Sekondari zisizo za amali zaingia mkenge kufundisha mtaala mpya

Sekondari zisizo za amali zaingia mkenge kufundisha mtaala mpya

Usishangae mkuu,
Nilipotia mada nilikuwa sahihi kwamba sekondari kadhaa zisizo za amali zimeshaingia mkenge.
Huyo jamaa unayemshangaa ni mmojawapo waliouvaa mkenge.

Kibaha wameingia mkenge huo sekondari nyingi tu na hakuna wa kuwaamsha.
Ndiyo maana nimeshangaa. Sisi wengine ni business as usual.
 
Unachosema ni kweli, na siye huku mkuu wetu na mtaaluma walieleza hivyo kwenye kikao; tuanze kutumia mtaala na mihitasari mipya(syllabi), bahati nzuri tukawepo watu wenye ufuatiliaji na uelewa wa protokali za serikali, tukawaeleza mabadiliko ya syllabus huja na waraka wenye kuonyesha mpango wa utekelezaji.

Baada ya kujadiliana na kuwekana sawa baadae ilibidi mkuu aulize kwa Afisa elimu ambaye alieleza vyema kuwa mtaala mpya na mihitasari yote mipya iliyo tolewa na utekelezaji wake ni kwa shule chache teule. Zingine ziendelee na utaratibu wa zamani hadi waraka utakapotolewa.

Nikupongeze mtoa mada kwa kutanabahisha hili, ni kweli kuna watu wakisikia tu Jambo limeongelewa bungeni au kwenye vyombo vya habari, hukurupuka na kuanza utekelezaji bila ya waraka au miongozo ya utekelezaji wa Jambo husika na hivyo kuleta mikanganyiko.
 
Safari ya Elimu yetu bado inakipindi kigumu kufikia malengo sawa na Dunia inavyotaka.
 
WTF is amali?? Kwani neno “ufundi” lina shida gani?
Zanzibarization of Tanzania. Amali ni neno linalotumika Zanzibar kumaanisha ufundi. Mafunzo ya amali = mafunzo ya ufundi = vocational training.
 
Unachosema ni kweli, na siye huku mkuu wetu na mtaaluma walieleza hivyo kwenye kikao; tuanze kutumia mtaala na mihitasari mipya(syllabi), bahati nzuri tukawepo watu wenye ufuatiliaji na uelewa wa protokali za serikali, tukawaeleza mabadiliko ya syllabus huja na waraka wenye kuonyesha mpango wa utekelezaji.

Baada ya kujadiliana na kuwekana sawa baadae ilibidi mkuu aulize kwa Afisa elimu ambaye alieleza vyema kuwa mtaala mpya na mihitasari yote mipya iliyo tolewa na utekelezaji wake ni kwa shule chache teule. Zingine ziendelee na utaratibu wa zamani hadi waraka utakapotolewa.

Nikupongeze mtoa mada kwa kutanabahisha hili, ni kweli kuna watu wakisikia tu Jambo limeongelewa bungeni au kwenye vyombo vya habari, hukurupuka na kuanza utekelezaji bila ya waraka au miongozo ya utekelezaji wa Jambo husika na hivyo kuleta mikanganyiko.
Ni kweli. Hutakiwi kukldanganywa na watendaji wa halmashauri ya Kibaha.
 
Ungerahisisha sana kwa kuelezea Maana ya Amali/kama ina kirefu chake pia..
Inavyofanya kazi n.k..

Hilo tuu, kuhusu kujichanganya hilo sio shida kwa Tz.
Kitu unachotakiwa ujue wa Tz walicho serious nacho ni Majungu na Unafiki..

NB. Vidada vingi vya Jf ni vijizi na vishirikina.
Halafu vikekomaa na vinapenda pesaaaa.
 
Neno 'amali' ungejaribu kuliweka hata kwa kiingereza,tujue.
amali ni neno la wazanzibari linalovuka bahari kwa kasi kimatumizi kuja bara , huku sisi tunatumia maneno 'ufundi stadi' badala ya neno hilo amali

mathalan, veta ni vyuo vya ufundi stadi ila kwa zenji wanaita vyuo vya amali
 
Zanzibarization of Tanzania. Amali ni neno linalotumika Zanzibar kumaanisha ufundi. Mafunzo ya amali = mafunzo ya ufundi = vocational training.
IMG-20240129-WA0000.jpg
Wamezingatia mazingira
 

Attachments

  • IMG-20240129-WA0000.jpg
    IMG-20240129-WA0000.jpg
    66.7 KB · Views: 5
  • IMG-20240129-WA0000.jpg
    IMG-20240129-WA0000.jpg
    66.7 KB · Views: 9
  • IMG-20240129-WA0001.jpg
    IMG-20240129-WA0001.jpg
    63 KB · Views: 5
kwani mtaala mpya lazima shule iwe na ufundi? Mtaala mpya hata masomo ya sayansi na arts bila ufundi Kuna mtaala wake mpya
 
Hatimaye Commissionerwa Elimu ametuma taarua ya kuzionya secondary zilizoingia mkenge tena akatishia kuzifutia registration iwapo zitaendelea kufundisha mkenge ziliouingia.
 
Ndugu wadau,

Wote tunajua kwamba mtaala mpya umeanza mwaka huu 2024 kama ilivyoelezwa mara nyingi na wakuu wa wizara ya Elimu na hadi Waziri mwenyewe.

Kadiri ya maelezo ni kwamba shule za sekondari zitakazoanza na mtaala mpya hasa kwa form one ni zile chache tu zenye mkondo wa amali.

Shule hizi chache ambazo orodha yake tumeiona wote ndizo pekee zitakazoanza na mtaala huo mwaka huu.

Jambo la ajabu ni kwamba zipo sekondari ambazo hazimo katika orodha ya shule za amali lakini eti nazo zimeanza mtaala mpya.

Binafsi sikuamini lakini katika kuulizia wenzangu nimegundua ni kweli kwamba zipo shule zimeshafanya kosa la kuanza kufundishia mtaala mpya wakati siyo shule za amali.

Ndugu wadau, hili ni jambo very serious. Hii maana yake shule hiyo walimu wote na uongozi wote umeingia mkenge kwa kufundisha masomo yasiyotakiwa kufundishwa.

Kwa mfano, shule hiyo inatakiwa ifundishe somo la Civics kwa formo one lakini kumbe kimakosa wanafundisha somo la Historia ya Tanzania la mtaala mpya.

Kwa sababu hii ni hatari na shule hizi zinaweza kuchelewa sana kugundua ni bora tujadili humu na ikibidi tuziorodheshe na kwa kupitia Jamii Forum shule hizo zijirekebishe mapema au wizara ilijue hili iziiingile mapema kabal ya hasara kubwa kutokea.

Kuna tetesi kwamba watenaji wa Halmashauri ya Kibaha wamekosea na wamezipotosha baadhi ya sekondari kufuata mtaala mpya
kwa form one kimakosa.

Hii maana yake shule hizo za Kibaha sasa hazifundishi somo la Civics amacho ni kosa kubwa na kwa kweli ni scandal.
Amali ni nini na hizo shule ni zipi?

Kinyume na hapo hii ni chai kama chai zingine.
 
Back
Top Bottom