Senzo aliuawa mwaka gani?

Senzo aliuawa mwaka gani?

Kuna Senzo wawili. Mmoja ni Senzo Robert Meyiwa. Huyu alikuwa mcheza mpira na goalkeeper was Orlando Pirates ya Afrika Kusini. Alikuwa pia kipa na kapteni wa timu ya Bafana Bafana. Senzo Meyiwa Aliuawa kwa kupigwa risasi na wezi Oktoba 26, 2014. Alifanyiwa mazishi ya kitaifa.

Mwingine ni Senzo Mthethwa. Huyu ni mwanamuziki wa gospel reggae. Kuna mkanganyiko kama yupo hai au alishafariki. Hata hivyo, nadhani mkanganyiko huu unatokana na kifo cha mchezaji mpira Senzo Robert Meyiwa.

Oktoba mwaka jana Senzo Mthethwa alitarajiwa ku-perform kwenye Sand Music Festival huko Malawi. Ila hasikiki sana na sidhani kama bado anatoa nyimbo mpya kutokana na kupoteza sauti yake baada ya kupata cerebral ya malaria. Labda ndio maana hasikiki. Ila mke wake alishafariki.
Ahsante sana mkuu kwa taarifa hii....

Ambacho nilikuwa sifahamu ni kama alishapona kiasi hiki cha kurejea kwenye muziki....

Nimefarijika sana na kufurahi sana kuone amerejea tena...


Welcome back Senzo...
 
Shukran mkuu,nilishafahamu ukweli kuwa yupo hai na niliangalia documentary moja kuna jamaa aliiweka hapa...

Ahsante sana mkuu...

Ahsante kaka, nilimpenda sana Lucky Dube na kusikiliza nyimbo zake toka nikiwa mdogo, ikaja kuibuka uvumi kwamba jamaa alifanya njama za kumuua Senzo kwa maslahi ya kibiashara. Hii habari ilinichefua sana na kunisikitisha, ilibidi niichimbe sana.

Ukweli kwamba hakuhusika na vile vile hakuwa anatumia kilevi chochote viliniongezea kupenda nyimbo zake na kumheshimu zaidi.

Umeadimika sana kiongozi, au ulikua kwenye kamati ya makinikia?
 
Senzo alikuwa mpiga drums wa luck dube,ukiangalia video nyingi za luck utamwona jamaa akigonga drums vilivyo,ila alifanyiwa njama na dube mpaka kauawa baada ya senzo kuibuka na album zake kadhaa km vile rasta stand up,kikolele na nyinginezo
Acha kudanganya watu Senzo yuko sauzi anajiuguza kijijini kwao huko
 
Ahsante kaka, nilimpenda sana Lucky Dube na kusikiliza nyimbo zake toka nikiwa mdogo, ikaja kuibuka uvumi kwamba jamaa alifanya njama za kumuua Senzo kwa maslahi ya kibiashara. Hii habari ilinichefua sana na kunisikitisha, ilibidi niichimbe sana.

Ukweli kwamba hakuhusika na vile vile hakuwa anatumia kilevi chochote viliniongezea kupenda nyimbo zake na kumheshimu zaidi.

Umeadimika sana kiongozi, au ulikua kwenye kamati ya makinikia?
Mkuu,nadhani tupo wengi tunaompenda sana Dube na nina nyimbo zake nyingi sana mkuu na ni miongoni mwa wanamuziki ninaowaheshimu sana....

Hizi story za kushiriki kifo hewa cha Senzo sikuzipenda na ndiyo kitu kilinifanya nikaanzisha uzi hapa na nashukuru Mungu nilipata majibu maana sikupenda kabisa hizo propaganda....

Senzo ninapenda sana nyimbo zake maana ana falsafa fulani hivi ya kiinjili ambayo inafanana na ya Don Carlos,mmoja kati ya wanamuziki wa reggae ninayemheshimu sana mkuu.....

Nilipopata habari kuwa Senzo alishauawa nilisikitika sana lakini kumbe haikuwa kweli....

Kuna mwingine naye ni "Msauzi" anaitwa Sipho Johnson au "Jambo",huyu naye anaimba roots reggae na sijuwi alipotelea wapi maana ni miaka mingi badhani 20 hivi sijasikia chochote kumhusu na hakuwahi kuwa maarufu sana....

Ana vibao hatari kama "No man kill another man", Sharing,Shine on brighter,This is mine,The world na vingine vingi unaweza kuzicheki mtandaoni,huyu naye ni hazina nyingine iliyozimika bila kueleweka....

Inasikitisha sana maana hakuna taarifa za kuwahusu....


Mkuu nimepotea lakini siyo sana maana nachungulia chungulia kule Intelligance....

Kuna mambo fulani nayafuatilia mkuu na ninatarajia kuandika kitabu nikiyakamilisha kunako majaaliwa...

Tupo pamoja na tuombeane uzima mkuu wangu....
 
Nimefarijika sana kujua Senzo yuko Hai, uzushi wa kwamba Dube alishiriki kumuua ulikua unaniumiza sana, nilikua nawaza binadamu ni wanafki sana, ukisikiliza nyimbo za Dube ni MTU mpenda haki na usawa, sasa ikawa inanivuruga sana!

Na kujua kama Senzo yukohai kumenifanya niamini kua huenda ni kweli waliomua Dube walimuua kimakosa kwa kudhani wanamuua mlengwa wao!
 
Mkuu,nadhani tupo wengi tunaompenda sana Dube na nina nyimbo zake nyingi sana mkuu na ni miongoni mwa wanamuziki ninaowaheshimu sana....

Hizi story za kushiriki kifo hewa cha Senzo sikuzipenda na ndiyo kitu kilinifanya nikaanzisha uzi hapa na nashukuru Mungu nilipata majibu maana sikupenda kabisa hizo propaganda....

Senzo ninapenda sana nyimbo zake maana ana falsafa fulani hivi ya kiinjili ambayo inafanana na ya Don Carlos,mmoja kati ya wanamuziki wa reggae ninayemheshimu sana mkuu.....

Nilipopata habari kuwa Senzo alishauawa nilisikitika sana lakini kumbe haikuwa kweli....

Kuna mwingine naye ni "Msauzi" anaitwa Sipho Johnson au "Jambo",huyu naye anaimba roots reggae na sijuwi alipotelea wapi maana ni miaka mingi badhani 20 hivi sijasikia chochote kumhusu na hakuwahi kuwa maarufu sana....

Ana vibao hatari kama "No man kill another man", Sharing,Shine on brighter,This is mine,The world na vingine vingi unaweza kuzicheki mtandaoni,huyu naye ni hazina nyingine iliyozimika bila kueleweka....

Inasikitisha sana maana hakuna taarifa za kuwahusu....


Mkuu nimepotea lakini siyo sana maana nachungulia chungulia kule Intelligance....

Kuna mambo fulani nayafuatilia mkuu na ninatarajia kuandika kitabu nikiyakamilisha kunako majaaliwa...

Tupo pamoja na tuombeane uzima mkuu wangu....
mkuu nitahitaji kitabu chako pindi kikikamika, we ni legendary wangu hapa Jf.
kupitia wewe nimejifunza,nimejua,nimegundua mambo mengi kuhusu dunia na ulimwengu..
elimu uliyonayo haipatikani darasani...

nilijipa kazi ya kupitia kila komenti yako uliyowaikuchangia hapa Jf, bado sijamaliza zote, ile nimepata kitu hadhimu sana...
nimemjua KRISTO na mpinga Kristo halisi, (sio yule dhehebu langu lilinikaririsha kuwa ndiye mpinga Kristo) kupitia wewe..

Much blessed Bro
 
Back
Top Bottom