Serikali ilipozuia bodaboda kuingia mjini ilikuwa sahihi sana

Serikali ilipozuia bodaboda kuingia mjini ilikuwa sahihi sana

Muite

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2013
Posts
2,971
Reaction score
6,607
Sasahivi ukifika Kariakoo ni vurugu sana za pikipiki na Bajaji. Yaani ni mafuriko.

Nadhani hizi Bodaboda na Bajaji zisingeruhusiwa kuingia Posta na Kariakoo. Mbona vile vidaladalq vidogo/Hiace iliwezekana kuvizuia kuingia Mjini?

Au ni issue za kisiasa za kuogopa kukosa kura.
 
Kwa kweli japokuwa Boda na Bajaji zinatusaidia ila kwa kweli zinaelekea kuwa Janga Kubwa. Zimekuwa nyingi sana na Pia hazifati sheria kabisa za Barabarani, Yaani wanafanya wanavyotaka wao na huwaambii kitu, Na ikatokea umewagonga basi wanakupiga, Yaani ni shida kweli kweli.

Kuna Mbunge mstaafu mmoja wa chama pinzani aliwahi kutoa angalizo kwenye swala hili lakini ni kama akapuuziwa.

Nashauri serikali iangalie namna ya kufanya regulation ya uwingi wa Bodaboda na namna zinavyofanya kazi.


Pia vijana washauriwe kuwa ajira sio kuendesha pikipiki tu. Jamani hili swala ni Linaelekea kuwa janga lisipofanyiwa kazi.

Ushauri tu huu ,
 
Africa haikustahili kabisa kupata uhuru mapema, kwa IQ zetu hizi tulitakiwa kuanza kupata uhuru mwanzoni mwa 2000. Kuna mambo mengi yanayofanyika katika hizi nchi zetu unagundua ni uwezo wetu Kifikra.

Fikiria watu wapo radhi City centre kuwe na vurugu za mapikipiki na bajaji sababu tu ya kupata kura. Halafu hawahawa wanasiasa wanaposafiri kwenda nje wakirudi wanaanza kutoa mifano ya maendeleo na mipangilio ya miji ya wenzetu.

Fikiria Barabara inajenjwa leo then baada ya miaka miwili inabomolewa ili kuongeza ukubwa. YAANI SISI HATUNA UWEZO WA KUONA MIAKA MITANO, KUMI AU ISHIRINI TU MBELE, WAKATI WENZETU WAZUNGU WANAONA MIAKA 100 MBELE.

Najiuliza ilikuaje uwanja wa Taifa ukajengwa eneo Moja na uwanja wa zamani, najiuliza ilikuaje DART ikajengwa pale Jangwani, najiuliza ilikuaje stand ya mabasi ikajengwa pale Mbezi wakati mabasi mengi hayataki kuitumia stand ile(wanatumia ofisi zao kule Shekilango), najiuliza ni kwanini iwe tu ni kariakoo na kusiwe ni mini kariakoo sehehu kama tatu ndani ya jiji. Ninawasifu walioianzisha Mloganzila(nchi inahitaji ideas kama hii).
 
Kwa kweli japokuwa Boda na Bajaji zinatusaidia ila kwa kweli zinaelekea kuwa Janga Kubwa. Zimekuwa nyingi sana na Pia hazifati sheria kabisa za Barabarani, Yaani wanafanya wanavyotaka wao na huwaambii kitu, Na ikatokea umewagonga basi wanakupiga, Yaani ni shida kweli kweli.

Kuna Mbunge mstaafu mmoja wa chama pinzani aliwahi kutoa angalizo kwenye swala hili lakini ni kama akapuuziwa.

Nashauri serikali iangalie namna ya kufanya regulation ya uwingi wa Bodaboda na namna zinavyofanya kazi.


Pia vijana washauriwe kuwa ajira sio kuendesha pikipiki tu. Jamani hili swala ni Linaelekea kuwa janga lisipofanyiwa kazi.

Ushauri tu huu ,
Kila kitu kina pande mbili boda zina hasara na zina faida kwa wakazi wa uswahilini maboda walikuwa ndo wakabaji ila hizi pikipiki zimepunguza kero ya ukabaji wengi mnaolaumu boda boda hamjui ugumu wa kitaa ukitaka kuondoa boda boda mjini ni kuzalisha tatizo la ajira kubwa zaidi serikali kwa kujua kuwa imeshindwa kuzalisha ajira ndo maana imewaachia waendelee Nchi yetu ina umuhimu mkubwa wA kujenga viwanda ili kuzalisha ajira mpya hii kero itapungua.
 
Sasahivi ukifika Kariakoo ni vurugu sana za pikipiki na Bajaji. Yaani ni mafuriko.

Nadhani hizi Bodaboda na Bajaji zisingeruhusiwa kuingia Posta na Kariakoo. Mbona vile vidaladalq vidogo/Hiace iliwezekana kuvizuia kuingia Mjini?

Au ni issue za kisiasa za kuogopa kukosa kura.
Boda boda zinaweza kuzuiwa kukiwa na alternative, bila boda boda biashara haziendi kuanzia Delivery za wateja, mizigo inayoenda Cargo na shughuli nyengine.
 
Boda boda zinaweza kuzuiwa kukiwa na alternative, bila boda boda biashara haziendi kuanzia Delivery za wateja, mizigo inayoenda Cargo na shughuli nyengine.
Hizo changamoto unazosema zitakuwa adjusted automatically. Akili zitakaa sawa tu na kila mtu atapambaa kwa njia zingine. Tusiwe rigid.
 
Africa haikustahili kabisa kupata uhuru mapema, kwa IQ zetu hizi tulitakiwa kuanza kupata uhuru mwanzoni mwa 2000. Kuna mambo mengi yanayofanyika katika hizi nchi zetu unagundua ni uwezo wetu Kifikra. Fikiria watu wapo radhi City centre kuwe na vurugu za mapikipiki na bajaji sababu tu ya kupata kura .
Halafu hawahawa wanasiasa wanaposafiri kwenda nje wakirudi wanaanza kutoa mifano ya maendeleo na mipangilio ya miji ya wenzetu. Fikiria Barabara inajenjwa leo then baada ya miaka miwili inabomolewa ili kuongeza ukubwa. YAANI SISI HATUNA UWEZO WA KUONA MIAKA MITANO, KUMI AU ISHIRINI TU MBELE, WAKATI WENZETU WAZUNGU WANAONA MIAKA 100 MBELE.
Najiuliza ilikuaje uwanja wa Taifa ukajengwa eneo Moja na uwanja wa zamani, najiuliza ilikuaje DART ikajengwa pale Jangwani, najiuliza ilikuaje stand ya mabasi ikajengwa pale Mbezi wakati mabasi mengi hayataki kuitumia stand ile(wanatumia ofisi zao kule Shekilango), najiuliza ni kwanini iwe tu ni kariakoo na kusiwe ni mini kariakoo sehehu kama tatu ndani ya jiji. Ninawasifu walioianzisha Mloganzila(nchi inahitaji ideas kama hii).
Mkuu umeongea vzr Sana tena kwa kutumia akili kubwa, mi naamini waafrika wengi tuna IQ ndogo ya kutuwezesha Kula tu basi kwenye planning na usimamizi wa maendeleo ni zero kabisa. Mpaka some time tunauza na rasilimali zetu bure kabisa. Nahisi nchi hii kutakuwa na watu wamejipenyeza serikalini ambao sio raia wa Tanzania
 
Hizo changamoto unazosema zitakuwa adjusted automatically. Akili zitakaa sawa tu na kila mtu atapambaa kwa njia zingine. Tusiwe rigid.
Kwamba warisk na biashara za matrilion huku ukiamini zitaji Adjust?

Kunatakiwa kuwe na alternative ya bei rahisi, mathalan mikokoteni ya umeme ama vigari vidogo visivyoenda kasi kwa ajili ya usafiri wa ndani ya soko kabla hujafikiria kuwatoa. Hiace hazikupigwa marufuku watu wakatembea kwa Miguu, bali walihakikisha kuna costa za kutosha ndio wakapiga marufuku Hiace.
 
Kila kitu kina pande mbili boda zina hasara na zina faida kwa wakazi wa uswahilini maboda walikuwa ndo wakabaji ila hizi pikipiki zimepunguza kero ya ukabaji wengi mnaolaumu boda boda hamjui ugumu wa kitaa ukitaka kuondoa boda boda mjini ni kuzalisha tatizo la ajira kubwa zaidi serikali kwa kujua kuwa imeshindwa kuzalisha ajira ndo maana imewaachia waendelee Nchi yetu ina umuhimu mkubwa wA kujenga viwanda ili kuzalisha ajira mpya hii kero itapungua.
Tusiwe na rigid mind kiasi hiki. Eti tuogope kuzuia bodaboda kuingia mijini kisa tu vibaka wataongezeka, kuna shughuli nyingi sana binafsi za kufanya sema tu sisi hatuna akili na akili zetu ni mgando sana kuwa bila kuuza mitumba , bila kuingia mjini na boda, bila kuuza chips hakuna kingine cha kufanya.
Halafu sio kila kitu Serikali inahusika kuandaa maana naona kila changamoto ni kuilaumu Serikali, HATA MWANAO AKIVUTA BANGI UNAILAUMU SERIKALI.
Tujiulize Diamond, Ali Kiba, Mwijaku, Ndaro , Steve, Dr Cheni, Samata , Msuva, Mzize waliandaliwa mazingira gani na Serikali. Huo ni mfano tu, lakini wapo wafanyabiashara, wakulima na wasomi ambao wamejibeba wenyewe . KUNA MAMBO YA SERIKALI KWELI LAKINI MENGI NI AKILI NA STRUGGLING YA MTU BINAFSI.
SASA TUKIWA NA RIGID MIND KAMA HIZO TUNAZIDI KUDUMAZA WATU WETU HASA VIJANA NA KUCHELEWESHA MAENDELEO.
 
Kila kitu kina pande mbili boda zina hasara na zina faida kwa wakazi wa uswahilini maboda walikuwa ndo wakabaji ila hizi pikipiki zimepunguza kero ya ukabaji wengi mnaolaumu boda boda hamjui ugumu wa kitaa ukitaka kuondoa boda boda mjini ni kuzalisha tatizo la ajira kubwa zaidi serikali kwa kujua kuwa imeshindwa kuzalisha ajira ndo maana imewaachia waendelee Nchi yetu ina umuhimu mkubwa wA kujenga viwanda ili kuzalisha ajira mpya hii kero itapungua.
Hawaoongelei kuzuia bodaboda. Wanaongelea kuziruhusu kuingia mjini na kutumia Highways.
Boda na Bajaji ziwepo lakini waendeshe huko mitaani sio highways na city centre. Mfano ukishuka kimara korogwe, boda na bajaji zikupeleke huko ndani ndani.
Nairobi wana mfumo huu bajaji haziruhusiwi kwenye highways na city centre...boda ndo wameruhusu nazo zimeharibu kweli muonekano wa Nairobi
 
Kwamba warisk na biashara za matrilion huku ukiamini zitaji Adjust?

Kunatakiwa kuwe na alternative ya bei rahisi, mathalan mikokoteni ya umeme ama vigari vidogo visivyoenda kasi kwa ajili ya usafiri wa ndani ya soko kabla hujafikiria kuwatoa. Hiace hazikupigwa marufuku watu wakatembea kwa Miguu, bali walihakikisha kuna costa za kutosha ndio wakapiga marufuku Hiace.
Hata boda zikizuiwa kuingia mijini automatically taxi, canter zitachukuwa nafasi. Bajaji na Bodaboda zitafanya kazi kwenye intermediate ambazo zitajipanga zenyewe tu. Tusiwe kama nyumbu kuwa ni lazima uendelee kufuata mstari wa wenzako hata kama kuna mamba. Zipo njia nyingi tu sema wengi tuna fikra hizi kama zako za uwoga na mgando
 
Hawaoongelei kuzuia bodaboda. Wanaongelea kuziruhusu kuingia mjini na kutumia Highways.
Boda na Bajaji ziwepo lakini waendeshe huko mitaani sio highways na city centre. Mfano ukishuka kimara korogwe, boda na bajaji zikupeleke huko ndani ndani.
Nairobi wana mfumo huu bajaji haziruhusiwi kwenye highways na city centre...boda ndo wameruhusu nazo zimeharibu kweli muonekano wa Nairobi
Kwani huko ulikotaja kwa sasa hamna boda?
 
Tusiwe na rigid mind kiasi hiki. Eti tuogope kuzuia bodaboda kuingia mijini kisa tu vibaka wataongezeka, kuna shughuli nyingi sana binafsi za kufanya sema tu sisi hatuna akili na akili zetu ni mgando sana kuwa bila kuuza mitumba , bila kuingia mjini na boda, bila kuuza chips hakuna kingine cha kufanya.
Halafu sio kila kitu Serikali inahusika kuandaa maana naona kila changamoto ni kuilaumu Serikali, HATA MWANAO AKIVUTA BANGI UNAILAUMU SERIKALI.
Tujiulize Diamond, Ali Kiba, Mwijaku, Ndaro , Steve, Dr Cheni, Samata , Msuva, Mzize waliandaliwa mazingira gani na Serikali. Huo ni mfano tu, lakini wapo wafanyabiashara, wakulima na wasomi ambao wamejibeba wenyewe . KUNA MAMBO YA SERIKALI KWELI LAKINI MENGI NI AKILI NA STRUGGLING YA MTU BINAFSI.
SASA TUKIWA NA RIGID MIND KAMA HIZO TUNAZIDI KUDUMAZA WATU WETU HASA VIJANA NA KUCHELEWESHA MAENDELEO.
Wewe hao uliwataja ni idadi ndogo sana na mfano wa mafanikio kitu usichokijua ni kwamba Serikali ni kama Mzazi kwa Raia wake ukisema kila kitu kuichia Serikali sasa hiyo Serikali ina faida gani kuwepo kama haina jukumu kwa Raia wake? Ni LAZIMA kwa Serikali kutatua changamoto za Wananchi kinachotokea ni kwamba Viongozi Wameshindwa kutatua matatizo ya Watu umetaja watu ambao wote wamefanikiwa kwa njia ya kubahatisha kwani kuna vijana wangapi wanafanya wanachofanya na hawajatoboa.
 
as long as matatizo ya usafiri wa uhakika ziendelee kukuepo. Ustegemee nyumba kuwa safi wakati maji ndani nyumba ni shida.
 
Hata boda zikizuiwa kuingia mijini automatically taxi, canter zitachukuwa nafasi. Bajaji na Bodaboda zitafanya kazi kwenye intermediate ambazo zitajipanga zenyewe tu. Tusiwe kama nyumbu kuwa ni lazima uendelee kufuata mstari wa wenzako hata kama kuna mamba. Zipo njia nyingi tu sema wengi tuna fikra hizi kama zako za uwoga na mgando
Kwamba mteja katoa order kitu bei rahisi 5000-10,000 upakize kwenye Tax ama canter? Thank God hupo kwenye hao wanaopanga mipango.

Na hio demand ya kkoo hizo tax foleni ndio ingezidi. Sasa hivi tu kuna boda na foleni haipitiki imagine tax kwa maelfu zinaingia na kutoka kkoo.
 
Kwani huko ulikotaja kwa sasa hamna boda?
Maswali gani unaniuliza sasa. Hujanielewa au ni ubishi tu? Nani kasema huko hakuna? Au hujaelewa mfano wangu.

Hebu soma vzr reply yangu. Halafu tuongee
 
Back
Top Bottom