Serikali ikikosea kesi ya Mbowe, naamini Ujerumani watafunga ubalozi

Paskali,unapenda kujitoa ufahamu bila sababu.Wewe ni mfano kwetu hasa katika uandishi.Kweli umeshindwa kuona na kuangalia kwa nini mabalozi washawishike kufika mahakamani katika kesi hii?Huoni kama ni itu extra ordinary pamoja na vitisho vya Mulamula?
 
Uhuru gani na wakati kesi yenyewe ya kubumba fake?
 
Halafu baadae DPP anaibuka kama kwa Mzee Rugemalila kwamba serikali haina nia ya kuendelea na kesi [emoji12][emoji12] haya banaa ngoja tuendelee kupiga mtori....
 
Mkondo wa Sheria ulifuata mkondo wa kuanzishwa kwa kesi hii? Kama mkondo wa kuanzishwa kwa kesi hii ni batili, iweje mkondo wa Sheria ufuatwe?
 

P,

Sheria ifuate mkondo ni vema kama mahakama kweli ni huru. Lakini kwenye nchi ya kidemokrasia kumshitaki mwenyekiti wa chama cha upinzani kwa ugaidi sio kitu kidogo kama tunavyofikiria. Lakini vilevile historia inatusuta. Mpaka leo hakuna hata shitakiwa mmoja kwa kesi ya Lissu kupigwa risasi na ndiyo maana Lissu alivyoenda ubalozi hawajampuuza. Kuna wanasiasa wengi wapo magerezani bila kesi, Lissu mwenyewe ana kesi tano nyingine!!. Lakini mikutano imekatazwa hata ya ndani! sasa kama ni balozi ni lazima uangalie mbali na kujiuliza je hii ni nchi ambayo inakuwa kidemokrasia au inarudi nyuma?

Lakini vilevile wawekezaji wanaangalia miaka 20 mbele. Je Tanzania yenye 70% chini ya miaka 27 itakuwaje miaka 20 ijayo kama sasa upinzani ambao pamoja na mambo yote ulipata zaidi ya 30% ya kura 2015 lakini waangalizi wa kimataifa wameona uchaguzi wa 2015 ulivyokuwa. Tujue Tanzania ni nchi inayoendelea hivyo mabadiliko yatakuwepo lakini kwa wawekezaji hasa wa nchi hizi za magharibi mazingira ya uwazi na demokrasia ni muhimu sana kwao. Ukweli ni kwamba hao wajinga wajinga walikuwa wanamshauri Magu awe Raisi kama wa China. Maana yake hakuna demokrasia na yeye ni kama mtakatifu

Watanzania tusije tukajidanganya kama vile hawa wazungu wanawapenda wakina Mbowe na Lissu si kweli ufuatiliaji ni kupima wawekezaji wao wa sasa na ambao wanafikiria kuwekeza baadae. Vilevile usalama wao.

Lakini kuna mambo mengi sana nilishasema huko nyuma watu wakachukuwa miaka mingi kunielewa

1. Vitambulisho vya taifa nilisema miaka ya zamani sana
2. mikopo ya bank kuwa juu sasa ndiyo bank kuu imeamka
3. Niliongelea kwamba Magufuli akiondoka bandari ya bagamoyo itarudi
 
Ila majizi ya maccm ndiyo yenye akili sana kwa kukingiana vifua huku yakiliibia Taifa letu. 😳


hawa chadema wana akili za kushikiwa, ni shida juu ya shida kwa wenyewe kwa wenyewe. wamewatoa kina halima mdee ambao walikuwa na hekima kidogo, sasa wamebaki mazuzu watupu. tupa kuleeeeee
 
Shida ya mzee wangu Paschal ndio hiyo kuuma na kupuliza ,,kikwetu tunawaita Ndimi mbili..
 
Tangu lini Serikali ya Tanzania ilifuata sheria? Si unawasikia akina Kingai wanavyofanya kazi? Ni sheria ipi wanayofuata?

Vyombo vya serikali vinafanya kazi kama magenge ya majambazi.
Aisee nimewaza Sana Kama komandoo anashikwa halafu anateswa Kama popo je sisi akina pangu pakavu tunaoshikwa gizani tunateswaji !!! Hii imeniuma Sana..
 
Uzi wa chini ya kiwango sana huu, anyway umetumia haki yako ya kujieleza inayotambuliwa na Katiba.
 

Hivi ile mahakama ya Afrika kusini ilipomfunga Mandela alikuwa na kosa kwahiyo ilikuwa sawa kumfungia ndicho unachokisema au kwakuwa wewe siyo Mbowe ndiyo maana unatetea tumbo lako tu. Kwani mbona DPP alipofuta kesi ya Lissu hujalalamika kwamba ameingilia uhuru wa mahakama ila kwenye kesi ya Mbowe DPP akifuta atakuwa ameingilia uhuru wa mahakama. Halafu na wewe unasema umesoma sheria. Yaani hii nchi ina wanafiki wengi sana kama hata wewe umepoteza utu na heshima yote uliyokuwa nayo miaka yote. Duh shida sana.
 
Mbona nikama unakuwaga siboya....
mahakama haipaswi kuacha kesi za kipumbafu mahakamani mpaka dpp aseme hamania nazo.

mahakama itoe onyo pale inapoonekana inatumika kushikilia watu mahabusu huku kesi haina maana wala mwelekeo.

tumeona rugemalila ameteseka takribani miaka minne nakutishiwa eti waongee na dpp pembeni kumbe hakuna kesi

hatuwezi kuiacha mahakama kwenyetope kisa kisingizio cha kuingilia kesi!! mbona mwenda aliingilia mahkama alivyotaka??? Acheni maujinga
 
Mahakama itimize wajibu wake kwa kutekeleza maagizo ya rais? Rais anasema wana ushahidi wa kutosha,kisha ushahidi unaoendelewa kutolewa uko tofauti na utashi wake,huku mahakama ikiwa na hukumu mfukoni tayari!
 
Bora umemwambia. Kila siku kutishia watu na ku post picha za afisa wa ubalozi. Interest ya Ujerumani nchini Tanzania ni kubwa kuliko Mbowe. Hata akifungwa Mbowe uhusiano wetu utaendelea vyema. Ndiyo utawala wa kisheria ulivyo.
 
Kubambikiwa watu kesi ndo kufuata sheria
 
Achana na ujinga. Kesi inaendeshwa kisheria na wana sheria. Maamuzi yatakuwa ya kisheria. Hakuna mahakama inaamuwa kesi kwa kuogopa eti wageni watasemaje. Kama wana hatia watapata stahili. Kama hawana hatia wataachiwa huru. Ubalozi wa TZ au TZ haiwezi kuingilia sheria za Ujeremani au USA, kwea vivyo hivyo Ujeremani au nchi yoyote haiwezi kuingilia mjaamuzi yetu.

Yaani tukubali uingiliwa mambo yetu kwa sababu ya kusaidiwa, hii ni kutufanya sisi kama ombaomba. Yaani kama unataka usaidiwe fanya hiki. Hivi wewe ukienda kuomba au kukopa kwa jirani, akakuambia uendeshe nyumba/familia yako namnaq anavyotaka utakubali. Naona sisi kama taifa tunataka kujidhalalisha mbele ya mataifa mengine.

Kitu cha muhimu ni kuwa kesi ya Mbowe iendeshwe na kuamuliwa kwa haki na siyo kwa kuogopa eti tukiamuwa namna fulani Wajeremani wataondoka. Kama wanataka kuondoka na waondoke, hii haitakuwa mara yao ya kwanza. Mbona bwaliondoka wakarudi.
 
But if you think of the law as some kind of church doctrine that’s pure, neutral, unbiased, apolitical, and beyond fallibility, then you are going to end up in tears. Laws like a sword, it’s double-edged and cuts both ways.
Often, laws are a class imposition by a hegemonic group, or elites in society over subordinate, or subaltern, strata.
In a modern society, even a democratic one, laws are made by the political branches of the state.
 
Hivi Pasco na wewe kweli na taalum yako ya sheria kwa ushahidi ulioteolewa hadi sasa unataka serikali na jeshi lake viendelee tu kuchorwa na kudharirishwa kwa matendo yao, si watoe tu Nolle? kupigwa mtu hadi kuninginizwa kama popo ni zaid ya Guantanamo na je ndivyo PGO inawaambiwa? Hawa watu (Goodluck na washirikia wake ) walipaswa hadi sasa wawe mahakamani kwa unyama waliowawafanyia wengine wakiwa ndani ya uniform za polisi... ni aibu sana watu hao bado wanadunda tu kwenye uniform hizo... siku IGP akija natamani aulizwe kama je kuningizswa imo ndani ya PGO au la ? na kama haimo ni kwa ni hawa maaskari wake wanaoninginiza watu kama popo bado wapo madarani mpaka sasa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…