Sensa ilipoanza niliulizwa nyumba ina choo cha kuvuta au cha shimo, leo wamekuja kuona kama nyumba ipo na ni ya aina gani?!

Sensa ilipoanza niliulizwa nyumba ina choo cha kuvuta au cha shimo, leo wamekuja kuona kama nyumba ipo na ni ya aina gani?!

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Sensa ilipoanza nilisema walioandaa sensa hawajawahi kushiriki sensa, hii ilitokana na aina ya maswali yakiwemo ya uchuro, yaani umewahi kufiwa humu ndani.

Leo nimeulizwa namba ya mita ya umeme, nategemea watarudi tena kuuliza namba ya mita ya maji. Kingine ni je, unategemea kuifanyia matengenezo nyumba.

Ni nini faida ya swali hili kama si kuchoshana tu, hivi kuna nyumba isiyofanyiwa matengenezo! Kwa ujumla maswali yaliyoulizwa leo tayari yako kwenye sensa halisi ya mwanzo, kama nilijibu nyumba yangu ina choo cha shimo basi hiyo nyumba ipo kweli japo leo hawakuuliza aina ya choo.
 
hili zoezi wamefeli sana. wanawake ukiwaachia kila kitu wanaweza kukulaza njaa aisee. hivi kweli hii ishu wangeshikilia wanaume kama ilivyo kuwa zamani, tungeishia hadi leo hii mimi sijahesabiwa,kweli kweli? yaani kweli?
 
Hapo kinachotafutwa ni kupanua wigo wa tozo, zitaongezwa tozo kutakuwa hadi tozo ya tozo. Hadi kufika 2025 tutakuwa tuko taabani sana. CCM ni adui mkubwa wa Watanganyika.
 
Kama umewaambia ukweli, basi jiandae kulipa tozo ya jengo ya elfu 60 kila mwezi! Maana hakuna namna.

Kinachofanywa na serikali ya ccm kwa sasa hakina tofauti na uharamia/uporaji. Yaani wewe uhangaike kutafuta juani, halafu wenyewe wanakuja kula wakiwa kivulini.
 
Mwingereza alikuwa na huruma kwani aliweka utaratibu wa kutoa msamaha kwa asiyejiweza.
 
Sensa ilipoanza nilisema walioandaa sensa hawajawahi kushiriki sensa, hii ilitokana na aina ya maswali yakiwemo ya uchuro, yaani umewahi kufiwa humu ndani.

Leo nimeulizwa namba ya mita ya umeme, nategemea watarudi tena kuuliza namba ya mita ya maji. Kingine ni je, unategemea kuifanyia matengenezo nyumba.

Ni nini faida ya swali hili kama si kuchoshana tu, hivi kuna nyumba isiyofanyiwa matengenezo! Kwa ujumla maswali yaliyoulizwa leo tayari yako kwenye sensa halisi ya mwanzo, kama nilijibu nyumba yangu ina choo cha shimo basi hiyo nyumba ipo kweli japo leo hawakuuliza aina ya choo.
Ni kusumbua wananchi bure na ujinga wao
 
Tatizo maswali mengi wamecopy na kupaste , kiuhalisia maswali mengi hayaaksi uhalisia wa watanzania ....!! Hata kazi zilizopo kwenye kishikwambi ni tofaut na za watanzania wengi
 
Back
Top Bottom