Serikali ifunge ukurasa wa Ben Saanane ukweli ujulikane

Serikali ifunge ukurasa wa Ben Saanane ukweli ujulikane

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,282
Reaction score
117,244
Niseme wazi kuwa sikuwahi kuwa fan wa Ben Saanane Kwa lolote lile lakini Kwa sababu alikuwa member mwenzetu hapa nilimuona kama mtu wa karibu au ninaefahamiana nae hivi sababu ya kushiriki pamoja mijadala mbalimbali hapa JF.

Alipoanza kuandikia gazeti la Raia mwema na kuanza kuhoji PHD ya Magufuli binafsi sikuwahi kuwa na interest na huo mjadala. Kwanza niliuona hauna maana sana. Pili niliona hautaweza badilisha lolote Kwa hiyo ni kama anajisumbua.

Ilipoanza kutangazwa kapotea nilistuka sana..binafsi nilifikiri labda kajificha ili apate attention kubwa akiibuka tena. Lakini hadi leo hatuna majibu sahihi hasa nini kilimkuta Ben Saanane.

Alipofariki Magufuli nikahisi labda alikuwa amefungwa rumande kimyakimya na sasa ataachiliwa lakini hadi sasa naona kimya kabisa.

Natamani sasa ukweli ujulikane tuweze funga ukurasa kama yupo hai aachiwe.

Kama alikufa ijulikane alikufaje?

Wahusika kina nani?Mwili upo wapi?

Ilikuwa kusudi au ajali kwenye interogation?

Naaamin familia yake inahitaji kujua ukweli na Sisi wengine tuzungumze kitu kilichothibitishwa.

Nafikiri wakati wa ukweli kujulikana umefika.

Familia na marafiki waombe kumuona Rais asaidie uchunguzi tupate majibu
 
Swali zuri lakini umejitetetea mno. In such a preemptive ways! Paragraph ya kwanza na ya pili haina maana. But Ujumbe baada ya hapo ni mzuri. Kwenye paragraph mbili za kwanza, uliona kuwa ni kitu hakina maana alipohoji kuhusu PhD ya jiwe, halafu tena unataka nini? Be straight.
 
Wakati ule kuizungumzia shahada ya uzamivu ya mtawala ilikuwa ni sawa kabisa na kujitoa muhanga. Hata kwenda pale maktaba ya UDSM kule East Africana kuiomba tu kwa ajili ya kuifanyia rejea ilikuwa ni jambo lenye kuhitaji uthubutu uliopitiliza.
Hilo andiko la PLAGIARISM la Mwendazake alilokopi kwa Dr Y Philip na kusimamiwa na Prof Buchweshaija iliondolewa makataba ever since, huwezi kupewa kwa ajili ya rejea

Katika AIBU za UDSM wanaojipambanua kuwa ndiyo Chuo Kikuu bora Tanzania, na kuviponda vyuo vingine kuwa havina Ma Profesa wenye majina, au sijui vyuo vingine vinatoa degree za kuandikiwa THESIS, basi nao hii ni AIBU yao.

Itafika siku CCM ikiwa nje ya madaraka, tutaweka petition ya UDSM kuifuta PhD ya Mwendazake kama ambavyo LSE walivyofuta PhD ya mtoto wa Gaddafi mwaka 2011. Na hapo tutakuwa timekamiklsha kazi ya Ben Saanane na tutakuwa TUMEMUENZI inavyostahili
 
Anaweza kuwa anachungulia kwa mbali.
... Boss, unamaanisha kitu kama hicho?

Akasema, “Palikuwa na tajiri mmoja aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, nguo za gharama kubwa, kila siku. Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima, alikuwa akiletwa mlangoni kwa huyo tajiri kila siku. Lazaro alikuwa akitamani kula makombo yaliyodondoka mezani kwa tajiri. Hata mbwa walikuwa wakiramba vidonda vyake.

“Hatimaye, yule maskini alikufa. Malaika wakamchukua akakae pamoja na Ibrahimu mbinguni. Yule tajiri naye pia akafa, akazikwa. Alipokuwa kuzimuni ambapo alikuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Ibrahimu kwa mbali na Lazaro karibu yake. Akaita, ‘Baba Ibrahimu, nionee huruma umtume Lazaro achovye japo ncha ya kidole chake katika maji aupoze ulimi wangu maana ninateseka kwenye moto huu.’ Lakini Ibrahimu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba ulipokuwa hai ulipata kila kitu kizuri ulichotaka, ambapo Lazaro alipokea mabaya. Lakini sasa anafarijika hapa na wewe unateseka.
 
... Boss, unamaanisha kitu kama hicho?

Akasema, “Palikuwa na tajiri mmoja aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, nguo za gharama kubwa, kila siku. Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima, alikuwa akiletwa mlangoni kwa huyo tajiri kila siku. Lazaro alikuwa akitamani kula makombo yaliyodondoka mezani kwa tajiri. Hata mbwa walikuwa wakiramba vidonda vyake.

“Hatimaye, yule maskini alikufa. Malaika wakamchukua akakae pamoja na Ibrahimu mbinguni. Yule tajiri naye pia akafa, akazikwa. Alipokuwa kuzimuni ambapo alikuwa akiteseka, alitazama juu, akamwona Ibrahimu kwa mbali na Lazaro karibu yake. Akaita, ‘Baba Ibrahimu, nionee huruma umtume Lazaro achovye japo ncha ya kidole chake katika maji aupoze ulimi wangu maana ninateseka kwenye moto huu.’ Lakini Ibrahimu akamjibu, ‘Mwa nangu, kumbuka kwamba ulipokuwa hai ulipata kila kitu kizuri uli chotaka, ambapo Lazaro alipokea mabaya. Lakini sasa anafarijika hapa na wewe unateseka.
Asante sana kwa "neno" hili.
 
Back
Top Bottom