Jana usiku, majira ya saa mbili hivi, nilikuwa mahali nikibadilishana mawazo na washkaji, lakini bila kutarajia, nilijikuta macho yangu yakielekea angani ambapo yaliona kitu kilichotafsiriwa kichwani mwangu kuwa cha ajabu.
Kwanza, nilidhani ni msururu wa ndege zinazopita kwenye anga la kimataifa, lakini zikienda wapi na kwanini ziliongozana vile, sikuelewa na sikuwa na majibu. Sikuweza hata kubaini haraka ni nini, na ufahamu wangu ulikuwa challenged.
Nilipowaonesha wenzangu, tukaanza kujadili kama kile tulichokiona kilikuwa kitu cha asili au kilichotengenezwa na binadamu. Sote hatukuwa na majibu ya hakika. Tulikiangalia mpaka kilipotokomea. Hakukuwa na wingu angani ambalo labda lingekificha, ila inaonekana kilitoweka tu mwishoni mwa upeo wa macho yetu.
Hata hivyo, katika kujaribu kupata uelewa zaidi, leo asubuhi nimeonesha video hii iliyoambatanishwa hapa kwa baadhi ya watu wenye udadisi wa masuala ya teknolojia na anga. Ingawa si wataalamu, ni watu tu wanaopenda kujua mambo. Kabla sijamaliza sentensi, wakanieleza kuwa nilichokuwa nimekiona ni satelaiti za Starlink.
Baada ya kuperuzi mtandaoni, picha zilithibitisha kuwa tulichokiona angani jana usiku kilikuwa ni satelati za Starlink. Andiko moja linaeleza kuwa satelaiti hizo zikiwa angani zinaweza kuonekana kama vile ni mstari wa taa angavu. Na hiki ndo hasa nilichokiona.
Jana usiku, majira ya saa mbili hivi, nilikuwa mahali nikibadilishana mawazo na washkaji, lakini bila kutarajia, nilijikuta macho yangu yakielekea angani ambapo yaliona kitu kilichotafsiriwa kichwani mwangu kuwa cha ajabu.
Kwanza, nilidhani ni msururu wa ndege zinazopita kwenye anga la kimataifa, lakini zikienda wapi na kwanini ziliongozana vile, sikuelewa na sikuwa na majibu. Sikuweza hata kubaini haraka ni nini, na ufahamu wangu ulikuwa challenged.
Nilipowaonesha wenzangu, tukaanza kujadili kama kile tulichokiona kilikuwa kitu cha asili au kilichotengenezwa na binadamu. Sote hatukuwa na majibu ya hakika. Tulikiangalia mpaka kilipotokomea. Hakukuwa na wingu angani ambalo labda lingekikificha, ila inaonekana kilitoweka tu mwishoni mwa upeo wa macho yetu.
Hata hivyo, katika kujaribu kupata uelewa zaidi, leo asubuhi nimeonesha video hii iliyoambatanishwa hapa kwa baadhi ya watu wenye udadisi wa masuala ya teknolojia na anga. Ingawa si wataalamu, ni watu tu wanaopenda kujua mambo. Kabla sijamaliza sentensi, wakanieleza kuwa nilichokuwa nimekiona ni satelaiti za Starlink.
Baada ya kuperuzi mtandaoni, picha zilithibitisha kuwa tulichokiona angani jana usiku kilikuwa ni Starlink. Andiko moja linaeleza kuwa satelaiti za Starlink zikiwa angani zinaweza kuonekana kama vile ni mstari wa taa angavu. Na hiki ndo hasa nilichokiona. Je, ulibahatika kuiona?
View attachment 3134684 Hii ni video niliyochukuwa ikionesha satelaiti za Starlink zikipita angani, hapa Dar es Salaam.
View attachment 3134685
Hii ni picha ya kutoka mtandaoni ikionesha satelaiti ya Starlink ikiwa angani.
Musk anatumia uhuru vizuri, na ujinga wetu ndio utakao tuangusha.
Satellite zinaruka outer space kwenye anga ambalo halipo controlled na Tanzania lakini je tukijiuliza vizuri hizo starlink hazina military capability yeyote ? Na mmarekani anashindwa kumblackmail musk na kuweka military capable instrument kwenye starlink?
Kama kila nchi inamiliki space iliyojuu ya ardhi yake na maji kwa umbali wa hadi 100KM, hawa wapuuzi watakosa camera zinazofikia hiyo distance from space. Ni muda sasa wakuangalia regulation zetu kuhusiana na space. Ni vitu vingi vinaruka below 100KM ambavyo Jeshi letu walitakiwa kuvishoot down.