Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 15,692
- 23,038
Taifa Stars imetolewa kwenye mashindano ya fainali za OFCON za mwaka 2019, kwa kushindwa mechi zote tatu za awali.
Lakini kufukuzwa kwa Emanuel Amunike kuwe ni kigezo cha kuanza kuwatayarisha wachezaji wenye elimu ya mpira kutoka katika nchi zilizoendelea.
Katika nchi zilizostua wengi kwenye fainali za mwaka huu ni timu ya Madagascar au kwa jina la utani la Barea.
Madagascar inafundishwa na kocha mfaransa Nicolas Dupuls ambae aliwahi kuwa mchezaji aliecheza nafasi ya beki wa kushoto wa timu ya FC Souvigny.
Pia amewahi kuchezea timu ya FC Beaumont ya Marekani na baadae kuanza kufundisha mpira kweyne timu ya AS Yzeure ya Ufaransa.
Mwaka 2017 Dupuls aliteuliwa kuwa kocha wa timu ya taifa Madagascar na kama Tanzania mwaka 2018 timu hiyo ikafuzu kucheza fainali za AFCON za mwaka huu nchini Misri.
Dupils bado ni mkurugenzi wa ufundi wa timu ya FC Fleury 91 ya Ufaransa na pia anaifundisha Madagascar.
Nchi nyingi sasa hivi zinatumia wachezaji wake wa kimataifa kufundisha timu za taifa za nchi zao au kuwa wachezaji wanafunzi yaani "understudy" kwa makocha wa kigeni ambao huja kwa mikataba maalum.
Tatizo kuwa nililoliona kwa wachezaji wetu na timu nzima ya taifa ni kuwepo kwa lugha- gongana inayofanya kazi ya ufundishaji kuwa ngumu na pia mawasiliano baina ya kocha na wachezaji kuwa si sahihi.
Tanzania kwa sasa ina wachezaji watatu tu wanaocheza mpira barani Ulaya ambako hata iwe ni timu ya daraja la tatu bado viwango vya mpira vipo juu kuliko Tanzania.
Pia mbinu za ufundishaji kutoka kwenye vitalu vya soka hadi kwenye timu za ligi mbalimbali pamoja na timu ya taifa ni za hali ya juu.
Mwaka huu tumeshuhudia fainali za kombe la dunia la wanawake ambapo timu za wanawake pamoja na waamuzi wameonyesha viwango vya juu vya uchezaji na usimamizi wa mpira wa miguu.
Kama taifa tukae chini tutafakari na tuje na uamuzi wa kuanza kuundeleza mpira wa miguu na michezo kwa ujumla.
Litakuwa ni jambo la busara na mbolea iwapo Bwana Samatta ataandaliwa kuwa kocha wa timu ya taifa ya Tanzania kwa miaka michache ijayo pindi atakapoacha kucheza soka.
Huko aliko barani Ulaya kuna kozi maalum ambazo wachezaji wa zamani husomea na mwisho hupewa leseni maalum za kuanza kufundisha mpira wa kisasa kwa kutumia usomi na mbinu za kisasa za ufundishaji.
Kwenye mpira kuna vitu vitatu muhimu ambavyo timu ikikosa basi hushindwa kiujumla.
!. Mawasiliano baina ya kocha, jopo la ufundi na wachezaji ambalo wanapaswa kuongea lugha moja.
Madagascar wanatumia lugha ya kifaransa na hivyo kufanya kazi ya ufundishaji kwa wachezaji kuwa rahisi na tumeona matunda yake.
2. Mbinu za uchezaji - Timu kama haina mbnu za uchezaji basi huishia kufngwa mapema na kukata tamaa. Mbinu hizo ni pamoja na kuangalia kama mnacheza na timu kubwa au ngumu na kujaribu kwenda mapumziko mkiwa sare ya 0-0.
Mwisho mnajarbu kutafuta goli moja tu , na kuhaikisha mnalinda hilo goli kwa hali na mali.
3. Udhibiti wa mchezo yaani "Game Management" yaani kuhakikisha kila mchezaji anakuwa na nidhamu katika uchezaji bila kucheza rafu nyingi zisizo na maana na kuhakikisha wachezaji wote uwanjani wanawasiliana na kumsikiliza nahodha.
Hivyo basi serikali ifikirie kuwagharamia wachezaji khasa wale walio nje ya nchi barani Ulaya na iwe tayari kuwandaa khasa Bwana Samatta ambae anaonekana na uwezo mkubwa wa kuhamasisha timu hivyo kuifanya kazi ya ufundishaji kuwa rahisi.
Bila hivyo tutaendelea kushangaa timu kama Madagascra ikicheza robo fainali za AFCON 2019 na hata kufikia fainali.
Lakini kufukuzwa kwa Emanuel Amunike kuwe ni kigezo cha kuanza kuwatayarisha wachezaji wenye elimu ya mpira kutoka katika nchi zilizoendelea.
Katika nchi zilizostua wengi kwenye fainali za mwaka huu ni timu ya Madagascar au kwa jina la utani la Barea.
Madagascar inafundishwa na kocha mfaransa Nicolas Dupuls ambae aliwahi kuwa mchezaji aliecheza nafasi ya beki wa kushoto wa timu ya FC Souvigny.
Pia amewahi kuchezea timu ya FC Beaumont ya Marekani na baadae kuanza kufundisha mpira kweyne timu ya AS Yzeure ya Ufaransa.
Mwaka 2017 Dupuls aliteuliwa kuwa kocha wa timu ya taifa Madagascar na kama Tanzania mwaka 2018 timu hiyo ikafuzu kucheza fainali za AFCON za mwaka huu nchini Misri.
Dupils bado ni mkurugenzi wa ufundi wa timu ya FC Fleury 91 ya Ufaransa na pia anaifundisha Madagascar.
Nchi nyingi sasa hivi zinatumia wachezaji wake wa kimataifa kufundisha timu za taifa za nchi zao au kuwa wachezaji wanafunzi yaani "understudy" kwa makocha wa kigeni ambao huja kwa mikataba maalum.
Tatizo kuwa nililoliona kwa wachezaji wetu na timu nzima ya taifa ni kuwepo kwa lugha- gongana inayofanya kazi ya ufundishaji kuwa ngumu na pia mawasiliano baina ya kocha na wachezaji kuwa si sahihi.
Tanzania kwa sasa ina wachezaji watatu tu wanaocheza mpira barani Ulaya ambako hata iwe ni timu ya daraja la tatu bado viwango vya mpira vipo juu kuliko Tanzania.
Pia mbinu za ufundishaji kutoka kwenye vitalu vya soka hadi kwenye timu za ligi mbalimbali pamoja na timu ya taifa ni za hali ya juu.
Mwaka huu tumeshuhudia fainali za kombe la dunia la wanawake ambapo timu za wanawake pamoja na waamuzi wameonyesha viwango vya juu vya uchezaji na usimamizi wa mpira wa miguu.
Kama taifa tukae chini tutafakari na tuje na uamuzi wa kuanza kuundeleza mpira wa miguu na michezo kwa ujumla.
Litakuwa ni jambo la busara na mbolea iwapo Bwana Samatta ataandaliwa kuwa kocha wa timu ya taifa ya Tanzania kwa miaka michache ijayo pindi atakapoacha kucheza soka.
Huko aliko barani Ulaya kuna kozi maalum ambazo wachezaji wa zamani husomea na mwisho hupewa leseni maalum za kuanza kufundisha mpira wa kisasa kwa kutumia usomi na mbinu za kisasa za ufundishaji.
Kwenye mpira kuna vitu vitatu muhimu ambavyo timu ikikosa basi hushindwa kiujumla.
!. Mawasiliano baina ya kocha, jopo la ufundi na wachezaji ambalo wanapaswa kuongea lugha moja.
Madagascar wanatumia lugha ya kifaransa na hivyo kufanya kazi ya ufundishaji kwa wachezaji kuwa rahisi na tumeona matunda yake.
2. Mbinu za uchezaji - Timu kama haina mbnu za uchezaji basi huishia kufngwa mapema na kukata tamaa. Mbinu hizo ni pamoja na kuangalia kama mnacheza na timu kubwa au ngumu na kujaribu kwenda mapumziko mkiwa sare ya 0-0.
Mwisho mnajarbu kutafuta goli moja tu , na kuhaikisha mnalinda hilo goli kwa hali na mali.
3. Udhibiti wa mchezo yaani "Game Management" yaani kuhakikisha kila mchezaji anakuwa na nidhamu katika uchezaji bila kucheza rafu nyingi zisizo na maana na kuhakikisha wachezaji wote uwanjani wanawasiliana na kumsikiliza nahodha.
Hivyo basi serikali ifikirie kuwagharamia wachezaji khasa wale walio nje ya nchi barani Ulaya na iwe tayari kuwandaa khasa Bwana Samatta ambae anaonekana na uwezo mkubwa wa kuhamasisha timu hivyo kuifanya kazi ya ufundishaji kuwa rahisi.
Bila hivyo tutaendelea kushangaa timu kama Madagascra ikicheza robo fainali za AFCON 2019 na hata kufikia fainali.