Ashakum si matusi, ila nachelea kusema kuwa taaluma ya habari imevamiwa na vilaza

Ashakum si matusi, ila nachelea kusema kuwa taaluma ya habari imevamiwa na vilaza

ministrant

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2014
Posts
754
Reaction score
1,478
Nimekuwa nikifuatilia mahojiano kadhaa yanayofanywa na viongozi mbalimbali wa taasisi za Serikali na Wana habari, ila kilichonisikitisha ni kuona mwanahabari anahoji swali ambalo hata uelewa wa hilo jambo hana kiasi kwamba swali likirudishwa kwake kwa ufafanuzi zaidi anabaki kumbwelambwela tu.

Mathalani, mwandishi anamuuliza kiongozi wa Serikali kuwa sheria ya kodi inamtaka ofisa wa forodha anapotekeleza majukumu yake lazima aambatane na ofisa wa Polisi, mwandishi huyo anapoulizwa ni kifungu kipi cha sheria ya kodi kinachoamuru iwe hivyo katika utekelezaji wa majukumu ya ofisa wa forodha kulazimika kuambatana na ofisa wa Polisi anabaki kukosa majibu kwakuwa kichwani hana authority inayotamka hivyo.

Mwanahabari mwingine anasema ndugu walisema mara ya mwisho simu ya ndugu yao ilisoma yuko maeneo ya Chang'ombe Polisi, mwanahabari huyo anapotakiwa aeleze kwa kina kuwa competent authority zenye access na kusoma location ni vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), je, hizo taarifa walizipatia wapi kuwa location ilisoma maeneo hayo? Mwanahabari anakosa cha kueleza.

Binafsi naona wanahabari wengi wamekuwa wakijikita kuhoji maswali ambayo huwa vyanzo vyao ni kutoka kwa whistle blower wa mitandaoni ambapo sio jambo baya, lakini wanakosa weledi wa kuchanganya na zao kwa kwenda deep juu ya kile ambacho kimekuwa kimechapishwa huko mtandaoni,badala yake wao huingia kichwakichwa na kuishia kupigwa za uso kwenye press.

Nadhani haya ni matokeo ya taaluma hii kuvamiwa na vilaza ambao huishia kufanya table investigation na kwenda kwenye press kichwa kichwa.

Wanapaswa kutambua kuwa wakati mwingine hizi taarifa za mitandaoni huwa zinachapishwa kwa watu wenye mrengo fulani kwa maslahi fulani na wao kwa kuwa hawajitambui hujikuta wanaingia kwenye mtego kwa kutozingatia weledi wa taaluma zao na kujikita kuamini umbea bila kuwa na competent information.
 
Nimekuwa nikifuatilia mahojiano kadhaa yanayofanywa na viongozi mbalimbali wa taasisi za Serikali na Wana habari, ila kilichonisikitisha ni kuona mwanahabari anahoji swali ambalo hata ...
Mkuu samahani na wewe ni muadishi wa habari?
 
Taifa limejaa machawa hadi sio poa. Sio vyombo vya habari tu hata huku mtaani.

Zamani Bajaji, daladala ziĺikua zinabandika au kuchora picha za watu mashuhuri kuonesha wanavyowahusudu. Ila siku hizi zinawekwa picha za wanasiasa au msanii fulani lengo akiiona amuite ofisi ampatie chochote kitu apoze makali ya tumbo.
 
Asubuhi sikiliza Wasafi fm kile kipindi chao cha asubuhi! Utakuta wamleta mgeni mada nzuri sana mgeni anaongea, sasa sikiliza maswali ya Zembwela, mpka anapoingia na kuuliza Gerald Hando ndiyo utaona tofauti ya Mwandishi na Kanjanja..
 
Niende moja kwa moja kwenye pointi

Kumeibuka na wimbi la waaandishi wa habari uchwara kutokana na ongezeko kubwa la onlineTVs lakini ukiangalia utendaji kazi wao 98% wengi ni vilaza na hawana uelewa wowote kuhusu taaluma ya uandishi wa habari ila unaweza kusema unawaona onlineTVs ila ukichunguza pia kwenye Mainstream Media hali ya ukosefu wa weledi ndo mbaya zaidi

Yani akipatikana tu mtu yeyote anaeweza kununua kamera na mic au anauwezo wa kuanzia radio na tv basi anamtafuta mtu yeyote anamuweka hapo na yeye tayari anakua mwandishi wa habari.

Sijajua kwa wengine ila kwa upande wangu sijajua kama uandishi wa habari wa kisasa ili uonekane mwandishi mkali ni lazima uulize maswali ya kimbeya au maswali ya kutaka kuchonganisha watu pasipo sababu yani imekua ndo fasheni

Mfano juzi kuna mwandishi mmoja nimemsikia anamuuliza msanii DullySykes studio swali eti "chidbenz anatumia madawa ya aina gani"?!...ili iweje ndugu muhandishi

Jana nimemsikia mwandishi mwigine anamuuliza mama mmoja kungwi ili atoe maoni yake "kwanini Rushyna anadai kuwa kwa hadhi ya Hamisa hakustahili kuolewa na Aziz Ki na hajui eti kampendea nini mwanume mwenye mdomo kama ule" unauliza maswali ili uchonganishe watu si ndio ndugu mwhandishi?!..

Leo tena naamka tu asubuhi namsikia mwandishi mwingine anamuuliza mama zuchu kwanini zuchu wanamuita king'ang'a...ivi unauliza swali kama ili upate nini na hadhira yako umepanga kuilisha nini ndugu mwandishi?!...yani daah fani ya uhandishi wa habari siku hizi inachezewa sana ni kinyaa kwa kweli na kuna mifano mingi sana siwezi kuimaliza yote

Naomba kuwauliza nyie wanahabari wa media za bongo ni nini hasa lengo la uhandishi wenu

1.Kuchonganisha na kugombanisha watu?
2.Kuijenga au kuibomoa jamii?
3.Kuforce content ili habari zenu zitrend?
5.Ukosefu wa weledi na profesionalism?
4. Au ni njaa tu na ukosefu wa ajira kwahiyo mmeamua kubeba vitonge kuingia mitahani kufanya vihoja?

Naiomba serikali iingilie kati kuhusu hii taaluma ya uanahabari ingefaa waandishi wote wachunguzwe elimu zao na wapewe leseni na ambao wana elimu ndogo na wasio na elimu kabisa wote warudi shuleni wakasome kwasababu 98% ya waandishi hawana weledi kabisa na fani ya uanahabri.. tasnia imejaa vilaza watupu
 
Watu ndiyo wanataka kusikia ujngujing huo,media zinaenda jinsi soko linavyotaka 😄
Sahv wee ongeaa sana porojo nyingi tayari mtangazaji

Ova
 
Ni Mwandishi au Waandishi.
Labda kuna mabadiliko ya Waandishi kwenda Wahandishi yametokea.
Kwahiyo ni wanaabari au ni wanahabari?!....waandisi au wahandisi?!.. lugha sahihi ni wahandishi na sio waandishi..jifunze lugha fasaha mkuu
 
Ni Mwandishi au Waandishi.
Labda kuna mabadiliko ya Waandishi kwenda Wahandishi yametokea.
Akiwa mmoja sio mwandishi ila ni muhandishi na wakiwa wengi ni wahandishi...mwandishi na waandishi ni katika kutamka lakini sio katika kuandika mkuu
 
Labda nawao waende Veta ila kwasaizi ajira ya fasta ni kuwa content creator au kuwa na mic na recorder unaingia mtaani,unabeba takataka zote tu
 
Muhandishi ni mtu wa namna gani huyo kabla sijachangia mada
 
Akiwa mmoja sio mwandishi ila ni muhandishi na wakiwa wengi ni wahandishi...mwandishi na waandishi ni katika kutamka lakini sio katika kuandika mkuu
Thibitisha kwa kuleta vielelezo visivyotiliwa mashaka.
 
Kwahiyo ni wanaabari au ni wanahabari?!....waandisi au wahandisi?!.. lugha sahihi ni wahandishi na sio waandishi..jifunze lugha fasaha mkuu
Mkuu umechemka. Wahandishi haiendani hata na mzizi wa neno lenyewe.

Mwandishi......ni mtu anayefanya kazi ya kuandika.

Andika .......mwandishi.
Lima ......mkulima.

Tuje kwenye mhandishi sasa. Unataka kusema ni mtu anyehandika??

Handika......mhandishi!!!!? ××
 
Tasnia ya habari hasa broadcast iko intensive care unit, Waandishi wengi ni sasa wanapenda yellow stories
 
Back
Top Bottom