Second selection yafutwa kwa kidato cha kwanza

Second selection yafutwa kwa kidato cha kwanza

Rais Samia Suluhu anaendelea kuupiga mwingi sekta ya elimu alianzisha mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa 8000 nchi nzima vyenye thamani ya Tsh Bilioni 160 sasa madarasa yamekamilika kwa asilimia 95 na kupelekea wanafunzi wote kuanza masomo kwa pamoja.

Wanafunzi wanaotarajia kujiunga na kidato cha kwanza kuanzia 9 January 2023 ni jumla ya wanafunzi 1,073,941 (wavulana 514,846 na wasichana 559,095)

Lakini pia tangu Rais Samia Suluhu aingie madarakani amefanikiwa kujenga madarasa zaidi ya elfu 20 nchi nzima ndio maana wanafunzi wote wataanza masomo kwa wakati mmoja na kufutwa kwa second selectio pia wazazi wamenufaika na ujenzi huu wa madarasa kwasababu hawakutozwa chochote ukilinganisha na hapo awali.

Rais Samia Suluhu anaendelea kuboresha sekta ya elimu kwa kupita kuboresha mazingira ya kusomea pia kuajiri walimu wa kutosha na kujali maslahi ya walimu .
Tatizo Madarasa yanaongezeka ila ongezeko la walimu halipo
 
Ahaaa ndio lile la walimu wa diploma kufundishe msingi tu?? Maana Kwa uhaba walimu hata sekondari kwenyewe uliwatoa wenye diploma si Ndio uhaba utazidi mara dufu
Sasa mwalimu wa sekondari anakuwaje na Diploma tu, its better wachukue Degree nyinginezo kama Statistics, Physics, Chemistry zifundishe sekondari kuliko Diploma.
Na uhaba wa walimu sio kwamba hawapo ila ni serikali haitaki kuwaajiri
 
Sasa mwalimu wa sekondari anakuwaje na Diploma tu, its better wachukue Degree nyinginezo kama Statistics, Physics, Chemistry zifundishe sekondari kuliko Diploma.
Na uhaba wa walimu sio kwamba hawapo ila ni serikali haitaki kuwaajiri
Kuna walimu wa degree za miaka hii Bora wa diploma za miaka ya nyuma.

Ni sawa na kusema diploma mmoja ni sawa na walimu 5 bachelor.

Take my word muulize MTU yyt mwenye uelewa.

Miaka hii watoto mnakwenda kuchukua vyeti tu
 
Mtoa mada ni kichwa box. Tumia akili yako vyema tumbo lisikupelekeshe.
Usitumie kichwa kama box la kamasi.
 
Rais Samia Suluhu anaendelea kuupiga mwingi sekta ya elimu alianzisha mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa 8000 nchi nzima vyenye thamani ya Tsh Bilioni 160 sasa madarasa yamekamilika kwa asilimia 95 na kupelekea wanafunzi wote kuanza masomo kwa pamoja.

Wanafunzi wanaotarajia kujiunga na kidato cha kwanza kuanzia 9 January 2023 ni jumla ya wanafunzi 1,073,941 (wavulana 514,846 na wasichana 559,095)

Lakini pia tangu Rais Samia Suluhu aingie madarakani amefanikiwa kujenga madarasa zaidi ya elfu 20 nchi nzima ndio maana wanafunzi wote wataanza masomo kwa wakati mmoja na kufutwa kwa second selectio pia wazazi wamenufaika na ujenzi huu wa madarasa kwasababu hawakutozwa chochote ukilinganisha na hapo awali.

Rais Samia Suluhu anaendelea kuboresha sekta ya elimu kwa kupita kuboresha mazingira ya kusomea pia kuajiri walimu wa kutosha na kujali maslahi ya walimu .
Kwakuwa mimi Mtoto wa Shule ni mdau katika Sekta hii WACHA NIPIGE KIMYA!!!
 
Kuna walimu wa degree za miaka hii Bora wa diploma za miaka ya nyuma.

Ni sawa na kusema diploma mmoja ni sawa na walimu 5 bachelor.

Take my word muulize MTU yyt mwenye uelewa.

Miaka hii watoto mnakwenda kuchukua vyeti tu
upo sahihi,tena hao wa degree wanabaki mara shakespear kasema hivi,sijui plato kasema vile na ubishi mwiingi
 
Second Selection imefutwa? Wakati wanafunzi waliofutiwa matokeo ya darasa la saba yaliyotoka awali, wamerudia mtihani Majuzi tu na inatakiwa kuwepo 2nd selection Ili na wao waingie sekondari mwaka huu. Au sijaelewa maana ya 2nd selection?
 
Wale waliorudia mtihani baada ya kufutiwa matokeo ya awali wanapangiwa lini shule mwenye ufahamu?
 
Back
Top Bottom