ibanezafrica
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,261
- 6,553
Niliongea kauli hii mapema leo kijiweni nikabezwa na kutupiwa maneno ya ukali, huku Watanzania wenzangu wakijigamba kuwa Senegal ni moto wa kuotea mbali bila hata ya Mane kuwapo.
Wakati wa mchezo wa Iran na Uingereza nikarudia tena kauli yangu na nikawatahadharisha kuwa mpira Duniani umegawanyika katika makundi matano ki uwezo;
1)Mpira wa Ulaya
2)Mpira wa America ya Kusini
3)Mpira wa Asia
4)Mpira wa Waarabu
5)Mpira wa Afrika
Ni vigumu au si rahisi sana kutoboa nyie wa kundi la chini kumshinda aliyeko kundi la juu yako, labda kwa yale makundi mawili ya juu lakini kwa yaliyobaki kiukweli bado kuna kazi kubwa ya kufanya.
Wenzetu walitutangulia mapema katika uwekezaji na pia walisaidiwa sana na hali zao za ki uchumi, lakini tujipe moyo tufurahie michuano hii ya Quatar 2022, lakini kusema nchi moja wapo ya Afrika kufika hata nusu fainali ni ndoto.
Afrika tuwekeze kwenye mchezo wa kandanda tukianzia na kuwajenga watoto wakiwa wadogo kwenye utamaduni mzima wa kandanda, tulete wakufunzi toka nchi tofauti zilizopiga hatua waje kufanya mafunzo ya muda mrefu tuzalishe vizazi na vizazi vyw wachezaji bora.
Kikubwa Mungu ametujaalia vipaji vya ukweli Waafrika, ni sisi tu kuviendeleza. Tuache rushwa na kupunguza siasa, vita vya wenyewe kwa wenyewe n.k, siku moja tutashinda.
Mungu ibariki Afrika.
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Wakati wa mchezo wa Iran na Uingereza nikarudia tena kauli yangu na nikawatahadharisha kuwa mpira Duniani umegawanyika katika makundi matano ki uwezo;
1)Mpira wa Ulaya
2)Mpira wa America ya Kusini
3)Mpira wa Asia
4)Mpira wa Waarabu
5)Mpira wa Afrika
Ni vigumu au si rahisi sana kutoboa nyie wa kundi la chini kumshinda aliyeko kundi la juu yako, labda kwa yale makundi mawili ya juu lakini kwa yaliyobaki kiukweli bado kuna kazi kubwa ya kufanya.
Wenzetu walitutangulia mapema katika uwekezaji na pia walisaidiwa sana na hali zao za ki uchumi, lakini tujipe moyo tufurahie michuano hii ya Quatar 2022, lakini kusema nchi moja wapo ya Afrika kufika hata nusu fainali ni ndoto.
Afrika tuwekeze kwenye mchezo wa kandanda tukianzia na kuwajenga watoto wakiwa wadogo kwenye utamaduni mzima wa kandanda, tulete wakufunzi toka nchi tofauti zilizopiga hatua waje kufanya mafunzo ya muda mrefu tuzalishe vizazi na vizazi vyw wachezaji bora.
Kikubwa Mungu ametujaalia vipaji vya ukweli Waafrika, ni sisi tu kuviendeleza. Tuache rushwa na kupunguza siasa, vita vya wenyewe kwa wenyewe n.k, siku moja tutashinda.
Mungu ibariki Afrika.
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app