Sensa ya watu na makazi: Maswali ambayo hayakupaswa kuwepo kwenye dodoso

Sensa ya watu na makazi: Maswali ambayo hayakupaswa kuwepo kwenye dodoso

Jerlamarel

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2021
Posts
843
Reaction score
2,525
Hii ni sensa ya watu na makazi, lengo kuu la sensa ni kupanga maendeleo ya muda mrefu. Unapoingiza siasa kwenye dodoso utaishia kupata data ambazo ni useless ndani ya mwaka tuu.

Pia kuna data zingine ambazo tayari serikali na vyombo vyake wanazo, sikuona haja ya kuwepo kwenye dodoso, ni kuwachosha makarani tuu na kuifanya kazi ya sensa kuwa ngumu sana na inayoboa kwa anayehojiwa.

Moja ya maswali ambayo ni useless kwenye dodoso la mwaka huu ni kama yafuatayo:

1. Namba ya simu

Kila siku watu wanabadili namba, baada ya mwaka tuu nusu ya data hizi huenda ziwe useless.

2. Mahali unaposhinda
Mahali mtu anaposhinda inasaidia nini kwenye maendeleo ya taifa? Hizi data ndani ya mwaka tuu zitakuwa obsolete maana asilimia kubwa hawatakuwa wanashinda pale pa mwanzo.

3. Kitambulisho na namba ya NIDA
Hizi data tayari zipo NBS. Kuziuliza tena kwenye dodoso ni kuwachosha makarani tuu.

4. Kitambulisho cha ujasiriamali
Huu mradi ulishasitishwa siku nyingi. Unawekwa kwenye dodoso kwa lengo gani wakati toka mwendazake aondoke na wenyewe ukasitishwa na hivi vitambulisho havitambuliki tena?

5. Simu janja na Kompyuta
Hizi data zote ziko pale TCRA, wao ndiyo wanajua exactly namba ya hivi vifaa vilivyopo hewani. Kwa vyovyote vile data watakazopata makarani hazitaendana na za TCRA maana siyo wote watatoa data kamili, kwa maswali yalivyo mengi watu wataamua kufupisha kwa kujibu "HAPANA SINA".

6. Uzazi na vifo

Hizi data zinatumwa kila mwezi kwenye wizara zinazohusika. Kuziuliza tena kwenye dodoso ni kuwachosha makarani tuu.

7. Anuani ya makazi

Hili zoezi limefanyika juzi tuu. Kwa kuwa visimbuzi vinatumia GPS nilitegemea kila kikifika kwenye kaya husika basi automatically kidetect kama nyumba ina anuani ya makazi ama laah.

Ongezeeni mengineyo...
 
Una hoja muanzisha uzi. Hata mimi kuna amswali yalinishangaza miongoni mwa uliyoyataja.

Tatizo la nchi yetu mifumo ya taasisi haipo synced. Ni sawa na kadhia wanayoipata wawekezaji pale TIC the so called one stop centre ya uwekezaji, pale zipo ofisi zote necessary, lakini cha ajabu akitoka pale anasumbuliwa tena.
 
Maneno matupu hayawezi kufanya hoja zangu zikakosa mashiko.. Na wala sijapinga sensa... Na siyo kweli kwamba ni vitu vilivyo nje ya uwezo wangu.
Unaposema data za NIDA teyari zipo NBS..hao NBS watajuaje walio hai na waliokufa kwa usahihi bila kupta takwimu za sensa?

Ikumbukwe ni idadi kubwa ya watu wanaokufa bila kufuata certificate za vifo kutoprocess certificate ya kifo kunaikosesha serikali takwimu sahihi za vifo...

Ukiona familia inafuatilia cheti cha kifo kwa sehemu kubwa huwaga ni kwaajiri ya matumizi ya kisheria kwenye masuala ya mirathi ya Mali za marehemu ila wengi ambao hawanaga shuguli maalumu na hawana mali za kulithiwa huwaga ndugu zao hawasumbuki kufuatilia vyeti vya vifo pale RITA...
 
Una hoja muanzisha uzi.
Hata mimi kuna amswali yalinishangaza miongoni mwa uliyoyataja.
Tatizo la nchi yetu mifumo ya taasisi haipo synced. Ni sawa na kadhia wanayoipata wawekezaji pale TIC the so called one stop centre ya uwekezaji, pale zipo ofisi zote necessary, lakini cha ajabu akitoka pale anasumbuliwa tena.
Ni kweli maeneo mengine Kuna changamoto Sana na usumbufu mwingi Ila kwenye issue ya sensa ni lazima uulizwe kwakuwa hata Kama mifumo itakuwa na taarifa zako bado phyisical verification itahitajika ili kupata usahihi wa taarifa zilizopo kwenye mifumo ya kidigitali.
 
Kwakweli hukuninako ishi Mimi kigoma hapa mjini kunasehemu kunaitwa kwa padri nijirani nakambi yajeshi nilitegemea kuulizwa VP mnatumia barabara gani kufata huduma ndio changamoto kwetu watoto wanasoma kufata shule umbali gani huduma yasoko mnapata wapi unawatoto walisoma diploma au digee wanakazi au hawana kazi ningesifu kwakusema sensa hii imekuja kuboresha maisha lakini unakuta unaulizwa hali yandoa unasikia eti nyumbayako inavyumba vingapi na mengine sikuyapenda kabisa tuwe siriasi tuulizwe changamoto muhimu nchi tuache porojo kerokubwa ni ajira namiundombinu ambayo hayaulizwi ndiomuhimu
 
Nakubaliana na mleta mada kuna haja gani kuuliza kama mtu ana smart au laptop? au kutaka kujustify kuwa watanzania wana maisha ya kati kwa sababu ya kumiliki laptop na simu
Hiyo inapima technology literacy/infrastructure. Hizi data muhimu sana kwenye mambo ya Tehama hasa kwa wawekezaji na serikali inapoandaa sera za ICT
 
Una pasi feni au brenda? Sasa inasaidia nini kwenye takwimu za nchi
Kila swali lipo coded, so ukisema ndio au hapana Ina tally kule so Yale maswali yote ya poverty index yatakua bundled in one dummy variable kutoa picha ya index au ratio ya umaskini kupitia "umiliki" wa vitu kadhaa.

Survey nyingi sana za kuhoji kuhusu umaskini huwa maswali hayo yapo.
 
Kila swali lipo coded, so ukisema ndio au hapana Ina tally kule so Yale maswali yote ya poverty index yatakua bundled in one dummy variable kutoa picha ya index au ratio ya umaskini kupitia "umiliki" wa vitu kadhaa.

Survey nyingi sana za kuhoji kuhusu umaskini huwa maswali hayo yapo.
Acha vingereza vingi wewe brenda linasaidia nini badala ya kuuliza umeathirika vipi na tozo na kupanda kwa mafuta unaulizwa eti unatumia brenda?.Halafu wewe nawe unakuja na vingereza vyako kama Vanesa mdee hapa.
 
Aliniacha Hoi qliponiuliza, jee una pasi ya umeme? Nikamjibu ndio. Jee na ya mkaa? Nikakumbuka ninayo ila sijui kule store imewekwa eneo gani maana mara ya mwisho kuitumia ni wakati wa mgao mkali wa umeme 2009 Rais akiwa Kikwete.

Michosho mitupu!
 
Aliniacha Hoi qliponiuliza, jee una pasi ya umeme? Nikamjibu ndio. Jee na ya mkaa? Nikakumbuka ninayo ila sijui kule stood imewekwa eneo gani maana mara ya mwisho kuitumia ni wakati wa mgao mkali wa umeme 2009 Rais akiwa Kikwete.
Michosho mitupu!
Wanauliza maswali yasiyo na miguu wala kichwa.

Haya maswali hata mwaka 2012 wakati tupo enzi za giza hayakuwepo...
 
Back
Top Bottom