Serikali haitaki watoto wa Masikini wajue lugha ya Kiingereza?

Serikali haitaki watoto wa Masikini wajue lugha ya Kiingereza?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Hivi kuna mtu asiyejua umuhimu wa mtoto kufahamu lugha ya Kiingereza katika karne hii? Kuna mtu asiyefahamu kuwa shule za St. Kayumba ni kwa ajili ya watoto wa masikini?

Unajua kwa nini miaka ya nyuma vigogo wengi walikuwa wakiwapeleka watoto wao shule za Kenya?

Kwa asiyefahamu:
1. St. Kayumba ni kwa ajili ya maskini
2. Shule za English medium ni kwa ajili ya wenye hela. Ndiko wanakosomea watoto wengi wa vigogo.

Sisi tuliosoma St. Kayumba tunafahamu changamoto tuliyoipata miaka ya mwanzoni Sekondari. Silaha kubwa tuliyokuwa tukiitumia ilikuwa ni kukariri. Unahamisha maelezo ya kwenye daftari kama yalivyo, lakini tungeambiwa tuelezee kwa Kiswahili, tusingeweza. Tulikuwa tukikariri kwa mafanikio makubwa bila kujua tafsiri ya tulichokikariri.

Hiyo ndiyo changamoto wanayokutana nayo watoto waliotoka St. Kayumba. Na sijui kama hiyo changamoto itakaa ipatiwe ufumbuzi. Itapatiwaje ikiwa watoto wa watunga sera na wafanya maamuzi wanasoma kwenye shule zenye hadhi ya shule?

Pole ni kwa wale wasioweza kuwapeleka watoto wao shule za English medium.

Lakini kwa nini Serikali imeamua kuweka ubaguzi mkubwa kama huo? Naamini, kama shule zote nchini zingetumia "English" tokea chekechea hadi Chuo Kikuu, hali ingekuwa hivi:

1. Watoto wangejizoesha kusoma kwa kuelewa badala ya kukariri kama kunavyofanywa Sasa na wanafunzi wengi wa Sekondari

2. Viongozi wa Serikali na vigogo wengine wangehamasika kuwapeleka watoto wao shule za Serikali

3. Taifa lingejipatia wasomi wake wanaojiamini hata katika ngazi ya Kimataifa

4. Idadi ya Watanzania wanaofanya kazi na biashara Mataifa mbalimbali ingekuwa kubwa zaidi

5. Wakenya wansingewazodoa Watanzania na viongozi wao kuwa hawajui lugha ya Malkia.

Hivi Serikali haioni faida zote hizo? Inataka hizo fursa ziendelee kuwanufaisha watoto wa vigogo peke yao?
 
Watawala wanataka watoto wa masikini wawe wapiga kura tu tena wale wasiojielewa wanahongwa mataputapu,fulana na kofia na wake zao wanahongwa khanga, imetoka.
 
Umeeleweka vizuri kabisa kiongozi..hili sio sawa, tunataka shule zote toka Vidudu hadi Chuo Kikuu iwe kiingereza..NDIO ..

Tuanze sasa hatujachelewa ..tunaweza anza na shule 50 kila mkoa huku tunaongeza kila mwaka( maana inahitajikq resources za kutosha)
 
Nadhani ungeshauri sasa wafanyaje kutatua hiyo shida.

Process ya kubadilisha wameanza nadhani zipo baadhi ya shule wanzolipia au changia kidogo kwenye shule za serikali kwa msingi wenye kutumia kingereza.


Tatizo ni kuwa process yake ni ndefu sana maana kuna kuwarudisha shule walimu wote ambao ni karibia nusu ya wajiri wote wa Tanzania. Hapo kumbuka kufundisha mtu mzima ilivyongumu kunasa kingereza. alafu wafundishwe namna ya kutumia hicho kingereza darasani.
 
Huwa nashindwa kuelewa kwanini tumeamua lugha yetu ya taifa iwe Kiswahili....Hii lugha ina umuhimu gani hasa?? tena ukizingatia sisi nchi yetu ndio hii hii ambayo hatujitegemei kwa lolote!!
 
Sio lugha ya kingereza uliza kwanini serikali haitaki watoto wapate elimu yenye tija.

Utakuja gundua serikali inapenda kundi kubwa la wajinga ili waendelee kuwatawala.

Elimu ya kuhamisha vitu kwenye kitabu kwenda kwenye karatasi ya mtihani imefanya tumekuwa na PhD wapumbavu Masters wapumbavu. Angalia tunaowaita wasomi mahali walipo tufikisha leo
 
Mwalimu mwenyewe anayemfundisha mwanafunzi hajui kingereza unategemea mwanafunzi kujifunza nini? Kwa kifupi kama tutaamua kubadilisha mfumo wa elimu na walimu pia wabadilike. Walimu wengi ni mambumbumbu waliofeli shule.
 
Ujinga/upumbavu wetu, subiri uchaguzi ndo utaamini...
 
Huwa nashindwa kuelewa kwanini tumeamua lugha yetu ya taifa iwe Kiswahili....Hii lugha ina umuhimu gani hasa?? tena ukizingatia sisi nchi yetu ndio hii hii ambayo hatujitegemei kwa lolote!!
Hatukuamua sisi, waliamua wao!
 
Mimi niliapa ingali nipo hai watoto wangu hatosoma hizi shule za elimu bure.

mimi naona kwa suala la kuandaa watu kujitegemea somo la kipaumbele namba moja ni Hesabu.
Watu ambao wamekosa msingi wa hesabu ni vigumu kufikiri na kuchambua mambo vizuri na ndio changamoto kubwa inayotukabili
Natamani Roho mtakatifu atupe maono ya kulipatia uvumbuzi kwani hali ni mbaya sana hasa huko msingi kwani hakuna waalimu wa hesabu kabisa. sijui kwa nini watu hawashtuki kusikia kila mwaka Hesabu inaongoza kwa kufelisha?
 
Umeeleweka vizuri kabisa kiongozi..hili sio sawa, tunataka shule zote toka Vidudu hadi Chuo Kikuu iwe kiingereza..NDIO ..

Tuanze sasa hatujachelewa ..tunaweza anza na shule 50 kila mkoa huku tunaongeza kila mwaka( maana inahitajikq resources za kutosha)
Serikali ikitaka hata kesho shule zote ziwe English medium inawezekana sababu vitabu vipo na walimu wapo

Hao wanaofundosha shule za English medium wamesoma vyuo vyetu hivi hivi vya ualimu

Ni jeuri tu ya serikali wabunge watoto wao hawasomi kayumba,mawaziri akiwemo wa elimu hawasomi kayumba viongozi wote akiwemo Raisi waJukuu hawasomi kayumba sasa hizo shule za kayumba hada wanamlenga nani wasivyokuwa na haya usoni loo

Shule zote ziwe English medium full stop
 
Umeeleweka vizuri kabisa kiongozi..hili sio sawa, tunataka shule zote toka Vidudu hadi Chuo Kikuu iwe kiingereza..NDIO ..

Tuanze sasa hatujachelewa ..tunaweza anza na shule 50 kila mkoa huku tunaongeza kila mwaka( maana inahitajikq resources za kutosha)
Kwani resources ni tatizo basi mkuu? Maamuzi tu! Serikali ikiamua na resources zitapatikana. Mbona za kujengea shule za Kata ziliweza kupatikana ndani ya muda mfupi?
 
Hivi kuna mtu asiyejua umuhimu wa mtoto kufahamu lugha ya Kiingereza katika karne hii? Kuna mtu asiyefahamu kuwa shule za St. Kayumba ni kwa ajili ya watoto wa masikini?

Unajua kwa nini miaka ya nyuma vigogo wengi walikuwa wakiwapeleka watoto wao shule za Kenya?

Kwa asiyefahamu:
1. St. Kayumba ni kwa ajili ya maskini
2. Shule za English medium ni kwa ajili ya wenye hela. Ndiko wanakosomea watoto wengi wa vigogo.

Sisi tuliosoma St. Kayumba tunafahamu changamoto tuliyoipata miaka ya mwanzoni Sekondari. Silaha kubwa tuliyokuwa tukiitumia ilikuwa ni kukariri. Unahamisha maelezo ya kwenye daftari kama yalivyo, lakini tungeambiwa tuelezee kwa Kiswahili, tusingeweza. Tulikuwa tukikariri kwa mafanikio makubwa bila kujua tafsiri ya tulichokikariri.

Hiyo ndiyo changamoto wanayokutana nayo watoto waliotoka St. Kayumba. Na sijui kama hiyo changamoto itakaa ipatiwe ufumbuzi. Itapatiwaje ikiwa watoto wa watunga sera na wafanya maamuzi wanasoma kwenye shule zenye hadhi ya shule?

Pole ni kwa wale wasioweza kuwapeleka watoto wao shule za English medium.

Lakini kwa nini Serikali imeamua kuweka ubaguzi mkubwa kama huo? Naamini, kama shule zote nchini zingetumia "English" tokea chekechea hadi Chuo Kikuu, hali ingekuwa hivi:

1. Watoto wangejizoesha kusoma kwa kuelewa badala ya kukariri kama kunavyofanywa Sasa na wanafunzi wengi wa Sekondari

2. Viongozi wa Serikali na vigogo wengine wangehamasika kuwapeleka watoto wao shule za Serikali

3. Taifa lingejipatia wasomi wake wanaojiamini hata katika ngazi ya Kimataifa

4. Idadi ya Watanzania wanaofanya kazi na biashara Mataifa mbalimbali ingekuwa kubwa zaidi

5. Wakenya wansingewazodoa Watanzania na viongozi wao kuwa hawajui lugha ya Malkia.

Hivi Serikali haioni faida zote hizo? Inataka hizo fursa ziendelee kuwanufaisha watoto wa vigogo peke yao?
Mm sidhani km lugha ya kiingereza ndio muhimu ila elimu inapaswa kutolewa kulingana na mazingira ya sasa mitaala yetu haiendani na mazingira ya sasa kabisa..

Nchi km malawi, zambia, uganda, rwanda kwa sasa na nyingine nyingi zinatumia kiingereza kifundisha since kindergarten ila bado kiuchumi tumewapita.
 
Kiingereza siyo maarifa. Kwanza tuendako AI itakuwa inatafsiri kila kitu. Unaongea kiswahili mtu anasikia kiingereza and vice versa. Unasoma gazeti au kitabu cha kiingereza yenyewe inafasiri. Unasikiliza movie ya kiingereza lakini unasikia kwa kiswahili. Tuwekeze kwenye hii technolojia.
 
Back
Top Bottom