Serikali iingilie kati Makanisa ya Miujiza? Watanzania masikini wa kutupwa wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli huku wahubiri wakigeuka mamilionea

Serikali iingilie kati Makanisa ya Miujiza? Watanzania masikini wa kutupwa wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli huku wahubiri wakigeuka mamilionea

Wanabodi
Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa. Topic ya leo, ni kutoa wito kwa Serikali yetu kuingilia kati kitu kinachoendelea kwenye baadhi ya makanisa ya wakovu yanayojinasibu kufanya miujiza, kutoa mapepo, kutoa uchawi na kufanya miujiza ya uponyaji?.



Naomba kuwasilisha.

Paskali
Wajinga ndio waliwao,acha waliwe maana wanadai wanapata miujiza.
 
Serikali haina mamlaka kuwapangia wananchi nini cha kuamini na nini cha kutoamini kitendo hicho cha serikali kuingilia uhuru wa kiimani wa jamii fulani ni kinyume na matakwa ya katiba ya JMT.

Ukiruhusu serikali iingilie na kupangia taratibu imani fulani tambua fika na imani yako umeikabidhi mikononi mwa serikali anaweza tokea kiongozi akaona imani yako ni ya kishenzi na akamua lolote atakalo juu ya imani yako na usiwe na nguvu ya kikatiba kupinga hilo.

Tanzania kila mtu yupo huru kiimani kwa kuzingatia katiba ya JMT tuheshimu hilo.
 
huko mwanza ZUMARIDI alisema atamrudisha KANUMBA, kamsumbua mama kanumba kwelikweli, mwisho wa siku hamna kanumba wala kayumba
Alisema alipokuwa gerezani alienda mbinguni, akasema mbinguni kuna magorofa na nyumba za chini, ila magorofa ni mengi zaid, akasema alikutana na mtu petro na amemchumbia anataka kumuoa kwa hyo kinachosubiriwa ni siku ya harusi tu.

kanisa likalipuka kwa shangwe na vigelegele, nilishangaa sana.
 
alisema alipokuwa gerezani alienda mbinguni, akasema mbinguni kuna magorofa na nyumba za chini, ila magorofa ni mengi zaid, akasema alikutana na mtu petro na amemchumbia anataka kumuoa kwa hyo kinachosubiriwa ni siku ya harusi tu.

kanisa likalipuka kwa shangwe na vigelegele, nilishangaa sana.
Mimi siwezi kumshangaa,
Ni sawa na mtu anayekuambia nikifa nitaenda kuimba na kuruka katika kiti cha enzi
Mwingine anakuambia nikifa nitaenda kukutana na mabikra 72 na mito ya pombe.

Hio ndio IMANI inapaswa kuwa.
 
Acha wakamuliwe hakuna aliyeshikiwa fimbo au kulazimishwa kwenda huko ni kwa hiari yao!

Kanisa kiongozi ni 1 tu ndo kusema ndo kupanga ndo kila kitu hadi biblia yeye tu ndo kavuviwa kuichambua wengine hamna acha wakome!


Viongozi wa kisiasa wanaona wanchi kama takataka viongozi wa kiimani ndo kabisaaa!
 
Mkuu hata Serikali za Mataifa Tajiri duniani zimeshindwa kuzuia hili wimbi....

Haya mambo unayoyaona huku kwetu usifikiri yameanza leo, hata Marekani, Ulaya na baadhi ya mataifa ya Asia kumekuwepo na hali kama hii miaka mingi tuu...

Hapa serikali ni vigumu kujiingiza kwa sababu ya kinachoitwa Uhuru wa kuabudu...na unaposema Ibada basi sadaka na matoleo ni sehemu muhimu sana ya kukamilisha ibada hiyo..

Serikali ikijaribu kujiingiza hapo kama Kiongozi huyo ni wa Dini nyingine utasikia.. "Anatubagua kwa sababu yeye siyo Mkristo"

Na kama ni wa upande Mwingine utasikia "Anatutesa kwa sababu yeye siyo Muislamu"

Na hata kama Serikali ikiingilia kati Je itatumia kipimo gani Kujua kwamba huyu ni Wa Kweli na huyu ni Tapeli?

Achilia mbali hao manabii feki, hata Makanisa yaliyozoeleka Kama Roman Catholic, Lutheran, Anglican na Moravian huwa kuna Sadaka na michango ya hiyari Kama vile Zaka10% , Mavuno, Shukrani, Nadhiri, Ahadi, Ujenzi, Nk ...sasa serikali itatumia kigezo kipi kumshtaki nabii Fake aliyepokea mil 1 kwa kigezo cha kumuombea mtu apate mtoto na kumuacha Padri aliyechukua Mil 1 kwa ajili ya sadaka ya Zaka??

Kwa sababu huyu Anasali Kanisa Katoliki ametoa milioni Moja akaiita ni Zaka na huyu ametoa mil moja hiyo hiyo kwa Nabii wa Uongo akaiita ni Mbegu (toa ubarikiwe) unamkamata yupi na kumuacha yupi? Kwa sababu wote wanasema wametoa sadaka.. Je kati yao hapo nani ana haki kuliko mwingine?

Serikali ikiingilia suala hili itaibua migogoro zaidi na Uhasama usio na faida...cha muhimu ni kila mtu atumie akili na hekima.....
Ni kweli kabisa mkuu serikali ikiingilia kati kwa namna yoyote utazuka mgogoro kwa namna moja ama nyingine, ila kama ingekuwa busara kwa serikali kupitia wizara ya maendeleo ya jamii kutoa elimu ama angalizo kwa muktadha wa mada hii
 
alisema alipokuwa gerezani alienda mbinguni, akasema mbinguni kuna magorofa na nyumba za chini, ila magorofa ni mengi zaid, akasema alikutana na mtu petro na amemchumbia anataka kumuoa kwa hyo kinachosubiriwa ni siku ya harusi tu.

kanisa likalipuka kwa shangwe na vigelegele, nilishangaa sana.
Mm nahisi hawa manabii huwa wana tumia magic power kuwapumbaza waumini wao maana hii sio kawaida.

Urokole ni moja wapo ya ugonjwa wa akili hasa barani Africa ,alafu bora Tz ukienda Nigeria ndo top wa ushenzi wa hawa watu,hawa manabii uchwara wanaelekea kuumeza ukrisito kabisa Iwapo wakiristo wasipo chukua hatua kudhibiti huu upuuzi.

Ndio maana Urusi iliupiga marufuku urokole maana ni tatizo.
 
Baadhi ya wahubiri hawa wanatumia nguvu za giza za kiini macho kwa kitu kinachoitwa auto suggestion kwa Watanzania Masikini wa Kutupwa, kuaminishwa umasikini wao ni kwasababu wamelogwa, hivyo ili kuuondoa uchawi wa umasikini,
unatakiwa kufanya appointment kumuona Mtumishi, ambapo utapangiwa kiwango cha fedha kumuona mtumishi.
Hili umelithibitishaje ?....halafu serikali haiamini hili, Sasa kwa nini unatumia kujenga hoja yako?


Kwenye matangazo yao kupitia redio na TV, unaambiwa njoo na sadaka yako bila kuambiwa kiwango. Ukifika kanisani,
utaandikishwa na kuambiwa kiwango cha kumuona mtumishi akueleze jinsi ulivyologwa na ni nani amekuloga. Kiwango kilianzia 10,000, baadae ikawa 20,000, ikapanda kuwa 50,000, 100,000 sasa ni 200,000.

Unatakiwa kuitafuta hiyo pesa popote ulipe ndipo umuone mtumishi. Hivyo ni waumini wenye pesa tuu ndio watamuona mtumishi
Hawa wanaofanya haya sio watumishi ili matapeli tu wanaotumia imani za watu kuchuma faida , hawa washitakiwe kwa utapeli na kujipatia mali isivyo halali.

Bahati nzuri wapo waliotapeliwa na hao wahuni ni vyema wakashitaki kwenye vyombo husika.
 
Wanabodi
Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa. Topic ya leo, ni kutoa wito kwa Serikali yetu kuingilia kati kitu kinachoendelea kwenye baadhi ya makanisa ya wakovu yanayojinasibu kufanya miujiza, kutoa mapepo, kutoa uchawi na kufanya miujiza ya uponyaji?.

Baadhi ya wahubiri hawa wanatumia nguvu za giza za kiini macho kwa kitu kinachoitwa auto suggestion kwa Watanzania Masikini wa Kutupwa, kuaminishwa umasikini wao ni kwasababu wamelogwa, hivyo ili kuuondoa uchawi wa umasikini,
unatakiwa kufanya appointment kumuona Mtumishi, ambapo utapangiwa kiwango cha fedha kumuona mtumishi.

Kwenye matangazo yao kupitia redio na TV, unaambiwa njoo na sadaka yako bila kuambiwa kiwango. Ukifika kanisani,
utaandikishwa na kuambiwa kiwango cha kumuona mtumishi akueleze jinsi ulivyologwa na ni nani amekuloga. Kiwango kilianzia 10,000, baadae ikawa 20,000, ikapanda kuwa 50,000, 100,000 sasa ni 200,000.

Unatakiwa kuitafuta hiyo pesa popote ulipe ndipo umuone mtumishi. Hivyo ni waumini wenye pesa tuu ndio watamuona mtumishi!.

Baada ya kuingia kumuona, mtumishi atakuambia prophesy yako na ku conclude matatizo yako yote, ya kiuchumi, umasikini, maradhi, au majanga yoyote, ni umelongwa na watu wa jijijini kwako!.

Baada ya hapo sasa ndio utapewa bili ya sadaka. Mtumishi atajifanya anamuuliza Mungu, then unaambiwa Mungu amesema njoo na sadaka ya milioni 2, 5, 10, 20, kutegemea na ukubwa wa tatizo lako, ya kuleta hiyo sadaka ndipo Mungu atalimaliza tatizo lako!.

Kutokana na wewe kuwa ni tayari umesha pigwa ganzi, utakwenda kuzitafuta hizo pesa na kuzileta cash!.

Watanzania masikini wa kutupwa, wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli, na baadhi ya hawa ma Pastor, huku hao ma Pastor na wahubiri wakineemeka na kuageuka mamilionea na mabilionea huku wakivuta mi ndinga ya nguvu!.

Kuna Mama mmoja alifiwa na mtoto wake, the only son, amedanganywa mtoto wake hajafa, amechukuliwa tuu kichawi, mama kaambiwa akatafute sadaka kiasi fulani, arejeshewe mwanae!, huyo mama ana haha kusaka hiyo pesa ili kumrejesha mwanae!.

Japo haya ni mambo ya imani, na waumini wanakwenda wenyewe kwa hiyari yao na wana toa fedha kwa ridhaa zao, na serikali yetu imetoa uhuru wa kuabudu, lakini ikifikia kiwango Watanzania wanatapeliwa, serikali ina wajibu wa kuingilia kati wananchi wake wasiendelee kutapeliwa!.

Namalizia kwa ile hoja ya msingi jee kuna haja ya serikali iingilie kati shughuli za haya makanisa ya wakovu ya miujiza ili Watanzania masikini wa kutupwa, wasiendelee kukamuliwa mamilioni kwa utapeli, huku wahubiri wakizidi kunona kwa kuwa mamilionea!.

Naomba kuwasilisha.

Paskali
Paskali, hakuna kitu kigumu na hatari kuingilia imani ya mtu, kumbuka mamia waliojiua Johnstown, Kibwetere na ujerumani. Unaweza ukapiga marufuku leo kesho ukakuta maiti zaidi ya elfu moja barabarani, wamejiua kwa kile walichokiamini.
Hebu tuangalie upande wa pili, huko nako kunasemekana kulikuwa au nako kunavuta kitu kidogo, haiwezekani serikali ikaachia mali yake itumike kuendesha utapeli hivihivi tu ikiangalia. Serikali imeacha kukirudisha kiwanda cha nyama TP na kuridhika na utapeli unaofanyika hapo, Moshi kulitokea vifo vya watu vilivyosababishwa na utapeli huo, lakini huenda mambo yakamalizwa kimyakimya nipe nikupe.
Kuondoa tatizo hili ni kuwa na mpango nafuu wa tiba za maradhi badala ya hizi za kulazwa hospitali ya Mwananyamala kuwa aghari kuliko Bondeni Gesti, mapokezi na kumuona dakitari kwa malipo, unaishia kushindwa kununua dawa alizokuandikia dakitari na uombe Mungu usifie hosipitali, ukoo utafilisika kwa kuuziwa maiti yenu.
 
Wanabodi
Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa. Topic ya leo, ni kutoa wito kwa Serikali yetu kuingilia kati kitu kinachoendelea kwenye baadhi ya makanisa ya wakovu yanayojinasibu kufanya miujiza, kutoa mapepo, kutoa uchawi na kufanya miujiza ya uponyaji?.

Baadhi ya wahubiri hawa wanatumia nguvu za giza za kiini macho kwa kitu kinachoitwa auto suggestion kwa Watanzania Masikini wa Kutupwa, kuaminishwa umasikini wao ni kwasababu wamelogwa, hivyo ili kuuondoa uchawi wa umasikini,
unatakiwa kufanya appointment kumuona Mtumishi, ambapo utapangiwa kiwango cha fedha kumuona mtumishi.

Kwenye matangazo yao kupitia redio na TV, unaambiwa njoo na sadaka yako bila kuambiwa kiwango. Ukifika kanisani,
utaandikishwa na kuambiwa kiwango cha kumuona mtumishi akueleze jinsi ulivyologwa na ni nani amekuloga. Kiwango kilianzia 10,000, baadae ikawa 20,000, ikapanda kuwa 50,000, 100,000 sasa ni 200,000.

Unatakiwa kuitafuta hiyo pesa popote ulipe ndipo umuone mtumishi. Hivyo ni waumini wenye pesa tuu ndio watamuona mtumishi!.

Baada ya kuingia kumuona, mtumishi atakuambia prophesy yako na ku conclude matatizo yako yote, ya kiuchumi, umasikini, maradhi, au majanga yoyote, ni umelongwa na watu wa jijijini kwako!.

Baada ya hapo sasa ndio utapewa bili ya sadaka. Mtumishi atajifanya anamuuliza Mungu, then unaambiwa Mungu amesema njoo na sadaka ya milioni 2, 5, 10, 20, kutegemea na ukubwa wa tatizo lako, ya kuleta hiyo sadaka ndipo Mungu atalimaliza tatizo lako!.

Kutokana na wewe kuwa ni tayari umesha pigwa ganzi, utakwenda kuzitafuta hizo pesa na kuzileta cash!.

Watanzania masikini wa kutupwa, wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli, na baadhi ya hawa ma Pastor, huku hao ma Pastor na wahubiri wakineemeka na kuageuka mamilionea na mabilionea huku wakivuta mi ndinga ya nguvu!.

Kuna Mama mmoja alifiwa na mtoto wake, the only son, amedanganywa mtoto wake hajafa, amechukuliwa tuu kichawi, mama kaambiwa akatafute sadaka kiasi fulani, arejeshewe mwanae!, huyo mama ana haha kusaka hiyo pesa ili kumrejesha mwanae!.

Japo haya ni mambo ya imani, na waumini wanakwenda wenyewe kwa hiyari yao na wana toa fedha kwa ridhaa zao, na serikali yetu imetoa uhuru wa kuabudu, lakini ikifikia kiwango Watanzania wanatapeliwa, serikali ina wajibu wa kuingilia kati wananchi wake wasiendelee kutapeliwa!.

Namalizia kwa ile hoja ya msingi jee kuna haja ya serikali iingilie kati shughuli za haya makanisa ya wakovu ya miujiza ili Watanzania masikini wa kutupwa, wasiendelee kukamuliwa mamilioni kwa utapeli, huku wahubiri wakizidi kunona kwa kuwa mamilionea!.

Naomba kuwasilisha.

Paskali
Kanisa lako lenyewe lina mlolongo wa sadaka,kuna masikini nako wanaokamuliwa...labda tu serikali ipitie upenyo wa 'tiba' huko kwenye makanisa ya maajabu,kwamba iwatake wathibitishe wanaponyaje
 
Hizo ni biashara za watu...Labda kwa ushauri taasisi za ya kidini (wakristo) wakemee kwa kufanyoa usajili hayo makanisa ili kuwabana wahusika..

Matendo hayo yanaleta image mbaya kwa taasisi na wakristo wote ,ni vizuri taasisi kubwa za kikristo kuwa na mamlaka ya kukemea hata kufngua hao manabii
Pamoja na udini sana ulionao leo umeongea point sana, kumbe kuna muda huwa unakuwaga na akili.
 
Pascal Mayalla , Sifa ya mwanaume kamili ni kuwa na msimamo, na kusimamia kule unachokiamini

Hivi wewe kama mwandishi... Ni lini utaandika nyuzi zilizojitisheleza na kuacha nyuzi za kuandika kwa kuuliza!?

Wewe ni mwandishi, unakuwa Muoga Muoga unashindwa kuandika kama waandishi wengine!? ... Kisa unaogopa kuitwa na kuhojiwa!?

Umri ulishaenda... Usitegemee uteuzi mkuu!... Punguza uchawa!
 
Back
Top Bottom