Sensa 2022: Kwanini Samia hakutangazia Taifa kupitia vyombo vya habari ili kuokoa mapesa yaliyoteketea?

Sensa 2022: Kwanini Samia hakutangazia Taifa kupitia vyombo vya habari ili kuokoa mapesa yaliyoteketea?

voicer

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2020
Posts
5,545
Reaction score
11,935
Ilikuwa rahisi zaidi Rais angetutangazia idadi yetu, kwa kulihutubia taifa, na Dunia nzima kupitia vyombo vya habari.Na tungeelewa bila kuharibu mapesa ya walipa kodi.

Badala Kutumia Mamilioni kama sio mabilioni, eti kisa Sherehe ya kutangaza Matokeo ya Sensa,Ni ubadhirifu mkubwa kwa pesa za Watanzania.

Ni kwa utajiri gani ilionao nchi hii hadi kufikia kuwa inafanya Sherehe zisizo na tija kama hizi,kila mwezi hapa nchini?

Hivi hao wafadhili wanaotoa hizo fedha na kuifadhili miradi hii,huwa wanafurahia sherehe kama hizi?

Hivi tunafurahia kipi baada ya kujua idadi yetu nchi nzima?

Tulipaswa kufanya sherehe kama hizo endapo tungekuwa walau tumefanikiwa kuzifuta mojawapo ya kero kubwa za kitaifa kama vile "Umaskini",:Ujinga","Njaa" na "Maradhi".

Lakini tunaposherehekea kuwajua watanzania wanaoteseka bila hata kuwa na Uhakika wa mlo wao!

Huku tukishindwa kupata suluhisho la utatuzi wa matatizo lukuki yanayoliandama taifa!

Huu unakuwa ni ubadhirifu mwingine tena mbele ya rais wa nchi mwenyewe akishuhudia!

Serikali inayotumia mabilioni ya pesa kutuhesabu raia,ambao hata milo miwili ni tatizo!

Serikali inayotumia mabilioni kwa gharama za kututajia idadi ya watanzania,mpaka na helkopta zinarushwa!

Serikali ya matabaka Mawili moja la Walamba "Asali" na Walamba "Shubiri"

Serikali ya matabaka ya "Walala Hai" na
"Walala Hoi"

Serikali ya matabaka Mawili ya "Wapanda Bodaboda" na "Wapanda V8"

Serikali ya matabaka mawili ya "Royal Tour" na "Roho Tua"

Halafu anatokea Mtu asie na "SHAKA" na kutuambia tumuunge mkono "Queen Safari"

Mambo haya yakiendelea kuachwa yalivyo.

Alamsikhi!

WhatsApp-Image-2021-12-09-at-2.02.06-PM.jpg
 
Naunga hoja, msg ya mama kunikaribisha KWENYE uzinduzi niliona, ila ata ingetosha kunijulisha idadi yetu tuko wangapi, naunga mkono sherehe hii ubadhilifu wa pesa za umma, ila yana mwisho.
 
AKILI NDOGO HIYO
HOJA NI MATUMIZI YA KODI ZA MASIKINI kwa Mambo yasiyo na TIJA Kama RAIS ALITAMKA KUWA TUPO MILIONI 61 KULIKUWA NA UMUHIMU GANI WA HELKOPTA KUTANGAZA KUWA TIPO MIL 61?
Kutangaja hili ilikua ni kwepesi mno, hapakua na sababu ya sherehe, angeweza ata kutangazia ikulu.
 
Hiyo haihusiani na pale inapokuja suala la pesa za walipa kodi wa nchi hii.

Gatumpangii masuala yanayomhusu yeye na familia yake.

Lakini sio kwenye matumizi mabaya ya pesa zetu.
Ila Magufuli alipotumia pesa zetu kwa kununulia wanasiasa uliona sawa?
Mbona hukung'aka kama leo
 
AKILI NDOGO HIYO
HOJA NI MATUMIZI YA KODI ZA MASIKINI kwa Mambo yasiyo na TIJA Kama RAIS ALITAMKA KUWA TUPO MILIONI 61 KULIKUWA NA UMUHIMU GANI WA HELKOPTA KUTANGAZA KUWA TIPO MIL 61?
Yaani nchi hii kuna mambo yanafikirisha sana!
 
Ila Magufuli alipotumia pesa zetu kwa kununulia wanasiasa uliona sawa?
Mbona hukung'aka kama leo
Wewe endelea kuteseka na mzimu wa Magufuli mpaka siku ukiokota cheti halali.

Tunaongelea yaliyopo wewe unawaza walioko akhera!

Shame on all of your brainwashed mind!

Hao wanasiasa ulikuwepo wewe labda wakati wakinunuliwa.

Mimi huwa siongelei jambo la kufikirika,naongelea vitu live,kwa sababu pia mimi niko "Live"

Wewe endelea na mambo ya ukewenza,ningejua ulipo ningekuzawadia na "Dera" ili upigie umbeya vizuri,
Sawa!
 
Na nnateseka kwa alichontenda Mshenzi yule? Kunilaza miaka 6 bila kupandishwa daraja!

Natamani kama arudi tumnange weeee kisha ndo life tena Shetani la hatari sana lile

Wewe endelea kuteseka na mzimu wa Magufuli mpaka siku ukiokota cheti halali.

Tunaongelea yaliyopo wewe unawaza walioko akhera...
 
Hiyo haihusiani na pale inapokuja suala la pesa za walipa kodi wa nchi hii.

Gatumpangii masuala yanayomhusu yeye na familia yake.

Lakini sio kwenye matumizi mabaya ya pesa zetu.
Ulitegemea majibu gani toka Kwa wanaofaidi matumizi ya Tozo?
 
Na nnateseka kwa alichontenda Mshenzi yule? Kunilaza miaka 6 bila kupandishwa daraja!
Natamani kama arudi tumnange weeee kisha ndo life tena Shetani la hatari sana lile
Kwa sasa ndio unateseka zaidi huku yeye akiwa mapumzikoni.

Leo unashinda njaa huku ukiendeleza msongo wa mawazo milele.

Kama unamtamani meza sumu ili umfuate mkamalizane,hakuna aliyekuzuia mbwa koko wewe!
 
Back
Top Bottom