SoC01 Serikali ifanye nini kukuza uchumi wa viwanda nchini na kutengeneza ajira

SoC01 Serikali ifanye nini kukuza uchumi wa viwanda nchini na kutengeneza ajira

Stories of Change - 2021 Competition

Mwamba 777

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
2,055
Reaction score
3,535
Ili kukuza uchumi wa viwanda nchini na ili viwanda viendelee kuwepo, kuzalisha na kutengeneza ajira kwa watanzania ni lazma yafuatayo yatekelezwe;

Kuwekeza kwenye kilimo cha umwagiliaji, kama chanzo cha malighafi za kwenda viwandani

Tanzania ni nchi kubwa sana na sehemu isiyoishi watu (mapori) ni makubwa kuliko sehem waishizo watu. Serikali iuze ndege inunue matrekta ya kilimo, ndege za kumwagilia na kuunganisha mabomba na pamp za maji kutoka ziwa victoria, tanganyika na bahari ya hindi kwaajili ya umwagiliaji mashambani vijana wachape kazi. Hii itasaidia viwanda kukua na kuzalisha masaa 24 bila kupungukiwa malighafi na kusafirisha bizaa zizalishwazo nje ya nchi ambapo kiwanda kitapata faida na kuajiri watu wengi hadi kupelekea ongezeko la pato la taifa. Mfano wa nchi zinazofanya kilimo cha umwagiliaji na zinaongoza kwa uchumi wa viwanda duniani ni Israel, Cuba, USA na China.

Kilimo cha Ufugaji

Hapa wafugaji wapewe vipaumbele na wahamasishwe kwa kupewa madawa ya mifugo bure na watengewe maeneo maalum kwaajili ya ufugaji na machungio. Pia iandae na kutengeneza mashamba makubwa ya mifugo (ranches) za serikali yatakayo sapoti ufugaji wa mifugo mbalimbali kama; ng'ombe, punda, ngamia, kuku, nguruwe, nyuki, mbuzi, kondoo n.k, hivi vyote vitazalisha malighafi kama ngozi, maziwa, mayai, nyama na asali, ambapo vitapelekwa viwandani na kuzalisha bidhaa mbalimbali na zitauzwa ndani na nje ya Tanzania na kuingiza faida kubwa kwa kiwanda hatimae ajira kuongezeka. Mfano wa nchi zinazoongoza kwa viwanda vinavyotokana na malighafi za ufugaji duniani ni India; ambao wanafuga kondoo aina ya merino wanaotengeneza sufu, USA; ambao wanafuga ng'ombe wengi wa nyama na maziwa.

Kutafta wawekezaji na kuandaa mazingira mazuri kwa wawekezaji watakao wekeza katika viwanda

Mfano; kuwapunguzia gharama za uwekezaji kama kodi ili kuwahamasisha wawekeze kwa wingi na wawe wengi zaidi na kuongeza idadi ya viwanda nchini, ambapo serikali na wakulima watawauzia malighafi kwenye viwanda vyao na bado kutokana na viwanda hivyo watanzania watapata ajira na pesa.

Kwa kutekeleza hayo pato la nchi na mtu mmoja mmoja litaongezeka kwakua ajira zitakuwa nyingi na nchi itatoka kwenye uchumi wa kati daraja la I na kuwa uchumi wa kati daraja la II au kuwa uchumi wa viwango vya juu hatimae maendeleo na kuitwa nchi iliyoendelea.
 
Upvote 4
vp naona watanzania hawataki uchumi wa viwanda. Rais Samiah Suluh nipe hiyo sekta ya viwanda niinyooshe baraaabaraaaa.
 
wakiamua wanaweza, kupitia kodi hizohizo za miamala walizozianzisha na kuziongeza.
 
Serikali haiko serious kabisa na kuendelea nchi. Nchi ISIYO na exports ni takataka kabisa na itaishia kuwa milele.
Sera kuu ya CCM ni uombaomba, ndio maana haina mikakati yoyote ya dhati ya kujitegemea.

Kwa madini ya chuma tuliyonayo, nchi serious kama Rwanda na KENYA zingekuwa mbali sana kimaendeleo, sisi hatutaki hata kuyagusa, tuko busy na almasi, dhahabu na tanzanite ambayo kwa miaka yote yameshindwa kutuvusha.
Hata hivyo chuma kinatumika kila siku ukilinganisha na hayo madini mengine
 
Serikali haiko serious kabisa na kuendelea nchi. Nchi ISIYO na exports ni takataka kabisa na itaishia kuwa milele.
Sera kuu ya CCM ni uombaomba, ndio maana haina mikakati yoyote ya dhati ya kujitegemea.

Kwa madini ya chuma tuliyonayo, nchi serious kama Rwanda na KENYA zingekuwa mbali sana kimaendeleo, sisi hatutaki hata kuyagusa, tuko busy na almasi, dhahabu na tanzanite ambayo kwa miaka yote yameshindwa kutuvusha.
Hata hivyo chuma kinatumika kila siku ukilinganisha na hayo madini mengine
inabidi wakazie sana kwenye kilimo na viwanda ili export ikue na kuongezeka, hakika tutatoboa kama taifa.
 
Unalima kwa jasho ukitaka kuuza mahindi yako popote unakatazwa

Unalima korosho unaambiwa huwezi kuuza popote serikali inatuma jeshi kuja kununua

Huna uhuru wa kufanya biashara maana serikali imebeba madaraka yote hadi ya kuonea mtu

Nikirushwa mazao yangu sina pa kwenda kushitaki maana mahakama zimeharibiwa na serikali yenyewe hazitoi haki maana waziri akipiga simu tu haki inapindishwa

It is very tough to do uzalishaji TZ sababu ya mfumo mbovu wa serikali

Weka katiba mpya ondoa usenge wote huu wa serikali kua na madaraka hadi ya kunyang'anya mtu mali yake bila kupita mahakamani

Bila hivyo haiwezekani
DAWA NI KATIBA MPYA TU.
 
Back
Top Bottom