Serikali iitishe kura ya maoni Wazanzibari waamue upya kama wanautaka muungano ili isionekane tunawalazimisha

Zanzibar ingekuwa huru, ingepinga hatua kubwa kimaendeleo na ingepata fursa nyingi kuliko kuendelea kukaliwa na mkoloni Tanganyika
Comoro na Madagascar ni visiwa huru, kuna maendeleo yoyote ya maana?
 
Ukanda wa pwani hawawezi kuupata.

Haijawahi kutokea mahali popote Duniani, kisiwa kumiliki inland, ila kuna inland countries nyingi zinazomiliki visiwa.
Kasema kimhemko tu na udini, toka lini kisiwa kikawa na inland 🤣
 
Wazibar walioko Tanganyika,wote wahame,warudi Zanzibar,hiyo ni kura ya maoni tosha,kama hawataki muungano.
Mkuu kwani wale wasomali pale Ilala au Wahindi kule Posta tumeungana nao?

Kuishi somewhere hakuhusiani na muungano.
 
Na sisi Watanganyika tuulizwe kama tunautaka muungano.Huyo kupe katuchosha maana ni jeuri.
 
Nyerere alikosea sana hicho kisiwa kinatakiwa kuchukuliwa jumla kama India alivyofanya pale Kashmir.
 
Kwa Leo ni kama gumu ipo siku litawezekana kwa mtutu wa bunduki
 
Ni sawa
 
Hakuna Uhuru wa kugawa nchi! Wwchaga hawawezi kuamka kesho asubuh na kutaka kujitenga, kwa sababu yoyote ile! Hilo ni kosa la uhaini! Muungsno sio tatizo hata kidogo, tatizo ni siasa mbovu za ccm!
 
Wakitaka tuwaongezee na mafia
 
Mkishaungana. Kuulinda sio lelemama. Mfano wa Kosovo ilikuwa nguvu kutoka nje kama hao wanaolialia Zanzibar dhidi ya muungano. India ina majimbo 3 yanatawaliwa kutoka serikali kuu kwa sababu ya vuguvugu ya kujitenga. Qubec, Canada ukiwaachia kidogo tu wanameguka. California, USA inatamani mpaka kesho imeguke kutoka ilipo. Catalunya, Hispania vuguvugu ni hizo hizo lakini dola ipo lazima ilinde eneo lake. Hakuna dola inapenda ardhi yake imeguke.
muungano udumu tu na matatizo yaliyopo.
 
Kura ya maoni ya nini wakati wa muungano watu hawakuulizwa. Kwanza muungano uvunjwe alafu anayetaka muungano aseme kama hawa Comoro
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…