Sekeseke kati ya Polisi na Wanafamilia laibuka katika harakati la kufukua mwili wa marehemu kupimwa DNA

Sekeseke kati ya Polisi na Wanafamilia laibuka katika harakati la kufukua mwili wa marehemu kupimwa DNA

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610

Mwili unaogombaniwa na familia mbili ambao ulizikwa katika kitongoji cha Dungi, Kijiji cha Kibosho Kindi, Wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, umefukuliwa leo kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya vina saba (DNA).

Mwili huo unaodaiwa kuwa wa Richard Shoo, (31)aliyefariki Juni 16,2024 na kuzikwa Juni 25, mwaka huu, nyumbani kwao Dungi, umefukuliwa kwa ajili ya uchunguzi na vipimo vya vinasaba (DNA) baada ya familia ya Jackson Joseph (29) kuibuka na kudai kuwa mwili huo uliozikwa sio wa marehemu Shoo na kwamba ni wa kijana wao Jackson.

Polisi walilazimika kuomba kutumiwa kibali hicho kwa simu ambacho walidai walikiacha ofisini, ambapo hata hivyo familia ilikataa na kudai wanahitaji kukiona hali ambayo ilifanya kuahirishwa kwa zoezi hilo.

Leo Septemba 4,2024, familia zote mbili, zilifika mahakamani na amri kutolewa kaburi likafukuliwe ili mwili huo utolewe na kupimwa DNA, kujiridhisha ni mwili wa nani.

Baada ya amri hiyo, saa 9:20, Askari polisi sita wakiongozwa na mkuu wa upelekezi Wilaya ya Moshi, wakiambatana na Madaktari wawili na familia ya Jackson Joseph akiwemo mama yake mzazi, walifika nyumbani kwa Shoo kwa ajili ya kufukua kaburi hilo, ambapo pia kuliibuka vurugu za baadhi ya wananchi na familia kuonyesha hawajaridhishwa na kinachotaka kuendelea.

PIA SOMA

- Polisi wafeli kufukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi baada ya Familia kudai kutoshirikishwa
 
Nafikiri kuna makosa katika Mchakato wa ufukuaji wa maiti hiyo. Familia za pande zote mbili zingekutanishwa pamoja na zoezi hilo lingefanyika chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Mahakama ukiwashirikisha wadau wote kabisa wanaohusika, Yaani wanafamilia wa pande zote mbili zinazokinzana, Jeshi la Polisi, Madaktari wa Afya ya binadamu, Ustawi wa Jamii (endapo kama ni muhimu), n.k, n.k.
 
Nasubiri taarifa ya ndugu kugombana kumuuguza ndugu yako , kila siku kugombania maiti tu .
 
Back
Top Bottom