Serikali ibane matumizi wakati huu wa dharura

Serikali ibane matumizi wakati huu wa dharura

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Amani iwe Kwenu

Benki kuu (BOT) imeshatoa takwimu kuonesha mfumuko wa bei umeongezeka kwa zaidi ya asilimia 1 ndani ya miezi michache. Sasa mfumuko unafikia asilimia 4 na ushei.

Dunia nzima sasa inaputia wakati mgumu kiuchumi hususan kipindi hiki cha mtanange wa kule Ukraine.

Kwa serikali inayojali ustawi na hali bora za raia wake inawajibika kuangalia kwa tahadhari mwenendo wake wa matumizi hasa kuweka umhimu kwenye kukabilii ukali wa maisha unaozidi kupanda kila siku. Kuna mambo ambayo tunaweza kuyazingatia au kuyafanyiakazi katika kuikabili hali hii ngumu

1. KUBANA MATUMIZI
Serikali ibadili vipaumbele vya matumizi yake hasa izingatie ununuzi wa bidhaa kutoka nje hususani usafiri, samani na mahitaji ya kiteknoljia yazingatie ukwasi uliopo na kupunguza kutumia sana dola ili iweze kuwa na hifadhi ya kutosha

2. DHAHABU
Serikali itunge sheria ya kuiwezesha BOT kuanzisha hazina ya dhahabu ambapo iweze kuwa na hifadhi yake ya dhahabu ambayo itatumika rasmi kama kigezo cha ukwasi sambamba na foreign currency

3. MISHAHARA NA POSHO
Serikali iboreshe mishahara ya wafanyakazi wake iendane na uhalisia wa kukabili mfumuko wa bei ambao imeshindwa kuudhibiti kwa sababu ya kuwafuta machozi wafanyabiashara wa mafuta ambao walibanwa vilivyo na regime iliyopita

Serikali iondoe utitiri wa masurufu na posho kwa shughuli za kiofisi za watendaji wake na kupunguza msururu wa idadi ya delegates wanaosafiri nje. Mabalozi watimize wajibu wao kwa sababu itasaidia kubana matumizi

4. MIRADI
Serikali itathmini miradi yake ya kimkakati iendane na mahitaji makuu ya kimsingi. Kwa mfano ujenzi wa moundombinu ni muhimu sana kutokana na jiographia ya nchi yetu lakini kununua ndege mpya sidhani kama mradi huo una umuhimu mkubwa kwenye kipindi hiki. Pesa ipelekwe kwenye kununua chakula,mafuta na madawa ili kuhakikisha taifa halitetereki kwenye kipindi hiki kigumu

5. TRADE
Serikali ipeleke muswada wa dharura bungeni unaohusu masuala ya exports ambapo sheria iweke unafuu na kuwapatia ruzuku wafanyabiashara wanaosafirisha bidhaa nje.

Serikali iimarishe ulinzi wa sheria za kibenki ambapo akaunti za wafanyabiashara zisigeuke fimbo za kuwachapia na wanasiasa. Wataalam wa fedha hapa waumize kichwa kuhakkkisha usalama wa wawekezaji nchini unaanzia kwenye mazingira hadi ulinzi wa mitaji yao benki.

Muswada wa uanzishaji wa viwanda na biashara nchini uendane na hitaji ya soko la dunia. Kwa mfano hivi leo mitishamba ama tiba mbadala zina demand kubwa duniani hivyo uchakataji, uhifadhi na usafiri wake uzingatie I.S.O. na serikali kisheria ifabikishe hilo ili kuongeza forex ndani ya nchi

6. KODI
Serikali irekebishe sheria ya kodi kwa kuondoa msururu wa kodi kwa muda ili kussidia startups na kodi hizi zihusu startups peke yake lakini iweke kiwango nafuu kwa kodi ili wananchi walipe kwa ufahari ambapo tofauti na sssa kodi inawabana koo Watanzania na Wafanyabiashara

7. VITUO VYA UTAFITI
Serikali ianzishe vitengo vya utafiti aina mbalimbali ndani ya majeshi yetu na iruhusu raia kupeleka mawazo ama tafiti zao huko ili kufanikisha uvumbuzi ama maboresho ya bidhaa zenye tija kwa jamii...

Msanii
 
VITUO VYA UTAFITI
Serikali ianzishe vitengo vya utafiti aina mbalimbali ndani ya majeshi yetu na iruhusu raia kupeleka mawazo ama tafiti zao huko ili kufanikisha uvumbuzi ama maboresho ya bidhaa zenye tija kwa jamii...
A word
 
Amani iwe Kwenu

Benki kuu (BOT) imeshatoa takwimu kuonesha mfumuko wa bei umeongezeka kwa zaidi ya asilimia 1 ndani ya miezi michache. Sasa mfumuko unafikia asilimia 4 na ushei...
Haya umesema wewe.

Soma magazeti ya kila siku utatambua wapi tuliko na tunakoenda. Waandishi nao mnatuzingua. Sifa Sifa hadi Musifa.

Wanasema mama ameifungua Tanzania!? Kweli? Ilifungwa na Nani?Sifa zimezidi na ndio hapo kunaharibika kwani wamekuwa walaji watupu.

Kama kupiga basi acha waendelee kupiga.
 
N
Haya umesema wewe.
Soma magazeti ya kila siku utatambua wapi tuliko na tunakoenda. Waandishi nao mnatuzingua. Sifa Sifa hadi Musifa..
Nimeacha kusoma magazeti na kufuatilia media houses za bongo.

Updates zangu nyingi zinatoka hapa JF, sosho midia na tafiti zangu
 
Big up kw Sana
1. bajet 90%+ulaji, only 9% maendleo.

2. Mishahara kima ch chni midogo kliko posho ya ck ya viongozi.

3 misafara misururu mifefu inayokula fedha bila sababu.

4 faini kuwa kubwa knasabbisha rushwa. km. traffic offense fine inaruhusu mkosaji ktoa rushwa aachliwe.

5 Kodi z biashara Makadirio badla kuchaji toka faida ilopatkana.

6 wahsika ktk tra kusumbkia rushwa ktk sehemu z biashara badla kuwa na mfumo unao jiendesha wa ukusanyaji.

7 maruprup na posho makbw za viongozi wanaostaafu na walostaafu znazoongezka kila wkt - mawazr, maaskari, Marais, majaji.

8 kungekuwa na uwiano unao eleweka kati ya bajet ya Maendleo na ya Kawaida. kw jinsi ilivo ni kama vile maendleo wameachiwa Hao wanaotupa mikopo (90% kawasaki 9% maendleo!).

10 viongzi w kisiasa kusafiri/ziara sana bila sbb...nk
inaelekea wanapopanga bajeti wanaulizana... "hapa tujiwekee ngapi?"
 
VITUO VYA UTAFITI
Serikali ianzishe vitengo vya utafiti aina mbalimbali ndani ya majeshi yetu na iruhusu raia kupeleka mawazo ama tafiti zao huko ili kufanikisha uvumbuzi ama maboresho ya bidhaa zenye tija kwa jamii...
Kwann ndani ya majeshi na siyo vyuo vikuu?

Mkuu hivi unawafahamu vyema aina ya watu wanaojiunga na jeshi ?
 
Kwanza sikubaliani na hiyo takwimu kuwa mfumuko wa bei ni asilimia 4...mfumuko wa bei kwa sasa ni double digit ndiyo hali ya mtaani na duniani....tunadanganya kuficha kitu gani?wananchi wanaumia mjue
 
Kwann ndani ya majeshi na siyo vyuo vikuu?

Mkuu hivi unawafahamu vyema aina ya watu wanaojiunga na jeshi ?
Usihofie hali hiyo kwa sababu mwisho wa nyakati tutaunda jeshi lenye personels wanaoweza kuvunja tofali kwa akili na siyo kwa kichwa
 
Wasiagize yale mataka taka yao Vieti wanayoyaamini kuliko kitu kingine chochote...yaani gharama yake ni madarasa kadhaa au Zahanati moja wahuni wanaipitisha ili wale bata tuu hakuna kingine...
 
Kwanza sikubaliani na hiyo takwimu kuwa mfumuko wa bei ni asilimia 4...mfumuko wa bei kwa sasa ni double digit ndiyo hali ya mtaani na duniani....tunadanganya kuficha kitu gani?wananchi wanaumia mjue
Mama yangu alikuwa anapata allowance ya laki tano kwa mwezi lakini sasa hivi hunipigia kuniariu kuwa pesa hiyo haitoshi hata kabla ya tarehe 15.
 
Back
Top Bottom