Serikali hujifanya kiziwi haki ya wananchi ikidaiwa kwa taarifa za media au maandamano, sasa migomo ndio iwe lugha mpya kwa Serikali hadi kieleweke!

Serikali hujifanya kiziwi haki ya wananchi ikidaiwa kwa taarifa za media au maandamano, sasa migomo ndio iwe lugha mpya kwa Serikali hadi kieleweke!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Naunga mkono asilimia 100% mgomo wa wafanyabiashara. Tena ningependa kuona ukienea nchi nzima!

Sababu ni kwamba uongozi wa Tanzania huwa unajifanya kiziwi pale Watanzania wanapoonyesha kutopendezwa na jambo fulani, na kutoa madai yao kwa njia ya vyombo vya habari au maandamano. Serikali imejengea tabia sugu ya kutosikiliza wananchi.

Wananchi wamefikia hatua ya kudai haki zao hata kwa kutukana, na kwa kuwa hawasikilizwi wanamtukana hadi Rais wakidhani labda kwa njia hiyo watasikilizwa. Ndio kwanza waambia mimi chura siwasikilizi.

Sasa iliyobaki ni migomo. Lazima tuweke mfumo wa kugoma, iwe ni mishahara au huduma. Tukiiambia serikali BRT iboleshwe wasisikie, basi tugome kutumia BRT. Tukiseme TRA wanatuumiza wasisikie, basi tutafute namna ya kugoma!

Tuanzishe mifumo ya ushirika iliyo na nguvu ya kusimamia migomo, iwe ni biashara au vyama vya wafanyakazi katika ngazi mbalimbali. Tuanze kugoma hadi kieleweke.

Tukiwaambia Poilisi msitusumbue barabarani kutufanya tusubiri muda mrefu ili kiongozi apite, kama hawasikii, siku nyingine tugome kuupisha msafara wa kiongozi. Tuanzishe umoja wa watumiaji wa magari barabarani.

Tugome, tugome, tugome hadi serikali iwe na masikio ya kutusikiliza tunapotoa kero zetu

Pia, soma=> Nguvu ya Umma: Bunge lalazimika kubadilisha Muswada wa Sheria ya Fedha baada ya maandamano ya Wananchi
 
Hakuna haja ya kuchekacheka na wapumbavu, hasahasa hawa wapumbavu wanaojiita chawa hawatakiwi kupewa nafasi kabisa, ndiyo wanarudisha maendeleo nyuma.
 
Hakuna haja ya kuchekacheka na wapumbavu, hasahasa hawa wapumbavu wanaojiita chawa hawatakiwi kupewa nafasi kabisa, ndiyo wanarudisha maendeleo nyuma.
Serikali ya ajabu sana hii, inaongozwa kwa kusikiliza hawa chawa wanasema nini!
 
Hawapo wa kugoma wiki mfululizo.
Serikali inawachekea mnaona mnaimudu. Serikali ni dude lenye mabavu.

Rais anaiheshimu serikali na waliobaki wanaogopa serikali.

Ukigomea msafara wa rais, makam na pm unapelekwa kuzimu dk hiyo hiyo.

Serikali ikiwa siriaz na kukusanya Kodi bila kucheka na wakwepa Kodi hakuna wa kuitisha tena.

Ukifirisika anaibuka mwingine.

Wewe ndo utafirisika sio serikali.
 
Acheni hujuma...Serikali imejitahidi kusikiliza madai yote ya wafanyakazi. Kuna baadhi ya watendaji wabovu tu walioaminiwa na serikali ndiyo wenye shida na Mh. Rais amekuwa mwaminifu sana kuwaondoa wote ambao public imeonyesha kugoridhika nao, what else do you want the government do?

Kilichobaki no kuacha uchawa makazini na kutoa maoni yenu Ili yatimizwe na wahusika
 
Baada ya kudai kile kilicho itwa uhuru wa mtu mweusi,Mtu mweusi alijikuta kaingia kwenye Ukoloni mbaya zaidi wa mkoloni mweusi.

Tanzania inaumizwa na kundi la wachache,wajionao wenye nchi.
 
Hawapo wa kugoma wiki mfululizo.
Serikali inawachekea mnaona mnaimudu. Serikali ni dude lenye mabavu.

Rais anaiheshimu serikali na waliobaki wanaogopa serikali.

Ukigomea msafara wa rais, makam na pm unapelekwa kuzimu dk hiyo hiyo.

Serikali ikiwa siriaz na kukusanya Kodi bila kucheka na wakwepa Kodi hakuna wa kuitisha tena.

Ukifirisika anaibuka mwingine.

Wewe ndo utafirisika sio serikali.
Kugomea msafara wa raisi au PM sio individual move. Ni move lazima ifanyike kwa kuwa coordinated. Na mara nyingine tu kuiambia serikali tutagomea kupisha msafara wa raisi kwa sababu ya usumbufu mnaotunfanyia kutuweka barabarani masaa mawili kama vile sie hatuna kitu cha maana cha kufanya, ujumbe utakuwa umefika na watarekebisha
 
Acheni hujuma...Serikali imejitahidi kusikiliza madai yote ya wafanyakazi. Kuna baadhi ya watendaji wabovu tu walioaminiwa na serikali ndiyo wenye shida na Mh. Rais amekuwa mwaminifu sana kuwaondoa wote ambao public imeonyesha kugoridhika nao, what else do you want the government do?

Kilichobaki no kuacha uchawa makazini na kutoa maoni yenu Ili yatimizwe na wahusika
Na kwa nini wahusika hadi tuwalalamikie ndio watende kile ambacho ni wajibu wao wanapaswa kutenda bila kusukumwa? Kwa mfano, hawaoni kero za wananchi BRT? Hawaoni vifo vinavyotokea barabarani kwa sababu TANROADS hawatimizi wajibu wao angalau kufukia tu mashimo? Hawaoni hospitali zetu hazina madokta wa kutosha wakati wapo ambao hawana ajira?
 
Mgomo hata hii ya CHADEMA,watawala hawawezi kusikia kama hai-disrupt social order .............mfano CHADEMA wanafanya mgomo DSM kwa siku moja tu then wanahamia Mbeya, huwezi kuishinda serikali unabaki kuipa sifa kwenye macho ya media za kimatafifa kwamba,utawala uliopo unatoa haki ya kujieleza via maandamano, Ukifanya maandamano mfano kwa wiki nzima jiji la DSM,utakwamisha baadhi ya mambo, watawala watakusikiliza tu........
 
Mgomo hata hii ya CHADEMA,watawala hawawezi kusikia kama hai-disrupt social order .............mfano CHADEMA wanafanya mgomo DSM kwa siku moja tu then wanahamia Mbeya, huwezi kuishinda serikali unabaki kuipa sifa kwenye macho ya media za kimatafifa kwamba,utawala uliopo unatoa haki ya kujieleza via maandamano, Ukifanya maandamano mfano kwa wiki nzima jiji la DSM,utakwamisha baadhi ya mambo, watawala watakusikiliza tu........
Hakuna serikali ya watu wenye akili inapenda itoke kwenye media kwamba watu wake wamegoma. Kama hii yetu sio wapumbavu basi watasikia pia. Kugoma ni kuifedhehesha serikali, hata kama ni kwa siku moja. Ukitaka kujua, siku moja mke muudhi mkeo akuambie anagoma kulala chumba kimoja na wewe analala kwa watoto, uone kama mgomowa siku moja ni fedhaha au sawa tu
 
Back
Top Bottom