SAUT na Vyuo vingine, Shule za kanisa havina malengo ya kweli kumkomboa mtoto wa maskini wa TZ.

matatizo makubwa yapi? Acha kukuza mambo wewe. Mbona hao wengine kati ya hayo majina mia 2 unayoyasema wamepewa ID? Huyo rafiki yako kukosa id anamatatizo yake mwenyewe. Na kama shida yake haitatuliki haraka kuambiwa aandike barua ya special ni shida? Hayo ni mambo madogo ambayo yapo kwenye kila taasisi yenye watu wengi.
 
Nenda kasome Morogoro kwenye kile chuo kilikuwa cha Tanesco Mkapa akawapa Waislamu pale hawalipi ada

Hata hapo MUM watafanya mitihani kwa ID, nao wanadaiwa ada iwapo hawatoilipa kufikia kesho baada ya mshuko wa swalaat-ul-jumaa ndio mwisho wa kulipia, @1700hrs kesho chuo kitatoa ID za kufanyia mitihani kwa wale tu ambao wamekamilisha ADA stahili, hakuna BURE
 
Mtoa maada we mwaka wa ngapi SAUT, binafsi nimesoma SAUT tatizo kuna uelewa mdogo juu ya neno "kumsaidia mtoto wa maskini" hawajasema bure.

Pili hiyo ada yenyewe uliyoisema imepanda mwaka huu, miaka ya nyuma ilikuwa laki 9 na nusu tu, sasa kama wewe Bodi hawajakuletea ada utamlalalmikiaje mwanjonde? Na pia si kweli kwamba wote hawapewi vitambulisho, mtu anatakiwa aende yeye binafsi kwa DVFA, unajieleza kulingana na sababu zako unapewa kitambulisho, SAUT hawataki hata siku moja kuwahukumu watu kwa ujumla wao, unatakiwa ujieleze wewe kama wewe.

Pia hujafanya utafiti wa ada za vyuo nchi hii ukifanya utakubali kuwa SAUT is the cheapest university in Tz, halafu hata kama huna uwezo watu wanakwenda kwa dean wanajieleza na kujaza form kulingana na vigezo vyao unlipiwa ada, na sio mkopo! Ni wapi Tanzania wanafanya mi sijui, ila ninamifano ya watu wamesoma kwa kulipiwa bure SAUT
 


duh, kuna watu mmejaliwa kusema uongo... hapa niko na jamaa yuko kwenye yale majina 215 hadi sasa hajapata ID, wamemfrastuate hata anataka aarishe mtihani. Na wala si yeye pekeyake kuna wanafunzi zaidi ya watano kutoka darasa langu ndio tunawahangaikia hapa wametujibu turudi kesho...yaani Ijumaa.
 
Mleta mada,SAUT ni kati ya vyuo vya private ambavyo bado ada iko chini,kujiunga hapo maana yake unakubaliana nao,uzuri umesema kuna special exam,hivyo mjipange ili mfanye hiyo september.

mkuu ukisema hivyo unakosea sana 7bu waTz tulio wengi ni maskini na kulipa kiasi kama hicho kwa wakati mmoja wakati bodi ya mikopo ndo imechelewesha hela ni jambo baya sana na halitegemewi kufanywa na taasisi za kidini, huku raisi wa nchi aliahidi hakuna mwanafunzi wa chuo atayenyimwa kufanya mtihani kama hajalipa ada. Inamaana hii ahadi ilikuwa ya kisanii? Na SAUT wamekosa njia mbadala kama ya kushikilia matokeo mpaka watakapolipa ada?
 

mkuu unapotosha,SAUT ni moja ya vyuo vinavyomilikiwa na kanisa katoliki vinavyopata ufadhili wa kuosha kutoka nje ya nchi hasa kwenye taasisi za dini za nje,kutoka Canada,UK,USA na Ufaransa kuzitaja kwa uchache ndo mana unaona kuna cozi zinafundishwa pale vyuo vingine havizifundishi mfano Kifaransa,pia ujenzi wa majengo yanajengwa kwa misaada ya nje mfano library ya Mgulunde,Mwanjonde,jengo jipya la utawala na hosteli zinazojengwa kuvitaja kwa uchache,bt SAUT kama chuo ambacho kinamilikiwa na kanisa hakipaswi kukataa kupokea sababu ZOZOTE,hii sio nzuri watu hatulingani uwezo.
 
1. 60% ya bajeti ya SAUT inaenda kwenye mishahara, wakati vyuo vya serikali vina tuition fee kama hizo na mishahara inalipwa na serikali moja kwa moja.

2. Wafadhili wanaweza kuwa wanatoa fedha kwa ajili ya ujenzi, hizo ni za ujenzi na zinatolewa ripoti na haziwezi kuhamishiwa kwenye shughuli yoyote ile tofauti na hiyo. Hakuna mfadhili anayetoa fedha kwa ajili ya uendeshaji.

3. Kwa wanafunzi wenye shida, tangu siku wanaripoti kuna utaratibu wa kuomba wasaidiwe kwa DVCAF baada ya kuthibitisha uhitaji toka kule wanakotoka na wanasaidiwa. Sio kiholela

4. Wewe ndiwe unapotosha, kwani unasema wanakudai zote 1.3m wakati wanadai si zaidi ya 723,000 kwa first semester.

5. Kwenye mambo ya malipo, ukishawapa watu loopholes, utashindwa kabisa kuendesha chuo.

SAUT bado ni chuo chenye gharama nafuu kuliko vyuo vyote Tanzania. Kama ulikuwa na matarajio tofauti, pole umepotoka.
 

Kwahiyokikubali sababu yoyote ya mwanafunzi ambaye hajamaliza au hajalipa ada?
Hii tafsiri yako ya kusaidia maskiinaona ina maana ya pekee kabisa.

Watanzania hawapendi kufuata utaratibu, bila kuwabana wanakuwa na sababu milioi kidogo.
Hata wazazi bila kuwabana hawalipii watoo wao ada....huo ndio ukweli mchungu.

Hayo mambo ya misaada wanayopata uliambiwa inatolewa ili ikulipie ada?
Kama livrary imejengwa kwa msaada kwahiyo wewe usilipe ada?
What kind of thinking is that!
 

Kwa taaria tu chuo kimekataa kupokea sababu yoyote ile mpaka leo tarehe 26,suala la kufanya research ya ada ti}vyuo vingne sio dili sana bt ukweli ni huo SUT ya leo si ya miaka yako,siku hizi hakuna kufanya mtihani bila kulipa ada yote ya muhula,hata ule utaratibu wa kuwaruhusu wanafunzi wadiwa kufanya mtihani kisha wayazuie matokeo yake haupo na kinachoumiza zaid ni faini(pena)ya shilingi laki moja ukichelewa kulipa ada,
 
Mimi niko SAUT pia, nina mkopo na nyumbani kwetu pia hawana uwezo kama ambavyo wewe unavyojieleza. Lakini kwa fedha hiyo hiyo ya mkopo, nimelipa chumba, nimelipa ada yote ya muhula wa kwanza, na ninakula vizuri tu na nitafanya mitihani.

Tatizo la wengi wanaopata mkopo ni Personal Financial Management ni mbaya.

SAUT ninayoijua ni SAUT ya leo, na sioni tatizo na hayo mambo. Suala la ulipaji wa ada wanapaswa kukazia hivyo hivyo, vinginevyo watashindwa kulipa walimu, watashindwa kulipa umeme, na baadaye wewe huyo huyo utarudi hapa na kufurahia hali hiyo.

Uongozi wa SAUT uko sawa kubana watu walipe, wenye matatizo inabaki ni "exceptional cases" ambazo zinapaswa kuwa handled in an exceptional way. Na wengi waliopeleka hizo "exceptional cases" wamefanyiwa exception na kupewa kadi za kufanya mtihani.

Inawezekana kweli una shida, lakini naona mada hii umeileta ukiwa na lako jambo. Kichwa chako cha habari kinaweka wazi kuwa una kampeni ya majitaka dhidi ya SAUT, vyuo na shule za kanisa!

I am proud to be a SAUT student.

Mkuu wewe unasoma kozi gani?
 


LLB3 mkuu na wewe?
 
LLB3 mkuu na wewe?

wanywaji wa pombe na wapenda starehe utawajua tu! Chuo kikiruhusu taratibu unazotaka wewe itafika hatua lecturers watakosa mishahara. Hela ya bodi mnayopewa kwa meals siku hizi kama we unajijua maskini unalipa ada kabisa! Unataka kuniambia una asilimia sifuri ya mkopo? Acheni kuwa na management ovyo ya boom ili mlipe ada. Hata kama boom limechelewa- unashindwa kukopa?
 

wewe Kitima nini?mbona unatokwa povu la hasira kuitetea SAUT?me ada nalipiwana bodi elfu 85 kwa mwaka japo boom napata,so gawa milioni 2 za awamu 4 za boom toa ada milioni 1 laki 2 na 35,toa he;la ya chumba shilingi laki3,stationary na hela ya chakula,kwa mwaka mzma na huna supotin yoyote kutoka kwa mtu yoyote zaidi ya Bodi,lazima ushindwe kulipa ada yote kwa wakati.tumia kichwa kufikiri na c kufugia nywele mkuu


 
nimesoma saut sijawah kukutana na ulichokiandika,nijuavyo mimi hadi kufikia muda wa kufanya mitihani ya semesta ya kwanza unatakiwa uwe ushalipa nusu ya ada au angalau uwe umelipa laki 5,6 au 7,unafanya mtihani bila shida na unapata matokeo.


hakuna palipo andikwa kuwa mpaka umalize ada yote ya mwaka,isipokuwa ada ya nusu muhula ambayo ni laki 7 na 35,kwa watoto wa wakulima wengi tuinashindwa kuilipa kwa wakati since boom ndo linatulisha,kupangisha vyumba na kutusomesha,wanaposema hakuna excuse wanatuonea.
 
Kaka unataka usome bure halafu upate elimu gani? Au walimu wawe wanajitolea tu?

Acha kukurupuka bro tena we unajiita mwanaharakati,jishughurishe kufikiri kama ungekuwa wewe ungefanyaje?


  • 😕
 

Better to remain silent &people think ua crazzy than to speakout and remouve all doubt

  • :shut-mouth:
 

Nawachukia sana watu wanaotoa majibu mepesi kwenye issue nyeti inayogusa maisha ya watu kama hii,sio lazima upost mkuu
 
Mkuu kama unapata boom, usilaumu mtu ni kushindwa kwako kupanga vizuri.

Mimi ni mwanafunzi wa BBA 3, ni mtoto wa mkulima, nina boom, nimepanga chumba Sweya, nimelipa malipo yote yanayohitajika kwa kutumia boom hilo hilo, na bado ninakula vizuri tu. Sidaiwi chochote na nitafanya mtihani vizuri tu kwa amani tele.

Nina wenzangu wengi ninaowafahamu wa hali kama yangu, na wanamudu kila kitu kutokana na boom, na wana amani.

Mkuu, kusoma ni pamoja na kujua namna ya kukabiliana na hali uliyo nayo.

Jiongeze mkuu!!!!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…