Security alert kwa Serikali yetu: Tuwe makini sana na Marekani, kuna kitu kinapangwa halafu wajifanye walionya kabla. Je, wanapanga kutu-Libya?

Yaani CCM walishinda uchaguzi wa serikali za mitaa kwa 99% +?
Tunachojua CCM ilipora mchakato wa uchaguzi huo na hivyo kupora ushindi.
Uwongo hautaisaidia CCM bali utawapa mabeberu sababu.
Baada ya kusoma uongo huo wa ushindi nimeachia hapo siwezi endelea kusoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe unaishi wapi uauliza maswali ya kitoto namna hii? Au unaandika kwa sababu bando ni la kwako? Nitakupa machache ya Makonda;
1. Kumuua Ben Saa Nane
2.Kumshambulia na kumjeruhi Lissu
3. Kuzuia CDM wasipewe barua za usimamizi wa uchaguzi mdogo wa Kinondoni kisha kuuawa kwa Akwilina na mashtaka kufunguliwa viongozi wa CDM badala ya Polisi.
4. Kumteka Mohamed Dewji na Roma Mkatoliki
5. Kusumbua wafanya biashara kwa kisingizio cha madawa ya kulevya

Na ya Kabudi:
1. Ushauri kuhusu biashara ya Korosho kwa mfanya biashara wa Kenya
2. Mkataba usio na faida wa Barrick na Tanzania
 
We all die once, unapenda kuish kwanini hutaki kufanya mabadiliko, mbna machifu wako walipigana na wakoloni na kupigania uhuru wao ambao ndio leo tupo hapa. Mbna hili uliongelei

unaona ni sawa Tanzania kuwa hapa ilipo zaid ya miaka 50 ?

We ulishapigana vita? Au ulikuwepo mwanza wakati wa vita vya kagera? Mig 21 tu ikipita chini unaweza kuzimia. Vita isikie kwa mwenzako. Tatizo ushabiki
 
Huyo tangu aitwe kwa Ndugaye siku hizi haeleweki kabisa
In God we Trust
 
Mpaka umeona hadi wewe ukatuletea huku basi ishafika pabaya ni suala la mda tuu
 
We all die once, unapenda kuish kwanini hutaki kufanya mabadiliko, mbna machifu wako walipigana na wakoloni na kupigania uhuru wao ambao ndio leo tupo hapa. Mbna hili uliongelei

unaona ni sawa Tanzania kuwa hapa ilipo zaid ya miaka 50 ?
Nakaa kimya
 
Pascal kuna watu wanaitwa ma lobbiest ambao wapo hapo Capital hill Washington ambao wanajaribu kuichafua serikali ya Tanzania nina uhakika Rais Donald Trump hawezi kukubaliana na hawa wahuni wachache wakisaidiana na wanasiasa wa hapa Tanzania. Kinachotakiwa ni serikali kujipanga na wanadiplomasia wazuri katika wizara ya mambo za nchi ya nje ili kujibu mapigo.
Sera za Rais Donald Trump hazina kitu kinaitwa Regime Change na ndio maana amelaani kitendo cha kuondolewa madarakani hayati Mohamed Ghaddafy pili kwasasa Marekani imejitoa hata vita vya Syria kwa sera hizo hizo za Rais Donald Trump.
Rais Magufuli ni kiongozi pekee katika bara la Africa aliyeonyesha nia ya kuleta maendeleo kwa wananchi wake pili ni kiongozi pekee ambaye anatumia fedha za walipa kodi, mikopo na wahisani kwa maendeleo ya wananchi wake.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usitulishe matango pori. Sisi wote ni Watanzania na tunajuwa anachokifanya Magufuli ni cha kawaida. Marais wote kuanzia Awamu ya 1 hadi ya 4 wamefanya kadri ya uwezo wao kwa nyakati zao. Hakuna cha ajabu anavyofanya huyu ambacho wengine hawakufanya. Kwa hiyo sitaki hiyo miradi anayofanya iwe ni kichaka cha kujificha anapofanya mauaji ya wakosoaji, kukandamiza uhuru wa kujieleza na kukandamiza vyama vya upinzani.
 
Kama unaushahidi hongera. Lkn kama ni haya haya ya akina Kigogo kuwa makini na matumizi ya bando lako. Sbb utapaswa kuthibitisha na mm sitakuwepo huko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama unaushahidi hongera. Lkn kama ni haya haya ya akina Kigogo kuwa makini na matumizi ya bando lako. Sbb utapaswa kuthibitisha na mm sitakuwepo huko.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi unadhani ndiyo umenitisha kwa akili yako finyu!! Hatutaacha kuandika kuhusu vitendo vya ukatili vunavyofanywa na Paul Makonda kwa baraka za Jiwe kwa kuogopa kuuliwa au kubambikiziwa kesi za utakatishaji fedha.

Kama ID ni ya afnhondya ni ya kwako Makonda au mtu wa karibu na Makonda, kaa ukijua kuwa siku zako zinahesabiwa utafikishwa tu ICC.
 
Ni kweli Pascal,ushahidi mwingine huu hapa.


Siku moja niliweka bandiko linalotoa alert kuhusu uwezekano wa Marekani kuifanyia nchi yetu kitu kibaya.Katika hali ya kushangaza bandiko lile Mods walilifuta mara moja.Frankly sikuelewa kwa nini,na nilijiuliza maswali mengi sana.Kwanza kwa nini wafute,kwa kuwa what I was doing was good for my country.Na kwa msingi huo Mods tuwaweka upande gani?Are they with us?Anyway let bygones be bygones.
 
Acha uoga. Nikutishe mm nakujua wewe? Nimekupa fact ya unayoandika uwe na ushahidi wake ndio kanuni ya jinai ilivyo.

Kama unaandika kwa kufuata mkumbo tu. Jihadhari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…