Sauti ya Mkandara Lufufu kwenye tangazo la ngumi za Azam Tv.

Sauti ya Mkandara Lufufu kwenye tangazo la ngumi za Azam Tv.

Bando la wiki

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2023
Posts
911
Reaction score
3,017
Ki ukweli sauti ya Mkandara Lufufu ilikuwa na upekee fulani hivi ambao haupati kwa watu wengi.

Ila hivi juzi nimeona tangazo la ngumi kati ya Karim Mandonga na Mada Maugo huku kuna jamaa kaingiza sauti kama ya Lufufu akisimulia namna mabondia hao wanavyotafutana msituni.

Sasa mimi nilikuwa naona ili kumuenzi shujaa Mkandara Lufufu (ni shujaa kwa sababu ndie mwanzilishi wa utaratibu wa kuingiza sauti na kutafsiri movies kutoka kwenye lugha za kigeni kuja kwenye kiswahili)

Huyo kijana apewe kuingiza sauti ya Lufufu kwenye movie itakayokuwa imeigizwa kuzingatia maudhui ya kitanzania hasa ikiwa ya kilugha kama kichaga, kihehe, au kisukuma ikionesha harakati za mashujaa wa kitanzania enzi za ukoloni walivyo jaribu kupambana na ukoloni.

Hapa movie inaweza kumhusu Shujaa kama Mangi Meri, Chief Mkwawa, au Mirambo n.k Movie ikiwa kwa mfano ya chief mkwawa kwa lugha ya kihehe na kibena, kijana huyo (Lufufu) itasikika sauti yake kwa kiswahili huku subtitles zikiwa kwa kiingereza.

Au movies nyingine inaweza kuwa pure action huku sauti ya Lufufu (kijana huyo) ikipita kwa maelezo.
Nadhani kwa kufanya hivi tutakuwa tumemuenzi sana Lufufu huku familia yake nayo ikifurahia matunda ya kazi ya baba yao.
 
Yule Afroo nae huwa ni wa 🔥
Hajamfikia Captain Derick Gasper Mkandala Lufufu

Mpaka sasa sijaona wa kumfunika Mkandala

"Wapeeenzi watazamaji ndugu zanguni wapendwa, Mkandala Lufufu Video Tech iliyopo Mbagala Makuka jijini Daslaam, kwa mara nyingine tena inakuletea picha kali, movie ni The Hard Way the Only Way."

Oyaa huyu mwamba alikuwa anajua aisee
 
Ki ukweli sauti ya Mkandara Lufufu ilikuwa na upekee fulani hivi ambao haupati kwa watu wengi.
Ila hivi juzi nimeona tangazo la ngumi kati ya Karim Mandonga na Mada Maugo huku kuna jamaa kaingiza sauti kama ya Lufufu akisimulia namna mabondia hao wanavyotafutana msituni.
Sasa mimi nilikuwa naona ili kumuenzi shujaa Mkandara Lufufu (ni shujaa kwa sababu ndie mwanzilishi wa utaratibu wa kuingiza sauti na kutafsiri movies kutoka kwenye lugha za kigeni kuja kwenye kiswahili)
Huyo kijana apewe kuingiza sauti ya Lufufu kwenye movie itakayokuwa imeigizwa kuzingatia maudhui ya kitanzania hasa ikiwa ya kilugha kama kichaga, kihehe, au kisukuma ikionesha harakati za mashujaa wa kitanzania enzi za ukoloni walivyo jaribu kupambana na ukoloni.
Hapa movie inaweza kumhusu Shujaa kama Mangi Meri, Chief Mkwawa, au Mirambo n.k Movie ikiwa kwa mfano ya chief mkwawa kwa lugha ya kihehe na kibena, kijana huyo (Lufufu) itasikika sauti yake kwa kiswahili huku subtitles zikiwa kwa kiingereza.
Au movies nyingine inaweza kuwa pure action huku sauti ya Lufufu (kijana huyo) ikipita kwa maelezo.
Nadhani kwa kufanya hivi tutakuwa tumemuenzi sana Lufufu huku familia yake nayo ikifurahia matunda ya kazi ya baba yao.
Vijana wa 2000 hawawez kumjua Rufufu. Rufufu alivuma sana sana mwaka 1990s
 
Dah huyu mwamba kweli pengo lake halitakuja kuzibwa na mtu yeyote, nakumbuka kwenye tafsiri zake za movie alikua anawapachika wahusika majina ya kihaya.

Kuna movie moja nilicheki kitambo Ila nishasahau jina lake hapo movie ikiwa Inanza lufufu mkandala namnukuu akisema. """Wapenzi watazamaji ndugu zangu wapendwa mkandala lufufu video tech iliyopo mbagala dar es salaam inawaletea picha Kali kabisa ambapo jambazi sugu kacheza katika picha hii akiwa anaitwa (KALEKEZI). Duh sema kweli nilicheka sana afu jambazi nilizungu.
 
Bongo movie hawana jeuri ya kutengeneza kitu kikaitwa MOVIE KALI, BONGE MOJA LA MOVIE.

HAWAWEZI
Wapo baadhi wameanza kuonesha uthubutu wa kufanya movies kali mfano tamthilia kama "zahanati ya kijiji" iko vizuri. Lakini pia kuna hii movie ya Bunji naona pia imeanza vizuri.
 
Back
Top Bottom