
ni kweli mla ndizi husahau lakini mtupa maganda hasahau..
ndizi yangu ni kweli aliimung'unya mung'unya bila cha msalie..
miye nilimvumilia lakini sasa mlalamishi ni yeye yawaje hivyo?
Sukari tulilambishana na sote kufurahiana sasa kejeli na dharau zatoka wapi?
ni kweli mla ndizi husahau lakini mtupa maganda hasahau...
alikula ndizi yangu nami sijasahau lakini yeye hakumbuki hilo
anachokumbuka ni kunisigina kila mahali, hivi yawaje hivyo?
mwafaka nautafuta lakini sioni wa kutusuluhisha..
AMA kwa hakika ni kweli mla ndizi husahau lakini mtupa maganda hasahau...