Sayansi ya vikwapa

Sayansi ya vikwapa

Tulikuwa na housemaid under 20 hicho kikwapa akioga ndiyo anakitibua harufu kali mno.
Akibeba mtoto anamchafua na hiyo harufu mwili mzima wote wawili wananuka.
Ilibidi atafutiwe shower gel, deodorant na dawa zingine za asili na hospital.
Ikapungua wahuni wakatia mimba.
Ukweli alikuwa mrembo sana wa sura, rangi na umbo.
Mahousemaid wengi wenye umri huo wako hvyo sjui huwa ni kwann,asubuh akiwa anafanya usafi eneo lote la nyumba linanuka
 
Aisee hii ni kweli nusu saa ndogo.
Nimeshuhudia hali mbaya mkikaa ndani mnakosa hewa.
Unahisi una suffocate.
😹😹😹 ukute na mdomo nao unanuka, km upo kwenye daladala utashuka kituo sio chako.

Sipendi watu wanaonuka aisee..
 
Papuchi je?
Chances are, kama unazo genes zinazosababisha kikwapa kutema, basi hata sehemu zingine za mwili zitakuwa zinatoa harufu iliyo zaidi ya kawaida.

Lakini yote hayo can be overcame by good personal hygiene.

Ni suala la kujitambua tu na kuchukua hatua.
 
Ungana nami hapa tujadili suala la vikwapa kwa kutumia sayansi.

Je, wajua kwamba watu wa Asia ya mashariki huwa hawanuki vikwapa?

Eneo la Asia ya mashariki linajumuisha nchi za China, Japan, Korea za kusini na kaskazini, Mongolia, na Taiwan.

Inakadiriwa kuwa asilimia kati ya 80 -95 ya watu wa hizo nchi wana aina ya vinasaba [variant] vinavyotambulika kama ABCC11.

Aina hiyo ya ABCC11 ndo huhusika na kutokuzalisha harufu mbaya ya kikwapa.

Namna moja ya kugundua kama aina ya ABCC11 uliyonayo inazalisha bakteria wa kikwapa au la, angalia aina ya nta ya masikio yako.

Ukiwa na nta iliyo kavu, basi jua wewe una hiyo aina ya ABCC11 ambayo haizalishi kikwapa.

Nta yako ikiwa nyevunyevu, utakuwa ni mtema kikwapa hatari 🤣.

Katika makundi ya watu wa huko Asia mashariki, Wakorea ndo wanaongoza kuwa na hivyo vinasaba visivyozalisha vikwapa.

Kwa msingi huo, Wakorea wengi huwa hawanuki vikwapa.

Kwa wale ambao waliwahi kufika Korea miaka ya nyuma watakuwa wanajua kwamba kupata deodorant madukani, ilikuwa ni shida.

Siku hizi mambo yamebadilika kidogo na deodorants zipo madukani.

Lakini deodorants ziuzwazo kwenye hayo maduka yao si zile zenye nguvu sana, kama vile 72hr na 96hr zipatikanazo kwenye nchi za magharibi.

Licha ya nasaba, harufu ya kikwapa huchagizwa pia na mambo mengine, japo kwa uchache au udogo.

Mambo hayo ni chakula, usafi wa mwili, jinsia, na umri.

Katika uzoefu wangu mimi, nadhani wa Asia ya Kusini ndo wanaongoza kwa vikwapa vikali.

Asia ya Kusini inajumuisha nchi za India, Pakistan, Bangladesh, Sri Lanka, Nepal, Maldives, na pia hata Afghanistan.

Vikwapa vya hao watu ni moto wa kuotea mbali.

Kama umewahi kufanya kazi na Wahindi ambao ndo wametokea kwao huko India, utanielewa.

Vikwapa vyao huwa vinatema balaa. Halafu pia yawezekana hawana utamaduni wa kupaka deodorant.

Ole wako ukutane na Mhindi gym halafu awe anatema kikwapa.

Hamu yoyote ya mazoezi uliyokuwa nayo utaitupa kule.


View: https://youtu.be/qBIc8iKExDU?si=fYGdjph7x6rpj8Zm

20241205_131944.jpg
 
Back
Top Bottom