Serikali ije na mkakati wa kuhakikisha mabenki na mitandao ya simu wanapunguza gharama za kuhamisha fedha kielektroniki

Serikali ije na mkakati wa kuhakikisha mabenki na mitandao ya simu wanapunguza gharama za kuhamisha fedha kielektroniki

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Hivi sasa mabenki wanatutumia sms wakitushauri tuache utaratibu wa kufanya miamala kwa kutumia cash money na badala yake tutumie huduma za kielektroniki(mobile banking) kufanya miamala hiyo kama njia mojawapo ya kupambana na ugonjwa wa corona.

Binafsi naupokea ushauri huo ila nawashauri kwanza wao wenyewe(mabenki na makampuni ya simu za mikononi) wajiongeza kwa kupunguza gharama za kufanya miamala husika ili kui-encourage watu kutumia huduma hizo na sio wao ku-focus tu katika kufanya kibiashara i wakati hili tatizo kwa sasa ni jambo la dharura hivyo nao wao wanapaswa kuli-handle kidharura ikiwa ni pamoja na kushusha gharama za kutumia huduma hizi za kimtandao.

Vile vile,katika kuhamasisha matumizi ya simu za mikunoni kufanya miamala hii,nawashauri watazame upya vigezo na mashari vilivyopo, mfano kukatwa hela hata kama huduma ulioomba imefeli/haijafika mwisho lakini wao wanakata tuhela kwenye simu yako na kwenye akaunti yako ya benki bila kujali huduma uliohitaji imekamilika(hili jambo huo nalliona ni kama kuibia wateja).

Mwisho,napenda kuishauri serikali kuwa huu ndio wakati muafaka wa kupeleka miswaada/sheria Bungeni kwa hati ya dharura ili kutunga sheria au kurekebisha sheria zinazoweza kusaidia kupambana na janga hili endapo ugonjwa huu utageuka tishio humu nchini na mojawapo ya mabadiliko nayopendekeza(iwapo kutakuwa na huo ulazima kulingana na hali ya huu ugonjwa) ni kupunguza kodi ya kufanya miamala kwa njia za kieletroniki.

Hivyo, Serikali kupitia BOT,TCRA na Wizara ya Fedha, huu ni wakati wa nyie ku-monitor hii situation na kufanya kile kilicho katika mamlaka yenu katika kupambana na janga hili na mojawapo ni kutazama pendekezo hili iwapo hali ya ugonjwa huu kweli italazimisha hatua kama hizo kuchukuliwa.

Kila mtu kwa nafasi yake ni mdau katika hili janga kwani linagusa karibu kila eneo mbali na kugusu karibu kila mtu kiuchumi na kijamii.
 
Kufa kufaana, huu ndio wakati wetu Benki ku boost mapato kupitia sim banking.
 
Yako ambayo yanatuchanganya yanatufanya tuonekane ni watz tuliogawanyikana hasa ya kisiasa, lkn kuna mambo ambayo yanatutambulisha kama Wa Tz wamoja kama hivi, @salarysilp nimekukubali haswaa
 
Active Mod Five Mod Four naomba mfanye marekebisho heading ya huu uzi ili uanze na maneno haya ya utangulizi:

Vita dhidi ya Corona:

AU

katika kupambana na Conoravirus,
 
Katika Kipindi hiki kigumu cha COVID-19, Serikali ulimwenguni zinasaidia wananchi wake. Tanzania kuna wananchi wanyonge na masikini wengi, hawana akiba ya fedha, kwa sababu ya udogo wa kipato.

Mfano, Sekta ya Utalii imepata pigo kubwa, wafanyakazi kupewa likizo bila malipo. Pia kukosekana mapato katika tourism, agriculture consumers imedrop mno, Kilimo kimeathirika, wakulima wameathirika kimapato.

Ni vigumu kugawa pesa kama USA, Serikali ifanye Subsdize katika huduma muhimu kama Unga, Mafuta kupikia, Gesi ya kupikia, Umeme. Serikali ipunguze kodi katika hizi bidhaa ili zipungue bei na wanyonge wasiteseke. Kuna PESA za Mwenge na pesa za maafa ..ziende huko.

Serikali iongee na Bakresa na Mo, na wazalishaji wengine, ili Wapunguze bei za unga na Mafuta, then Serikali ifidie. Na Wasambazaji wa gesi za majumbani, serikali iongee nao, gesi ipungue bei...Pili itaokoa mazingira na kufuta matumizi ya mkaa.

Wabunge wote, na wanaharakati, muishauri serikali.
 
Hao unaowataka wahakikishe gharama zinashuka ndio hao hao wanaosababisha zinakuwa kubwa.

- Fines zisizoeleweka kutoka TCRA kila wakijisikia

- Sera zisizotabirika ( mtu anaamka tu anaamua kuzima SimCards za wateja bila maandalizi )

- Siasa kuingilia faragha za wateja na kujenga taswira ya makampuni kutokuaminika.

Kwa nchi takataka kama Tanzania hayo makampuni yanapata faida kwa janja janja tu, ndio maana kila kampuni ya simu inaendesha bahati nasibu za kijanja janja.

Unatumiwa SMS kama 'Umejishindia Tsh 100, Tuma Neno MSHINDI kwenda 1557 na utakatwa Tsh 100/Sms.
 
Katika Kipindi hiki kigumu cha COVID-19, Serikali ulimwenguni zinasaidia wananchi wake. Tanzania kuna wananchi wanyonge na masikini wengi, hawana akiba ya fedha, kwa sababu ya udogo wa kipato.

Mfano, Sekta ya Utalii imepata pigo kubwa, wafanyakazi kupewa likizo bila malipo. Pia kukosekana mapato katika tourism, agriculture consumers imedrop mno, Kilimo kimeathirika, wakulima wameathirika kimapato.

Ni vigumu kugawa pesa kama USA, Serikali ifanye Subsdize katika huduma muhimu kama Unga, Mafuta kupikia, Gesi ya kupikia, Umeme. Serikali ipunguze kodi katika hizi bidhaa ili zipungue bei na wanyonge wasiteseke. Kuna PESA za Mwenge na pesa za maafa ..ziende huko.

Serikali iongee na Bakresa na Mo, na wazalishaji wengine, ili Wapunguze bei za unga na Mafuta, then Serikali ifidie. Na Wasambazaji wa gesi za majumbani, serikali iongee nao, gesi ipungue bei...Pili itaokoa mazingira na kufuta matumizi ya mkaa.

Wabunge wote, na wanaharakati, muishauri serikali.
Una mawazo mazuri sana, shida ni watekelezaji kuyapokea na kuyafanyia kazi.
 
Hao unaowataka wahakikishe gharama zinashuka ndio hao hao wanaosababisha zinakuwa kubwa.

- Fines zisizoeleweka kutoka TCRA kila wakijisikia

- Sera zisizotabirika ( mtu anaamka tu anaamua kuzima SimCards za wateja bila maandalizi )

- Siasa kuingilia faragha za wateja na kujenga taswira ya makampuni kutokuaminika.

Kwa nchi takataka kama Tanzania hayo makampuni yanapata faida kwa janja janja tu, ndio maana kila kampuni ya simu inaendesha bahati nasibu za kijanja janja.

Unatumiwa SMS kama 'Umejishindia Tsh 100, Tuma Neno MSHINDI kwenda 1557 na utakatwa Tsh 100/Sms.
Gonjwa hili linakwenda kuathiri vipato vya watu na hivyo kupunguza uwezo wa watu wa kufanya manunuzi, kwahiyo wasipojiongeza,watu watashindwa kumudu gharama na mwisho wa siku hata makampuni haya nayo yatayumba kama sio kufungwa kabisa unless ugonjwa huu utaishia kuwa hatari kwenye media tu kwa hapa kwetu.
 
Leo BoT wametoa taarifa kwamba noti na sarafu za Tanzania zimetengenezwa kwa kiwango na ubora ambao haziwi contaminated na coronavirus (COVID-19) never ever. So, kwa maelezo hayo ya BoT ambaye ndiye custodian wa noti na sarafu za nchi hii, shaka ondoa Mkuu.
 
Leo BoT wametoa taarifa kwamba noti na sarafu za Tanzania zimetengenezwa kwa kiwango na ubora ambao haziwi contaminated na coronavirus (COVID-19) never ever. So, kwa maelezo hayo ya BoT ambaye ndiye custodian wa noti na sarafu za nchi hii, shaka ondoa Mkuu.
Unaamini hicho wanachokisema?
 
Ulichosema ni kweli kabisa. Mobile banking na wakala wa bank gharama zote zimeongezwa kwa mteja. Wateja wameshutuka ndio maana misururu mirefu bank na kwenye ATM. Tcra inaona mteja anavyopunjwa lakini wanachekelea.
Hivi sasa mabenki wanatutumia sms wakitushauri tuache utaratibu wa kufanya miamala kwa kutumia cash money na badala yake tutumie huduma za kielektroniki(mobile banking) kufanya miamala hiyo kama njia mojawapo ya kupambana na ugonjwa wa corona.

Binafsi naupokea ushauri huo ila nawashauri kwanza wao wenyewe(mabenki na makampuni ya simu za mikononi) wajiongeza kwa kupunguza gharama za kufanya miamala husika ili kui-encourage watu kutumia huduma hizo na sio wao ku-focus tu katika kufanya kibiashara i wakati hili tatizo kwa sasa ni jambo la dharura hivyo nao wao wanapaswa kuli-handle kidharura ikiwa ni pamoja na kushusha gharama za kutumia huduma hizi za kimtandao.

Vile vile,katika kuhamasisha matumizi ya simu za mikunoni kufanya miamala hii,nawashauri watazame upya vigezo na mashari vilivyopo, mfano kukatwa hela hata kama huduma ulioomba imefeli/haijafika mwisho lakini wao wanakata tuhela kwenye simu yako na kwenye akaunti yako ya benki bila kujali huduma uliohitaji imekamilika(hili jambo huo nalliona ni kama kuibia wateja).

Mwisho,napenda kuishauri serikali kuwa huu ndio wakati muafaka wa kupeleka miswaada/sheria Bungeni kwa hati ya dharura ili kutunga sheria au kurekebisha sheria zinazoweza kusaidia kupambana na janga hili endapo ugonjwa huu utageuka tishio humu nchini na mojawapo ya mabadiliko nayopendekeza(iwapo kutakuwa na huo ulazima kulingana na hali ya huu ugonjwa) ni kupunguza kodi ya kufanya miamala kwa njia za kieletroniki.

Hivyo, Serikali kupitia BOT,TCRA na Wizara ya Fedha, huu ni wakati wa nyie ku-monitor hii situation na kufanya kile kilicho katika mamlaka yenu katika kupambana na janga hili na mojawapo ni kutazama pendekezo hili iwapo hali ya ugonjwa huu kweli italazimisha hatua kama hizo kuchukuliwa.

Kila mtu kwa nafasi yake ni mdau katika hili janga kwani linagusa karibu kila eneo mbali na kugusu karibu kila mtu kiuchumi na kijamii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Salary Slip,
Ni ushauri mzuri naunga mkono!

Siyo kila jambo siasa leo umeonyesha ukomavu!
Nimesoma hotuba ya kambi ya kiongozi wa Upinzani Bungeni ambapo wamesema Rwanda wamefanya kitu kama hiki nilichoshauri(kupunguza gharama za kufanya miamala kwa njia ya kieletroniki katikia kupambana na corona)

Sisi viongozi wetu sijui hawaoni?!!

Hii ndio sehemu ya hotuba ya Kiongozi wa Upinzani Bungeni inayoongelea swala hili ni hii hapa:

Mheshimiwa Spika, kutokana na tishio la Virusi vya Corona katika uchumi; nchi nyingi Duniani zimechukua hatua madhubuti kuzia chumi zao zisianguke. Mathalan Nchi Jirani ya Rwanda Katika kukabiliana na hali hiyo, mamlaka ya nchi hiyo imetangaza hatua kadhaa kukabiliana na kupanda kwa bei kiholela. Kwa mujibu wa tovuti ya Rfi[1]Benki Kuu ya Rwanda imetangaza kupunguza masharti ya ulipaji wa mikopo ya benki kwa kampuni na watu walioathirika na ugonjwa wa Covid-19. Ili kufanikisha mpango huo, Karibu Euro milioni 50 pia zimetolewa kwa benki za biashara, ambazo zitahitaji ukwasi zaidi. Aidha, Ili kuzuia maambukizi ya virusi kupitia biashara ya fedha (kutoa na kupokea fedha), mamlaka pia imesitisha ada ambayo ilikuwa ikitozwa kwa kutoa fedha kupitia mfumo wa kidijitali.Hatua hizo zinalenga kupunguza athari za Covid-19 kwenye uchumi wa Rwanda. Mojawapo ya sekta zilizoathiriwa zaidi ni sekta ya utalii. Angalau matukio 20 yaliyokuwa yamepangwa kufanyika mwezi Machi na Aprili yamesogezwa mbele, kwa hali hiyo Rwanda itapoteza euro milioni 7, kulingana na Mamlaka ya Mapato ya Rwanda.
 
Back
Top Bottom