Sehemu kuu 3 za maisha ya ndoa

Sehemu kuu 3 za maisha ya ndoa

Maisha ya ndoa ni wewe mwenyewe unaamu yawe vip! Ishi kama ulivyo, siyo. Mwanzoni mkiwa out unakunywa soda ili umfurahishe mwenzako wakati moyoni unatamani bia. Mimi nina miaka mitano ya ndoa furaha na upendo inazidi kuongezeka.

hongera sana. Na mwenzi wako anafuraha na upendo kama wewe? Huenda ikawa wewe unafuraha kwa sababu umeshika mpini katika hiyo ndoa yako.
 
punguza uongo kidogo hakuna ndoa ya namna hiyo kama ni yako sawa kama mmechokana kila mtu anaweza kuendelea na maisha yake na sio kuombeana vifo

Endless, hujawahi kusikia mtu kamuua mke/mume wake? Hawa ndio huwa wanaombea wenzi wao wafe, wakiona maombi hayakubali huwa wanafanya wenyewe. Pia kumbuka ndoa za kikristo hazina u-turn sasa mtaachana vipi?
 
hallow! hallow!!! kuna ukweli!!! unajua watu wengi siku hizi wanaoa kwa mkumbo! unaweza muoa dada ati kwa mavazi tu kibaya zaidi yale ya uchi uchi!! so ukianza kupata uzoefu ktkt ndoa unagundua ulikosea na dada anakueleza ulimuoa akivaa hivyo . kinadada wengi hushindwa kutofautisha kabla ya ndoa na ndani ndoa!!! haiwezekani ukiwa ndani ya ndoa ubehave km ulivyokuwa hujaolewa ni tatizo!! maisha ya chuoni ni tofauti na maisha ya mtaani jamani!! ajabu sikuhizi kwa tatizo la miundombinu vyuoni wanachuo wengi wanakaa outcompus so kwa dada zetu hali ni mbaya sana wengi wanaolewa na kufanyiwa mambo mabaya kwakuwa wanakuwa wameolewa bila kujijua.wanapomaliza vyuo waingiapo mtaani watu huwakimbilia kuoa bila kuagalia background, unaoa mtu anaekushinda ujanaja hususan wa kingono ni hatari lazima matatizo yawepo. anyway maadili hayawezi kuwepo nyumbani wala kazini km miundombinu ya vyuo vyetu hatajengwa!! msomi hawezilala kwenye banda la kuku maisha yake yote ya chuo halafu ukategemea awe na maadili safi ni upuuzi!! km unabisha njoo uone CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AGOSTINO - MWANZA
 
Maisha ya ndoa ni wewe mwenyewe unaamu yawe vip! Ishi kama ulivyo, siyo. Mwanzoni mkiwa out unakunywa soda ili umfurahishe mwenzako wakati moyoni unatamani bia. Mimi nina miaka mitano ya ndoa furaha na upendo inazidi kuongezeka.

Wewe una miaka mi 5 tu unaanza kutamba. Mie nina mwaka wa 20 sasa. Ndiyo kwaaaaaanza kichinachina kimeanza. Nasubiri kienyeji.

Aliyosema yote ni ukweli mtupu na chanzo cha yote ni wanawake.
 
mkuu umenena kweli kweli tupu tatizo wengi humu ni wanafiki hawapendi kupewa ukweli, ndoa nyingi nowdays ni yeboyebo!
 
Wewe una miaka mi 5 tu unaanza kutamba. Mie nina mwaka wa 20 sasa. Ndiyo kwaaaaaanza kichinachina kimeanza. Nasubiri kienyeji.

Aliyosema yote ni ukweli mtupu na chanzo cha yote ni wanawake.

G'mboto umenichekesha sana, hapo ilipo siyo mbali sana na Kizungu. Jitahidi uirudishe kwenye mstari. Kienyeji noma!
 
Ungejua ndoa ni kama gurudumu? vicious cycle huanza vizuri kama ulivyotaja hatimaye mambo yanaharibika lakini baadaye yanatengemaa kuliko kabla hapo ndiyo wanandoa wanapofaidi ndoa kuliko maelezo lakini haikomi itajirudia tena....huu ndiyo upepo unaovuma halafu unatulia siyo wa mkwe.re anaoudai umevuma kumbe hautaisha mpaka anguko la serikali yake
 
kila sehemu kwenye hayo maisha ya ndoa kwa utafiti wako hudumu kwa muda gani? miezi? miaka?
maana me nna miaka 9 bado niko kidhungu.
 
kila sehemu kwenye hayo maisha ya ndoa kwa utafiti wako hudumu kwa muda gani? miezi? miaka?
maana me nna miaka 9 bado niko kidhungu.

hongera sana. Hakuna muda maalumu, mnaweza kuishi Kizungu maisha yenu yote. Muombeni sana Mwenyezi Mungu.
 
Pamoja na kwamba hakuna binadamu aliyekamilika, uchaguzi mbaya wa umuoe/uolewe na nani hupelekea ndoa ngumu hadi kufikia stage ya kuombeana kifo.

Yale mapenzi moto moto ya mwanzo wa uchumba yasikufanye ukawa kipofu na kushindwa kugundua/kuona tabia halisi za mchumba wako. Yale makosa uliyoyagundua, usiyarahisishe ukaona yataisha tu mkishaoana. Kuweni waangalifu wakati wa kipindi cha uchaguzi wa mchumba.
 
Bra-joe

Usizungumzie ndoa wakati haujakaa kwenye ndoa hata kwa muda wa miezi mitatu.

kubali au kataa. Umekwishawahi kuzungumzia habari za kifo/vifo. Je, umewahi kufa hata dakika 1? Upo ktk sehemu gani? Kichinachina au...?
 
Back
Top Bottom