Serikali iingilie kati Makanisa ya Miujiza? Watanzania masikini wa kutupwa wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli huku wahubiri wakigeuka mamilionea

Serikali iingilie kati Makanisa ya Miujiza? Watanzania masikini wa kutupwa wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli huku wahubiri wakigeuka mamilionea


Serikali ina kazi moja tu na ni ndogo sana. Waige alichofanya Kagame na wala kuiga mazuri sio kosa. Sheria itungwe, mtu asiruhusiwe kufungua kanisa mpaka awe na degree ya theology.

Baada ya hapo watakaokubali kutapeliwa waendelee.
Kwani mwenye degree ya theology hawezi kuwa mpigaji?

Si ndiyo atakupiga ki degree degree ya theology hapo?
 
Inasikitisha sn ndo kwanza viongozi wakubwa wasaka madaraka wanachangia ujenzi wa makanisa hayo.

Yani watanzania wanaishi kwa kubahatisha sana
 
Wanabodi

Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa. Topic ya leo, ni kutoa wito kwa Serikali yetu kuingilia kati kitu kinachoendelea kwenye baadhi ya makanisa ya wakovu yanayojinasibu kufanya miujiza, kutoa mapepo, kutoa uchawi na kufanya miujiza ya uponyaji?.

Baadhi ya wahubiri hawa wanatumia nguvu za giza za kiini macho kwa kitu kinachoitwa auto suggestion kwa Watanzania Masikini wa Kutupwa, kuaminishwa umasikini wao ni kwasababu wamelogwa, hivyo ili kuuondoa uchawi wa umasikini, unatakiwa kufanya appointment kumuona Mtumishi, ambapo utapangiwa kiwango cha fedha kumuona mtumishi.

Kwenye matangazo yao kupitia redio na TV, unaambiwa njoo na sadaka yako bila kuambiwa kiwango. Ukifika kanisani,
utaandikishwa na kuambiwa kiwango cha kumuona mtumishi akueleze jinsi ulivyologwa na ni nani amekuloga. Kiwango kilianzia 10,000, baadae ikawa 20,000, ikapanda kuwa 50,000, 100,000 sasa ni 200,000.

Unatakiwa kuitafuta hiyo pesa popote ulipe ndipo umuone mtumishi. Hivyo ni waumini wenye pesa tuu ndio watamuona mtumishi!.

Baada ya kuingia kumuona, mtumishi atakuambia prophesy yako na ku conclude matatizo yako yote, ya kiuchumi, umasikini, maradhi, au majanga yoyote, ni umelongwa na watu wa jijijini kwako!.

Baada ya hapo sasa ndio utapewa bili ya sadaka. Mtumishi atajifanya anamuuliza Mungu, then unaambiwa Mungu amesema njoo na sadaka ya milioni 2, 5, 10, 20, kutegemea na ukubwa wa tatizo lako, ya kuleta hiyo sadaka ndipo Mungu atalimaliza tatizo lako!.

Kutokana na wewe kuwa ni tayari umesha pigwa ganzi, utakwenda kuzitafuta hizo pesa na kuzileta cash!.

Watanzania masikini wa kutupwa, wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli, na baadhi ya hawa ma Pastor, huku hao ma Pastor na wahubiri wakineemeka na kuageuka mamilionea na mabilionea huku wakivuta mi ndinga ya nguvu!.

Kuna Mama mmoja alifiwa na mtoto wake, the only son, amedanganywa mtoto wake hajafa, amechukuliwa tuu kichawi, mama kaambiwa akatafute sadaka kiasi fulani, arejeshewe mwanae!, huyo mama ana haha kusaka hiyo pesa ili kumrejesha mwanae!.

Japo haya ni mambo ya imani, na waumini wanakwenda wenyewe kwa hiyari yao na wana toa fedha kwa ridhaa zao, na serikali yetu imetoa uhuru wa kuabudu, lakini ikifikia kiwango Watanzania wanatapeliwa, serikali ina wajibu wa kuingilia kati wananchi wake wasiendelee kutapeliwa!.

Namalizia kwa ile hoja ya msingi jee kuna haja ya serikali iingilie kati shughuli za haya makanisa ya wakovu ya miujiza ili Watanzania masikini wa kutupwa, wasiendelee kukamuliwa mamilioni kwa utapeli, huku wahubiri wakizidi kunona kwa kuwa mamilionea!.

Naomba kuwasilisha.

Paskali
Update

Mkuu Mywangu, usimwingize Mtumishi kweli wa Mungu, Kuhani Mussa, kumuona Kuhani Musa ni bure ila unaweza kuleta sadaka yako yoyote.

Kazi ya ujenzi wa Ngome ya Yesu pale Kimara Temboni, inafanyika kupitia kadi zinaitwa Partnership, hupangiwi kiwango, unajifanyia personal assessment ndipo unajaza!.

Watumishi matapeli kumuona ni lazima utoe 200,000, kuna watu walikuwa na 100,000 walitoa na zikapokelewa, watu wa 200,000 walipoongezeka, wale wa 100,000 walirudishiwa fedha zao, wakaambiwa wakadundulize mpaka zitimie 200,000 ndipo warudi.

Ukimuona Kuhani Mussa anakuombea na kukupatia vifaa vya kiroho bure extra utalipia lakini kuwaona matapeli hawa, unatakiwa kwenda kuleta kwanza sadaka, with the amount, from 6 figures ndipo uombewe!.

P
Kwani Kuna mtu huwa anawachapa fimbo ili waende Makanisani kwa lazima???

Watu wanajipeleka wenyewe kuibiwa, wewe unaumia utadhani huwa wanatoa pesa zako.

Acha wajanja akina Lusekelo waendesha ndinga za maana.
 
Serikali haiwezi kuingilia uhuru wa kuabudu. Acha waendelee kupigwa maana ni wabishi sana
Umeiweka kifupi na kibabe lakini ukweli ndio huu.

Unaweza kumdaka mchungaji kama kafanya kosa la jinai, mfano akifanya kosa la money laundering kuchukua pesa chafu na kuzipitisha kanisani makusudi huku akijua hizi pesa chafu, halafu kuwarudishia wahalifu zimetakasishwa kanisani kwenye akaunti za kanisa, ukathibitisha knowledge na intent, hapo unaserereka naye. Na hata hiyo si kesi rahisi, ni kesi complex.

Ila, haya mambo ya kuwapiga watu pesa za sadaka, tena kuzitumia kujenga kanisa, kununua magari ya mchungaji, ku support lifestyle ya mchungaji, hapo ni vigumu sana kumshitaki huyo mchungaji, kwa sababu kimsingi hakuna sheria inayovunjwa. Watu wanatoa hela zao wenyewe bila kulazimishwa, katika jambo complex sana la imani ambalo limepewa kinga kikatiba. Yani kuna kinga ya kikatiba ya mtu mjinga kutoa hela yake na kuliwa na mchungaji wake.

Hapo kitu cha kufanya ni kuongeza elimu kwa watu wayastukie haya makanisa na kujiongeza wenyewe.

Na hii ni kazi yetu sote, si kazi ya serikali tu.

Marufuku za serikali haziwezi kumaliza tatizo hili. Ukipiga marufuku ndiyo kwanza watu wanaenda underground.

Ukristo una uzoefu mkubwa sana wa kukua huku ukipigwa vita na serikali, tangu enzi za utawala wa Warumi.

Ukisoma hata vitabu vya Mtume wa Wakristo Paul, utaona jinsi Wakristo walivyokuwa wanafanyiwa figisu na serikali, na Paul alivyokuwa anawapa moyo wapambanie imani yao.

Serikali ikitunga sheria kuwabana hawa wachungaji, ndiyo kwanza wataenda underground na kuwapa waumini wao aya zinazosema kuwa siku za mwisho atakuwepo mpinga Kristo atakayekuja kulisakama kanisa, watasema serikali ndiye huyo mpinga Kristo. Matokeo yake watapata huruma zaidi kutoka kwa waumini wao ambao watakubali kuwa serikali ni mpinga Kristo aliyetabiriwa kwenye Biblia.

Marufuku ya serikali itawaongezea kiki hawa wachungaji.

Hapa hakuna njia ya kuepuka kuongeza level ya elimu kwa watu wote, na kujenga utamaduni wa kukataa hizi habari za miujuza.

Ndiyo maana kila siku nasisitiza sana watu wajikite kwenye mambo ya uthibitisho, kuachana na habari za kuamini amini mambo tu.
 
Kwani Kuna mtu huwa anawachapa fimbo ili waende Makanisani kwa lazima???

Watu wanajipeleka wenyewe kuibiwa, wewe unaumia utadhani huwa wanatoa pesa zako.

Acha wajanja akina Lusekelo waendesha ndinga za maana.
Ni uhalifu kama uhalifu wa upatu unapaswa kukemewa na kushughulikiwa. Kwa hiyo tapeli akimtaja Mungu basi asichukuliwe hatua? Basi sasa matapeli wote wamepata njia isiyo na usumbufu ya kutapeli kwa raha zao!
 
Ni ujinga tu. Wewe kama unahitaji kitu kutoka kwa mzazi wako eti mpaka upitie kwa ndugu yako au jirani yako akakuombee. Huo siyo ukristo ni ushirikina na ushetani tu.
Of course, kuomba kwa kupitia mtu mwingine ni jambo la kawaida. Kuna baadhi ya familia mtoto anaomba kitu fulani kwa baba yake kupitia mama yake au mtu ambaye baba yake anapenda kumsikiliza. Kuna pia kuomba msamaha kupitia mtu au watu wengine au kuomba kazi kwa bosi kupitia rafiki yake etc. Haya mambo huwa yapo.
 
Umeiweka kifupi na kibabe lakini ukweli ndio huu.

Unaweza kumdaka mchungaji kama kafanya kosa la jinai, mfano akifanya kosa la money laundering kuchukua pesa chafu na kuzipitisha kanisani makusudi huku akijua hizi pesa chafu, halafu kuwarudishia wahalifu zimetakasishwa kanisani kwenye akaunti za kanisa, ukathibitisha knowledge na intent, hapo unaserereka naye. Na hata hiyo si kesi rahisi, ni kesi complex.

Ila, haya mambo ya kuwapiga watu pesa za sadaka, tena kuzitumia kujenga kanisa, kununua magari ya mchungaji, ku support lifestyle ya mchungaji, hapo ni vigumu sana kumshitaki huyo mchungaji, kwa sababu kimsingi hakuna sheria inayovunjwa. Watu wanatoa hela zao wenyewe bila kulazimishwa, katika jambo complex sana la imani ambalo limepewa kinga kikatiba. Yani kuna kinga ya kikatiba ya mtu mjinga kutoa hela yake na kuliwa na mchungaji wake.

Hapo kitu cha kufanya ni kuongeza elimu kwa watu wayastukie haya makanisa na kujiongeza wenyewe.

Na hii ni kazi yetu sote, si kazi ya serikali tu.

Marufuku za serikali haziwezi kumaliza tatizo hili. Ukipiga marufuku ndiyo kwanza watu wanaenda underground.

Ukristo una uzoefu mkubwa sana wa kukua huku ukipigwa vita na serikali, tangu enzi za utawala wa Warumi.

Ukisoma hata vitabu vya Mtume wa Wakristo Paul, utaona jinsi Wakristo walivyokuwa wanafanyiwa figisu na serikali, na Paul alivyokuwa anawapa moyo wapambanie imani yao.

Serikali ikitunga sheria kuwabana hawa wachungaji, ndiyo kwanza wataenda underground na kuwapa waumini wao aya zinazosema kuwa siku za mwisho atakuwepo mpinga Kristo atakayekuja kulisakama kanisa, watasema serikali ndiye huyo mpinga Kristo. Matokeo yake watapata huruma zaidi kutoka kwa waumini wao ambao watakubali kuwa serikali ni mpinga Kristo aliyetabiriwa kwenye Biblia.

Marufuku ya serikali itawaongezea kiki hawa wachungaji.

Hapa hakuna njia ya kuepuka kuongeza level ya elimu kwa watu wote, na kujenga utamaduni wa kukataa hizi habari za miujuza.

Ndiyo maana kila siku nasisitiza sana watu wajikite kwenye mambo ya uthibitisho, kuachana na habari za kuamini amini mambo tu.
Well said kaka
 
Wanabodi

Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa. Topic ya leo, ni kutoa wito kwa Serikali yetu kuingilia kati kitu kinachoendelea kwenye baadhi ya makanisa ya wakovu yanayojinasibu kufanya miujiza, kutoa mapepo, kutoa uchawi na kufanya miujiza ya uponyaji?.

Baadhi ya wahubiri hawa wanatumia nguvu za giza za kiini macho kwa kitu kinachoitwa auto suggestion kwa Watanzania Masikini wa Kutupwa, kuaminishwa umasikini wao ni kwasababu wamelogwa, hivyo ili kuuondoa uchawi wa umasikini, unatakiwa kufanya appointment kumuona Mtumishi, ambapo utapangiwa kiwango cha fedha kumuona mtumishi.

Kwenye matangazo yao kupitia redio na TV, unaambiwa njoo na sadaka yako bila kuambiwa kiwango. Ukifika kanisani,
utaandikishwa na kuambiwa kiwango cha kumuona mtumishi akueleze jinsi ulivyologwa na ni nani amekuloga. Kiwango kilianzia 10,000, baadae ikawa 20,000, ikapanda kuwa 50,000, 100,000 sasa ni 200,000.

Unatakiwa kuitafuta hiyo pesa popote ulipe ndipo umuone mtumishi. Hivyo ni waumini wenye pesa tuu ndio watamuona mtumishi!.

Baada ya kuingia kumuona, mtumishi atakuambia prophesy yako na ku conclude matatizo yako yote, ya kiuchumi, umasikini, maradhi, au majanga yoyote, ni umelongwa na watu wa jijijini kwako!.

Baada ya hapo sasa ndio utapewa bili ya sadaka. Mtumishi atajifanya anamuuliza Mungu, then unaambiwa Mungu amesema njoo na sadaka ya milioni 2, 5, 10, 20, kutegemea na ukubwa wa tatizo lako, ya kuleta hiyo sadaka ndipo Mungu atalimaliza tatizo lako!.

Kutokana na wewe kuwa ni tayari umesha pigwa ganzi, utakwenda kuzitafuta hizo pesa na kuzileta cash!.

Watanzania masikini wa kutupwa, wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli, na baadhi ya hawa ma Pastor, huku hao ma Pastor na wahubiri wakineemeka na kuageuka mamilionea na mabilionea huku wakivuta mi ndinga ya nguvu!.

Kuna Mama mmoja alifiwa na mtoto wake, the only son, amedanganywa mtoto wake hajafa, amechukuliwa tuu kichawi, mama kaambiwa akatafute sadaka kiasi fulani, arejeshewe mwanae!, huyo mama ana haha kusaka hiyo pesa ili kumrejesha mwanae!.

Japo haya ni mambo ya imani, na waumini wanakwenda wenyewe kwa hiyari yao na wana toa fedha kwa ridhaa zao, na serikali yetu imetoa uhuru wa kuabudu, lakini ikifikia kiwango Watanzania wanatapeliwa, serikali ina wajibu wa kuingilia kati wananchi wake wasiendelee kutapeliwa!.

Namalizia kwa ile hoja ya msingi jee kuna haja ya serikali iingilie kati shughuli za haya makanisa ya wakovu ya miujiza ili Watanzania masikini wa kutupwa, wasiendelee kukamuliwa mamilioni kwa utapeli, huku wahubiri wakizidi kunona kwa kuwa mamilionea!.

Naomba kuwasilisha.

Paskali
Update

Mkuu Mywangu, usimwingize Mtumishi kweli wa Mungu, Kuhani Mussa, kumuona Kuhani Musa ni bure ila unaweza kuleta sadaka yako yoyote.

Kazi ya ujenzi wa Ngome ya Yesu pale Kimara Temboni, inafanyika kupitia kadi zinaitwa Partnership, hupangiwi kiwango, unajifanyia personal assessment ndipo unajaza!.

Watumishi matapeli kumuona ni lazima utoe 200,000, kuna watu walikuwa na 100,000 walitoa na zikapokelewa, watu wa 200,000 walipoongezeka, wale wa 100,000 walirudishiwa fedha zao, wakaambiwa wakadundulize mpaka zitimie 200,000 ndipo warudi.

Ukimuona Kuhani Mussa anakuombea na kukupatia vifaa vya kiroho bure extra utalipia lakini kuwaona matapeli hawa, unatakiwa kwenda kuleta kwanza sadaka, with the amount, from 6 figures ndipo uombewe!.

P
..,Ndio maana Tapeli ' Kiboko ya Wachawi' aliwaingiza Wengi Mkenge!!!....na badohawakomi. 'Watu wangu wanaamhamia Kwa Kukosa Maarifa' !....Kweli.
 
Umeiweka kifupi na kibabe lakini ukweli ndio huu.

Unaweza kumdaka mchungaji kama kafanya kosa la jinai, mfano akifanya kosa la money laundering kuchukua pesa chafu na kuzipitisha kanisani makusudi huku akijua hizi pesa chafu, halafu kuwarudishia wahalifu zimetakasishwa kanisani kwenye akaunti za kanisa, ukathibitisha knowledge na intent, hapo unaserereka naye. Na hata hiyo si kesi rahisi, ni kesi complex.

Ila, haya mambo ya kuwapiga watu pesa za sadaka, tena kuzitumia kujenga kanisa, kununua magari ya mchungaji, ku support lifestyle ya mchungaji, hapo ni vigumu sana kumshitaki huyo mchungaji, kwa sababu kimsingi hakuna sheria inayovunjwa. Watu wanatoa hela zao wenyewe bila kulazimishwa, katika jambo complex sana la imani ambalo limepewa kinga kikatiba. Yani kuna kinga ya kikatiba ya mtu mjinga kutoa hela yake na kuliwa na mchungaji wake.

Hapo kitu cha kufanya ni kuongeza elimu kwa watu wayastukie haya makanisa na kujiongeza wenyewe.

Na hii ni kazi yetu sote, si kazi ya serikali tu.

Marufuku za serikali haziwezi kumaliza tatizo hili. Ukipiga marufuku ndiyo kwanza watu wanaenda underground.

Ukristo una uzoefu mkubwa sana wa kukua huku ukipigwa vita na serikali, tangu enzi za utawala wa Warumi.

Ukisoma hata vitabu vya Mtume wa Wakristo Paul, utaona jinsi Wakristo walivyokuwa wanafanyiwa figisu na serikali, na Paul alivyokuwa anawapa moyo wapambanie imani yao.

Serikali ikitunga sheria kuwabana hawa wachungaji, ndiyo kwanza wataenda underground na kuwapa waumini wao aya zinazosema kuwa siku za mwisho atakuwepo mpinga Kristo atakayekuja kulisakama kanisa, watasema serikali ndiye huyo mpinga Kristo. Matokeo yake watapata huruma zaidi kutoka kwa waumini wao ambao watakubali kuwa serikali ni mpinga Kristo aliyetabiriwa kwenye Biblia.

Marufuku ya serikali itawaongezea kiki hawa wachungaji.

Hapa hakuna njia ya kuepuka kuongeza level ya elimu kwa watu wote, na kujenga utamaduni wa kukataa hizi habari za miujuza.

Ndiyo maana kila siku nasisitiza sana watu wajikite kwenye mambo ya uthibitisho, kuachana na habari za kuamini amini mambo tu.
Respect my comrade! Ila bado tuna safari ndefu sana. Sijui kama kizazi chetu hiki tunaweza kukibadilisha kifikra . Tumejitahidi mno kutoa elimu sijui labda wapo wachache waliobadilika na kuachana na huu upumbavu wa miujiza ambao hata huyo Yesu wanayemwamini alikemea vikali tabia hiyo na kuifananisha na UZINZI.
 
Of course, kuomba jambo Kwa kupitia mtu mwingine ni la kawaida. Kuna baadhi ya familia mtoto anagomba kitu fulani kwa baba yake kupitia mama yake au mtu ambaye baba yake anapenda kumsikiliza. Kuna pia kuomba msamaha kupitia mtu au watu wengine au kuomba kazi Kwa bosi kupitia rafiki yake etc. Haya mambo huwa yapo.
Ni sawa kabisa hata biblia inasema tuombeane lakini sasa imegeuka kuwa ndiyo excuse ya mtu kuacha jitihada za kujiweka karibu na Mungu wake na kutumainia mwanadamu mwingine amuombee. Hii ni ibada ya sanamu na chukizo mbele za Mungu
 
..,Ndio maana Tapeli ' Kiboko ya Wachawi' aliwaingiza Wengi Mkenge!!!....na badohawakomi. 'Watu wangu wanaamhamia Kwa Kukosa Maarifa' !....Kweli.
Na kuna wengine wapo tena hewani kwa style ile ile ya kiboko wa wachawi. Fungulia hivyo viredio vyao utamsikia
 
Mkuu sr
Wanabodi

Kama kawa kila nipatapo fursa huja na makala zangu elimishi za kwa maslahi ya taifa. Topic ya leo, ni kutoa wito kwa Serikali yetu kuingilia kati kitu kinachoendelea kwenye baadhi ya makanisa ya wakovu yanayojinasibu kufanya miujiza, kutoa mapepo, kutoa uchawi na kufanya miujiza ya uponyaji?.

Baadhi ya wahubiri hawa wanatumia nguvu za giza za kiini macho kwa kitu kinachoitwa auto suggestion kwa Watanzania Masikini wa Kutupwa, kuaminishwa umasikini wao ni kwasababu wamelogwa, hivyo ili kuuondoa uchawi wa umasikini, unatakiwa kufanya appointment kumuona Mtumishi, ambapo utapangiwa kiwango cha fedha kumuona mtumishi.

Kwenye matangazo yao kupitia redio na TV, unaambiwa njoo na sadaka yako bila kuambiwa kiwango. Ukifika kanisani,
utaandikishwa na kuambiwa kiwango cha kumuona mtumishi akueleze jinsi ulivyologwa na ni nani amekuloga. Kiwango kilianzia 10,000, baadae ikawa 20,000, ikapanda kuwa 50,000, 100,000 sasa ni 200,000.

Unatakiwa kuitafuta hiyo pesa popote ulipe ndipo umuone mtumishi. Hivyo ni waumini wenye pesa tuu ndio watamuona mtumishi!.

Baada ya kuingia kumuona, mtumishi atakuambia prophesy yako na ku conclude matatizo yako yote, ya kiuchumi, umasikini, maradhi, au majanga yoyote, ni umelongwa na watu wa jijijini kwako!.

Baada ya hapo sasa ndio utapewa bili ya sadaka. Mtumishi atajifanya anamuuliza Mungu, then unaambiwa Mungu amesema njoo na sadaka ya milioni 2, 5, 10, 20, kutegemea na ukubwa wa tatizo lako, ya kuleta hiyo sadaka ndipo Mungu atalimaliza tatizo lako!.

Kutokana na wewe kuwa ni tayari umesha pigwa ganzi, utakwenda kuzitafuta hizo pesa na kuzileta cash!.

Watanzania masikini wa kutupwa, wanakamuliwa mamilioni kwa utapeli, na baadhi ya hawa ma Pastor, huku hao ma Pastor na wahubiri wakineemeka na kuageuka mamilionea na mabilionea huku wakivuta mi ndinga ya nguvu!.

Kuna Mama mmoja alifiwa na mtoto wake, the only son, amedanganywa mtoto wake hajafa, amechukuliwa tuu kichawi, mama kaambiwa akatafute sadaka kiasi fulani, arejeshewe mwanae!, huyo mama ana haha kusaka hiyo pesa ili kumrejesha mwanae!.

Japo haya ni mambo ya imani, na waumini wanakwenda wenyewe kwa hiyari yao na wana toa fedha kwa ridhaa zao, na serikali yetu imetoa uhuru wa kuabudu, lakini ikifikia kiwango Watanzania wanatapeliwa, serikali ina wajibu wa kuingilia kati wananchi wake wasiendelee kutapeliwa!.

Namalizia kwa ile hoja ya msingi jee kuna haja ya serikali iingilie kati shughuli za haya makanisa ya wakovu ya miujiza ili Watanzania masikini wa kutupwa, wasiendelee kukamuliwa mamilioni kwa utapeli, huku wahubiri wakizidi kunona kwa kuwa mamilionea!.

Naomba kuwasilisha.

Paskali
Update

Mkuu Mywangu, usimwingize Mtumishi kweli wa Mungu, Kuhani Mussa, kumuona Kuhani Musa ni bure ila unaweza kuleta sadaka yako yoyote.

Kazi ya ujenzi wa Ngome ya Yesu pale Kimara Temboni, inafanyika kupitia kadi zinaitwa Partnership, hupangiwi kiwango, unajifanyia personal assessment ndipo unajaza!.

Watumishi matapeli kumuona ni lazima utoe 200,000, kuna watu walikuwa na 100,000 walitoa na zikapokelewa, watu wa 200,000 walipoongezeka, wale wa 100,000 walirudishiwa fedha zao, wakaambiwa wakadundulize mpaka zitimie 200,000 ndipo warudi.

Ukimuona Kuhani Mussa anakuombea na kukupatia vifaa vya kiroho bure extra utalipia lakini kuwaona matapeli hawa, unatakiwa kwenda kuleta kwanza sadaka, with the amount, from 6 figures ndipo uombewe!.

Mkuu serikali ndo inapenda hao wajinga wazidi kuongeza ujinga ili iwerahisi kwao kuwatawala kama mifugo!...
 
Serikali ndo inawapenda hao wajinga na inafurahi wanavyoongezwa ujinga ili iwe rahisi kuwatawala kama mifugo
 
Mkuu we a secular state. You being a lawyer unajua human rights mojawapo ni freedom to religion! Unless kuna mambo ambayo extremist sadaka wacha wakamuliwe wajinga hao.
 
Serikali haina mamlaka kuwapangia wananchi nini cha kuamini na nini cha kutoamini kitendo hicho cha serikali kuingilia uhuru wa kiimani wa jamii fulani ni kinyume na matakwa ya katiba ya JMT.

Ukiruhusu serikali iingilie na kupangia taratibu imani fulani tambua fika na imani yako umeikabidhi mikononi mwa serikali anaweza tokea kiongozi akaona imani yako ni ya kishenzi na akamua lolote atakalo juu ya imani yako na usiwe na nguvu ya kikatiba kupinga hilo.

Tanzania kila mtu yupo huru kiimani kwa kuzingatia katiba ya JMT tuheshimu hilo.
Kama ni hivyo ndio maana matapeli wengi wamepata green pastures. Ukijificha kwenye dini unatapeli kwa raha zako bila bugudha! Hii ni hatari kwa taifa.
 
Mimi Napendekeza SIRIKALI ipitishe kodi ya 30% kwenye makusanyo yanayo patikana kupitia ayo makanisa ili tuweze kupata vyanzo VIPYA vya mapato 🤗🤗
Watoze kodi kwenye mapato haramu? Maana mapato yanatokana na kuwahubiria watu uongo!
 
Kosa ni Kukamuliwa au Kosa ni Makanisa ya Miujiza ?

Ukiniuliza takwambia hizi Imani karibia zote (Opium of the Mass) ni mwendo wa Makamuzi hivyo usingepigilia mstari yapi ya kuingilia kati bali labda useme waangalia ni watu Sheria zetu za Nchi zimevunjwa.... Na katika sheria hizo wasiangalia cha Mhazini, mnadi Sala wala Mswalia Mtume.....
 
Back
Top Bottom