Sera ya Kuwawezesha watanzania weusi ni ya lazima?

Sera ya Kuwawezesha watanzania weusi ni ya lazima?

Sikimbii hoja. Mimi ni mmoja katika hao ambao wanatakiwa kuwasaidia wenzake kujitoa katika umasikini. Isipokuwa mimi simlaumu mtu mwingine yeyote kwa mapungufu yangu. Naamini kuwa ninapaswa kujirekebisha na si serikali inipendelee dhidi ya mwenzangu tuliotofautiana rangi!

Amandla......

Fundi,
kufanikiwa wewe haimaanishi kuwa wengine wasiofanikiwa hawakujituma au hawajitumi. Kuna mambo mengi ambayo yamewakwaza hadi wakashindwa kufanikiwa.Na sababu kubwa ya watu wengi kushindwa kufanikiwa ni mfumo wetu wa uendeshaji serikali. Mathalani kila siku tunaimbishwa kuwa kilimo ni uti wa mgongo, na ama kwa hakika sekta hiyo imeajiri watanzania zaidi ya asilimia themanini(hapa namaanisha walioajiriwa na kujiajiri wenyewe).Na kwa sehemu kubwa hawa ndio wana matatizo makubwa pamoja na wamachinga ambao pia ni zao la kilimo chetu kukosa tija kwahiyo vijana wameamua kukimbilia mijini na kujiajiri kwa kuendesha maduka ya mikononi.Kwakuwa hupendi kusikia waarabu au wahindi wakitajwa, nakuomba niwatumie hapa kidogo.Je ni wangapi wanaotaabika na hizi shughuli za kilimo kama akina masanja, akina mkude na akina mwakifamba?Ndio maana tukasema hatuna sababu yoyote ya kuwakwamisha wale ambao tayari wamefanikiwa, ingawa miongoni mwa hao watanzania waasia wapo ambao hawajafanikiwa lakini nao bado hawatazuiwa kunufaika na huo uwezeshaji.Isipokuwa ni lazima tutilie mkazo kuwakwamua hawa wamatumbi ambao bado wengi sana ndio wenye hali mbaya.Mwenyewe Umekiri kuwa hawa jamaa wanasaidiana huko jamatini, kwahiyo wengi wao wanapata misaada toka kwa wenzao, je sisi wamatumbi tunawasaidiaje wenzetu?. Ndio sabau tukasema basi ni vizuri serikali yetu iweke utaratibu wa kuwasaidia hawa wamatumbi choka mbaya.
 
Fundi,
kufanikiwa wewe haimaanishi kuwa wengine wasiofanikiwa hawakujituma au hawajitumi. Kuna mambo mengi ambayo yamewakwaza hadi wakashindwa kufanikiwa.Na sababu kubwa ya watu wengi kushindwa kufanikiwa ni mfumo wetu wa uendeshaji serikali. Mathalani kila siku tunaimbishwa kuwa kilimo ni uti wa mgongo, na ama kwa hakika sekta hiyo imeajiri watanzania zaidi ya asilimia themanini(hapa namaanisha walioajiriwa na kujiajiri wenyewe).Na kwa sehemu kubwa hawa ndio wana matatizo makubwa pamoja na wamachinga ambao pia ni zao la kilimo chetu kukosa tija kwahiyo vijana wameamua kukimbilia mijini na kujiajiri kwa kuendesha maduka ya mikononi.Kwakuwa hupendi kusikia waarabu au wahindi wakitajwa, nakuomba niwatumie hapa kidogo.Je ni wangapi wanaotaabika na hizi shughuli za kilimo kama akina masanja, akina mkude na akina mwakifamba?Ndio maana tukasema hatuna sababu yoyote ya kuwakwamisha wale ambao tayari wamefanikiwa, ingawa miongoni mwa hao watanzania waasia wapo ambao hawajafanikiwa lakini nao bado hawatazuiwa kunufaika na huo uwezeshaji.Isipokuwa ni lazima tutilie mkazo kuwakwamua hawa wamatumbi ambao bado wengi sana ndio wenye hali mbaya.Mwenyewe Umekiri kuwa hawa jamaa wanasaidiana huko jamatini, kwahiyo wengi wao wanapata misaada toka kwa wenzao, je sisi wamatumbi tunawasaidiaje wenzetu?. Ndio sabau tukasema basi ni vizuri serikali yetu iweke utaratibu wa kuwasaidia hawa wamatumbi choka mbaya.

Si wote wanaoshindwa maisha kwa sababu ati mfumo haukuwapa nafasi. Mimi nisingekimbia umande ningekuwa mhandisi. Wangapi kama mimi, pamoja na kubembelezwa na walimu, walikataa kata kata shule na kuendekeza starehe? Wakati wa ujana wetu kulikuwa na walimu waliokuwa wakizunguka mjini wakitafuta wanafunzi wao waliotoroka darasani. Wakiwakuta ni bakora tu! Lakini haikusaidia. Naam, wako ambao kweli hawakupata nafasi, wengi wao wakiwa ni wanawake, lakini kuna wengi tu waliokataa au walioweka mkazo wao kwenye maisha mbadala.

Tukizungumzia hili suala la ubaguzi. Wakina Mwita kibao wamejazana kwenye majeshi kwa matakwa yao na si kulazimishwa. Wakina Maro wengi wamejikita kwenye biashara kwa hiari yao. Wakinga nao wemgi tu wamejikita kwenye biashara. Wakina Patel pia. Hawa wote wamefanya hivyo kwa hiari yao na mtazamo tawala wa jamii au kabila lao. Patel akitaka kujiunga na jeshi, ruksa. Lakini kama hataki na Mwita akajiunga hana haki ya kudai kuwa amebaguliwa. Wakina Patel asili yao ni biashara na hata wakihamia huko vijijini watafanya biashara. Kipimo cha uzalendo au utaifa si kuwa ni lazima waonekane wanataabika na kilimo au wanasukuma mkokoteni. Popote pale watakapokuwepo, kwa shughuli yeyote watakayofanya kihalali, wanahaki ya kukubalika kama mtanzania mwingine.

Serikali wajibu wake ni kuwasaidia raia wake wote choka mbaya bila kuangalia kama ni mmatumbi, mhindi, mwarabu, mzungu au mchanganyiko. Ikianza kutofautisha hao wananchi wake choka kwa misingi ya rangi, itastahili lawama kuwa inaingiza sera ya kibaguzi. Kitu gani kitatuzuia sisi wamatumbi tukianza kupewa upendeleo kusema kuwa hapana wachaga na wahaya wasipewe maana wao wana uwezo, wapewe wazaramo tu na wamakua? Si hata katika makabila yetu uwezo tumetofautiana?

Nimesema hawa jamaa wanasaidiana kijamii. Hakuna mtu atakayepinga kama wakina Mwita mtaamua kusaidiana kijamii. Au wakina Sikonge. Au wakina Fundi Mchundo. Tunachopinga ni kudai mpewe upendeleo na serikali ambayo ni ya wote, Sikonge, Mwita, Fundi Mchundo, Patel na Alnadaby. Hapo ndipo mnapokosea.

Amandla......
 
Hivi leo Tanzania kuna UBAGUZI? Jibu ni hakuna. Sasa nikashika kundi la vijana na kuwapa KALUFUNDI ka kufanya biashara pamoja na mtaji kidogo kama Mkopo inakuwa ni UBAGUZI? Nimembagua nani? Mwisho wa siku ni SERIKALI yenyewe itaamuwa nani akasome na nani asisome. Ni kama ilivyokuwa Tabora Girls na Boys. Kuna vijana maalumu walikuwa wakisoma hapo. Mna maana Nyerere alikuwa Mbaguzi siyo? Kuna watu hapa neno UBAGUZI wanali-copy na ku-past kila sehemu. Hebu tuondoleeni hizi habari zenu mnazotaka kutupandikiza. Kama twataka kuendelea lazima tujifunze KUUMA na KUPULIZA. Mataifa yote duniani yanafanya hivyo. Hii hutakuta imeandikwa POPOTE. Ila wanafanya. Sisi tukifanya basi eti tumekuwa WABAGUZI. Kwa taarifa yenu ni kuwa kama leo akionekana Mhindi au Mwarabu au Mzungu anataka kugombea Urais na final wanafika na Lowassa au Mramba au ......... basi milele lazima ujuwe kwamba NTAMCHAGUA NGOZI NYEUPE. Si kwamba ntamchagua kwa ngozi yake, ila kwa matendo yake.
Muda UFIKE sasa Tanzania ile iwe na BALANCE. Hii kitu ya kutokuwa na BALANCE siku moja inaweza ikalipuka. Hapo na ubaguzi wenu mnaoukataa mtaona kumbe ulikuwepo. Siku moja atakuja Mswahili, mwenye maneno matamu kama Obama au Hitler aseme jinsi Wahindi, Waarabu na Wazungu walivyoshika Tanzania. Atatoa na mifano kibao. Kitakachofuatia kila mmoja wenu anakijua. Hii BALANCE itakuja zuia upupu kama huu. Sasa kama hamtaki basi SUBIRINI. Mrema aligusia na jambo likanyamaza. Si kuwa limekufa ila lipolipo linaiva taratiiiibu likisubiri kama JIPU siku moja LIPASUKE.

Sikonge, mbona unasema uongo? Kama kweli tunawasujudia watu weupe basi Salim Ahmed Salim angekuwa raisi! Ilihitajika kunong'oneza tu kuwa yeye ni mwarabu na kibarua kikaota majani!

Kabla ya kusema Tanzania kuwa hakuna ubaguzi kawaulize wahindi na watu weupe! Kwa mfano, vijana wengi wa kihindi walikataliwa scholarship kwa dhana kuwa watatoroka. Sisi wamatumbi tuliendelea kupeana scholarship hata baada ya wengi wetu kutoroka! Hakuna anayemuona mmatumbi aliyezamia ughaibuni baada ya kusomeshwa na taifa lake bali tunawang'ang'ania wasio weusi! kama huu si ubaguzi, ni nini?
 
Si wote wanaoshindwa maisha kwa sababu ati mfumo haukuwapa nafasi. Mimi nisingekimbia umande ningekuwa mhandisi. Wangapi kama mimi, pamoja na kubembelezwa na walimu, walikataa kata kata shule na kuendekeza starehe? Wakati wa ujana wetu kulikuwa na walimu waliokuwa wakizunguka mjini wakitafuta wanafunzi wao waliotoroka darasani. Wakiwakuta ni bakora tu! Lakini haikusaidia. Naam, wako ambao kweli hawakupata nafasi, wengi wao wakiwa ni wanawake, lakini kuna wengi tu waliokataa au walioweka mkazo wao kwenye maisha mbadala.

Tukizungumzia hili suala la ubaguzi. Wakina Mwita kibao wamejazana kwenye majeshi kwa matakwa yao na si kulazimishwa. Wakina Maro wengi wamejikita kwenye biashara kwa hiari yao. Wakinga nao wemgi tu wamejikita kwenye biashara. Wakina Patel pia. Hawa wote wamefanya hivyo kwa hiari yao na mtazamo tawala wa jamii au kabila lao. Patel akitaka kujiunga na jeshi, ruksa. Lakini kama hataki na Mwita akajiunga hana haki ya kudai kuwa amebaguliwa. Wakina Patel asili yao ni biashara na hata wakihamia huko vijijini watafanya biashara. Kipimo cha uzalendo au utaifa si kuwa ni lazima waonekane wanataabika na kilimo au wanasukuma mkokoteni. Popote pale watakapokuwepo, kwa shughuli yeyote watakayofanya kihalali, wanahaki ya kukubalika kama mtanzania mwingine.

Serikali wajibu wake ni kuwasaidia raia wake wote choka mbaya bila kuangalia kama ni mmatumbi, mhindi, mwarabu, mzungu au mchanganyiko. Ikianza kutofautisha hao wananchi wake choka kwa misingi ya rangi, itastahili lawama kuwa inaingiza sera ya kibaguzi. Kitu gani kitatuzuia sisi wamatumbi tukianza kupewa upendeleo kusema kuwa hapana wachaga na wahaya wasipewe maana wao wana uwezo, wapewe wazaramo tu na wamakua? Si hata katika makabila yetu uwezo tumetofautiana?

Nimesema hawa jamaa wanasaidiana kijamii. Hakuna mtu atakayepinga kama wakina Mwita mtaamua kusaidiana kijamii. Au wakina Sikonge. Au wakina Fundi Mchundo. Tunachopinga ni kudai mpewe upendeleo na serikali ambayo ni ya wote, Sikonge, Mwita, Fundi Mchundo, Patel na Alnadaby. Hapo ndipo mnapokosea.

Amandla......

Kwahiyo fundi unataka kutuambia kuwa huoni umuhimu wa serikali kutoa upendeleo kwa hawa watanzania maskini wanaohangaika na kilimo cha cha jembe la mkono kila siku?Hebu nisaidie kukuelewa vizuri fundi, hivi kuwa na shahada ya uhandisi au shahada yoyote ndio kufanikiwa?mbona we unasema usingekimbia umande ungekuwa mhandisi, lakini mbona umefanikiwa?Je ndio kusema kuwa wote wenye shahada mambo yao ni safi?kama unatambua kuwa serikali inawajibika kuwasaidia raia wake, mbona hutaki kukubali kuwa hawa wamatumbi wanaoteseka na umaskini wanahitaji kusaidiwa?huu upendeleo tunaouzungumzia hapa hautofautiani na ule uliofanywa enzi za marehemu mwl.Nyerere kwenye sekta ya elimu.Wengi wetu waliweza kupata angalau nafasi za kupata elimu ya sekondari kwa mfumo huo na bado hatukusema kuwa ulikuwa ubaguzi.Mtu anayehitaji kuwezeshwa ni yule mwenye hali mbaya/ muhitaji, mtu aliyejitosheleza haihitaji upendeleo wowote isipokuwa ni kuweka mazingira ya yeye kuendelea kunufaika na fursa zilizopo.Hawa ambao wako nyuma ndio wanahitaji uwezeshwaji, na hiyo si dhambi wala ubaguzi.
 
Kwahiyo fundi unataka kutuambia kuwa huoni umuhimu wa serikali kutoa upendeleo kwa hawa watanzania maskini wanaohangaika na kilimo cha cha jembe la mkono kila siku?Hebu nisaidie kukuelewa vizuri fundi, hivi kuwa na shahada ya uhandisi au shahada yoyote ndio kufanikiwa?mbona we unasema usingekimbia umande ungekuwa mhandisi, lakini mbona umefanikiwa?Je ndio kusema kuwa wote wenye shahada mambo yao ni safi?kama unatambua kuwa serikali inawajibika kuwasaidia raia wake, mbona hutaki kukubali kuwa hawa wamatumbi wanaoteseka na umaskini wanahitaji kusaidiwa?huu upendeleo tunaouzungumzia hapa hautofautiani na ule uliofanywa enzi za marehemu mwl.Nyerere kwenye sekta ya elimu.Wengi wetu waliweza kupata angalau nafasi za kupata elimu ya sekondari kwa mfumo huo na bado hatukusema kuwa ulikuwa ubaguzi.Mtu anayehitaji kuwezeshwa ni yule mwenye hali mbaya/ muhitaji, mtu aliyejitosheleza haihitaji upendeleo wowote isipokuwa ni kuweka mazingira ya yeye kuendelea kunufaika na fursa zilizopo.Hawa ambao wako nyuma ndio wanahitaji uwezeshwaji, na hiyo si dhambi wala ubaguzi.

Hakuna anayepinga serikali kusaidia wananchi wake. Tunachopinga ni serikali kufanya hivyo kwa kubagua. Haswa ubaguzi huu ukifanyika kwa kutumia rangi ya raia wake. Si weusi wote waliokuwa wanyonge na si weupe wote walokuwa nazo. Mtu apewe upendeleo kutokana na hali yake bila kujali rangi yake.

Mimi Fundi Mchundo (technician). Ningesoma zaidi ningekuwa mhandisi (engineer). Hata hivyo nimeridhika na hapa nilipofika na siwaonei wivu wahandisi.

Nyerere hakuwa mbaguzi. Alitoa elimu bure kwa mtanzania yeyote. Hakusema kwanza wamatumbi wajae darasani ndiyo wahindi wapewe nafasi. Alimkaripia Amin alipofukuza wahindi. Alimkaripia Iddi Simba alipoleta sera hii ya uzawa na kutamka wazi kuwa ni ya kibaguzi.

Huu upendeleo mnaouzungumzia hapa hata siku moja asingeukubali. Si Nyerere tuliyemjua. Angewatolea nje.

Amandla......
 
Hakuna anayepinga serikali kusaidia wananchi wake. Tunachopinga ni serikali kufanya hivyo kwa kubagua. Haswa ubaguzi huu ukifanyika kwa kutumia rangi ya raia wake. Si weusi wote waliokuwa wanyonge na si weupe wote walokuwa nazo. Mtu apewe upendeleo kutokana na hali yake bila kujali rangi yake.

Mimi Fundi Mchundo (technician). Ningesoma zaidi ningekuwa mhandisi (engineer). Hata hivyo nimeridhika na hapa nilipofika na siwaonei wivu wahandisi.

Nyerere hakuwa mbaguzi. Alitoa elimu bure kwa mtanzania yeyote. Hakusema kwanza wamatumbi wajae darasani ndiyo wahindi wapewe nafasi. Alimkaripia Amin alipofukuza wahindi. Alimkaripia Iddi Simba alipoleta sera hii ya uzawa na kutamka wazi kuwa ni ya kibaguzi.

Huu upendeleo mnaouzungumzia hapa hata siku moja asingeukubali. Si Nyerere tuliyemjua. Angewatolea nje.

Amandla......

Fundi,
Suala hapa si Idd Simba wala nini. Kama tunaijadili hii mada tukiwa na mtazamo kuwa Idd Simba aliileta hii hoja na Nyerere akaikatalia mbali utakuwa unakwenda nje. Kinachozungumzwa hapa ni huu umaskini wa watanzania natives, ni namna gani wanaweza wakakwamuliwa kutoka kwenye lindi la umaskini?kwahiyo katika kutafakari namna ya kuwasaidia hawa watu ndio maana tunaona ni muhimu wakapewa upendeleo, kwasababu ukweli uko dhahiri kuwa wameshindwa kujikwamua katika mfumo uliopo.Je ni busara kuacha asilimia 80 ya watu inateseka kwa kuwa itaonekana ni ubaguzi mbele ya macho ya watu asilimia 10?Tena uzuri ni kuwa hawa watu kama wakiwezeshwa watasaidia kuongeza uzalishaji na matokeo yake kuongezeka tija katika uzalishaji na hatimaye hawataishia kuinua vipato vyao tu, bali hata uwezo wa serikali na kukuza uchumi.
 
kinachonishangaza mimi ni kwamba, watetezi wa sera ya uzawa wanafahamu wazi kuwa ukija na sera ya "KUMWEZESHA MTANZANIA",ukafanikiwa kumwezesha Mtanzania ni wazi kuwa ndani yake utakuwa umemuwezesha mzawa na pia utakuwa umemuwezesha na yule asiyeitwa mzawa lakini wote ni watanzania , sera kama hii inatosha kuwaridhisha watetezi wa uzawa kwa sababu by default ndani mwake inamuwezesha mzawa , inavyoonekana wasichokitaka watetezi wa uzawa ni ile "kutomwezesha yule asiyeitwa mzawa", wakati kumbe ukimwezesha huyu asiyeitwa mzawa wala hakuzuii kumwezesha yule anayeitwa mzawa", hapa inaonekana kama choyo fulani hivi, kama unavyoona baadhi ya watoto baba akileta pipi yeye anataka apewe nyingi kuliko mwenzake!

sera inayofaa ni SERA YA KUMWEZESHA MTANZANIA, kwa sababu by default inamwezesha "yule mnayemwita mzawa", na at the same time inamwezesha yule "asiyeitwa mzawa", lakini siku ya siku ni Tanzania ndo inanufaika.

kama hoja ni kwamba wale wanaoitwa wazawa ni wengi asilimia 80, basi kumbe hao bado ni kidogo mbele ya Watanzania wote, kwa sababu watanzania wote ni asilimia 100 bali wale wanaoitwa wazawa ni asilimia 80 tu.
Kati ya hao asilimia 100 ya Watanzania mathalani asilimia zaidi ya 90 wakiwezeshwa si ni bora zaidi?
 
Sikonge, mbona unasema uongo? Kama kweli tunawasujudia watu weupe basi Salim Ahmed Salim angekuwa raisi! Ilihitajika kunong'oneza tu kuwa yeye ni mwarabu na kibarua kikaota majani!

Kabla ya kusema Tanzania kuwa hakuna ubaguzi kawaulize wahindi na watu weupe! Kwa mfano, vijana wengi wa kihindi walikataliwa scholarship kwa dhana kuwa watatoroka. Sisi wamatumbi tuliendelea kupeana scholarship hata baada ya wengi wetu kutoroka! Hakuna anayemuona mmatumbi aliyezamia ughaibuni baada ya kusomeshwa na taifa lake bali tunawang'ang'ania wasio weusi! kama huu si ubaguzi, ni nini?

FM,
Yaani naanza kupata wasiwasi kama tunajadiliana ama tunashindana. Kama tunashindana basi mie ntajibu hii ya mwisho. Kama tunajadiliana basi please andika vitu vilivyo na miguu na kichwa na siyo kusema mie naandika UONGO.
Salim Ahmed Salim angelishinda kwa Uarabu wake. Ila sema huko juu alipambana na wasomi wanaojua kuangamiza wapinzani wao kisiasa. Kumbuka Lowassa aliwamaliza wote na kuwasaga Vichwa kama nyoka na tena bila huruma. Unafikiri kama waliwamaliza akina Malecela na Sumaye, Salim angeliona ndani against Mtandao? Are you Kidding me? Na leo kama huyajui hayo unasema "mbona Salim hakuchaguliwa na weupe wake". Salim hakufika hata katika nafasi ya Taifa ya kugombea Urais. Hizo sijui NEC za CCM zilimpiga chini. Yaani kila siku watu wanaimba EPA wee hujui zilifanya nini? angeliingia chama kingine na akakataliwa na wananchi hapo tungeliongoa. Ila usiniambie kuwa kwa kuwa MAFIA wa NEC hawakumchagua na walihongwa kumchagua Kikwete basi ni kuwa asingelishinda.
Juu ya watu kuzamia, mhhhmmmmmm. Tuseme mie nimezamia nchi za Kiarabu, badala ya kurudi Tanzania. Ila kila mwezi zinaenda dola kadhaa. Namfahamu member mmoja humu ndani, alipata scholaship nje, kamaliza akabaki nje. Leo hii ingawa anaishi nje, kajenga MRADI mkubwa sana kwao Mbeya wa hela nyingi mno. Yes, nasema dola nyingi sana ambazo kama angelikuwa anafanya kazi Tanzania, labda kama FISADI ndiyo angelipata hela hizo. Hadi leo hii huko nje anaishi maisha ya kwaida sana ili kuendeleza mradi wake huo ambao unaajiri sasa watu wengi tu. Namfahamu dada mmoja kasomeshwa na Wanorway uganga. Anasema wazi kabisa siku moja anarudisha gamba lao na arudi kwao Musoma akajenge hospital.
Wahindi na mataifa mengine nao wakisomeshwa wakimaliza, uwezekano mkubwa ni kuwa watarudi kwao. Kuna Mtanzania mmoja alipelekwa kusoma nje. Alipomaliza shule akaomba karatasi ya kusafiria kurudi. Nikamuuliza kwa nini unafanya hivyo kwani huna passport? Akasema baba yake aliyekuwa nje ya nchi (baada ya kukosana na Banda wa Malawi) alishaacha kazi UDSM na kurudi kwao. Hivyo yeye amepewa ticket kurudi kwao Malawi. Sidhani hata alishawahi kurudi Tanzania kusalimia au kuaga.
Yangu katika mjadala yanaishia hapo. Serikali yenyewe itaamua nini cha kufanya. Mwisho wa siku sijui hata watafanya nini. Tunabishana hata hatujajua nini kitafanyika. Wakipitia hapa na kusoma watajua maoni yetu na kuchagua kama ya umoja wa Waislam.
 
Hakuna mtu anayepinga kuwa kuna wahindi wabaguzi. Kama ilivyo kuna waarabu wabaguzi, wachina wabaguzi, wahaya wabaguzi, wazaramo, wabaguzi, wazungu wabaguzi, watu weusi wabaguzi n.k. Lakini hii haihalashi kuwa na sheria ya kibaguzi kwa vile tuu baadhi yetu ni wabaguzi. Nchi yeyote yenye kuthamini uhuru wa wananchi wake inawapa uhuru wa kuamua nani wachanganyike nae. Uko huru kutompenda mhindi kama vile yeye alivyo huru kutokukupenda! Kinachopingwa ni kumnyima haki yeyote kwa vile tu ni mhindi au mwarabu. Sheria kamwe haiwezi kuondoa wabaguzi lakini inaweza kuzuia ubaguzi.

Wewe kama unawachukia wahindi WOTE kwa kuamini kuwa ni wanafik basi ni mbaguzi. Hauna tofauti na mzungu wa Mississippi anaechukia watu weusi WOTE kwa kuamini kuwa ni hawana akili, majambazi na kucha wanatamani kubaka wanawake zake. Wote ni wabaguzi (racists), period.

Amandla.....
Asante kwa maelezo yako, kwa hiyo tatizo ni letu sisi weusi au? yaani bado tuna inferiority complex na ndilo tatizo letu au? Kwa sababu kama ndio hivyo sehemu zote mf banki na nyingine wameshika weusi, ila ni kwa nini wanawaamini weupe kuliko weusi? Basi itabidi somo tuu. Kuna kitu ambacho nimewahi kuambiwa na watu wa West Africa (Wanigeria) likija suala la hela huwa hawaamini mtu hata mama zao (Sasa hilo ndilo tatizo letu au?)
 
FM,
Yaani naanza kupata wasiwasi kama tunajadiliana ama tunashindana. Kama tunashindana basi mie ntajibu hii ya mwisho. Kama tunajadiliana basi please andika vitu vilivyo na miguu na kichwa na siyo kusema mie naandika UONGO.
Salim Ahmed Salim angelishinda kwa Uarabu wake. Ila sema huko juu alipambana na wasomi wanaojua kuangamiza wapinzani wao kisiasa. Kumbuka Lowassa aliwamaliza wote na kuwasaga Vichwa kama nyoka na tena bila huruma. Unafikiri kama waliwamaliza akina Malecela na Sumaye, Salim angeliona ndani against Mtandao? Are you Kidding me? Na leo kama huyajui hayo unasema "mbona Salim hakuchaguliwa na weupe wake". Salim hakufika hata katika nafasi ya Taifa ya kugombea Urais. Hizo sijui NEC za CCM zilimpiga chini. Yaani kila siku watu wanaimba EPA wee hujui zilifanya nini? angeliingia chama kingine na akakataliwa na wananchi hapo tungeliongoa. Ila usiniambie kuwa kwa kuwa MAFIA wa NEC hawakumchagua na walihongwa kumchagua Kikwete basi ni kuwa asingelishinda.
Juu ya watu kuzamia, mhhhmmmmmm. Tuseme mie nimezamia nchi za Kiarabu, badala ya kurudi Tanzania. Ila kila mwezi zinaenda dola kadhaa. Namfahamu member mmoja humu ndani, alipata scholaship nje, kamaliza akabaki nje. Leo hii ingawa anaishi nje, kajenga MRADI mkubwa sana kwao Mbeya wa hela nyingi mno. Yes, nasema dola nyingi sana ambazo kama angelikuwa anafanya kazi Tanzania, labda kama FISADI ndiyo angelipata hela hizo. Hadi leo hii huko nje anaishi maisha ya kwaida sana ili kuendeleza mradi wake huo ambao unaajiri sasa watu wengi tu. Namfahamu dada mmoja kasomeshwa na Wanorway uganga. Anasema wazi kabisa siku moja anarudisha gamba lao na arudi kwao Musoma akajenge hospital.
Wahindi na mataifa mengine nao wakisomeshwa wakimaliza, uwezekano mkubwa ni kuwa watarudi kwao. Kuna Mtanzania mmoja alipelekwa kusoma nje. Alipomaliza shule akaomba karatasi ya kusafiria kurudi. Nikamuuliza kwa nini unafanya hivyo kwani huna passport? Akasema baba yake aliyekuwa nje ya nchi (baada ya kukosana na Banda wa Malawi) alishaacha kazi UDSM na kurudi kwao. Hivyo yeye amepewa ticket kurudi kwao Malawi. Sidhani hata alishawahi kurudi Tanzania kusalimia au kuaga.
Yangu katika mjadala yanaishia hapo. Serikali yenyewe itaamua nini cha kufanya. Mwisho wa siku sijui hata watafanya nini. Tunabishana hata hatujajua nini kitafanyika. Wakipitia hapa na kusoma watajua maoni yetu na kuchagua kama ya umoja wa Waislam.

Naona tunashindana wala hatujadiliani. Kama kweli unaamini kuwa sababu iliyomtoa Salim Ahmed Salim katika kinyang'anyiro cha kugombea urais ni hongo peke yake na kuwa sumu iliyoingizwa kuwa yeye ni muarabu haikuchangia, basi tunashindana.

Suala nililozungumzia ni dhana ya kuwanyima scholarship wahindi ati kwa sababu watakimbia nchi wakati kipimo hicho hicho hakitumiwi kwa mmatumbi. Kwamba jamaa yako alizamia halafu akajenga kwao halina nafasi hapa. Angekuwa mhindi hata hiyo nafasi asingepewa.

Unasema wahindi na weupe wakipata nafasi ya kwenda nje hawarudi nyumbani bali wanaenda kwao ( nadhani una maanisha uhindini na si Tanzania ambako wengi wamezaliwa na kukulia) na kuona hilo ni tatizo. Wakat huo huo unampongeza dada wa kimatumbi aliyesomeshwa na Norwegians ( bila shaka kupitia msaada kwa Tanzania) na kuwa amekana uraia wa Tanzania na kuchukua wa Norway. Huyu kwa vile ameahidi kurudi nyumbani siku ya siku unamuona shujaa! Wangapi wameahidi hivyo na wamejikuta wanakula pensheni huko ughaibuni? Kwa nini tuone kosa akifanya mhindi peke yake?

Unatoa mfano wa mMalawi mmoja kuwahukumu wote. Wangapi ambao ingawa wazazi wao wametokea nje walijitolea kikamilifu kwa taifa lao la Tanzania. Hao hao ( wakina Jenerali Ulimwengu na wenzake), baada ya kujitolea kwao, pengine kuliko hata wengi wetu, hatuchelei kuwatema na kuwaita wageni nchini mwao. Sasa wengine wakiona hivyo, kwa nini wangojee kudhalilishwa? Wangapi wamerudi na wakakuta kuna glass ceiling kwa sababu ya watu kudai ati yeye ni mrundi, mnyarwanda, mnyasa na kadhalika? Tumeruhusu sumu ya uzawa kuingia na imeanza kutumika na waovu kuwanyima haki zao watanzania wenzetu.

Kwa hayo machache, nakubaliana nawe. Hakuna siku tutakubaliana kwenye hili. Naona tukubali kutofautiana.

Amandla......
 
Nitarudia upya hadithi yangu na kama Fundi mchundo utaielewa nitashukuru sana kwa sababu inabeba kila kitu unachouliza wewe.. Nitaurudia mfano wangu tena soma kwa makini....
Wanachoomba wananchi ni huyu babaye tu serikali kumwesha mtoto wake kufika shuleni, hatuogopi Umande hata kidogo ila shule iko mbali sana..
Sasa tusiendelee kutumia lugha ya wazee wetu kuwa hakuna mtu aliyetuzuia kutembea kwa mguu wakati unashindwa kuona kwamba hao watoto wengine wanachukuliwa na magari, sisi tunaomba hela za daladala tu.. yaani kuwezeshwwa kwa kipimo kidogo sana. Tatizo kubwa ni kwamba serikali ina uwezo wa kufikisha shuleni na gari lake kwani linapakia hawa watoto wa kufikia, wanapewa tax exemption na kadhalika kirahisi kabisa...

Kama nilivyosema huko nyuma ni dhahiri serikali kwa mifano mingi sana inawapa ride hawa jamaa zetu na pengine kifuko cha lunch kutokana na kifuta jasho kinachotoka upande wa pili wakati sisi tunapuyanga na miguu isokuwa na hata kandambili..hatuombi makubwa ama tuwe sawa na wageni..Haiwezekani hawa jamaa zetu walikuja nchi zetu kutafuta maisha sio kutafuta Uraia. Uraia ni process tu inayowakuta lakini kilichowatoa huko walikotoka ni kufatuta ngawila!.
Tunachoomba mkuu ni kuwa treated sawa na hawa jamaa zetu ambao wewe hutaki kuwazungumzia isipokuwa Mtanzania ambaye unaona unyonge na uvivu wake.. Equal opportunity hutumika tu pale ground level iko sawa, sio sehemu ambayo mmoja yuko chini mwingine juu au kati ya mzima na kilema.

Umaskini ni kilema mkuu wangu na siku zote kipimo cha maendeleo ya nchi zetu za kiafrika hutazama maisha ya wazawa kwa ujumla hivyo hao wageni ambao wanatengeneza only 10 ya population hawawezi kubadilisha hali ya Watanzania asilimia 90 ktk mazingira tuliyokuwa nayo..Huko majuu ukitazama hesabu zao unaweza kukuta 40 kwa 60, 50/50 na pengine 20/80 wazawa kwa wageni hivyo kuna tofauti kubwa sana kulitazama swala hili kwa darubini za Ulaya..kumbuka uhuru wa hawa watu una zaidi ya miaka 200 na hawakuvamia equal opportunity kama tunavyoiga sisi, Hayo maswala ya rangi mimi simo kabisa kwani kesho tutaingia kuchunguzana makabila.

Tunachoomba ni serikali kuwatazama wazawa kama watoto wao wenyewe, hatuikatazi serikali kuwalea hawa wahamiaji kwa malezi sawa na sisi isipokuwa wasipewe hata wao malezi zaidi yetu.
 
Mkuu Mkandara.

Wote sisi ni wahamiaji ukiondoa waHadzabe! Hakuna mwenye haki zaidi ya mwingine kuishi katika nchi yetu. Mimi napinga ubaguzi wa aina yeyote kwa sababu najua kuwa leo tunawazungumzia wahindi, kesho tutawageukia wanyarwanda na kesho kutwa wazaramo watawageukia wachaga waliojenga Mkuranga!

Mimi bado sijaona sera au sheria inayopendelea mtu wa rangi moja dhidi ya mwingine. Kinachofanyika ni kupindishwa kwa taratibu kumsaidia mtu mwenye rupia bila kujali rangi yake. Hawa wanaopindisha sheria hiyo ndiyo wabanwe. Na kama kuna mtu anaewashawishi kufanya hivyo, nae abanwe bila kujali rangi yake.

Hivi, Mkuu unadhania kumnyang'anya lunch box au nike huyo unayeona amekuzidi kutabadilisha hali yako?

Maskini wa kutupwa Tanzania wanapatikana vijijini kwetu. Huko hao unaowanyoshea vidole wako wachache. Lakini sisi wengi wetu ambao tumetoka huko na tunaenda huko kila likizo ndiyo tunaoenda na maSUV yetu, lunch box na maji ya madukani. Sisi ndiyo tunaotakiwa tulete tofauti katika maisha ya wenzetu. Sisi kwa kukataa kurubuniwa na hawa wenzetu tunaowapa nafasi za ulaji kwa takhrima ya pilau na Khanga ya India. Nyinyi wakina Mkandara mnadai mikopo ya benki lakini masikini wa kutupwa anachohitaji ni mtaji wa kiroba cha mbegu. Benki gani iko tayari mikopo ya aina hii? Ni sisi tunaotakiwa kuanzisha njia mbadala za kuwapatia mitaji ndugu zetu na kwa vile tunajuana kuhakikisha kuwa mitaji hiyo inatumika ipasavyo ili na wengine wanufaike.

Hizo tax exemption zilikuwa zinatolewa kwa kila mwekezaji. Hata wakina Mengi wamefaidika nazo. Ni sisi kujielimisha namna gani tunaweza kufaidika na vitu kama hivi. Hata siku moja usitegemee serikali ikutafute ikuambie kuwa njoo ujichotee hela. Ni uongo kusema kuwa ni wageni tu ndiyo waliofaidika. Tofauti ni wenzetu wanafanya home work yao ( mara nyingi kwa kututumia sisi wamatumbi) kabla hawajawekeza na wanahakikisha wanatimiza masharti yote ili wanufaike na tax loop holes. Ndiyo biashara.

Sisi kama wananchi hatuna sababu ya kuomba serikali ituletee maendeleo. Huo ni wajibu wao tuliowatuma na wakishindwa tunatakiwa tunawafukuze na kumweka mwingine atakaeyaleta. Dawa si kumbagua mwenzetu bali ni kui-hold serikali accountable kwa kile tulichowatuma watufanyie. Hakuna njia ya mkato kwenye hili.

Amandla..........
 
Fundi Mchundo,
Hivi, Mkuu unadhania kumnyang'anya lunch box au nike huyo unayeona amekuzidi kutabadilisha hali yako?
..
Tunachoomba sisi ni kumpa mwanao pia lunch box, usimnyang'anye huyo mgeni..sasa hiyo equal opportunity yenu mbona inatazama toka upande mmoja tu mkuu wangu.. kwa nini unashindwa kumpa luch box mwanao hata kama ni kipande cha mkate au kande wakati yule mgeni unampa chapati na mahanjumati...
Mkuu hatuwezi kuepuka swala la Mimi na yule na ndio maana kuna neno Equal oppoturnity kwani kuna zaidi ya mtu mmoja wenye tofauti fulani fulani..sheria inatazama tofauti hizi.
 
Nitasherehesha maelezo yangu hapo juu kwa mfano mzuri na mdogo sana.
Soten tunafahamu kwamba asilimia karibu 80 ya watanzania ni wakulima kwa ni serikali isiwakopeshe matrekta au kuwakodisha kwa makato ya mapato kama alivyokuwa akifanya mkoloni. Hivi kweli serikali inashindwa kumwaga matekta hata 10 tu kila wilaya ambayo wakulima wanaweza ku lease wakati wa kilimo badala ya wao kutumia jembe la mkono?..hao kina Patel (oops wahindi) hawana haja ya kushika jembe na wala hawatalishika kwa sababu hawawezi kusubiri mavuno miezi sita au mwaka mzima.. Sii biashara yao, isipokuwa wao watawezeshwa ktk sehemu zao kama kawaida maadam mzawa pia anasogea mbele kuliko kukaa paleplae akisubiri mwanaye lini atakuwa TX mtaa wa Jamhuri.
Wavuvi kuwakodishia mashine ndogo za uvuvi na kadhalika hata kama kwa kutumia hizo Sacoos.. Pengine hata kuanzisha dock la kutengeneza mitumbwi ambayo wananchi wenyewe watafanya kazi kuzalisha, na pengine hata kufikia kutengeneza Yatch zikauzwa Ulaya..

New Zealand walikuwa wanunuzi wakubwa wa nyama toka Zimbabwe, leo hii wamekata, Somalia ilikuwa ikisafirisha mbuzi nchi za kiarabu,leo hii vita tupu kwao sisi tumezubaa.. kwa nini Tanzania isirudishe kitu kama Tanganyika Packers kutafuta soko la nyama yetu nje..Na wote hawa nakuhakikishia aliyekwenda kuweka mikataba ni marais wao sio wananchi waliotafuta soko hilo kwani kuna maswala ya kubadilishana na standards..

Sote tunafahamu kwamba sio kila mtu ana vision lakini anapoona mwanya wa kuweza kufanya kazi atajituma sasa yuel atakaye zembea na kuchagua uzururaji tutaweza kuwa na sababu ya kumnyooshea kidole. Ikiwa serikali haiwezi kutimiza promise zake za kuzalisha ajira kwa nini isifikire zaidi kuwafuata wananchi ktk mazingira wanayoishi na kujaribu kuwaonyesha njia, kuwapa mwanga kwamba Tanzania itajengwa na wao..
 
Hakuna anayepinga serikali kusaidia wananchi wake. Tunachopinga ni serikali kufanya hivyo kwa kubagua. Haswa ubaguzi huu ukifanyika kwa kutumia rangi ya raia wake. Si weusi wote waliokuwa wanyonge na si weupe wote walokuwa nazo. Mtu apewe upendeleo kutokana na hali yake bila kujali rangi yake.

Mimi Fundi Mchundo (technician). Ningesoma zaidi ningekuwa mhandisi (engineer). Hata hivyo nimeridhika na hapa nilipofika na siwaonei wivu wahandisi.

Nyerere hakuwa mbaguzi. Alitoa elimu bure kwa mtanzania yeyote. Hakusema kwanza wamatumbi wajae darasani ndiyo wahindi wapewe nafasi. Alimkaripia Amin alipofukuza wahindi. Alimkaripia Iddi Simba alipoleta sera hii ya uzawa na kutamka wazi kuwa ni ya kibaguzi.

Huu upendeleo mnaouzungumzia hapa hata siku moja asingeukubali. Si Nyerere tuliyemjua. Angewatolea nje.

Amandla......

Kwa kawaida huwa nasikitika sana mtu aki argue bila kuwa na backgroung ya facts nyuma yake.Matokeo yake ni kuwa na ierrelevancies ambazo haziwezi ku himili argument yake.
Ubaguzi ni dhambi tosha inayoweza kuleta mtafaruku mkubwa katika jamii yoyote.
Kwa wanaofuatilia argument hii ya kuwa wezesha watu wa nchi hii, lengo nafikiri ni kuwapo mikakati maalum ya kuwabadilisha watanzania wazawa ili waendelezwe.
Sasa huwa nashangaa mtu anapinga hili na kuliona ni kama kuwabagua wahindi na waarabu na wazungu!
Ni vyema mtu akajiuliza, kama hiyo siyo myopic argument, je hao wasio wazawa hapa nchini wako wangapi? as compared to masses.Tunaongea juu ya masses(waTanzania walio wengi) hapa na mass hii ya watanzania walio maskini ikiendelezwa ndio nchi itaendelea.
Kama wahindi waarabu na hao wazungu wakiingia katika hiyo mass ya watanzania maskini so be it, nao wataendelezwa.
Nafikiri ni vyema watu tukaelewa mantiki ya kuwawezesha waTanzania vizuri , ama sivyo kama ni haki sawa kwa wote, hata jeshi letu tulifanye huria basi, maana hata katika jeshi kuna utaalam wa hali ya juu kabisa lakini huko ni kwa wazawa tu!
 
Hivi Fundi Mchundo wewe ni mu-Hindi au unafanya kazi kwa Mu-hindi au umelipwa ili kutetea (LOL) hahahaha! I Just askin? Happy New Year Bro!
 
Fundi Mchundo,
..
Tunachoomba sisi ni kumpa mwanao pia lunch box, usimnyang'anye huyo mgeni..sasa hiyo equal opportunity yenu mbona inatazama toka upande mmoja tu mkuu wangu.. kwa nini unashindwa kumpa luch box mwanao hata kama ni kipande cha mkate au kande wakati yule mgeni unampa chapati na mahanjumati...
Mkuu hatuwezi kuepuka swala la Mimi na yule na ndio maana kuna neno Equal oppoturnity kwani kuna zaidi ya mtu mmoja wenye tofauti fulani fulani..sheria inatazama tofauti hizi.

Tatizo ndilo hili. Tunataka tupewe na sio tuwezeshwe. Badala ya kumpa lunch box ni bora kumuelimisha kuwa lunch box si lazima iwe na hamburgers bali unaweza kuweka maembe, mapapai na maziwa. Unaweza kumsaidia kwa kumweleza kuwa asijali lunch box ya mwenzake cha muhimu ni elimu na akifanikiwa, nae atawanunulia watoto wake lunch box na viatu vya Nike. Ni kumfahamisha kuwa pamoja na mwenzake kuwa na lunch box na raba mtoni hamzidi kitu kama binadamu na akijitahidi ataweza kumzidi.

Sera za kupewa zimejaribiwa sana na hazikutufikisha mbali. Hao wanakijiji wetu walichimbiwa visima na kuwekewa pump za Tanira. Kwa sababu walipewa, pamp hizi wakaziacha bila matengenezo hadi zikafa kabisa! Hao wananchi walipewa elimu ya bure lakini badala ya kuichangamkia baadhi yao wakaona ni wajibu wa serikali kuwapa hiyo elimu na kukataa kuchangia hata thumuni! Kama nilivyosema awali, nchi hii ilianzisha benki ya nyumba ili itoe mikopo nafuu kwa wananchi wake. Wananchi hao wakachukua mikopo, wakaolea wake wa ziada, wakanunua chenja, ili mradi wakafanya kila kitu ila kujenga nyumba. Na mikopo hawakurudisha. Benki hiyo sasa ni history. Si kweli kusema kuwa serikali haijafanya lolote kujaribu kumnyanyua mwananchi wake kutoka katika umasikini uliokithiri.

Unazungumzia uvuvi. Serikali hiyo hiyo ilianzisha Chuo cha Mbegani kuwasaidia wavuvi. Leo kiko wapi? Badala ya kutengeneza hizo mashua leo kinahifadhi timu za mpira.

Serikali hiyo hiyo ilianzisha vyuo vya maendeleo ( wakiiga mfano wa Folk Colleges za Scandinavia) sehemu mbalimbali kwa nia ya kuwapa elimu mbadala wanachi wake. Leo viko wapi?

Tanganyika Packers tuliibinafsisha. Tukashindwa ku-maintain standard zinazotakiwa za nyama za makopo na soko likayeyuka. Leo unataka tena serikali iingie katika biashara ya kusindika nyama? Kwa nini, kama mnaona kuna soko, msijikusanye na kuwekeza huko? Akija mgeni, akawekeza, mtamlaumu kuwa amependelewa!
Hivi unaamini kweli jawabu ni kuwapa wanakijiji hao matrekta? Vipi mafuta ya kuendesha hizo trekta? Vipi gharama za service za hayo matrekta? Vipi vipuri na gharama ya matengenezo yakiharibika? Au unadhani hao wakulima watakuwa na uwezo wa kukodi au kununua hayo matrekta? Watu ambao wanashindwa kununua chandarua cha shilingi 2000, leo mnataka wakodi trekta! Mnaujua kweli umaskini uliokuweko Tanzania au mnausikia redioni tu?

Katika yote mliyozungumza, hamjaweka bayana kuwa ni wapi serikali inamzuia mfanya biashara mtanzania mweusi kuwekeza. Sheria gani na sera gani zimewekwa ili kuhakikisha kuwa hawa hawaendelei kiasi cha kuhitaji sheria mbadala ya kuwakwamua!


Kwa kawaida huwa nasikitika sana mtu aki argue bila kuwa na backgroung ya facts nyuma yake.Matokeo yake ni kuwa na ierrelevancies ambazo haziwezi ku himili argument yake.
Ubaguzi ni dhambi tosha inayoweza kuleta mtafaruku mkubwa katika jamii yoyote.
Kwa wanaofuatilia argument hii ya kuwa wezesha watu wa nchi hii, lengo nafikiri ni kuwapo mikakati maalum ya kuwabadilisha watanzania wazawa ili waendelezwe.
Sasa huwa nashangaa mtu anapinga hili na kuliona ni kama kuwabagua wahindi na waarabu na wazungu!
Ni vyema mtu akajiuliza, kama hiyo siyo myopic argument, je hao wasio wazawa hapa nchini wako wangapi? as compared to masses.Tunaongea juu ya masses(waTanzania walio wengi) hapa na mass hii ya watanzania walio maskini ikiendelezwa ndio nchi itaendelea.
Kama wahindi waarabu na hao wazungu wakiingia katika hiyo mass ya watanzania maskini so be it, nao wataendelezwa.
Nafikiri ni vyema watu tukaelewa mantiki ya kuwawezesha waTanzania vizuri , ama sivyo kama ni haki sawa kwa wote, hata jeshi letu tulifanye huria basi, maana hata katika jeshi kuna utaalam wa hali ya juu kabisa lakini huko ni kwa wazawa tu!

lole gwakisa!
Kama hao wasio weusi ni wachache hivyo basi kuna haja gani ya kubagua? Kwa nini msiseme tu watanzania mkijua kuwa wengi watakuwa ni hao mnaowaita wazawa? Hao wahindi, waarabu na hao wazungu hawatakiwi kufanyiwa favour ati so be it. Wao kama watanzania wengine wana haki ya kutambuliwa hivyo bila ati kufanyiwa fadhila na walio wengi!

Sasa unaleta ubishi usio na mantik. Tangu lini jeshi limetangazwa kuwa la hao mnaowaita wazawa tu? Au la watu wa Musoma tuu? Mtanzania yeyote ana haki ya kujiunga na jeshi kama anataka. Jeshi letu mpaka sasa hivi ni volunteer based na si la conscripts. Mtu unajiunga kwa hiari yako. Halazimishwi mtu. Ni uongo kama huu ndiyo chimbuko la chuki dhidi ya wenzetu.

Lusajo. Hivi lazima niwe na uhusiano na wahindi ndiyo niwatetee?

Amandla......


 
Naona tunashindana wala hatujadiliani. Kama kweli unaamini kuwa sababu iliyomtoa Salim Ahmed Salim katika kinyang'anyiro cha kugombea urais ni hongo peke yake na kuwa sumu iliyoingizwa kuwa yeye ni muarabu haikuchangia, basi tunashindana.

Suala nililozungumzia ni dhana ya kuwanyima scholarship wahindi ati kwa sababu watakimbia nchi wakati kipimo hicho hicho hakitumiwi kwa mmatumbi. Kwamba jamaa yako alizamia halafu akajenga kwao halina nafasi hapa. Angekuwa mhindi hata hiyo nafasi asingepewa.

Unasema wahindi na weupe wakipata nafasi ya kwenda nje hawarudi nyumbani bali wanaenda kwao ( nadhani una maanisha uhindini na si Tanzania ambako wengi wamezaliwa na kukulia) na kuona hilo ni tatizo. Wakat huo huo unampongeza dada wa kimatumbi aliyesomeshwa na Norwegians ( bila shaka kupitia msaada kwa Tanzania) na kuwa amekana uraia wa Tanzania na kuchukua wa Norway. Huyu kwa vile ameahidi kurudi nyumbani siku ya siku unamuona shujaa! Wangapi wameahidi hivyo na wamejikuta wanakula pensheni huko ughaibuni? Kwa nini tuone kosa akifanya mhindi peke yake?

Unatoa mfano wa mMalawi mmoja kuwahukumu wote. Wangapi ambao ingawa wazazi wao wametokea nje walijitolea kikamilifu kwa taifa lao la Tanzania. Hao hao ( wakina Jenerali Ulimwengu na wenzake), baada ya kujitolea kwao, pengine kuliko hata wengi wetu, hatuchelei kuwatema na kuwaita wageni nchini mwao. Sasa wengine wakiona hivyo, kwa nini wangojee kudhalilishwa? Wangapi wamerudi na wakakuta kuna glass ceiling kwa sababu ya watu kudai ati yeye ni mrundi, mnyarwanda, mnyasa na kadhalika? Tumeruhusu sumu ya uzawa kuingia na imeanza kutumika na waovu kuwanyima haki zao watanzania wenzetu.

Kwa hayo machache, nakubaliana nawe. Hakuna siku tutakubaliana kwenye hili. Naona tukubali kutofautiana.

Amandla......

Fm,
Juu ya SAS ni kuwa akina Kikwete walitumia HONGO na kigezo cha Uarabu wa SAS na kumuondolea mbali. Hizi hongo zilitumia pia kuwamaliza akina Sumaye na Malecela. Kama huamini basi muulize FMes maana yuko karibu na Malecela. Huko utapata data kamili juu ya walivyowaliza wapinzani wao ndani ya NEC ambayo mwenyekiti ingawa alikuwa Mkapa, alishindwa kufurukuta jinsi Mtandao ulivyofanya kufuru. Kama hujui basi ngoja nikuambia kwamba, miezi kadhaa kabla ya uchaguzi, Mtandao walikuwa wameshika nchi. Hivyo walikuwa wanafuata wajumbe na kuwaambia kama maneno ya Bush kuwa AMA UKO NA SISI AMA NI MPINZANI WETU. Na wakaonyesha jinsi ambavyo tayari wameshika nchi (kuchota hela BoT, Meremeta, Deep Green nk), mawaziri wote walitetemeka, itakuwa wajumbe wa NEC? Nani angelimpigia kura SALIM? FM are you jocking? Better you study much more about Mtandao.
Kuhusu yule dada wa Kinorway, masikini wa watu kasoma shule ya msingi Tanzania wala hakumaliza. Kakaondoka kakiwa kadogo na mzazi wake. Secondary na University kamesomea Ulaya kwa hela za Wanorway. Hadi sasa ni kuwa anamalizia shule na kaanza kutibu kwenye hospital za huko Norway. Ila asante yake kwao ni kuwa atarudisha gamba lao alilotumia kusoma ili arudi Tanzania kwenye nchi aipendayo. Hivyo usisingize kuwa alipiga magoti kwa Rajaab pale Wizarani ili aende akasome Norway!!!
Juu ya kutowapa Waarabu na Wahindi au Wasomali scholaship, you are VERY MUONGO. Na kama Mama anakupa asante kwa hili basi na yeye ni MUONGO pia. Kama huamni basi nenda kitivo cha computer pale UDSM, na uliza Dr mmoja Mwaarabu. Uliza kasoma wapi na kwa scholaship ipi na akiwa huko alikuwa akipata msaada wa Tanzania au lahh? Wakati nikisoma nje, alikuwepo Mhindi ambaye sasa yuko USA ambaye ni ndugu na akina Mohammed Interprise, alikuwepo Msomali ambaye sasa ni Dr. huko UK, alikuwepo Mmalawi. Wote hawa walikuja kwa scholarship kutoka Tanzania.
Juu ya kugawa scholaship kwa UBAGUZI, nakubaliana na wewe kuwa hilo liko Zanzibar au niseme lilikuwepo Zenji. Ni weusi tu walikuwa wakipendelewa na nafikiri hili hutaliona popote limeandikwa. Hii ilifanyika ili Mipingo nao wanyenyuke kwani huko Zenji wako chini sana. Kwa tanzania bara, si kweli. Ila pamoja na kufanyika huko, tena Tanzania bara maana ndiko wizara ipo, sijasikia kuwa Tanzania imekuwa nchi ya Kibaguzi. Sasa leo kikianzishwa kitu kama hicho na tena kwa muda ili Lami nao waanza kujua kufanya biashara basi tumeshakuwa wabaguzi? ACHA TUWE WABAGUZI. Dunia ikilalamika sana, mnaanza kuchukua na Wahindi/Waarabu. Hii ndiyo inasemwa "kuuma na kupuliza..." Kama Wayahudi vile.........Dunia hii inaenda namna hiyo na si KILOKOLE. Ndiyo maana Rais wa USA anaapa kulinda biashara za USA kwa amani na hata kwa NGUVU kama IKIBIDI. Sisi wetu na akina Mama, FMes, FM, ..... wanataka aape kulinda Interest zetu KILOKOLE. Kazi kweeli.
 
...you are VERY MUONGO. Na kama Mama anakupa asante kwa hili basi na yeye ni MUONGO pia

hahahahaaaaa, ukiona mtu kaanza kwenda personal kuna kitu behind the scenes. Kama unataka asante omba nitakuwekea kwa kujilazimisha huku nikiangalia pembeni lol!
 
Tatizo ndilo hili. Tunataka tupewe na sio tuwezeshwe. Badala ya kumpa lunch box ni bora kumuelimisha kuwa lunch box si lazima iwe na hamburgers bali unaweza kuweka maembe, mapapai na maziwa. Unaweza kumsaidia kwa kumweleza kuwa asijali lunch box ya mwenzake cha muhimu ni elimu na akifanikiwa, nae atawanunulia watoto wake lunch box na viatu vya Nike. Ni kumfahamisha kuwa pamoja na mwenzake kuwa na lunch box na raba mtoni hamzidi kitu kama binadamu na akijitahidi ataweza kumzidi.
Sera za kupewa zimejaribiwa sana na hazikutufikisha mbali. Hao wanakijiji wetu walichimbiwa visima na kuwekewa pump za Tanira. Kwa sababu walipewa, pamp hizi wakaziacha bila matengenezo hadi zikafa kabisa! Hao wananchi walipewa elimu ya bure lakini badala ya kuichangamkia baadhi yao wakaona ni wajibu wa serikali kuwapa hiyo elimu na kukataa kuchangia hata thumuni! Kama nilivyosema awali, nchi hii ilianzisha benki ya nyumba ili itoe mikopo nafuu kwa wananchi wake. Wananchi hao wakachukua mikopo, wakaolea wake wa ziada, wakanunua chenja, ili mradi wakafanya kila kitu ila kujenga nyumba. Na mikopo hawakurudisha. Benki hiyo sasa ni history. Si kweli kusema kuwa serikali haijafanya lolote kujaribu kumnyanyua mwananchi wake kutoka katika umasikini uliokithiri.

Unazungumzia uvuvi. Serikali hiyo hiyo ilianzisha Chuo cha Mbegani kuwasaidia wavuvi. Leo kiko wapi? Badala ya kutengeneza hizo mashua leo kinahifadhi timu za mpira.

Serikali hiyo hiyo ilianzisha vyuo vya maendeleo ( wakiiga mfano wa Folk Colleges za Scandinavia) sehemu mbalimbali kwa nia ya kuwapa elimu mbadala wanachi wake. Leo viko wapi?

Tanganyika Packers tuliibinafsisha. Tukashindwa ku-maintain standard zinazotakiwa za nyama za makopo na soko likayeyuka. Leo unataka tena serikali iingie katika biashara ya kusindika nyama? Kwa nini, kama mnaona kuna soko, msijikusanye na kuwekeza huko? Akija mgeni, akawekeza, mtamlaumu kuwa amependelewa!
Hivi unaamini kweli jawabu ni kuwapa wanakijiji hao matrekta? Vipi mafuta ya kuendesha hizo trekta? Vipi gharama za service za hayo matrekta? Vipi vipuri na gharama ya matengenezo yakiharibika? Au unadhani hao wakulima watakuwa na uwezo wa kukodi au kununua hayo matrekta? Watu ambao wanashindwa kununua chandarua cha shilingi 2000, leo mnataka wakodi trekta! Mnaujua kweli umaskini uliokuweko Tanzania au mnausikia redioni tu?

Katika yote mliyozungumza, hamjaweka bayana kuwa ni wapi serikali inamzuia mfanya biashara mtanzania mweusi kuwekeza. Sheria gani na sera gani zimewekwa ili kuhakikisha kuwa hawa hawaendelei kiasi cha kuhitaji sheria mbadala ya kuwakwamua!

FM,
Hapo kwenye NYEKUNDU ndipo hapo mie nasema MIPINGO WAPEWE. Wafundishwe kufanya biashara. Hivi Viwanda baadaye wapewe wao na hao Wahindi Wazawa au Waarabu sawa kwa sawa ikibidi kwa masharti kuwa Mipingo lazima wawe na share zaidi au sawa na hawa wengine. Ni hilo tu tunataka. Ila kwa hali ilivyo leo, wenzetu wanajua tayari kufanya biashara, kusaidiana, kubebana nk ila kwa hali ilivyo leo, Matumbi hawawezi kufurukuta. Nafikiri jana niliandika kuwa UKIWAPA vya BURE basi wataowa wake wengine na kuweka LCD ukutani na ikibidi kagari ka kutembelea na kumuoza kijana wake arusi ya milion 15 na kula mtaji wote.
 
Back
Top Bottom