Serikali iingilie kati Makanisa ya Miujiza? Watanzania masikini wa kutupwa wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli huku wahubiri wakigeuka mamilionea

Kwaiyo mr mayala kuhani Musa sio tapeli ila hao usiowapenda ww ndo matapeli

Huna jpy na uzi wako hauna baransi kwaiyo makanisa mengne yote yakirokole ni matapeli sabu wanataka malipo kbla ya kaz
Ila kuhani Musa yy sio tapeli sabu anapokea pesa baada ya kutoa msaada
Je inawezekana atawa anatapeli wazungu wanampa misaada ya kuja kuwapa waumini yeye anakuja kuwauzia

Lakin pia kuhani musa akupangii kiwango cha pesa ila anapokea pesa kutoka kwa waumini

CRDB NA NMB zote ni bank ila kla mmoja anakatiba yake na anautaratibu wake wakufanya kaz

Ata ayo makanisa yakirokole yako tofauti tofauti na kla moja lina utaratibu wake wa kufanya kaz
 
Mimi pia sikubaliani na utapeli unaoendelea kwa baadhi yao. Lakini na wewe mwanasheria usiyejua madhara ya uhuru wa kuabudu; utatumia kigezo gani kujua huyu yuko sawa, huyu hapana?
 
Serikali ianze na kuondoa 'betting', kwani nayo inaongeza umaskini. Halafu, badala ya kuwabana wahubiri hao, iongeze elimu ya kuchanganua mambo kwa kina, mfano, kuweka somo la falsafa kuanzia shule za msingi, na kuanzisha viping redioni na TV ili kuwapa mwanga watanzania walio wengi.
Hakuna anayewakokota hao waamini wao.
Endapo serikali itafanya maisha bora kwa kila mtanzania, hayo mambo ya miujiza hayatakuwepo. Hivyo, hapa wa kuwajibika ni serikali!
 
Emu kaka mkubwa,acha kuuharibu biashara za watu bhanaπŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„.
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.
Kiufupi hao jamaa hawana tofauti na kautaratiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiibu ka Chama Dola.
CHUPA na Mfuniko.
Hakuna maskini hapa Nchini kwetu mkuu,ndo maana wenye akili wanachuma mifyezaπŸ€”πŸ€”πŸ€”.
Mtaji wa siasa hapa Nchini hauna tofauti na mtaji wa Kiimani.
Kiufupi,Nchi hii Ina MAZOMBI YALIYOCHANGAMKA.πŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ’“πŸ’“
 
Huo ndio unaitwa uhuru wa kuabudu!
 
Kweli upofu wa imani ni mbaya sana, na bila shaka ww mzee unazeeka vibaya.
Yn unawashauri watu waachane na manabii wanaojitajirisha kupitia sadaka zao huku wao walibaki watupu halafu tena unakuja kumtetea huyo nabii Mussa au umekuja kumtangazia biashara yake hapa.
Ww mzee hujitambui
 
Kaka paschal ni ngumu sanaa kuingilia Uhuru wa kuabudu....

Secular state & non_secular state

Cc. Bujibuji Simba Nyamaume , Mshana Jr , Kiranga , Mohamed Said , FaizaFoxy
Kila mtu ana haki ya kuamini au kutoamini anachotaka. Hata kama ni uongo na ujinga. Provided that it is in good faith with no malicious intent, which can be hard to disprove.

Hii ni haki ya kikatiba, ni haki ya utu, ipo katika Universal Declaration of Human Rights tangu December 10 1948.

Njia ya kuondokana na imani za uongo za kijinga ni kuongeza elimu kwa watu, si kupiga marufuku imani hizo.

Na hii kazi ni yetu sote, si ya serikali tu.

Ndiyo maana watu wengi hawaelewi kwa nini Kiranga anarudia sana hoja zake kuhusu kutafuta ukweli na kuachana na kwenda kwa imani tu, kila siku.

Tunahitaji elimu hii sana kupambana na haya mambo ya uongo katika jamii yetu.
 
hivi nikweli mwanamke anaweza kurogwa asiblid miaka miwili na akaombewa muda huohuo akaanza kumwaga midamu yahedhi mazabahuni?
Ni kweli...

Sababu ya Imani ya mwanamke huyo..

Imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa neno la Mungu, Imani ni kuwa na hakika ni bayana ya vitu visivyoonekana.
 
Pascal Mayalla kaka yangu, pole kwa kuumia [emoji23]. Maana watanzania wanatafunwa vibaya mno na wanaojiita watu wa Mungu. Wanatafunwa Mpaka na wewe wa pembeni unaumia unaona kama sinema. Ila huo ndio ukweli.

Kwa namna Fulani nilitaka niwalaumu sana wanaopigwa kwenye huu utapeli..lakini muda ni rafiki mzuri sana. Majibu niliyapata kwa kukawia ila yalinipa mwangaza mzuri...ambao ninadhani unaweza kutupa mwanga wa walau wapi tuanzie mama mpaka sasa rushapigwa na adui wetu ujinga magoli kadhaa.

Shida yetu kubwa Brother Pascal Mayalla ni lishe duni hasa kwa kipindi Cha siku elfu Moja za kwanza za uhai wa watoto tukianzia kutungwa kwa mimba mpaka mtoto anapotimiza miaka 2.

Kwa mujibu wa wanasayansi kipindi hiki ni muhimu sana kwa makuzi ya mtoto na.mtu kuliko.kipindi kingine chochote. Ni kimpindi ambapo silaha kubwa ya binaadamu, UBONGO wake ndiko unajengwa na kufikia ukomo wa ukuaji wake.

Mtoto akidumaa au asipopata virutubisho wa kusaidia ukuaji mzuri wa ubongo katika kipindi hiki ndio tunakuwa tumempoteza kabisa huyo. Atakomea kuwa na.akili za kusikia njaa na kula au kung'amua pini imemchoma.. zaidi ya hapo kumwambia hapa anapigwa utakuwa unampigia mbuzi gitaa.

Wengi baada ya taabu za miaka ya 80 na kuanza kufanya modernization ya maisha, kukimbilia mijini na kadhalika tumekiwa wahanga wa lishe duni. Na ndio sisi Sasa tuko maofisini, ndio madaktari, wakuu wa wilaya wakuu wa vyombo vya usalama na kadhali ambao ukisikia maamuzi yetu unagunda kabisa ubongo Kuna sehemu ulikomea kabla ya kudevelop fully.

Hapa tushajichanganya nadhani nimkukibali kuanza upya na Wamama wote na watoto chini ya mwaka mmoja. Tuboreshe lishe. Hawa.wa Sasa acha tuu wapeleke fedha kwa Manabii na mitume kwa maana hakuna namna utafanya wakuelewe.

Na huo Wito wa serikali hauna tija hata kidogo, maana wanaosimamia hiyo serikali ndio wanaopeleka huko mizigo na mizigo ili waombewe wasitumbuliwe. Tuwe wavumilivu tuu na tuiombe serikali iwekeze kwenye elimu ya Afya na lishe kwa msisitizo ili tuache kizazi chema huko mbele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…