Serikali ifuatilie semina wanazopewa Watumishi wa Umma wanaotaka kustaafu

Serikali ifuatilie semina wanazopewa Watumishi wa Umma wanaotaka kustaafu

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari zenu!

Ofisini kwetu kuna utaratibu wa semina elekezi kwa watumishi wanaanza kazi na wanaotaka kustaafu.

Kwa hii ya wanaoanza kazi iko vizuri maana hata Mimi nimeipata na kuona iko vizuri. Maana inabase kumjenga mtumishi mpya kiuzalendo zaidi na kuijua serikali yake. Imeanza wapi, iko wapi na inaelekea wapi.

Sasa hii ya wastaafu naiona ina kasoro although sijawahi kuhudhuria.

Imejaa vitisho, kuna mstaafu mmoja alinisimulia kuwa huko walikokwenda semina kuna mwanafunzi (mstaafu) mwenzao alizimia baada ya kupigwa masomo makali na waelimishaji. Alipozinduka akaeleza kuwa yeye hajajenga nyumba na hana kitega uchumi cha maana mpaka anastaafu. Utumishi wake wote alikuwa akilipwa mshahara mdogo uliomsaidia kusomesha watoto mpaka chuo kikuu na bado hawajaariwa.

Nimeona wastaafu kama 3 hivi baada ya kustaafu wanaanza kihangaika na kilimo, nilipowahoji kwanini wakimbilie kilimo ambacho hawakuwa wanakifanya tangu zamani wanasema waelimishaji kwenye semina wamewaelekeza pesa wakazitumie kulima na si njia nyingine kama kujenga nyumba za kupangisha na kufungua maduka.

Nijuavyo Mimi kilimo si cha kuingia kichwakichwa, mtu ana milioni 150 unamwambia akalime huku hajawahi kulima hapo possibility ya kuzika pesa ni kubwa sana kuliko anayekwenda kujenga nyumba za kupangisha.

Nimeona pia trend ya wastaafu wanaokuja kuomba mikataba ya muda mfupi imekuwa kubwa sasa. Sasa hizi seminar zinawasaidia nini huku hali za wastaafu zinazidi kuwa mbaya?

Wengine hata nguo mpya wanashindwa kununua bado wana mashati ya zamani. Mwingine nilimsikia akilalamika kuwa mezeshaji wa semina kawaambia wasinunue magari huku wao wamepark magari nje.

Hizi semina zifumuliwe au zifutwe.
 
Habari zenu !
Ofisini kwetu kuna utaratibu wa semina elekezi kwa watumishi wanaanza kazi na wanaotaka kustaafu.
Sasa ni kwanini usubiri kustaafu ndio ujenge nyumba za kupangisha? Kwanini usiwe unafyatua tofali hata 20 kila mwezi, kwa miaka kadhaa..,baada ya hapo unaanza kidogo kidogo
 
Yaani Mtu unaweza kuajiriwa Hadi unastaafu hujajenga nyumba Hilo kosa lao sio watoa seminar Wala Nini
 
Habari zenu!

Ofisini kwetu kuna utaratibu wa semina elekezi kwa watumishi wanaanza kazi na wanaotaka kustaafu...
Watalaamu wa semina hizo wapo ila hawajitokezi. Kila mtu anapaswa kushauriwa kulingana na jinsi alivyo siyo kama alivyosema Mh Mtaka anakandia kujenga nyumba
 
Mm nawashauri wastaafu wakale bia baada ya kupata mafao yao na wale wasio na pisi wale Mbususu kwani hawatapata pesa nyingi kama hizo katika maisha yao yote yaliyobakia duniani.
 
Pesa yangu, alafu unipangie jinsi ya kuitumia, hehehe!!!!

Shida wabongo wengi hawana akili kabisa. Wamebaki kuigaiga tu.

Unakuta mtu anakomaa kusomesha watoto private from kindergarten to university kisa tu jilani yake ambaye ni banker watoto wake wapo st nani nani. Sasa na yy anataka ajilinganishe nae.

Kama uwezo unaruhusu fanya kama hauruhusu usitake kuiga kunya kwa tembo.

Kuna watu kibao tu wemesoma hizi hizi st kayumba na kwa ada ya sh elf 20, enzi hizo na wametoboa mpaka chuo kikuu wengine madocta wengine mainjinia nk.

Watoto wenyewe mnaowahangaikia wakisha toboa tu mifumo ya magharibi inawameza hawawajali tena. Wanaenda kuwa watumwa wa wake na waume zao huko.

Haya sasa upo kazini huna plani yoyote ya kusevu . mshahara ukitoka ww ni kumwagilia moyo tu na kuchoma nyama na malaya. Unategemea uzeeni uweje zaidi ya kuseminishwa na uzimie😂.
 
Acha uongo kijana huyo mzee wako hana akili tu... Seminar zinaendeshwa vzuri na zimewasaidia wastaff... Huyo mzee wako kama analima ameamua mwenyew ktk seminar hawaelekezwi upuuzi kama huo...
 
Mtoa mada yupo sahihi
kuna mmoja niliwahi kumsikia akishauri kuwa kama umefikia hatua ya kustaafu hujaweza kununua gari basi ukistaafu isinunue kabisa! sijui yupo sahihi ama vipi.

Suala la ushauri huwa ni pana sana,kila mtu anatakiwa apate ushauri kulingana na mazingira,uelewa,fedha hata familia aliyonayo!
 
Mtoa mada yupo sahihi
kuna mmoja niliwahi kumsikia akishauri kuwa kama umefikia hatua ya kustaafu hujaweza kununua gari basi ukistaafu isinunue kabisa! sijui yupo sahihi ama vipi.

Suala la ushauri huwa ni pana sana,kila mtu anatakiwa apate ushauri kulingana na mazingira,uelewa,fedha hata familia aliyonayo!
Japo gari ni mkongojo wa msaafu, ila wengi yanawatesa.
Kuna mama mmoja alikuwa na Isis ina tembelea tairi ya spea na mbaya zaidi walikuwa wanamkimbiza mgonjwa hospt. Kufika kwenye kilima kigari kika kata wese, nikajua tu hapa mstaafu keshamaliza penshen 😀😀😀!
 
Sasa ni kwanini usubiri kustaafu ndio ujenge nyumba za kupangisha? Kwanini usiwe unafyatua tofali hata 20 kila mwezi, kwa miaka kadhaa..,baada ya hapo unaanza kidogo kidogo
Mkuu huwaga kuna "visingizio" vingi sana vya mtu kutokuendelea kutokana na kipato cha kazi anayofanya.

Utamsikia mtu: "nasomesha", sijui "mshahara mdogo" nk nk!

Unabakia kujiuliza, kusomesha hugharimu kiasi gani na ni kila mwezi kwani?

Na hao wanaodai mishahara ni midogo wakati fursa za kukopa kwa wafanyakazi ni kubwa, kauli zao hizo huwa siziungi mkono.

Kama ulivyoeleza mkuu, kujenga kidogo kidogo kuanzia nyumba za makazi na za kupangisha ku suport life after retirement, uwezo huo wanao bila kujali cheo ama kiwango cha mshahara cha mtu.

Jambo linalodidimiza watu wengi ni "bata", lakini hilo huwa halisemwi hata kwa mtu liliye mfirisi, lazima atoke na visingizio muflisi kama hivyo vya kusomesha nk nk.

Mtumishi yeyote wa serikali, tarehe yake ya kustaafu anaijua vizuri na ipo wazi, kwa hiyo anao uwezo mzuri wa kujiandaa na si kusubiri kwenda kushikiwa akili za mambo ya kufanya kwa njia ya semina.
 
Back
Top Bottom