Sasa rasmi Wapemba ni miongoni mwa Makabila zaidi ya 40 nchini Kenya yanayotambuliwa

Sasa rasmi Wapemba ni miongoni mwa Makabila zaidi ya 40 nchini Kenya yanayotambuliwa

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Sasa Wapemba waishio Kenya wametambuliwa kama kabila rasmi nchini humo

Kiongozi wa Wapemba Pwani ya Kenya amesema wamekuwepo Kenya kwa miaka Mingi na waliamua kufanya sensa na kuomba kusajiliwa miongoni mwa Makabila ya Kenya

Source: BBC Dira ya Dunia
 
wapemba sie watu wenye Roho nzuri, kabisa hatuna baya na Mtu yakheee
 
Wakenya wahstuke hawa jamaa hata tukiwa wanyamwezi Zanzibar bado utakaribishwa kama muwekezaji 😔
 
Kenya achaneni kutumia kabila Kama ni "official identity" ya raia wenu, huko ndiko kuendekeza ukabila, hivyo vitu ni "social identity".
 
Kenya achaneni kutumia kabila Kama ni "official identity" ya raia wenu, huko ndiko kuendekeza ukabila, hivyo vitu ni "social identity".
Hawangepata vitambulisho,ajira na huduma zozote za kiserikali hata kuwania nyadhifa za uongozi maana walikua wanaonekana Kama watanzania Ila Sasa hivi Wana haki sawa na wakenya wengine.
 
Hawangepata vitambulisho,ajira na huduma zozote za kiserikali hata kuwania nyadhifa za uongozi maana walikua wanaonekana Kama watanzania Ila Sasa hivi Wana haki sawa na wakenya wengine.
Kwanini wasiombe uraia Kama wanavyoomba huku Tanzania bila ya kutambua kabila la mtu?, Walipaswa waombe Kama raia wa nchi zingine.

Mtu akitoka Botswana akija hapo Kenya akiomba uraia atakataliwa kwababu Hana kabila, au kwasababu kabila lake bado halijatambuliwa rasmi hapo Kenya?.

Kwanini serikali ya Kenya inapenda kujua kabila la raia wake?, Inawasaidia nini katika kuongoza nchi yenu?.
 
Kwanini wasiombe uraia Kama wanavyoomba huku Tanzania bila ya kutambua kabila la mtu?, Walipaswa waombe Kama raia wa nchi zingine.

Mtu akitoka Botswana akija hapo Kenya akiomba uraia atakataliwa kwababu Hana kabila, au kwasababu kabila lake bado halijatambuliwa rasmi hapo Kenya?.

Kwanini serikali ya Kenya inapenda kujua kabila la raia wake?, Inawasaidia nini katika kuongoza nchi yenu?.
Kuomba uraia Ni tofauti na kutambulika Kama mwenyeji, kwenye kuomba uraia yapo Mambo mengi hata ukapewa uraia huwezi ukafanya lakini ukatambuliwa Kama kabila Kuna faida yake zaidi ya mhamiaji,pili watu zaidi ya laki moja kwa mfano hamuwezi kuomba uraia mkapewa uraia anapewa mtu mmoja mmoja Ila sio kwa halaiki ya watu,.
 
Kwanini wasiombe uraia Kama wanavyoomba huku Tanzania bila ya kutambua kabila la mtu?, Walipaswa waombe Kama raia wa nchi zingine.

Mtu akitoka Botswana akija hapo Kenya akiomba uraia atakataliwa kwababu Hana kabila, au kwasababu kabila lake bado halijatambuliwa rasmi hapo Kenya?.

Kwanini serikali ya Kenya inapenda kujua kabila la raia wake?, Inawasaidia nini katika kuongoza nchi yenu?.
Hata Tanzania serikali inajua kabila la kila mtu usijitie hamnazo , kwani wazawa wa Moshi Ni kabila gani? Wazawa wa morogoro Ni kabila gani, wazawa wa mtwara Ni kabila gani ? Mbona mnajifanya zuzu kwa Mambo ya hazarani? Leo hii ukatajwa tu kwa jina tayari unajulikana unatoka kabila lipi ,kwa mfano ukiniambia unaitwa kimaro najua wewe Ni mtu wa Moshi ,ukisema unaitwa mwakasitu najua unatoka mbeya ukisema unaitwa mkude najua anatoka uzaramoni ukisikia mtu anaitwa marwa unajua huko Ni ukuriani , mbona Leo unajifanya serikali ya Tanzania haijui watu kwa makabila yao ilihali hakuna mnyiramba anaejiita majina wa wasukuma au mnyaturu akajiita majina ya wanyamwezi kutoka huko tabora ,tuwe wakweli ndugu yangu maana hata serikali zote duniani zinaendeshwa na watu kutoka makabila ,Leo hii unajua speaker was bunge la muungano wa Tanzania Ni mnyakyusa, waziri mkuu majaliwa Kuna uwezekano Ni mngindo kutoka Lindi ,makamu wa rais mpango Ni mtu wa kigoma na watu wa kigoma wanajulikana kwa hivyo usilete ngonjera ndugu yangu,kila mtanzania anajulikana kwa kabila lake ,kwa mfano mtu hapa kenya akiniambia anatoka county flani Kuna uwezekano nijue kabila lake bila hata kutaja pengine Kuna mchanganyiko wa makabila lakini kwa kawaida kila mkoa una asili ya watu wa kabila flani,mfano ukisema unatoka nyanza nitajua wewe mkisii ,mjaluo au mkuria hao ndio wanapatikana nyanza lakini pia kwa lafudhi yako nitajua kabila lako hata usiposema, ukisema unatoka mkoa wa magharibi vilevile nitajua wewe Ni mluhya na ukisema unatoka mkoa wa Kati nitajua wewe Ni mkikuyu au mmeru na Tanzania pia Ni vilevile.
 
Hata Tanzania serikali inajua kabila la kila mtu usijitie hamnazo , kwani wazawa wa Moshi Ni kabila gani? Wazawa wa morogoro Ni kabila gani, wazawa wa mtwara Ni kabila gani ? Mbona mnajifanya zuzu kwa Mambo ya hazarani? Leo hii ukatajwa tu kwa jina tayari unajulikana unatoka kabila lipi ,kwa mfano ukiniambia unaitwa kimaro najua wewe Ni mtu wa Moshi ,ukisema unaitwa mwakasitu najua unatoka mbeya ukisema unaitwa mkude najua anatoka uzaramoni ukisikia mtu anaitwa marwa unajua huko Ni ukuriani , mbona Leo unajifanya serikali ya Tanzania haijui watu kwa makabila yao ilihali hakuna mnyiramba anaejiita majina wa wasukuma au mnyaturu akajiita majina ya wanyamwezi kutoka huko tabora ,tuwe wakweli ndugu yangu maana hata serikali zote duniani zinaendeshwa na watu kutoka makabila ,Leo hii unajua speaker was bunge la muungano wa Tanzania Ni mnyakyusa, waziri mkuu majaliwa Kuna uwezekano Ni mngindo kutoka Lindi ,makamu wa rais mpango Ni mtu wa kigoma na watu wa kigoma wanajulikana kwa hivyo usilete ngonjera ndugu yangu,kila mtanzania anajulikana kwa kabila lake ,kwa mfano mtu hapa kenya akiniambia anatoka county flani Kuna uwezekano nijue kabila lake bila hata kutaja pengine Kuna mchanganyiko wa makabila lakini kwa kawaida kila mkoa una asili ya watu wa kabila flani,mfano ukisema unatoka nyanza nitajua wewe mkisii ,mjaluo au mkuria hao ndio wanapatikana nyanza lakini pia kwa lafudhi yako nitajua kabila lako hata usiposema, ukisema unatoka mkoa wa magharibi vilevile nitajua wewe Ni mluhya na ukisema unatoka mkoa wa Kati nitajua wewe Ni mkikuyu au mmeru na Tanzania pia Ni vilevile.
Ninyi wakenya tatizo hamtaki kukubali pale mnapokosolewa. Tanzania tunayo makabila, tunajuana na kuyatumia Kama "Social identity pekee", kamwe serikali yetu haitambui jamii kwa kutumia kabila.

Huko kwenu juzi juzi nilisikia "wamakonde wametambuliwa rasmi na serikali Kama kabila la 43 hapo Kenya. Kwahiyo makabila yanatambuliwa rasmi na serikali, Kama kabila halijatambuliwa na serikali maana yake Hilo kabila sio "official resident".

Serikali ya Tanzania kamwe haijui makabila yaliyopo Tanzania, wanakisia kwamba ni zaidi ya 130 lakini hakuna idadi kamili kwasababu hakuna popote pale ambapo serikali inahitaji kujua kabila la raia wake, hata katika "census" Hilo swali halipo.

Hivi karibu Kenya iliwatambua wahindi Kama miongoni mwa makabila ya Kenya, huku Tanzania wahindi ni wengi Sana, hatuwatambui Kama kabila, ila ni watanzania wenye asili ya India, kwanini ninyi Kila jamii ya watu mnapenda kuwataja na kuwaweka katika fungi la ukabila?.

Kwa taarifa yako, wapemba hawana kabila, Sasa huko ndio mtaanzisha kabila la "wapemba", lakini hakuna kabila linaloitwa "wapemba". Punguzeni kutajana kwa ukabila.

Msikilize Nyerere, hivi ndivyo tunavyoishi
 
So Ili upate uraia wa kenya au utambulike ka raia kenya ni lazma uwe na kabila???
Kuwa na kabila pekee haitoshi, Hilo kabila lazima liwe limesajiliwa na kutambulika rasmi na serikali ya Kenya, wewe Kama ni mhehe huna nafasi kwasababu sio miongoni mwa makabila ya Kenya[emoji23][emoji23]
 
Ni miongoni mwa kabila linalotumia lugha ya kiswahili kama kilugha
 
So Ili upate uraia wa kenya au utambulike ka raia kenya ni lazma uwe na kabila???
Kama huna kabila utakua umetokea wapi? Maana hakuna mtu ambae anazaliwa kutoka mbinguni na akarushwa hapa ,kila mtu dunia nzima ana kabila hata Yesu ana kabila lake, hatutaki watu watoke nchi nyengine wanakuja tu kuchukua vitambulisho eti Ni wa Kenya abadan, kwanza ukienda kuchukua kitambulisho lazima mzee wa Kijiji awe anakujua au hata kujua mzazi wako au babu yako maana lazima utumie jina la ukoo na Kama wewe umezaliwa na single mother pengine utatumia jina la mjomba au babu mzaa mama na Kama hata babako kwa mfano anatoka singida na mamako Ni wa tabora na unataka kupata kitambulisho ukiwa tabora hautafaulu itakulazimu lazima usafiri hadi singida kwa babako ukapate huko kwa hivyo lazima uwe na kabila na kabila lako liwe miongoni mwa makabila ya Kenya ambayo yanatambuliwa na serikali na wakenya wengine Kama si hivyo utakua mgeni na mgeni yapo Mambo ambayo hawezi akayafanya.
 
Kuwa na kabila pekee haitoshi, Hilo kabila lazima liwe limesajiliwa na kutambulika rasmi na serikali ya Kenya, wewe Kama ni mhehe huna nafasi kwasababu sio miongoni mwa makabila ya Kenya[emoji23][emoji23]
Wapemba Sasa watapata huduma,hata wengine wajifunze angalau udereva maana Kama huna kitambulisho hata huwezi ukajifunza udereva ,na pia wasome maana sidhani Kama wamesoma pengine walio kuwa na akili wakaasi upemba na kujiita majina ya jirani wao Kama wadigo na wadhuruma ili wapate huduma za msingi na kumiliki ardhi.
 
Wapemba Sasa watapata huduma,hata wengine wajifunze angalau udereva maana Kama huna kitambulisho hata huwezi ukajifunza udereva ,na pia wasome maana sidhani Kama wamesoma pengine walio kuwa na akili wakaasi upemba na kujiita majina ya jirani wao Kama wadigo na wadhuruma ili wapate huduma za msingi na kumiliki ardhi.
Kwa jinsi mnavyoendekeza" kabila" kamwe hamuwezi kuepuka "ukabila". Kabila Lina maana gani katika nchi ya watu wenye akili timamu zaidi ya kutambika?.

Hupaswi kuuliza kabila la mtu labda Kama lengo lako ni kufanya utani "jokes", nchi yoyote inayojaribu kutaka kujua idadi ya makabila yake, au kwenda mbali zaidi kutaka kujua idadi ya watu katika Kila kabila, hiyo ni nchi ya hovyo Sana na lazima ukabila utawasumbua Sana.

Katika hili nchi zingine zote lazima mjifunze toka Tanzania, wacheni kujifanya wajuaji, hivi mnavyofanya ndio sababu ukabila unazidi kukomaa Kenya, na hivi tunavyofanya ndio sababu Tanzania ukabila unazidi kupotea, uchaguzi ni wenu, kuendelea kujifanya wajuaji na kukataa kuiga toka kwa nchi iliyofanikiwa kupunguza ukabila, au kuiga Yale mazuri toka kwa jirani yako.
 
Kenya achaneni kutumia kabila Kama ni "official identity" ya raia wenu, huko ndiko kuendekeza ukabila, hivyo vitu ni "social identity".
Kwanini mnapenda kuiponda Kenya wakati huku mashuleni tunajifunza kuhusu makabila yetu na idadi ya makabila Tanzania?
 
Kwanini mnapenda kuiponda Kenya wakati huku mashuleni tunajifunza kuhusu makabila yetu na idadi ya makabila Tanzania?
Unajua mtu akiwa mjinga usibishane nae utakua unampa cheo,yeye anajifanya hatukuzi ukabila ilihali jina lake Ni la kabila lake hajachukua jina la kabila lengine akajiwekea.
 
Back
Top Bottom