SoC02 Sensa kwa sasa haina umuhimu wala faida kubwa kwa maendeleo ya tanzania zitumike njia mpya kupata idadi ya raia kupunguza gharama

SoC02 Sensa kwa sasa haina umuhimu wala faida kubwa kwa maendeleo ya tanzania zitumike njia mpya kupata idadi ya raia kupunguza gharama

Stories of Change - 2022 Competition

mushi0763

Member
Joined
Jul 26, 2022
Posts
29
Reaction score
17
Tanzania ni miongoni mwa taifa linaloyoshiriki katika mchakato wa kupata idadi ya raia wake kwa mfumo wa sensa. Sensa ya watu na makazi ni zoezi la kitaifa linalofanyika kila baada ya miaka 10 ambapo sensa ya mwisho kufanyika nchini kabla ya mwaka huu 2022 ilikua sensa ya mwaka 2012 na kufikisha jumla ya sensa sita kufanyika nchini baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964. Sensa nyingine zilifanyika mwaka 1967, 1978, 1988, na mwaka 2002. Serikali huitaji idadi ya raia wake kwaajili ya maswala mbalimbali ya kitaifa kwani takwimu hizo huelezwa hutumika katika upangaji wa maendeleo na faida nyingine nyingi.

Mwaka huu 2022 serikali imetumia kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 400. Kiasi hiki cha fedha ni kikubwa sanaa kulinganisha na faida itakayotokana na kujua idadi ya raia kwani zipo sehemu nyingi ambazo pesa izi zingeweza kutumika na kuleta chachu ya maendeleo pasipo kuadhiriwa na kutojua idadi kamili ya raia. Mfano idadi ya wanachuo wasio na mikopo elimu ya juu inafahamika imetumika vipi kuwapatia ufumbuzi wa kuwapatia mikopo ikiwa serikali haina fedha za kutosha kuwapatia mikopo wote, ni wazi sio kila takwimu ni muhimu kwenye maendeleo kama hakuna mipango au ukwasi toshelevu.

Naamini zipo njia nyingi na nyepesi za kupata makadirio sahihi ya idadi ya raia wa Tanzania kwani hata kwa kuratibu tuu vizuri idadi ya uzazi na vifo unaweza pata ongezeko la raia kwa mwaka husika kwani tunayo idadai ya raia tuliyoipata pitia sensa za awali. Ni kuchukua idadi ya waliozaliwa au kuhamia na kutoa idadi ya waliofariki au kuhama na kupata idadi ya ongezeko au punguzo la raia na njia nyingine nyingi kama kweli serikali itaweka utaratibu sahihi wa kutaka kupata idadi kamili ya raia wake pasipo kufanya sensa ya watu na makazi.

Njia nyingine ambayo serikali
ingeweza kupata idadi ya raia wake pasipo sensa ni kupitia mchakato wa utambulisho wa uraia uliofanyika nchi nzima. Kila Mtanzania mwenye miaka 18 alijitokeza na kutoa taarifa zake muhimu kwa makarani wa NIDA kwanu utaratibu ungewekwa vizuri kwa kutumia gharama zile zile wangeweza kuboresha namna ya ufanyaji wa zoezi lile likasaidia pia kupata idadi ya raia na makazi kwa kuokoa gharama ambazo zinatumika kwenye sensa.

Njia nyingine ambayo serikali ingeweza kupata idadi ya raia wake pasipo kutumia gharama kubwa na za ziada ni kupitia zoezi la uandikishaji wa posti kodi na majina ya mitaa kwani waliajiriwa watu na kuzunguka nchi nzima kila nyumba na mtaa kutoa namba za nyumba na majina ya mitaa ilishindikana vipi kupata pia idadi ya watu wa sehemu izo na idadi ya makazi kama kila nyumba na mtaa ulifikiwa na idadi ya makazi zilifahamika pitia zoezi hilo. Hapa serikali pia ingiweza kuua ndege wawili kwa jiwe moja na kuokoa pesa nyingi.

Vilevile waatalamu wangeweza kutumia makadirio tuu kujua ongezeko la watu na makazi na kuokoa fedha hizo na kuja kufanya sensa hata baada ya mika 20 kwani makadirio hayo yanaweza yasipishane sana na uhalisia utakaopatikana kwenye sensa huku wakijikita kwenye kutatua matatizo ya raia ambayo hayaathiriwi na kutokujua idadi ya raia.

Kabla ya serikali kutumia sensa kama sehemu ya kupata idadi ya raia naona walipaswa kutumia idara ya takwimu ya taifa kupata taarifa muhimu za watanzania wenye uhitaji au sehemu muhimu serikali ipeleke nguvu za fedha na miradi ya maendeleo. Mfano idadi ya wahitimu wanaomaliza vyuo naamini serikali inayo na ikitaka inaipata pasipo sensa kwanini pesa hizi zinazotumika kwenye sensa wasipewe mikopo ya riba nafuu vijana hawa au kuandaliwa mipango itakayo wawezesha kiuchumi.

Malengo ya serikali katika ufanyaji wa sensa hii ndo imenifanya kuwaza na kuona hakuna faida kubwa ya mfumo huu wa sensa pamoja na kuigharimu serikali gharama kubwa ya raslimali fedha, watu na muda kwani haijawahi kubainishwa wazi ni mipango ipi ya maendeleo iliyokwamishwa kwa serikali kutojua idadi kamili ya raia wake ila ipo miradi mingi iliyoshindikana kwa kukosa fedha na mingine ikishindikana kwa kukosa tuu ubunifu. Mfano kujua idadi ya vijana nchi nzima wasio kua na ajira au wasio na elimu inasaidia vipi kuwasaidia kama pesa iliyotengwa kwajili ya vijana haijawahi kutosha ata idadi ndogo ya waombaji wa mikopo husika.

Pamoja na serikali kua na idadi ya raia kupitia sensa mbalimbali bado pamekua na changamoto ya kutimiza mahitaji ya raia hao kutokana na idadi ya raia. Mfano idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa darasa la kwanza, kidato cha kwanza na sita inafahamika ila serikali imeshindwa kutimiza kiwango cha fedha kwaajili ya ujenzi wa miondombinu ya shule kama madarasa na madawati na hata uwiano kati ya waalimu na wanafunzi haikakisi viwango vinavyopaswa, sasa sensa itaweza saidia kwenye hili wakati lipo wazi, na hapo ndo nawazwa kwanini pesa zote za sensa zisingetumika katika elimu, changamoto hii pia ipo kwenye idara na wizara nyingi kwani hata kwenye afya linafanana na mfano huo wa elimu, naona ni wakati wa serikali kutatua kwanza changamoto ambazo zinaonekana kwa macho kabla ya kutafuta takwimu na idadi ya watu.

Bado kama taifa tunapambana na maadui watatu ujinga, maradhi na umasikini ambapo bado tunaweza kukabiliana na maadui hawa pasipo kujua idadi ya raia kwani bado hatujawahi pata ziada ya fedha au bajeti ikarudi serikalini kwa kutosheleza idadi ya watu hivyo sio busara kupeleka pesa kwenye kutafuta idadi ya raia ambao shida zao zipo wazi na unaweza zitatua pasipo kujua idadi yao. Mfano ni Mbunge yupi alishawahi kuja na kero mpya au shida mpya inayowakabili wananchi mbali ya zile tuzilizozizoea kama ubovu, achakavu au ukosefu wa miondombinu, shida katika elimu au afya na nyingine nyingi ambazo nyingi zinaweza tatuliwa pasipo sensa ya watu na makazi.

Idadi ya wakulima, viwanda, mito, maziwa na sehemu muhimu za vyanzo vya maji yanayoweza kutumika katika kilimo inafahamika, sehemu zenye rutuba na maeneo makubwa ya kilimo Tanzania zinajulikana, idadi na aina ya mazao ya chakula na biashara yanafahamika na hata takwimu za mavuno ya nafaka na mazao yote zipo ila changamoto kubwa ni masoko ya uhakika na bei yenye tija ndo kilio cha wakulima wengi pamoja na ukosefu wa chanzo cha uhakika cha maji kweli na hili tunahitaji sensa kuyatatua? Hapana ni nia ya dhati na mikakati ya muda mfupi na mrefu na fedha yanaweza kuamaliza haya na hapa ndo idadi kubwa ya Watanzania wanategemea sekta hii ilikua pia ni busara pesa zilizotengwa kwa sensa zingeingizwa huku na kutumia akili nyingine ya kupata makadirio ya idadi ya watu kwani pesa iliyotumika kwa sensa mwaka huu unaweza kopesha wakulima 40,000 kila mmoja ukampa mtaji wa shilingi za kitanzania 10,000,000 binafsi naona ingekua na msaada mkubwa katika kuwaondoa vijana wengi na wananchi katika kujikwamua kiuchumi kuliko faida inayopatikana kwenye sensa.

Bado naamini maendeleo yanaweza patikana hata pasipo kupitia michakato mikubwa ya kisayansi kama sensa inayogharimu fedha nyingi huku ukiwa bado una safari ndefu ya kutatua kero za za awali ambazo pamoja na kua na idadi ndogo ya raia katika takwimu bado hapakua na utoshelevu wa kifedha. Kabla ya Raisi wa nchi wapo wasaidizi wengi sana wanaoweza kuakisi hali halisi ya sehemu wanazoishi kiuchumi pasipo kuathiri fedha za ziada na wakawa na makadirio halisi ya idadi ya wahitaji.Ukiwauliza watendaji wa mitaa ni nyumba ngapi hazina vyoo salama na maji watakupa idadi kamili, ukimuuliza Daktari mkuu wa wilaya akupe idadi ya vizazi hai na vifo kwa mwaka fulani anaweza kukupatia na kutumika katika maendeleo pasipo sensa, hivyo hivyo katika idara mbalimbali kwani ata afisa ardhi na makazi anajua ametoa vibali vingapi vya ujenzi ni kuweka na kusimamia utaratibu utakao wezesha kupata takwimu sahihi pasipo gharama mpya.

Hitimisho;
Ukweli zipo baadhi ya faida za sensa katika taifa changa kama Tanzania ila ni ndogo kulinganisha na gharama zinazotumika katika zoezi hili kwani hakuna uhaba mkubwa wa takwimu mbalimbali zinazoweza kutumika katika maendeleo ambazo zinakosekana kwa kutumia vyanzo vingine vya kupata takwimu kwani unaweza kutafuta idadi ya raia sehemu ndogo tuu ambayo unaelekeza huduma yako unayohitaji kupata idadi kamili ya raia na kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambazo ungetumia kuhesabu maeneo ambayo hutayafikia kihuduma kwa muda husika huku ukiwa na makadirio ya idadi ya nchi nzima kama njia tajwa huko juu za kupata idadi ya raia hazitutumika.(Andiko langu halijalenga kukosoa sensa yetu ila emelenga kutoa mawazo mbadala katika hili kwani sensa ni kwaajili ya maendeleo na ni muhimu ndio maana sikutoa chapisho langu mapema kipindi cha sensa ilivyokua ikifanyika)
 
Upvote 5
Tanzania ni miongoni mwa taifa linaloyoshiriki katika mchakato wa kupata idadi ya raia wake kwa mfumo wa sensa. Sensa ya watu na makazi ni zoezi la kitaifa linalofanyika kila baada ya miaka 10 ambapo sensa ya mwisho kufanyika nchini kabla ya mwaka huu 2022 ilikua sensa ya mwaka 2012 na kufikisha jumla ya sensa sita kufanyika nchini baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964. Sensa nyingine zilifanyika mwaka 1967, 1978, 1988, na mwaka 2002. Serikali huitaji idadi ya raia wake kwaajili ya maswala mbalimbali ya kitaifa kwani takwimu hizo huelezwa hutumika katika upangaji wa maendeleo na faida nyingine nyingi.

Mwaka huu 2022 serikali imetumia kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 400. Kiasi hiki cha fedha ni kikubwa sanaa kulinganisha na faida itakayotokana na kujua idadi ya raia kwani zipo sehemu nyingi ambazo pesa izi zingeweza kutumika na kuleta chachu ya maendeleo pasipo kuadhiriwa na kutojua idadi kamili ya raia. Mfano idadi ya wanachuo wasio na mikopo elimu ya juu inafahamika imetumika vipi kuwapatia ufumbuzi wa kuwapatia mikopo ikiwa serikali haina fedha za kutosha kuwapatia mikopo wote, ni wazi sio kila takwimu ni muhimu kwenye maendeleo kama hakuna mipango au ukwasi toshelevu.

Naamini zipo njia nyingi na nyepesi za kupata makadirio sahihi ya idadi ya raia wa Tanzania kwani hata kwa kuratibu tuu vizuri idadi ya uzazi na vifo unaweza pata ongezeko la raia kwa mwaka husika kwani tunayo idadai ya raia tuliyoipata pitia sensa za awali. Ni kuchukua idadi ya waliozaliwa au kuhamia na kutoa idadi ya waliofariki au kuhama na kupata idadi ya ongezeko au punguzo la raia na njia nyingine nyingi kama kweli serikali itaweka utaratibu sahihi wa kutaka kupata idadi kamili ya raia wake pasipo kufanya sensa ya watu na makazi.

Njia nyingine ambayo serikali
ingeweza kupata idadi ya raia wake pasipo sensa ni kupitia mchakato wa utambulisho wa uraia uliofanyika nchi nzima. Kila Mtanzania mwenye miaka 18 alijitokeza na kutoa taarifa zake muhimu kwa makarani wa NIDA kwanu utaratibu ungewekwa vizuri kwa kutumia gharama zile zile wangeweza kuboresha namna ya ufanyaji wa zoezi lile likasaidia pia kupata idadi ya raia na makazi kwa kuokoa gharama ambazo zinatumika kwenye sensa.

Njia nyingine ambayo serikali ingeweza kupata idadi ya raia wake pasipo kutumia gharama kubwa na za ziada ni kupitia zoezi la uandikishaji wa posti kodi na majina ya mitaa kwani waliajiriwa watu na kuzunguka nchi nzima kila nyumba na mtaa kutoa namba za nyumba na majina ya mitaa ilishindikana vipi kupata pia idadi ya watu wa sehemu izo na idadi ya makazi kama kila nyumba na mtaa ulifikiwa na idadi ya makazi zilifahamika pitia zoezi hilo. Hapa serikali pia ingiweza kuua ndege wawili kwa jiwe moja na kuokoa pesa nyingi.

Vilevile waatalamu wangeweza kutumia makadirio tuu kujua ongezeko la watu na makazi na kuokoa fedha hizo na kuja kufanya sensa hata baada ya mika 20 kwani makadirio hayo yanaweza yasipishane sana na uhalisia utakaopatikana kwenye sensa huku wakijikita kwenye kutatua matatizo ya raia ambayo hayaathiriwi na kutokujua idadi ya raia.

Kabla ya serikali kutumia sensa kama sehemu ya kupata idadi ya raia naona walipaswa kutumia idara ya takwimu ya taifa kupata taarifa muhimu za watanzania wenye uhitaji au sehemu muhimu serikali ipeleke nguvu za fedha na miradi ya maendeleo. Mfano idadi ya wahitimu wanaomaliza vyuo naamini serikali inayo na ikitaka inaipata pasipo sensa kwanini pesa hizi zinazotumika kwenye sensa wasipewe mikopo ya riba nafuu vijana hawa au kuandaliwa mipango itakayo wawezesha kiuchumi.

Malengo ya serikali katika ufanyaji wa sensa hii ndo imenifanya kuwaza na kuona hakuna faida kubwa ya mfumo huu wa sensa pamoja na kuigharimu serikali gharama kubwa ya raslimali fedha, watu na muda kwani haijawahi kubainishwa wazi ni mipango ipi ya maendeleo iliyokwamishwa kwa serikali kutojua idadi kamili ya raia wake ila ipo miradi mingi iliyoshindikana kwa kukosa fedha na mingine ikishindikana kwa kukosa tuu ubunifu. Mfano kujua idadi ya vijana nchi nzima wasio kua na ajira au wasio na elimu inasaidia vipi kuwasaidia kama pesa iliyotengwa kwajili ya vijana haijawahi kutosha ata idadi ndogo ya waombaji wa mikopo husika.

Pamoja na serikali kua na idadi ya raia kupitia sensa mbalimbali bado pamekua na changamoto ya kutimiza mahitaji ya raia hao kutokana na idadi ya raia. Mfano idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa darasa la kwanza, kidato cha kwanza na sita inafahamika ila serikali imeshindwa kutimiza kiwango cha fedha kwaajili ya ujenzi wa miondombinu ya shule kama madarasa na madawati na hata uwiano kati ya waalimu na wanafunzi haikakisi viwango vinavyopaswa, sasa sensa itaweza saidia kwenye hili wakati lipo wazi, na hapo ndo nawazwa kwanini pesa zote za sensa zisingetumika katika elimu, changamoto hii pia ipo kwenye idara na wizara nyingi kwani hata kwenye afya linafanana na mfano huo wa elimu, naona ni wakati wa serikali kutatua kwanza changamoto ambazo zinaonekana kwa macho kabla ya kutafuta takwimu na idadi ya watu.

Bado kama taifa tunapambana na maadui watatu ujinga, maradhi na umasikini ambapo bado tunaweza kukabiliana na maadui hawa pasipo kujua idadi ya raia kwani bado hatujawahi pata ziada ya fedha au bajeti ikarudi serikalini kwa kutosheleza idadi ya watu hivyo sio busara kupeleka pesa kwenye kutafuta idadi ya raia ambao shida zao zipo wazi na unaweza zitatua pasipo kujua idadi yao. Mfano ni Mbunge yupi alishawahi kuja na kero mpya au shida mpya inayowakabili wananchi mbali ya zile tuzilizozizoea kama ubovu, achakavu au ukosefu wa miondombinu, shida katika elimu au afya na nyingine nyingi ambazo nyingi zinaweza tatuliwa pasipo sensa ya watu na makazi.

Idadi ya wakulima, viwanda, mito, maziwa na sehemu muhimu za vyanzo vya maji yanayoweza kutumika katika kilimo inafahamika, sehemu zenye rutuba na maeneo makubwa ya kilimo Tanzania zinajulikana, idadi na aina ya mazao ya chakula na biashara yanafahamika na hata takwimu za mavuno ya nafaka na mazao yote zipo ila changamoto kubwa ni masoko ya uhakika na bei yenye tija ndo kilio cha wakulima wengi pamoja na ukosefu wa chanzo cha uhakika cha maji kweli na hili tunahitaji sensa kuyatatua? Hapana ni nia ya dhati na mikakati ya muda mfupi na mrefu na fedha yanaweza kuamaliza haya na hapa ndo idadi kubwa ya Watanzania wanategemea sekta hii ilikua pia ni busara pesa zilizotengwa kwa sensa zingeingizwa huku na kutumia akili nyingine ya kupata makadirio ya idadi ya watu kwani pesa iliyotumika kwa sensa mwaka huu unaweza kopesha wakulima 40,000 kila mmoja ukampa mtaji wa shilingi za kitanzania 10,000,000 binafsi naona ingekua na msaada mkubwa katika kuwaondoa vijana wengi na wananchi katika kujikwamua kiuchumi kuliko faida inayopatikana kwenye sensa.

Bado naamini maendeleo yanaweza patikana hata pasipo kupitia michakato mikubwa ya kisayansi kama sensa inayogharimu fedha nyingi huku ukiwa bado una safari ndefu ya kutatua kero za za awali ambazo pamoja na kua na idadi ndogo ya raia katika takwimu bado hapakua na utoshelevu wa kifedha. Kabla ya Raisi wa nchi wapo wasaidizi wengi sana wanaoweza kuakisi hali halisi ya sehemu wanazoishi kiuchumi pasipo kuathiri fedha za ziada na wakawa na makadirio halisi ya idadi ya wahitaji.Ukiwauliza watendaji wa mitaa ni nyumba ngapi hazina vyoo salama na maji watakupa idadi kamili, ukimuuliza Daktari mkuu wa wilaya akupe idadi ya vizazi hai na vifo kwa mwaka fulani anaweza kukupatia na kutumika katika maendeleo pasipo sensa, hivyo hivyo katika idara mbalimbali kwani ata afisa ardhi na makazi anajua ametoa vibali vingapi vya ujenzi ni kuweka na kusimamia utaratibu utakao wezesha kupata takwimu sahihi pasipo gharama mpya.

Hitimisho;
Ukweli zipo baadhi ya faida za sensa katika taifa changa kama Tanzania ila ni ndogo kulinganisha na gharama zinazotumika katika zoezi hili kwani hakuna uhaba mkubwa wa takwimu mbalimbali zinazoweza kutumika katika maendeleo ambazo zinakosekana kwa kutumia vyanzo vingine vya kupata takwimu kwani unaweza kutafuta idadi ya raia sehemu ndogo tuu ambayo unaelekeza huduma yako unayohitaji kupata idadi kamili ya raia na kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambazo ungetumia kuhesabu maeneo ambayo hutayafikia kihuduma kwa muda husika huku ukiwa na makadirio ya idadi ya nchi nzima kama njia tajwa huko juu za kupata idadi ya raia hazitutumika.(Andiko langu halijalenga kukosoa sensa yetu ila emelenga kutoa mawazo mbadala katika hili kwani sensa ni kwaajili ya maendeleo na ni muhimu ndio maana sikutoa chapisho langu mapema kipindi cha sensa ilivyokua ikifanyika)
nilivyokuelewa Mimi ni kwamba shida sio sensa au kwamba sensa haina faida, hapana. Unakosoa mfumo au njia zinazotumika kufanya sensa. Kwamba zinatumia gharama kubwa. Nafikiri hata serikali inafahamu jambo hili. Hapa sasa ni kazi yetu wananchi kwenye akili kuvumbua mifumo inayoweza kusaidia serikali kifanya sensa bila kutumia gharama kubwa kama ilivyokuwa kwa mwaka huu. Ndugu yangu, hakuna mbadala wa sensa. Kitaalamu ni kwamba takwimu za makadilio zina mapungufu kiasi ambacho huwezi kuzitumia kwa maendeleo. Sensa ni muhimu kuliko umuhimu ulioorodhesha hapo juu. Sensa sio idadi ya watu tu pekee. Ni zaidi ya hapo. Maendeleo ambayo unaweza kusema nchi yetu imeyapata hadi sasa ni kwa manufaa yaliyotokana na sensa kwa ujumla wake.
Tafadhali unaweza kusoma na kuchangia au kulipigia kura andiko langu pia SoC 2022 - Acheni kutusimanga sisi wasomi wa Tanzania
Asante
 
nilivyokuelewa Mimi ni kwamba shida sio sensa au kwamba sensa haina faida, hapana. Unakosoa mfumo au njia zinazotumika kufanya sensa. Kwamba zinatumia gharama kubwa. Nafikiri hata serikali inafahamu jambo hili. Hapa sasa ni kazi yetu wananchi kwenye akili kuvumbua mifumo inayoweza kusaidia serikali kifanya sensa bila kutumia gharama kubwa kama ilivyokuwa kwa mwaka huu. Ndugu yangu, hakuna mbadala wa sensa. Kitaalamu ni kwamba takwimu za makadilio zina mapungufu kiasi ambacho huwezi kuzitumia kwa maendeleo. Sensa ni muhimu kuliko umuhimu ulioorodhesha hapo juu. Sensa sio idadi ya watu tu pekee. Ni zaidi ya hapo. Maendeleo ambayo unaweza kusema nchi yetu imeyapata hadi sasa ni kwa manufaa yaliyotokana na sensa kwa ujumla wake.
Tafadhali unaweza kusoma na kuchangia au kulipigia kura andiko langu pia SoC 2022 - Acheni kutusimanga sisi wasomi wa Tanzania
Asante
kama umesoma andiko langu vizuri nimeonyesha njia ambazo ni nafuu na sahihi ambazo serikali inaweza kutumia kupata idada ya raia wake pasipo kutumia gharama kubwa kama hizi za sasa. hoja ya kusema ina faida sawa ila ni ndogo sanaa kwani mpka sasa watatizo ya watanzania yapo wazi na hayahitaji kujua idadi yao, mfano mfumuko wa bei na kutafuta idadi ya raia ina faida kwel, au idadi ya wanafunzi wa elimu ya juu si wanayo mbona hawapewi mikopo wote,
Shukrani kwa mawazo yako pia
 
nilivyokuelewa Mimi ni kwamba shida sio sensa au kwamba sensa haina faida, hapana. Unakosoa mfumo au njia zinazotumika kufanya sensa. Kwamba zinatumia gharama kubwa. Nafikiri hata serikali inafahamu jambo hili. Hapa sasa ni kazi yetu wananchi kwenye akili kuvumbua mifumo inayoweza kusaidia serikali kifanya sensa bila kutumia gharama kubwa kama ilivyokuwa kwa mwaka huu. Ndugu yangu, hakuna mbadala wa sensa. Kitaalamu ni kwamba takwimu za makadilio zina mapungufu kiasi ambacho huwezi kuzitumia kwa maendeleo. Sensa ni muhimu kuliko umuhimu ulioorodhesha hapo juu. Sensa sio idadi ya watu tu pekee. Ni zaidi ya hapo. Maendeleo ambayo unaweza kusema nchi yetu imeyapata hadi sasa ni kwa manufaa yaliyotokana na sensa kwa ujumla wake.
Tafadhali unaweza kusoma na kuchangia au kulipigia kura andiko langu pia SoC 2022 - Acheni kutusimanga sisi wasomi wa Tanzania
Asante
pesa iliyotumika kwa sensa mwaka huu unaweza kopesha wakulima 40,000 kila mmoja ukampa mtaji wa shilingi za kitanzania 10,000,000 binafsi naona ingekua na msaada mkubwa katika kuwaondoa vijana wengi na wananchi katika kujikwamua kiuchumi kuliko faida inayopatikana kwenye sensa.
 
pesa iliyotumika kwa sensa mwaka huu unaweza kopesha wakulima 40,000 kila mmoja ukampa mtaji wa shilingi za kitanzania 10,000,000 binafsi naona ingekua na msaada mkubwa katika kuwaondoa vijana wengi na wananchi katika kujikwamua kiuchumi kuliko faida inayopatikana kwenye sensa.
Bila sensa huwezi hata kujua io idadi ya wakulima, wanalima nini? na hata wanapatikana wapi..? sio rahisi kufanya maendeleo ya aina yoyote bila kuwa na takwimu sahihi..takwimu sahihi ndio msingi wa maendeleo
 
Bila sensa huwezi hata kujua io idadi ya wakulima, wanalima nini? na hata wanapatikana wapi..? sio rahisi kufanya maendeleo ya aina yoyote bila kuwa na takwimu sahihi..takwimu sahihi ndio msingi wa maendeleo
kama utajua idadi ya wakulima afu hakuna pesa au mapango uliyowapangia inasaidia nini? mipango ipi ilikwama kwa kutokujua idadi ya wakulima? bei ya mbolea itapungua kwa kujua tuu idadi ya wakulima wakati idadi ndogo tuu imeshindikana kuwatimizia mahitaji yao
 
kama utajua idadi ya wakulima afu hakuna pesa au mapango uliyowapangia inasaidia nini? mipango ipi ilikwama kwa kutokujua idadi ya wakulima? bei ya mbolea itapungua kwa kujua tuu idadi ya wakulima wakati idadi ndogo tuu imeshindikana kuwatimizia mahitaji yao
hao kidogo waliopata ni matokeo ya sensa...huwezi ukamkooesha mtu usiemjua..sensa hujumuisha takwimu za kidemografia ambazo huiwezesha serikali kujua taarifa za watu wake kwa undani. huwezi kuweka ruzuku ya mbolea kwa wakulima ambao hujui hata wanalima nini. Sensa hujumuisha takwimu za kiuchumi za watu wanaohesabiwa. Kaka ukiwa msomi na ubataka ufanye mambo kisomi wanasema lazina ufanye utafiti..kwa kifupi sensa ndio utafiti Mkuu unaojenga misingi ya utafiti nyingine ndogondogo..

Hata kama utashindwa kuwatimizia watu mahitaji yao ukiwa na takwimu sahihi utajua ni kwa kiasi gani umeshindwa na hivyo kujipanga tena. Duniani, hakuna mbadala wa sensa katka kuleta maendeleo
 
hao kidogo waliopata ni matokeo ya sensa...huwezi ukamkooesha mtu usiemjua..sensa hujumuisha takwimu za kidemografia ambazo huiwezesha serikali kujua taarifa za watu wake kwa undani. huwezi kuweka ruzuku ya mbolea kwa wakulima ambao hujui hata wanalima nini. Sensa hujumuisha takwimu za kiuchumi za watu wanaohesabiwa. Kaka ukiwa msomi na ubataka ufanye mambo kisomi wanasema lazina ufanye utafiti..kwa kifupi sensa ndio utafiti Mkuu unaojenga misingi ya utafiti nyingine ndogondogo..

Hata kama utashindwa kuwatimizia watu mahitaji yao ukiwa na takwimu sahihi utajua ni kwa kiasi gani umeshindwa na hivyo kujipanga tena. Duniani, hakuna mbadala wa sensa katka kuleta maendeleo
yaani wewe unatoka nje ya nlivyozungumza, kwani kuna mtu kasema sensa haina faida kwa nchi nyingine? hapa nimeeleza njia mbadala ya kupata idadai, labda umesoma tuu heading, sasa ukijua una wafugaji 100. afu huna ata mipango wala pesa ya kuwahudumia inasaidia nini, kwani serikali haijui upungufu wa madawati na waalimu, kwahyo kupata idadi kwa kutumia gharama kubwa ndio sahihi?
 
Unadhani kweli kuwa sijasoma? Labda wewe ndio hujui ulichokiandika.. hebu soma tena andiko lako kabla ya kuendelea kujikanganya wewe mwenyewe..
 
yaani wewe unatoka nje ya nlivyozungumza, kwani kuna mtu kasema sensa haina faida kwa nchi nyingine? hapa nimeeleza njia mbadala ya kupata idadai, labda umesoma tuu heading, sasa ukijua una wafugaji 100. afu huna ata mipango wala pesa ya kuwahudumia inasaidia nini, kwani serikali haijui upungufu wa madawati na waalimu, kwahyo kupata idadi kwa kutumia gharama kubwa ndio sahihi
yaani wewe unatoka nje ya nlivyozungumza, kwani kuna mtu kasema sensa haina faida kwa nchi nyingine? hapa nimeeleza njia mbadala ya kupata idadai, labda umesoma tuu heading, sasa ukijua una wafugaji 100. afu huna ata mipango wala pesa ya kuwahudumia inasaidia nini, kwani serikali haijui upungufu wa madawati na waalimu, kwahyo kupata idadi kwa kutumia gharama kubwa ndio sahihi?
Bado naamini maendeleo yanaweza patikana hata pasipo kupitia michakato mikubwa ya kisayansi kama sensa inayogharimu fedha nyingi huku ukiwa bado una safari ndefu ya kutatua kero za za awali ambazo pamoja na kua na idadi ndogo ya raia katika takwimu bado hapakua na utoshelevu wa kifedha
 
kama umesoma andiko langu vizuri nimeonyesha njia ambazo ni nafuu na sahihi ambazo serikali inaweza kutumia kupata idada ya raia wake pasipo kutumia gharama kubwa kama hizi za sasa. hoja ya kusema ina faida sawa ila ni ndogo sanaa kwani mpka sasa watatizo ya watanzania yapo wazi na hayahitaji kujua idadi yao, mfano mfumuko wa bei na kutafuta idadi ya raia ina faida kwel, au idadi ya wanafunzi wa elimu ya juu si wanayo mbona hawapewi mikopo wote,
Shukrani kwa mawazo yako p
Vilevile waatalamu wangeweza kutumia makadirio tuu kujua ongezeko la watu na makazi na kuokoa fedha hizo na kuja kufanya sensa hata baada ya mika 20

Njia za makadilio hazitoi takwimu sahihi..nimeeleza hili katika reply yangu ya kwanza..hakuna mbadala wa sensa
 
unaweza eleza kwa ufupi namna sensa ilivyoweza kugusa maisha yako baada ya serikali kutambua idadi ya raia wake, huduma ipi ilikufukia baada ya kutambua idadi yako na familia ako
 
unaweza eleza kwa ufupi namna sensa ilivyoweza kugusa maisha yako baada ya serikali kutambua idadi ya raia wake, huduma ipi ilikufukia baada ya kutambua idadi yako na familia ako
Bro sensa ni kila kitu yani..huduma za afya unazoziona katika Kata na vijiji zimepangwa kujengwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita. Serikali kwa kujua kuwa ina idadi ya watu wangapi mahali fulani huweka mipango ya kupeleka huduma eneo husika.

Shule za Kata ambazo Nina imani kuwa na wewe umepita huko ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Huduma za miundombinu ya maji na Barbara kupita katika maeneo ya watu ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na sensa zilizopita.

Mipango ya kukopesha wamachinga na fedha za asilimia kumi kwa kila halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita
Utoaji wa elimu bila malipo ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Bajeti za nchi katika miaka yote hupangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita. Huwezi kupanga bajeti kama hujui idadi mahususi ya watu unaotaka kuwahudumia
Ujenzi wa miundombinu ya intaneti na huduma za mawasiliano vijijini ni utekelezaji wa mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Utoaji wa ajira za serikali na kuwawezesha wananchi kuweza kujiajiri ni mipango inayopangwa kutokana na matokeo ya sensa..

Sasa wewe unafikiri kutumia bilioni 400 kila baada ya miaka kumi ni kupoteza pesa bila kujua kuwa hukuna chcochote serikali inaweza kufanya kuwahudumia watu wake bila kuwa na takwimu sahihi za watu na makazi.
Nyongeza ya halo kuna huduma za mama na mtoto, hizi ni matokeo ya mipango iliyopangwa na serikali kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Sensa haitazami idadi ya watu tu Bali hutazama hata idadi ya watu waliofariki na sababu sake iki serikali iweze kutatua changamoto izo.

Isingekuwa sensa hata io intaneti unayoitumia ungeisikia kwa shimesikio.

Sawa kijana??
 
Bro sensa ni kila kitu yani..huduma za afya unazoziona katika Kata na vijiji zimepangwa kujengwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita. Serikali kwa kujua kuwa ina idadi ya watu wangapi mahali fulani huweka mipango ya kupeleka huduma eneo husika.

Shule za Kata ambazo Nina imani kuwa na wewe umepita huko ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Huduma za miundombinu ya maji na Barbara kupita katika maeneo ya watu ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na sensa zilizopita.

Mipango ya kukopesha wamachinga na fedha za asilimia kumi kwa kila halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita
Utoaji wa elimu bila malipo ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Bajeti za nchi katika miaka yote hupangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita. Huwezi kupanga bajeti kama hujui idadi mahususi ya watu unaotaka kuwahudumia
Ujenzi wa miundombinu ya intaneti na huduma za mawasiliano vijijini ni utekelezaji wa mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Utoaji wa ajira za serikali na kuwawezesha wananchi kuweza kujiajiri ni mipango inayopangwa kutokana na matokeo ya sensa..

Sasa wewe unafikiri kutumia bilioni 400 kila baada ya miaka kumi ni kupoteza pesa bila kujua kuwa hukuna chcochote serikali inaweza kufanya kuwahudumia watu wake bila kuwa na takwimu sahihi za watu na makazi.
Nyongeza ya halo kuna huduma za mama na mtoto, hizi ni matokeo ya mipango iliyopangwa na serikali kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Sensa haitazami idadi ya watu tu Bali hutazama hata idadi ya watu waliofariki na sababu sake iki serikali iweze kutatua changamoto izo.

Isingekuwa sensa hata io intaneti unayoitumia ungeisikia kwa shimesikio.

Sawa kijana??
ayo ndo yanayoelezwa kwenye makaratasi, ila ukwel faida ake ndogo sana, na mm nilieleza njia mbadala za kupata idadi ya watu pia, ila ni mtazamo wako na mm nabaki na wangu, siwez tafuta matatizo na njia za kisayansi kutafuta tatizo wakati kwa macho naweza yaona, wali wa kushiba unaonekana kwenye sahani
 
Bro sensa ni kila kitu yani..huduma za afya unazoziona katika Kata na vijiji zimepangwa kujengwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita. Serikali kwa kujua kuwa ina idadi ya watu wangapi mahali fulani huweka mipango ya kupeleka huduma eneo husika.

Shule za Kata ambazo Nina imani kuwa na wewe umepita huko ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Huduma za miundombinu ya maji na Barbara kupita katika maeneo ya watu ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na sensa zilizopita.

Mipango ya kukopesha wamachinga na fedha za asilimia kumi kwa kila halmashauri kwa ajili ya vijana na akina mama ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita
Utoaji wa elimu bila malipo ni matokeo ya mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Bajeti za nchi katika miaka yote hupangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita. Huwezi kupanga bajeti kama hujui idadi mahususi ya watu unaotaka kuwahudumia
Ujenzi wa miundombinu ya intaneti na huduma za mawasiliano vijijini ni utekelezaji wa mipango iliyopangwa kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Utoaji wa ajira za serikali na kuwawezesha wananchi kuweza kujiajiri ni mipango inayopangwa kutokana na matokeo ya sensa..

Sasa wewe unafikiri kutumia bilioni 400 kila baada ya miaka kumi ni kupoteza pesa bila kujua kuwa hukuna chcochote serikali inaweza kufanya kuwahudumia watu wake bila kuwa na takwimu sahihi za watu na makazi.
Nyongeza ya halo kuna huduma za mama na mtoto, hizi ni matokeo ya mipango iliyopangwa na serikali kutokana na matokeo ya sensa zilizopita.

Sensa haitazami idadi ya watu tu Bali hutazama hata idadi ya watu waliofariki na sababu sake iki serikali iweze kutatua changamoto izo.

Isingekuwa sensa hata io intaneti unayoitumia ungeisikia kwa shimesikio.

Sawa kijana??
na siku zote wenye akili zinazo shahibiana inakua rahis kuelewana, wapo watakao elewa nilicholenga kwenye andiko langu na wapo watakao pinga, ila ndo maana ya mjadala, all in all thanks,
 
ayo ndo yanayoelezwa kwenye makaratasi, ila ukwel faida ake ndogo sana, na mm nilieleza njia mbadala za kupata idadi ya watu pia, ila ni mtazamo wako na mm nabaki na wangu, siwez tafuta matatizo na njia za kisayansi kutafuta tatizo wakati kwa macho naweza yaona, wali wa kushiba unaonekana kwenye sahani
Tafuta taarifa sahihi kaka..macho hudanganya. Hayo makaratasi ndio yameandika hata katiba na Sheria. Makaratasi ndio yameandika misaafu mitakatifu. Macho huwa na ukomo wa kuona..
 
Tafuta taarifa sahihi kaka..macho hudanganya. Hayo makaratasi ndio yameandika hata katiba na Sheria. Makaratasi ndio yameandika misaafu mitakatifu. Macho huwa na ukomo wa kuona..
idadi ya wafungwa inafahamika siku zote ni kubwa kuliko uwezo wa magereza zetu, kipi kimefanyika? idadi ya wanaojiandikisha kidato cha kwanza na darasa la kwanza inafahamika, je wamejenga madarasa au hawajui takwimu, mengine yanabaki siasa tuu na ndo maana nmesema sensa haina faida kubwa, means ipo faida ila ndogo snaa na haina faida kubwa kwa mtanzania
 
Back
Top Bottom