Sayansi ya Matetemeko ya Ardhi

Sayansi ya Matetemeko ya Ardhi

LEXAPRO3000

Member
Joined
Jul 20, 2013
Posts
61
Reaction score
99
Natanguliza pole kwa wahanga waliofikwa na maafa ya tetemeko la ardhi lilitokea tarehe 10/9/2016 katika mikoa ya Kagera na Mwanza.

Kuna mambo napenda kuuliza kwa wanajamvi wenye uelewa kuhusu matetemeko ya ardhi.

1. Je, kuna mfumo au sayansi inayoweza kugundua viashiria au dalili za kutokea tetemeko la ardhi na kutoa taarifa kabla halijatokea.

2. Je, kwa nchi yetu ya Tanzania kuna kituo cha kuratibu mateemeko ya ardhi
3.Kwa jiografia ya nchi yetu ni maeneno gani yako katika hatari ya kukumbwa na tetemeko la ardhi?
 
Wataalam wa geology wanaweza mujibu vizuri sana hilo swali na hil wanasoma kama module, kama kuna kituo kina deal na miamba bhasi walitakiwa kutoa viashiria maana wao ni wataalam juu ya hilo.

Maeneo yaliyo hatarini sana kushambuliwa na tetemmeko la ardhi ni eneo lote lililopitiwa na bonde la ufa lipo hatarini zaidi japokuwa maeneo yote yanaweza shambuliwa na tetemeko la ardhi.
 
Kwani hamna department ya majanga wakapewa hio task niliona wanafunzi wa hizo kozi au wao wanahusika na kuokoa tu!!?
 
Natanguliza pole kwa wahanga waliofikwa na maafa ya tetemeko la ardhi lilitokea tarehe 10/9/2016 katika mikoa ya Kagera na mwanza. Kuna mambo napenda kuuliza kwa wanajamvi wenye uelewa kuhusu matetemeko ya ardhi,
1.je kuna mfumo au sayansi inayoweza kugundua viashiria au dalili za kutokea tetemeko la ardhi na kutoa taarifa kabla halijatokea
2.Je kwa nchi yetu ya Tanzania kuna kituo cha kuratibu mateemeko ya ardhi
3.Kwa jiografia ya nchi yetu ni maeneno gani yako katika hatari ya kukumbwa na tetemeko la ardhi?

1: Pamoja na ukuaji mkubwa wa Technologia yenye vifaa vya kisasa kabisa hapa Duniani, hakuna kifaa au hakuna tekinolojia ya kuweza Kupredict kwamba tetemeko litatokea sehemu fulani na kwa muda fulani, watu wanachanganya sana na haya mambo ya kupatwa kwa jua au mwezi na mwisho wa siku wanaona ni kama vitu vinavyofanana kumbe sio
Mzunguko wa Jua, Mwezi na Dunia unajulikana na pia speed ya hivyo vyote inajulikana na kutokana na hivyo wanasayansi wanaweza kujua ni lini vitu hivyo (Dunia, Jua na Mwezi) vitakuwa kwenye mstari mmoja na uelekeo wake yaani sehemu gani huo muelekeo ndio utaonekana at maximum, so Dunia, Jua na Mwezi haviwezi kuwa kwenye mstari mmoja kwa dunia nzima bali ni sehemu tu na kwa Mwaka huu sehemu ya Wangingombe ndio hivyo vitu vilikuwa viko kwenye Mstari mmoja,

Kwa kifupi hakuna kipimo cha kupredict Tetemeko la Ardhi

2: sijui hapo unamaanisha nini, kuratibu kwa maana gani?,

3: East African lift Valley inaanzia Bahari ya Sham na kuishia Mozambique, inaanza kama lift valley moja na ikifika maeneo ya kuanzia Ethiopia, linaanza kugawanyika na kwa hapa Tanzania tunapata pande mbili za lift Valley, Eastern na Western na hizo branch zinaenda kuungangana tena kwenye ziwa Nyasa na zinaingia Mozambique kama rift valley moja
Kwa branch ya Eastern Mikoa inayokuwa na Matetemeko ni Arusha, Dodoma, Singida, Morogoro (kidogo) kisha lift valley ianenda kuungana na Western branch, Branch ya Western ina Mikoa ya Kagera, Kigoma, Rukwa, Katavi, Mbeya na kisha inaingia Nyasa

Vitu kama Lake Tanganyika, Lake Nyasa, safu za Milima (Kitonga, Senkeke), Mt. Kilimanjaro, Meru, Oldonyo Lengai, Ngorongoro Crater ni evidence za hizo lift Valley

Ziwa Victoria mpaka sasa halijathibitishwa kuwa lina uhusiano wowote na lift Valley
 
Tetemeko la Ardhi ni janga la asili (natural hazard) ambalo utokeaji wake hauwezi kubashiriwa kwa njia yoyote/chombo chochote licha ya kukua kwa teknolojia duniani.
Kwa Tanzania na duniani kote vipo tu vifaa/teknolojia inayoweza kubaini ukubwa Wa tetemeko katika mazingira husika na si vinginevyo.
Vilevile kwa Tanzania, maeneo ambayo yamepitiwa au yapo jirani na bonde la ufa yapo katika uwezekano mkubwa Wa kutokea kwa tetemeko la ardhi.
Kinachotakiwa ni wananchi kuchukua tahadhari tu.
 
Jamani nimeshangazwa na kufedheheka sana, kwanza sijui kwa uhakika nani ana husika na haya masuala ya Tetemeko katika Taasisi za Umaa kwasababu sijaona au kusikia Taasisi yoyote ikisema lolote la maana.
1. Kwanini Serikali au Taasisi zake hazitoi/kupendekeza njia au hatua za kufuata wakati wa Tetemeko? Kama ni kweli hakuna Teknolojia ya kufahamu kuhusu lini litatokea.
2. Kwanini hakuna Elimu, Taarifa au njia za kuweka bayana maeneo au mikoa na hata nyakati ambazo kwa matarajio au uwezekano wa Tetemeko kutokea, hii inajumuisha pia hata ushauri wa aina ya ujenzi na majengo?
3. Nini wajibu wa Kamati za maafa/majanga kwa Wahanga wa Tetemeko? Serikali ina Plan B ya kuwasaidia Wahanga ukizingatia kuwa tuna Mfuko wa Maafa/Majanga wa Taifa pia kuna Kamati hadi katika ngazi za Vitongoji/Mtaa?
 
ingekuwa kwenye nchi za walio starabika tungesikia waziri kajihuzuru lakini kwetu hapa.....
Umeishia darasa la ngapi ndugu? Ni sawa na kusema Waziri ajiuzulu kwa sababu nchi ina ukame, tufani ama mafuriko! Hayo ni majanga ya asili ambayo mwanadamu hawezi kuyazuia
 
Umeishia darasa la ngapi ndugu? Ni sawa na kusema Waziri ajiuzulu kwa sababu nchi ina ukame, tufani ama mafuriko! Hayo ni majanga ya asili ambayo mwanadamu hawezi kuyazuia
wewe ndo unapaswa kujihoji umeishia darasa la ngapi .... kwa ulimwengu wa sasa kila jambo linaweza kujulikana na likapimwa na kutolewa taarifa kwa wananchi husika wakachukua tahadhari...na si unavyo fikiri wewe
 
wewe ndo unapaswa kujihoji umeishia darasa la ngapi .... kwa ulimwengu wa sasa kila jambo linaweza kujulikana na likapimwa na kutolewa taarifa kwa wananchi husika wakachukua tahadhari...na si unavyo fikiri wewe
Kha, tetemeko la ardhi sio sawa na mvua kubwa zinazoweza mafuriko.
 
Kha, tetemeko la ardhi sio sawa na mvua kubwa zinazoweza mafuriko.
nini usicho kielewa wewe nazungumzia habari ya kutoa elimu ya tahadhari ya jambo... kama wakazi wa bukoba wangekuwa wanafahamu kuwa kunapotokea tetemekoo la ardhi wanapaswa kufanya nini wengi wao wasingekufa .... nenda bukoba kwa sasa baada ya kupata taarifa kuwa huenda likatokea tetemeko lingine wananchi kwa sasa wameanza kulala nje ya nyumba zao hii ni kwanini wanalala nje sababu ni kuwa wamepata elimu ya tahadhari
 
Itabidi watu wajue core,mantle na Crust. Kwenye Crust imeundwa na tectonic plates, zinafanya kuungana kama jigsaw puzzle.Sasa kutokana na ile mantle inayokuwa hot na ipo kama uji inasababisha hizi plates zinakuwa kwenye constant mouvement. Sasa hizi plates juu yake 2 ndo kuna continents ambapo sisi tunaishi. Zinapomove zingine zinaslide hasa kwenye fault ndo hapo zinaposlide ndo zinasababisha matetemeko, ndo tunayaita ma tetemeko ya ardhi, sasa kuleta madhara inatokana na Depth ikiwa siyo kubwa na epicenter yake ikiwa karibu na makazi ya watu ndo tunapata damage
 
Otherwise matetemeko hutokea kila dakika, sema yakatokea sehemu mbali na makazi ya watu, maana tectonic plates zipo katika movement constantly
 
nini usicho kielewa wewe nazungumzia habari ya kutoa elimu ya tahadhari ya jambo... kama wakazi wa bukoba wangekuwa wanafahamu kuwa kunapotokea tetemekoo la ardhi wanapaswa kufanya nini wengi wao wasingekufa .... nenda bukoba kwa sasa baada ya kupata taarifa kuwa huenda likatokea tetemeko lingine wananchi kwa sasa wameanza kulala nje ya nyumba zao hii ni kwanini wanalala nje sababu ni kuwa wamepata elimu ya tahadhari
Sema hivyo,sasa itabidi nchi nzima ipate elimu ya tufanye nini tetemeko linapotokea,sema Tanzania hatukuwa nchi ambayo yaani tupo promatetemeko kama ilivyo Japan ,tuliamini we are safe.Hata Japan Tsunami iliwafundisha ,maana walijenga nuclear power zao zinazoweza himili matetemeko ila wakasahau what if Tsunami ikija,ilipokuja kila mtu anajua kilichotokea Fukushima.Hopefuly sasa Tanzania kila mtu yupo aware,though tetemeko halina taarifa assume linatokea Dar kwenye yale magorofa hapo hata zile safety measures hazitasaidia,na hivi magorofa yetu yamejengwa bila kufuata what if tetemeko likitokea.
 
Back
Top Bottom