KERO Serikali iangalie jinsi ya kuondoa kero ya moshi karibu na Uwanja wa Nyamagana, Mwanza

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

KwetuKwanza

Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
82
Reaction score
150
Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.
Uwanja wa Nyamagana ambao upo katikati ya Jiji letu la Mwaka ni moja ya sehemu ambayo inatukutanisha Wadau wengi wa michezo hasa mchezo wa miguu.

Pamoja na maboresho ambayo yamefanyika uwanjani hapo lakini bado changamoto ni suala la moshi unaotokana na mapishi unaotawala eneo hilo mara nyingi hasa mida ya jioni.

Uwanja huo uliozungushiwa ukuta kwenye upande wake wa Kusini kuna shughuli za Wafanyabiashara wa dagaa ambao wanakaanga dagaa kwa nishati za kuni, hivyo kusababisha moshi mwingi kusambaa hewani na kuwa kero kwa watu wanaopita na kufanya shughuli zao kuzunguka eneo.

Kuna kipindi waliondolewa eneo hilo kwa kuwa ni karibu na reli lakini waliporejea hali imekuwa changamoto kwa watu wengine, kwani mbali na Uwanja pia ni karibu na Shule ya Msingi Nyamagana.

Wakati wa mechi au matukio mengine hasa michezo inayohusisha timu ya Pamba Jiji FC inayoshiriki Ligi Kuu pamoja na timu nyingine zinazoutumia uwanja huo hali ya hewa huwa ni changamoto kutokana na moshi kuwa kero na kuwaumiza baadhi ya Watu uwanjani hapo.

Mamlaka zinafahamu kuhusu tatizo hilo lakini zimekuwa kimya kutokana na hulka za Kisiasa kwasababu kundi hilo la Wafanyabiashara waliondolewa kwenye eneo hilo ili kupisha upanuzi wa eneo la ujenzi wa Reli ya Kisasa SGR lakini watu hao walirudi kimyakimya na kufanya eneo hilo ambalo linazungukwa na ofisi nyeti zikiwepo za Uhamiaji, TANROADS, TTCL na Posta.

Nashauri jambo hilo litafutiwe utatuzi, kuna watu watakuwa hawaendi uwanjani kutokana na moshi kuwa mwingi na hivyo ama kuwakera au kuwaumiza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…