Sera ya Vyuo Vikuu kubakiza wahitimu wenye ufaulu wa juu badala ya kuajiri wasomi walio- practice unaathri ubora wa elimu inayotolewa vyuoni

Watu upgrade sisi walimu wa sekondari twende kufundisha vyuo vya kati na vyuo vya kati wawe wanapanda waende kufundisha vyuo vikuu.
Unazifahamu sifa za kufundisha chuo kikuu? Tafuta hizo sifa uone kama unazo. Nijuavyo kufundisha ngazi ya sekondary au chuo cha kati siyo mojawapo ya sifa za msingi za kufundisha chuo kikuu
 
Kama ningewashauri serikali namna ya kuleta mageuzi katika elimu ya vyuo vikuu ningewaambia wafate model inayofanyika huko kwa vyuo vikuu vilivyotangulia. Kwenye hivyo vyuo vikuu waalimu wa vyuo vikuu hawaajiriwi kama njugu. Mwalimu wa Chuo Kikuu anapaswa awe mtu mkubwa sana, ili aitendee haki ile nafasi yake.

Wenzetu wanafanya hivi: kwa mfumo wa Western Universities na hata Easten huko Uchina, Japan, South Korea, Singapore, Indonesia, waalimu wa vyuo vikuu wanaitwa PIs (Principal Investigators). Principal Investigators ndio viini vya taaluma za vyuoni. Wanawajibika katika kuanzisha research agenda, kutengeneza research teams, kuattract research funding, kuhire research assistants kama postdocs na tecnicians, kurecruit PhD na Master students. Na kwa vile hawa watu watahitaji budget kubwa pale vyuo vinapotaka kuwaajiri hawaajiriwi kama njugu. Ni lazima itengwe initial budget ya kutosha kuajiri PI (wao wanaita seed funding) ili baadaye aweze kukiingizia chuo fedha zaidi kupitia grants atakazoattract. Department moja ya kitaaluma inaweza kuwa na PI 12 tu, halafu staff waliobaki ndani ya department wanafanya kazi chini ya hao PIs kwenye supporting roles. Ni ka mfumo ka ubepari vyuoni, lakini kako effective.

Hapa kwetu tunafanya tofauti. Mtu anaajiriwa kuanzia tutorial assistant (degree moja) hadi PhD. Wote hawa wanaajiriwa kupitia mfumo wa kawaida wa ajira serikalini. Akifika pale chuoni kama mwajiriwa mpya atapewa ofisi tu na courses atakazofundisha. Huyu mtu anatofauti gani na mwalimu wa sekondari? Wale tutorial assistants wataambiwa waende shule kwanza wapate masters. Ni utoto yaani, maana katika hiyo model hauwezi kupata excellence. Kama tunataka mabadiliko katika vyuo vyetu vikuu ni lazima mapinduzi yafanyike katika namna chuo kinavyoajiri wanataaluma wake. Lazima waajiriwe wanataaluma wachache wenye sifa na ubora wa juu kulingana na malengo ya chuo, lakini watakaowezeshwa vya kutosha ili wakiletee chuo tija katika malengo ya uwepo wa chuo hicho. Wenye sifa hizo wanaweza kupatikana kupitia uzoefu wao ndani na hata nje ya nchi.
 
Mbona kuna ofisi nyingi watu wanajitolea kufanya kazi ili kujiongezea umahili wa vitendo.Shida kama mnawaza kupiga pesa haraka haraka mtashindwa kupractise.
Unajitolea ukiwa na uwezo wa kujipandisha basi na kujilisha mchana 😂😂😂!!!

Kama ada ilikuwa inachangwa na kikao cha ukoo unadhani kujitolea ni rahisi mzee!?
 
You have a point brother! Sababu mie pia nimeenda fields mbili tofauti ila hakuna cha ajabu nilichojifunza! Zaidi niliishia kufanya kazi ya data entry tu kipindi natafta diploma ya IT na hapo ni TRA kikubwa tu niliasista kwenye installation ya kompyuta za Tancis zile!

Kwenye marketing ndio dah, hata sikumbuki la maana ni lipi! Ila ukinipa vitini niwamezeshe madogo madesa niko vizuri sana yani!
 
Elimu yetu sehemu kubwa ni theory, na walimu wetu ambao nao ni zao la theory wanafundisha bila hata ku-practice field husika, halafu eti tunatarajia tuweze kuwa na wahitumu wenye viwango! Itawezekana kweli?


✔✔💯%
 
Na ndiyo maana mtu anaajairiwa akiwa tutorial Assistant, na hapa hafundishi kabisa Bali anawasaidia tu ma lecture huku akijifunza. Then ataenda masters ambapo atajifunza zaidi kuhusu fani yake na kufanya utafiti, lakini pia ili awe lecture ataongeza PhD. So mpaka kufika huku kashaiva
 
Mleta mada ana PhD ila GPA zake kuanzia undergraduate sio nzuri. Ila mleta mada ana experience kwenye field yake. Mleta mada anapenda kazi ya kufundisha.
[emoji119][emoji119][emoji119][emoji119] hapa ndipo watu wanatafutaga sababu ili impe favor yeye.
 
Una wazo zuri ila kutekelezeka ndio ngumu hasa katika nchi za Africa.
Tangaza leo kazi ya chemical engineer mwenye PhD kama utapata.
Labda useme serikali ianzishe center of excellence moja halafu ichukue watafiti kokote kule duniani iwajaze hapo kitu ambacho pia haiwezi sababu haitaweza hata kuwalipa vizuri.
Ni bora tuendelee na mfumo huu huu wa kuajiri juniors halafu wakasome. Pia huo mfumo wa kubakiza kwa sasa haupo ajira huwa zinatangazwa na huyo mwenye GPA kubwa ashindane na wenzake.
 
Hoja ina mashiko tatizo ktk hizo field kunakuwa na shida ya ajira.
Wangeweza kuchukua waTZ wanaofanya ktk makpuni, taasisi au mashirika makubwa na kuwaomba kuja kufundisha kwa semester kama wanavyofanya vyuo duniani
 
Watu upgrade sisi walimu wa sekondari twende kufundisha vyuo vya kati na vyuo vya kati wawe wanapanda waende kufundisha vyuo vikuu.
Inawezekana kabisa ndugu regardless una gpa ya 3.8 undergraduate na 4.0 masters degree.
Kama mtu anavigezo na experience ya kutosha hakuna anaemzuia nikusubiri tangazo na kutuma maombi nashangaa mtoa mada anakuja kulia lia humu utadhani kuna mtu kamzuia kutuma maombi .
 
Ni vile tu watanzania hatupendi kubadilisha mifumo tuliyoizoea, na tunapenda kuishi kwenye comfort zones zetu. Tukipata kiongozi hata wa ngazi ya wizara mwenye maono na elimu ya juu na mwenye uthubutu kuubadlisha mfumo wa kitaaluma vyuo vikuu si ngumu kivile. Ni suala la kibajeti, pamoja na ushirikishwaji wa diaspora pamoja na watanzania wenye sifa waliomo nchini. Kuna watu hapa Tanzania ni maPI tayari na wanaendesha tafiti zao kwa mfumo wenye tija. Kuna mtu mmoja Dr. Joseph Ndunguru, huyu ni mtaalamu wa molecular biology na biotechnology zamani alikuwa MARI (Mikocheni Agricultural Research Institute) na ni PI wa ukweli. Ila eti undergraduate hakuwa na GPA ya 3.8 hivyo hakidhi sifa za kuajiriwa chuo kikuu! Utoto tu. Na bado kuna watanzania wa kutosha walio maPI huko nje ya nchi.

Unapobadilisha mfumo wa elimu ya juu ili kutengeneza maPI si lazima maPI wote wawe wazawa. Ujuzi na maarifa haviangalii uzawa, kabila au rangi. Weka fursa, weka dau, tangaza fursa duniani kote na kama mwenye sifa amepatikana kutoka Brazil mwache aje awe PI UDSM. South Africa wanarecruit ma PIs all over the world, US wanarecruit PIs all over the world, China (wacommunist wale) wanarecruit PIs all over the world, Botswana hivyo hivyo na sababu ni kwamba PIs ni watu highly skilled tena kwenye rare skills zinazohamasisha uchumi wa nchi kwa haraka, na watu wenye hizo skills wanaziuza kama biashara. Nchi ambazo zimebaki kuendesha vyuo vyao kama sekondari ndizo zimebaki kuwa nchi maskini na kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya kiwango cha ubora wa ujuzi na maarifa ngazi ya vyuo vikuu na kiwango cha uchumi wa nchi.
 
Kwani mwaka jana kulikuwa na uchaguzi?
Watu hawajui hata maana ya uchaguzi. Hivi kweli kilichofanyika mwaka jana nacho ni uchaguzi? Jamani! Kwani akili zenu zimeenda wapi? Ule hauna sifa ya kuitwa uchaguzi.
 
Kwa hiyo Prof kabudi ni sawa na judge sinde warioba au judge Julie, hutakuta mahali wamehukumu Kesi ila title zao ni kubwa
 
Kwa hiyo Prof kabudi ni sawa na judge sinde warioba au judge Julie, hutakuta mahali wamehukumu Kesi ila title zao ni kubwa
Warioba amekuwa Jaji wa Mahakama ya Afrika mashariki na Mahakama ya Kimataifa ya mipaka ya bahari (Special Tribunal on the law of the sea). Ukisoma kesi za hizi mahakama mbili utaliona sana jina la Jaji Warioba. Lakini Warioba ana jina kubwa kwasababu amewahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Tanzania.

Prof Kabudi yeye mbali na kuwa Corporate Counsel wa University of Dar-es-salaam, kufundisha na kuandaa machapisho mbalimbali: Hajawahi kufanya shughuli za uwakili sehemu yoyote ile kama wenzake wakina Rutinwa, Luoga na Fimbo.
 
Title ya ujudge, hata hivyo umetetea vyema learned counsel
 
Mkuu kwa sasa muongozo wa TCU ndiyo unafiatwa na vyuo vyote Tanzania. Nafasi hutangazwa na mwenye sifa huomba. Mambo yakubakizana yalikwisha. Vyuo hutangaza nafasi tofauti kuanzia tutorial assistant hadi full professor. Kila level ina qualification zake na kazi maalum ya kufanya. Waombaji hutoka nje ya chuo. Issue ni upatikanaji wa watu wenye sifa, je tunawatu wa kutosha?
Huko kwa wenzetu wanavitu viwili vikubwa 1. Research institutions nyingi katika nyanja tofauti na 2. Uwezo wa kulipa mishahara shindani kimataifa. Kwa hali hii wakitangaza kazi hupata watu wenye uzoefu au walomaliza degree za juu wakiwemo hao ma PI. Hapa kwetu hatuna phds wa kutosha (kumbuka phd ni research na academic degrees ). Hivyo vyuo lazima vijenge toka chini, yaani t.a. na hawa hupandishwa vyeo kwa vigezo maalumu na hopefully kila wanapopanda ujuzi huongezeka.
Kuhusu model yako ya PI ina tatizo ya kuwa huwezi kuitumia kwa kila nafasi na kila chuo. PIs basically ni waongoza utafiti fulani na siyo position kama ya uprofessor na ndio maana hata hapa kwetu kila research project huongozwa na PI. Ma PI huwa wameonyesha uwezo wa kuandika mradi na kuvuta hela za utafiti tofauti na kufundisha. Kama unahitaji mtu wa aina hiyo na wako wachache nchini kwako na huna pesa ya kulipa wa nje basi utakwama tu.
Lingine ni kuwa Tanzania iko nyuma sana tena saana kwenye kusomesha wataalamu tu wategemezi wa misaada na miradi. Wengi wa Masters na PhDs either ni private students au miradi kutoka nje hii inapunguza uwezo wetu wa kuzalisha wataalamu kama nchi. Hivyo hata hii model ya t.a hadi profesa inaface changa moto.
Mwisho naamini political will na commitment ndio dawa ya kutusogeza. All the best.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…