Serikali imekanusha madai ya uwapo wa kodi kandamizi kwa wafanyabiashara bali imetengeneza kodi rafiki

Serikali imekanusha madai ya uwapo wa kodi kandamizi kwa wafanyabiashara bali imetengeneza kodi rafiki

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Naibu Waziri wa Fedha, Mwanaidi Ali Hamis ameliambia Bunge leo Ijumaa Februari 12, 2021 Jijini Dodoma kuwa hakuna mfanyabiashara aliyekimbia biashara yake kwa sababu ya kodi.

Ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Stella Fiyayo (Chadema) ambaye amehoji upi mkakati wa Serikali katika kufanya marekebisho ya kodi iweze kuendana na hali ilivyo.

Naibu Waziri huyo wa fedha, amesema Serikali haitozi kodi kandamizi na wala haifikirii kufanya hivyo kwa wananchi na wafanyabiashara wake.

Majibu ya Naibu Waziri yamekuja wakati wabunge wamekuwa wakipiga kelele kwa wiki nzima wakilalamikia kodi kubwa wanazotozwa wafanyabiashara na Mamlaka ya Kodi (TRA).

Kwenye michango yao, wabunge hao walisema mfumo unaotumika kukadilia na kudai kodi siyo rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji.
 
Kodi inayotozwa Tanzanian ni rafiki sana hakuna haja ya kupunguza labda iongezwe kidogo
Yaani Sio Mitano tena ni milele kabisa tafadhali.....

Uchumi wa kati....
Nchi hii ni tajiri sana
Au nasema uongo ndugu zanguuuuu...
Unaijua vieite wewe!!!!

Sisi tunatembelea mavieitee vieitee
 

Attachments

  • IMG_20210127_125033.jpg
    IMG_20210127_125033.jpg
    86 KB · Views: 1
Wafanyabiashara sasa wasitake kuyumbisha serikali. Wapo wabunge wafanyabiashara wameanza ubinafsi kujiwakilisha binafsi na wako wabunge vibaraka wanatumikishwa na wafanyabiashara.

Tusijekuyumba makusanyo makubwa ya kodi ndio yanasababisha mapato haya yanayotumika vizuri kujenga nchi. Tusisahau ubepari ni unyama kama tulivyofundishwa enzi za ujamaa wa azimio la arusha.

Kabla ya ccm kuamua kutumia sekta binafsi kujenga ujamaa bila shaka walitafakari na kujua njia pekee ni kudhibitiwa ubepari na umma kusudi kupitia kodi serikali iweze kukidhi haja ya maendeleo kwa umma.

Hawa kina nappe wasituchanganye kodi ziko rafiki na zinalipika ila ndio ile ubepari ni unyama na ubinafsi lazima kudhibitiwa ili kama nchi sote twende mbele.
 
Wafanyabiashara sasa wasitake kuyumbisha serikali. Wapo wabunge wafanyabiashara wameanza ubinafsi kujiwakilisha binafsi na wako wabunge vibaraka wanatumikishwa na wafanyabiashara.

Tusijekuyumba makusanyo makubwa ya kodi ndio yanasababisha mapato haya yanayotumika vizuri kujenga nchi. Tusisahau ubepari ni unyama kama tulivyofundishwa enzi za ujamaa wa azimio la arusha.

Kabla ya ccm kuamua kutumia sekta binafsi kujenga ujamaa bila shaka walitafakari na kujua njia pekee ni kudhibitiwa ubepari na umma kusudi kupitia kodi serikali iweze kukidhi haja ya maendeleo kwa umma.

Hawa kina nappe wasituchanganye kodi ziko rafiki na zinalipika ila ndio ile upepari ni unyama na ubinafsi lazima kudhibitiwa ili kama nchi sote twende mbele.
Mkuu, huwezi kujua hivi vitu ukiwa mtu wa maneno tu. Ingia kwenye biashara uone.
 
Unaweza kuta Nape na Msukuma walikuwa wanashangilia kwa kupiga meza wakati waziri akitoa hiyo taarifa. Wanaccm akili zao wanazijua wenyewe
 
Kwani wewe Naibu Waziri huwaamini hata CCM wenzako? Nape na Msukuma wamesema namna maduka/biashara zinavyofungwa, mtu anadaiwa mpaka kupewa au kutishiwa kesi za uhujumu uchumi. Kwa hiyo mtaamini mpaka biashara zote mjini zikishingwa?

Leo hii ukiienda dukani kununua bidhaa, mfanyabiashara yupo tayari urudishe bidhaa kuliko akupe listi ya EFD yenye bei halali. Vinginevyo aandike bei pungufu kabisa. Hata hilo hamlioni au hamjawahi sikia? Lazima kuna tatizo sehemu fulani tunapofikia hatua wafanyabiashara wanadanganya kiasi hicho.

Mzigo wa Milioni 3 listi unaandika 300,000/-. Hebu Serikali isijibu kisiasa na kurahisisha mambo. Fuatilieni hayo yanayosemwa na wabunge kupitia vyombo vinavyoaminika kama Usalama wa Taifa mpatapa majibu sahihi. Asante
 


Wafanyabiashara 600 wamefunga biashara Geita​

Friday February 12 2021​



Wafanyabiashara zaidi ya 600 mkoani Geita wamefunga biashara zao mwaka 2020 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kubadilisha maeneo ya kufanyia biashara.





Wafanyabiashara 600 wamefunga biashara Geita
matoopic-data.jpg

By Rehema Matowo
More by this Author

IN SUMMARY​

  • Wafanyabiashara zaidi ya 600 mkoani Geita wamefunga biashara zao mwaka 2020 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kubadilisha maeneo ya kufanyia biashara.
Advertisement
Geita. Wafanyabiashara zaidi ya 600 mkoani Geita wamefunga biashara zao mwaka 2020 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kubadilisha maeneo ya kufanyia biashara.
Hayo yamesemwa na meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoani Geita, Hashim Ngoda wakati wa semina ya uzinduzi wa programu maalum ya Serikali ya kukagua na kufuatilia matumizi sahihi ya mashine ya kieletroniki (EFD) .
Ngoda amesema wafanyabiashara kuhama maeneo yao na wengine kubadili biashara ni miongoni mwa sababu za kufungwa kwa bishara hizo.
Wakati meneja wa TRA akitaja sababu hizo mwenyekiti wa bodi ya wafanyabiashara eneo la mji mdogo wa Katoro, Deogratius Sangalali amesema wafanyabiashara wamefunga kutokana na kodi kubwa zinazotozwa na TRA na kusababisha watu kufilisika.
Amesema wafanyabiashara wanalazimika kuandika barua za kudanganya kuwa wamehama au kutoa sababu za ugonjwa kwa kuwa wakieleza kufilisika TRA hukataa kufunga biashara na kuwataka waendelee kufanya kuzifanya hata kama haziwalipi.

Naibu Waziri wa Fedha, Mwanaidi Ali Hamis ameliambia Bunge leo Ijumaa Februari 12, 2021 Jijini Dodoma kuwa hakuna mfanyabiashara aliyekimbia biashara yake kwa sababu ya kodi.


Ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Stella Fiyayo (Chadema) ambaye amehoji upi mkakati wa Serikali katika kufanya marekebisho ya kodi iweze kuendana na hali ilivyo.

Naibu Waziri huyo wa fedha, amesema Serikali haitozi kodi kandamizi na wala haifikirii kufanya hivyo kwa wananchi na wafanyabiashara wake.

Majibu ya Naibu Waziri yamekuja wakati wabunge wamekuwa wakipiga kelele kwa wiki nzima wakilalamikia kodi kubwa wanazotozwa wafanyabiashara na Mamlaka ya Kodi (TRA).

Kwenye michango yao, wabunge hao walisema mfumo unaotumika kukadilia na kudai kodi siyo rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji.
 
Wafanyabiashara sasa wasitake kuyumbisha serikali. Wapo wabunge wafanyabiashara wameanza ubinafsi kujiwakilisha binafsi na wako wabunge vibaraka wanatumikishwa na wafanyabiashara.

Tusijekuyumba makusanyo makubwa ya kodi ndio yanasababisha mapato haya yanayotumika vizuri kujenga nchi. Tusisahau ubepari ni unyama kama tulivyofundishwa enzi za ujamaa wa azimio la arusha.

Kabla ya ccm kuamua kutumia sekta binafsi kujenga ujamaa bila shaka walitafakari na kujua njia pekee ni kudhibitiwa ubepari na umma kusudi kupitia kodi serikali iweze kukidhi haja ya maendeleo kwa umma.

Hawa kina nappe wasituchanganye kodi ziko rafiki na zinalipika ila ndio ile upepari ni unyama na ubinafsi lazima kudhibitiwa ili kama nchi sote twende mbele.
Utajuaje kuwa huyu mtu ni kula kulala bure?
 
Naibu Waziri wa Fedha, Mwanaidi Ali Hamis ameliambia Bunge leo Ijumaa Februari 12, 2021 Jijini Dodoma kuwa hakuna mfanyabiashara aliyekimbia biashara yake kwa sababu ya kodi.

Ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Stella Fiyayo (Chadema) ambaye amehoji upi mkakati wa Serikali katika kufanya marekebisho ya kodi iweze kuendana na hali ilivyo.

Naibu Waziri huyo wa fedha, amesema Serikali haitozi kodi kandamizi na wala haifikirii kufanya hivyo kwa wananchi na wafanyabiashara wake.

Majibu ya Naibu Waziri yamekuja wakati wabunge wamekuwa wakipiga kelele kwa wiki nzima wakilalamikia kodi kubwa wanazotozwa wafanyabiashara na Mamlaka ya Kodi (TRA).

Kwenye michango yao, wabunge hao walisema mfumo unaotumika kukadilia na kudai kodi siyo rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji.
Nafikili mda wa kujitafakari wapi tumekosea, wanyabiashara wanalalamika Sana,wanaumwizwa Sana, wanaona isiweshida wanaanza tumia vitambulisho vya wamachinga,
 
Back
Top Bottom