Serikali: Hatujapokea taarifa rasmi kuhusu ufugaji hatarishi wa kuku Broila

Serikali: Hatujapokea taarifa rasmi kuhusu ufugaji hatarishi wa kuku Broila

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
1663329311708.png

Serikali imethibitisha kutopokea taarifa rasmi ya utafiti unaoonesha wafugaji wa kuku wanatumia dawa za antibayotiki na hivyo kiasi kikubwa cha dawa hizo kuonekana kwenye maini, kisha kuwa na madhara kwa watumiaji wa kitoweo hicho kwa kusababisha usugu wa vimelea vya dawa.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki kwenye mahojiano maalum amethibitisha hilo na kusema amewaelekeza wataalam kutoka wizarani kuipata taarifa hiyo na kuifanyiakazi ili kuwaepusha watumiaji na madhara.

Chanzo: Azam TV

Kuhusu Utafiti soma:
Utafiti: Kuku wa kisasa kwenye Manispaa za Ilala na Kinondoni wana kiwango kikubwa cha dawa za kuua Bakteria
 
Ndo maana mahoteli ya kitalii hapa Zanzibar hayapokei kuku broiler wanaofugwa na wenyeji.
 
Unaweza kukuta ni utafiti tu umefanywa sehemu ambao bado haujatoa picha halisi ilivyo, ndo maana waandishi wa habari wanatakiwa kuwa makini na namna wanavyoripoti taarifa za kitafiti ili kuepusha taharuki miongoni mwa jamii......ni sawasawa na ile ya maji ya maiti na samaki.
 
hivi siku nikipata kisonono na kaswende Mke wangu ataniamini kweli kua nimepata huko ?🤔
 
Serikali imethibitisha kutopokea taarifa rasmi ya utafiti unaoonesha wafugaji wa kuku wanatumia dawa za antibayotiki na hivyo kiasi kikubwa cha dawa...
Huo uchunguzi uharakishwe kabla madhara hayajakuwa makubwa...
 
Back
Top Bottom