Sera Mpya ya Faragha ya WhatsApp: Usalama wa taarifa za watumiaji mashakani?

Sera Mpya ya Faragha ya WhatsApp: Usalama wa taarifa za watumiaji mashakani?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
1_20210113_094949_0000.png

Sera mpya ya faragha ya WhatsApp imesheheni maneno 8,000 ambayo yameandikwa wa lugha ya kisheria (ngumu kueleweka kwa mtu wa kawaida)

Sera imeeleza kuwa taarifa za watumiaji wa WhatsApp zitasambazwa kwa kampuni Mama (Facebook)

Taarifa hizo zitajumuisha eneo alilopo mtumiaji, kiwango cha chaji ya simu, namba ya IMEI, na mtandao anaoutumia

Pia watasambaza taarifa za mtumiaji kuhusu makundi sogozi ya WhatsApp aliyopo, picha yake ya 'Profile'
 
Upvote 0
Watu bana asa wanachekesha, hasa waTanzania. Mtu utaskia anasema hatumii tena whatsapp halafu anatumia fesibuku, instagramu halafu pia utakuta mtu huyo kwenye kufungua akaunti, ile sehemu ya kusoma mashrati na vigezo anaweka Tick kama amekubaliana navyo wakati ata hajasoma.
 
Sera za faragha za WhatsApp zimekuwa zaboreshwa tangu mwaka jana mwezi Julai.

Itakumbukwa WhatsApp walitoa tangazo la kuboresha sera za faragha na hii ya kuongeza kipengele taarifa za mtumiaji wakawekea hapo.

Taarifa hizo za faragha za mtumiaji ambae ana akaunti ya Facebook zaweza kujumuishwa kwa pamoja baina ya mitandao hiyo miwili pale mtumiaji atumiapo mitandao hiyo kwa shughuli za kibiashara.

Hivyo sera za kugawana, kubadilishana au kuchangiana taarifa za watumiaji wa mitandao hiyo kwa nje ya bara la Ulaya ni rahisi zaidi kwani barani Ulaya wana sera ngumu za kuwakinga raia wao wasianikwe taarifa zao za faragha.

Nje ya bara ya Ulaya nchi kadhaa hutumia mwanya huo kutafuta taarifa za faragha za watumiaji ambao hukosa serikali za nchi hizo.

Tukumbuke pia pamoja na taarifa hizo zilizotajwa hapo juu, pia kutatakiwa kutolewe taarifa za kujsajili kwenye WhatsApp, namba ya simu, mabadilishano ya ujumbe au "transactions data", taariza za kutumiana ujumbe wa papo kwa papo au "interaction"na anuani ya protokali ya simu ya mtumiaji au IP address.

Yawezekana kabisa kuwa serikali za nchi hizi ambazo zingine zimepitisha tayari sheria za mitandao na zipo "active" kwa kutumia mamlaka za mawasiliano na kuna vipengele kadhaa ambavyo vyabinya mitandao hii inapotaka kujipenyeza kwa upana wake katika nchi hizo.

Kwa mfano bara la Afrika kama uchumi ukuao au "emerging economy", uwingi wa watumiaji wa hii mitandao khasa vijana inakuwa ni sumaku ya kuvutia uwekezaji wa mitandao hii kibiashara.

Lakini katika kuingia kuwekeza barani humo na mabara mengine kama Asia masuala kama kuwekeana kamba za masharti "String attached" yanakuwa yalazimishwa kwa nguvu zote.
 
Najiuliza nni lini JF itaamua kuwa na mfumo wa platforms kama hizo za hao wahuni wa marekani.

We are much safe here kuliko nje ya hapa
 
Situmiiii tenah WhatsApp
Wengi hawajaelewa kitafutwacho na hawa jamaa.

Ila kama una WhatsApp lakini huna Facebook huna haja ya kuachana na WhatsApp.

Mtumiji wa WhatsApp akiwa ataka kuhifadhi data zake kule Facebook yaani anatumia mitandao yote miwili, huyu ndio ataathirika na sera hiyo mpya.

Issue ni business na watu wengi watumia Facebook kwa business lakini kwa private watumia WhatsApp.

Hivyo Facebook wataka kuisaidia WhatsApp lakini kwa kuwa karibu nao zaidi katika mifumo yao na pia kutumi amwanya huo kupenyesha bidhaa zake za kibiashara.

Nafikiri ushanifahamu hapo.
 
Najiuliza nni lini JF itaamua kuwa na mfumo wa platforms kama hizo za hao wahuni wa marekani.

We are much safe here kuliko nje ya hapa
Zipo Telegram na Signal ambazo hadi sasa ndio watu wengi wahamia huko.
 
Hivi na wewe uko huko buza umepangisha chumba kimoja umejifuni shuka na simu yako hata taarifa zako zkiwekwa facebook una hasara gani?
 
Hivi na wewe uko huko buza umepangisha chumba kimoja umejifuni shuka na simu yako hata taarifa zako zkiwekwa facebook una hasara gani?
Kama waishi Buza na una "impact" kwa WhasApp/Facebook kibiashara basi weye wafaa ati sio?
 
Tutatumia Telegram na Wechat sasa
Telegram haikufai yapigwa ban kila sehemu.

Telegram na Signal zatumiwa pia na makundi ya kigaidi na yale kama yaloingia Capitol.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom