Uchaguzi 2020 SAU yaja na sera za kumuwezesha Mtanzania kula kuku mzima

Uchaguzi 2020 SAU yaja na sera za kumuwezesha Mtanzania kula kuku mzima

Chama cha Sauti ya Umma (SAU) kimesema kina sera ya kuboresha maisha ya Mtanzania kwa kuhakikisha Mtanzania anakula lishe bora, ili mtu aweze kula kuku mzima na kama anakunywa chai basi aweze kuwa na siagi, matunda, mayai na mboga.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Moshi Mjini kupitia SAU amesema wanaonelea jambo la lishe bora kuwa sera nzuri kwa kuwa Watanzania wana afya mbaya kutokana na kula vipande vipande. Amesema unapokula kuku unapaswa kula kuku wote sio vipande.

Aidha kwa sera zake juu ya jimbo analogombea amesema atapanda miti ya matunda jimbo zima ili watu waweze kula matunda bure na wameshapanda matunda katika barabara ya New Street ambayo watu wanaendele kuyatumia matunda hayo.

Amesema zoezi hilo limesaidia kuleta kivuli aidha hadi sasa ameshafanikiwa kushusha jotoridi la Moshi kutoka Nyuzi Joto 40 na sasa zimefikia nyuzi joto 18.

Huyu mgombea wa chama cha sauti ya umma SAU ukitafakari kwa undani Sera yake ni muhimu sana coz lishe ndio iliyotusaidia kwy janga la corona

Ila ukiangalia kwa kufikiria kuku tu utakuwa bado huja muelewa

Hongera kwake
 
Hahahaha hivi hivi vyama vya siasa vingine huwa wanawazaga nn kutoa sela kama hizi ambazo haziwezekani na kutaka kudanganya Watanzania tuuu maana wafate vyama vingine mfano wa sela zao #Hapa kazi tu
 
Kila mwaka wa chaguzi huwa wanarudia haya haya. Hakuna jipya.

Ila naona kama haya ni matumizi mabaya ya demokrasia na kinachoendelea ni kejeli kwa watanzania, msajili aangalie namna ya kupunguza vyama vinavyokosa umakini na kuendekeza mizaha kwenye mambo ya msingi.
 
Back
Top Bottom