Serikali Iachane na Uwekezaji Unaotarajiwa Kufanywa na DP World Kwenye Bandari Yetu

Serikali Iachane na Uwekezaji Unaotarajiwa Kufanywa na DP World Kwenye Bandari Yetu

Dan Zwangendaba

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2014
Posts
5,814
Reaction score
8,118
Binafsi nikiri kwamba sijauona huo unaoitwa Mkataba au MOU (Intergovernmental Agreement, IGA) hivyo siwezi kutoa hoja zozote za kitaalam ikiwa mkataba au hiyo MOU ni nzuri au mbaya. Hata hivyo, kwa kuzingatia watanzania hawa wa leo, ambao walikaa miaka 10 chini ya uongozi wa Mhe. Jakaya Kikwete, kisha wakaishi miaka takribani 6 chini ya uongozi wa Mhe. John Magufuli, na "public outcry" iliyopo huko mitandaoni na mitaani, mimi nadhani BUSARA KUU kwa Serikali kwa Sasa ni kuachana na uwekezaji unaotarajiwa uufanywa na DP World kwenye bandari ya Dar es Salaam, hata kama uwekezaji huo una FAIDA kwa nchi.

Bila shaka, nchi itaendelea kuwepo pasipo uwekezaji wa DP World au pasipo uwekezaji wowote bandarini, lakini imani ya wananchi kwa Serikali yao ndio msingi wa Umoja, Amani na Mshikamano wa Taifa lolote duniani. Kwa sasa, approval rate ya serikali ya Samia kwenye jambo hili ni mbaya sana.

Kinachojadiliwa mitandaoni na mitaani, bila kujali kama ni kweli au sikweli, lakini ukweli unabaki kuwa havina afya kwa Serikali, havina afya kwa Rais Samia, na havina afya kwa Umoja wetu kama Taifa. Approval rate ya wananchi kwa Serikali na kwa Rais wao ni jambo muhimu sana. Ndiyo maana, kila pahali kuna mabango ya kusifu uongozi Rais, au matukio mubashara na recorded ya kusifu uongozi wa Rais, ni vipi tunaruhusu Serikali kufanya action kubwa yenye kushusha imani ya wananchi kwa Mhe. Rais na Serikali yake kwa kiwango hicho?

Na bahati mbaya, wanaoendesha mijadala ya kutoelewa na kutokubaliana na mkataba au uwekezaji huo huku mitandaoni na majukwaani si kundi dogo, au la wasiosoma. Karibu watanzania wote bila kujali kiwango chao cha elimu au makabila yao wameonyesha kutokubaliana na uwekezaji wa DP World, maana haueleweki na serikali imeshindwa kutoa maelezo yenye ushawishi kwa wananchi.

Nimalizie kwa kusema, pamoja na uchumi kuonekana kufunguka, lakini bado hali za wananchi ziko duni na makundi mengi yana makovu kwa sasa. Si vema kwa Serikali kufanya matendo ambayo yanaamsha hisia za wenye njaa, hata kama matendo hayo yataleta chakula baadaye kwa makundi hayo. Hakuhitaji tukio kubwa sana ili kusababisha kuvunjika kwa amani kwenye nchi yoyote, na infact, viongozi husika huwa hawaamini kama tukio fulani linaweza kubadilisha historia ya nchi hiyo. Mkataba au ushirikiano huu ni wazi haujaeleweka na umekuja wakati si muafaka, Serikali iachane nayo kwa sasa HATA KAMA UNA FAIDA kwa nchi.
 
Afadhali aje mwekezaji.

Kama mimi Mtanzania nikiagiza gari natumia pesa nyingi kuliko Mzambia ambaye bandari si yake kuna faida gani?

Nimewasaidia Wazambia na wa Zimbabwe kumalizia process za kupata magari yao kutoka Japan.
Nilipowahoji nikaona Tanzania tuna ushenzi, hatuna serikali.

Mzimbabwe mmoja nilimwoji ni kiasi gani cha tax atachajiwa na serikali yake mpaka gari anaitumia rasmi ? Akasema around milioni 1.2 - 2 hivi za Kitanzania . Ile gari kwa aina yake ukiagiza Mtanzania kodi ni kama milioni

8-10 za Kitanzania
 
Huna hoja nchi isipate faida kwasbb ya kelele za hao watanzania wasio weza hata kujilipia ada za shule na matibabu serikali inatafuta pesa ili ilipie ada na kutoa matibabu ya raia hao hao wapiga kelele.
 
Dear Tanzania Police and Military,

I am writing to you today with a heavy heart. As citizens of Tanzania, we are deeply concerned about the recent decision to give our ports and airports to foreign companies. This is a betrayal of our trust and a threat to our national security.

Our ports and airports are vital to our economy. They are the gateways to our country and the channels through which our goods and services flow. They are also essential for our national security. They allow us to import essential goods and equipment, and they allow us to project power and influence in the region.

The decision to give our ports and airports to foreign companies is a reckless and irresponsible act. It will make us more vulnerable to economic and political pressure from foreign powers. It will also make it easier for terrorists and other criminals to enter our country.

We call on you, the Tanzania Police and Military, to stand up for our country. We urge you to use your power and influence to protect our ports and airports from foreign control. We also urge you to investigate the decision-makers who made this reckless and irresponsible decision.

We the people of Tanzania demand that our ports and airports remain under our control. We will not stand for this betrayal of our trust. We will not allow our country to be sold off to foreign interests.

Sincerely,

The Concerned Citizens of Tanzania
 
Wadau huwa nawasikia baadhi ya viongozi wakidai Serikali ya Awamu ya 6 Ya MAMA ni SIKUVU. Najiuliza toka Suala la BANDARI vs DP WORLD limeibuka WANANCHI wamekuwa WAKIPINGA sana na leo Wamefanya MAANDAMANO ya AMANI KUPINGA Suala hilo. Tumewasikia VIONGOZI wa Dini Vyama vya SIASA wasomi na Watu mashuhuri Wakipinga.

Najiuliza USIKIVU wa SERIKALI upo Wapi? Hebu SERIKALI iwasikilize kile Wanachotaka WANANCHI kama kweli ni SIKIVU iache Ubabe kwani UBABE wa SERIKALI na BUNGE ktk HILI hauna TIJA kwa TAIFA.

Tanzania ni Yetu sote na Raslimali ni zetu sote
 
Wenye nchi ni masikni, hawajitambui wanaburuzwa

Mwarabu anauziwa nchi ili watanganyika wawe wakimbizi ndani ya nchi yao
 
Ni nyinyi tu humu mitandaoni, mitaani tumeshaanza kutuma maombi ya kazi hata wakati wa uchaguzi, huwa tunaaminishwa CCM itashindwa
 
Wenye nchi kina wepi...siye tukipewa buku ten tunaomba na kucheza CCM mbele Kwa mbelee! We kaka wewe!
 
Ndo ndoto zenu wakenya ili muendelee kutawala sekta ya Bandari Afrika Mashariki sio? Wafikishie salamu hapo Nairobi kuwa gari ishaanza safari, haturudi nyuma!!
 
Back
Top Bottom