Senegal wafalme wa Afrika, watwaa AFCON mbele ya Misri

Senegal wafalme wa Afrika, watwaa AFCON mbele ya Misri

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
1644215664536.png

#TeamSenegal imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) baada ya kuifunga #TeamMisri kwa penati 4-2 katika mchezo wa fainali ulichezwa kwenye Uwanja wa Olembe jijini Yaounde, Cameroon.

Timu hizo zilimaliza dakika 120 za mchezo huo kwa suluhu ya 0-0, hivyo kwa matokeo hayo ya penati #TeamSenegal imetwaa ubingwa huo kwa mara ya kwanza baada ya kucheza jumla ya fainali tatu za AFCON.

Mchezo huo ulikuwa wa ushindani mkali lakini #TeamSenegal ndiyo ambao walitawala muda mwingi.

Fainali hiyo iliwakutanisha mastaa wa Liverpool, Mohamed Salah na Sadio Mane ambao Mane alishindwa kufunga bao la mapema kwa #TeamSenegal baada ya kukosa penati katika kipindi cha kwanza.

#TeamMisri walikuwa wakiwania taji lao la nane baada ya kuwa wametwaa mara saba (1957, 19591, 1986, 1998, 2006, 2008 na 2010), wakati #TeamSenega waliingia fainali mara mbili (2002 na 2019) na kuishia kuwa washindi wa pili kabla ya ubingwa huo wa kwanza kwao.
 
Hongera Senegal, kumbe mikwaju ilifuatia, mm dk90 zilipoisha nikauchapa, nikajua dk 30 na kadi yellow zilivyotamalaki NI balaa. Gabaski zilimpita penalty?
 
Congratulations 👏🎉 to the Lions of Teranga.
 
Rais wa Senegal Bw. Macky Sall ametangaza leo kuwa ni siku ya mapumziko ili kusherekea ushindi wa The Lions of Teranga.
 
Back
Top Bottom